Mwasisi wa CHASO, Deogratius Kisandu ajiunga na CCM

Mwasisi wa CHASO, Deogratius Kisandu ajiunga na CCM

Mapema sana tulimshauri ajiunge na ccm akawa hatuelewi, tulimshauri hivyo kwasababu tangu mwanzo alionyesha tabia mienendo ya ccm, pls Nape Nnauye mpelekeni huyu kisandu kwenye matibabu ya majeraha aliyokua akilalamika enzi yupo nccr la siivyo atahamia ACT huyu
 
Last edited by a moderator:
Huyu si alishatoka CHADEMA siku nyingi akaenda NCCR kwa mbwembwe za mikutano na waandishi wa habari?Huyu Deo ni chizi na anasaka tuvicent,manake huko NCCR alifukuzwa kwa uchonganishi.
 
Mwasisi wa CHASO ajiunga na CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jana tarehe 27 Septemba 2014 kwenye uwanja wa mikutano wa kijiji cha Lwandai kata ya Mlola,lushoto mkoani Tanga.

Deogratius Kisandu ambaye wakati wake alipokuwa Chadema alikuja na hoja za kutaka urais jambo ambalo Dk.Slaa lilimpa tabu sana amejiunga na CCM akitokea NCCR Mageuzi ambapo alikuwa na nyadhifa mbali mbali.

Unajua mtu anayetafuta maslahi asipo yapata lazima atakwenda kuyatafutia sehemu nyingine. Huyu jamaa ndo mwisho wake kisiasa maana na huko ccm akikosa atahamia ACT. Vijana wasiokuwa na msimamo na kutanguliza tamaa zao mbele ni hatari sana
 
Huyu alikuwa kiongozi wa nccr kwanini usiseme kiongozi wa nccr kajiunga ccm?
 
Warioba amevutiwa na sera ya gongo ya babu Slaa

Mi nilidhani amekimbia aibu! Maana JK hamalizi mwezi lazima aende kwa Cameroon! Warioba hataki kuwa na mwenyekiti mwenye uswahiba sana na Cameroon
 
Nenda salama!!! nenda salama!! ndg yetu kisandu,nadhani ukitoka hapo kuna kadi ya ACT,UDP,TLP ,APPT-MAENDELEO zinakusubiri !!
 
Kama sikosei kuna mahali Kisandu alipokuwa analalamika kuhusu NCCR kuwa haimjali baada ya ajali na kuwa hata mkewe "hasaidiwi" maana yeye ajali "imempunguzia" uwezo wa kufanya kazi. Kwa kweli malalamiko yale najua wengi hawakumuelewa ila yalinisikitisha.
Swali langu kwa @Deugratius Kisandu jee CCM wamekubali "kumsaidia" wife wakati huu ukiwa kwenye matibabu?kama wamefanya hivyo basi ni jambo jema sana. Ni vema ukaweka wazi ni kiongozi gani aliyechukua jukumu la kutoa msaada huo, ingawa wengi wanajua mwenye moyo wa huruma "kusaidia" wake wa makada wa chama sii mwingine bali "kipenzi cha wengi" NAIBU KATIBU MKUU BARA.
 
Mwalimu Kisandu...ha ha ha ha ha ha huyu jamaa ana njaa sana. Maana alipokuwa CHADEMA alitangaza kugombea uraisi, alipoamia NCCR-Mageuzi alitangaza kugombea uraisi, ngoja tuone ataibuka na nini CCM. Hii ni mifano halisi ya vijana wengi wa kitanzania.
 
Wana jamvi kijana alie tangaza kugombea urais sasa amejiunga ccm huko rwandai lushoto,mtakumbuka hapo awali nilisha wahi kutoa taarifa hapa jf kuwa kijana ametoka chadema na kwenda nccr nakasema kuwa kabla ya 2015 atajiunga ccm,sasa yametimia
 
Amemaliza kazi aiyotumwa kufanya na bwana zake? Alikuwa anataka kuanzisha mgogoro nccr kwa kutangaza anataka urais ameona hamna aliye na time naye baada ya kupuuzwa na kushindwa kutimiza kazi aliyotumwa kufanya ameamua kurudi kundini akanufaike vizuri na ufisadi

ubakaha wa kisisasa
 
njaa ni kitu hatari sana ! Wito kwa vijana wa leo , fanyeni kazi kwa bidii sana , vinginevyo unaweza kutumia ajali ndogo sana uliyoipata kama kitega uchumi ili uweze kujikimu , SHAME !
 
Dah Kisandu kweli dunia adaha walimwengu shujaa naona anausaka ubunge maskini kaka yangu kama ni kweli imeniuma sana hii, CCM puuuuuh!
 
Mwasisi wa CHASO ajiunga na CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jana tarehe 27 Septemba 2014 kwenye uwanja wa mikutano wa kijiji cha Lwandai kata ya Mlola,lushoto mkoani Tanga.

Deogratius Kisandu ambaye wakati wake alipokuwa Chadema alikuja na hoja za kutaka urais jambo ambalo Dk.Slaa lilimpa tabu sana amejiunga na CCM akitokea NCCR Mageuzi ambapo alikuwa na nyadhifa mbali mbali.
attachment.php

Huyu Jamaa si alishahama Chadema siku nyingi sana, kwanini leo wakati anaingia CCM mnahusisha na Chadema tena, au haitakuwa na utamu akionekana kahamia CCM akitokea NCCR-MAGEUZI. hahahahaha kweli Chadema ndo habari ya Mjini?
 
Vijana wa Bavicha wana nunulika kirahisi sana!
Hongera deogratious kisandu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom