CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani nchini na chama kinachounda kambi rasmi ya upinzani Bungeni ni mwiba mchungu kwa CCM. CCM kama chama tawala kinatumia kila ain aya njia ili kupunguza au kumaliza kasi ya CHADEMA. Leo sijadili njia ZOTE zinazotumiwa na chama changu kudhibiti CHADEMA.
Nazungumzia hii ambayo ni ya mwisho kabisa. Ni ya kuwachanganya wapinzani pamoja na baadaye kuivuruga CHADEMA. Sasa CUF na NCCR-Mageuzi,baada ya rabsha za Bungeni,wanaonekana 'kuiva' na kufanya kazi pamoja. Hatari kubwa kwa CHADEMA. Amini nawaambieni,wapo wapinzani wa CUF na NCCR walioingia humo kwa kazi maalum. CHADEMA ikizubaa kidogo tu,itajuta miaka mingi ijayo.CHADEMA imetegwa mtego wa kisiasa na wa kimbinu.
Ifahamike kuwa siana nia ya kuwasambaratisha 'marafiki hawa wa sasa'.Lakini,nalazimika kusema ukweli.Hii ni kwakuwa,marafiki hawa watajadili pamoja;wataaminiana;watakuwa na msimamo mmoja.Wananchi watawaona hivyo.Mwisho wa sinema hii utakuwa pale ambapo mshirika mmoja au washirika wawili wa urafiki huu atakapotoa Taarifa kwa umma ya kutokubaliana na CHADEMA kwa kile watakachokuwa wamekizungumza faraghani. Hapo,wanachi wataaminishwa kuwa CHADEMA ni wakorofi na hawafai kushirikiana au hata kuaminiwa.
Mwenye kusikia na asikie!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
cc Tumaini Makene Ben Saanane Yericko Nyerere,Dr.W.P.Slaa na wengineo