alexander paulo
JF-Expert Member
- Dec 21, 2011
- 492
- 155
kinachonishangaza kila siku wakiitisha mikutano wanadai wanachama wa cdm wamehamia ccm je wanachama wa ccm ni wapi? je hawana staili nyingine ya kuongea zaidi ya hiyo?
Chadema ndio mwarobaini wa ccm.
Ccm walijua wataiangamiza chadema kwa mbinu walizorumia kwa nccr na Cuf lakini imeshindikana.
Tangu vyama vingi vianze ccm walikua hawajapata chama cha kuwavuruga akili kama chadema.
Wamejaribu kutumia mbinu zao zote kukiangamiza chadema wameshindwa. Sasa hivi wanasubiri kudra za Mwenyezi Mungu kwa kila Uchaguzi.
Yanayo tokea Bungeni na nje ya bunge ni matokeo ya kuchanganyikiwa kwa ccm sababu hawajui nini wafanye.
Hii katiba mpya wanaona ndo inawamaliza kabisaaaa....!!! Yaani sasa hivi wanamlaumu Rais kwanini alikubali mchakato wa katiba mpya wakati hakuwa katika ahadi za ccm.
Sasa hivi kila mtu anajitahidi kula ofisini kwake kwani wanajua fika 2015 ndo mwisho wa ccm.
Chadema ingekua kama vyama vingine vya upinzani hakika Tanzania ingekua taabani zaidi ya hapa.
Namuomba Mungu azidi kuilinda na kuibariki Chadema na Viongozi wake ili haki iendelee kuwepo. Mia
Mbona chadema imeshasambatatishwa? au huoni?
Nyie hangaikeni, 2015, ndo mtawajuwa CCM ni akina nani, si mnahangaika na M4c, Mara kunadi Katiba wao kimya, na uzuri CCM bwana wafuasi wao hawana papara kabisa siku wakianza kuwanyeshea mnaanza kumtafuta mchawi.
Possibly lakini mpaka 2015 hali itakuwa ngumu sana kwa ccm. Kwanza walishaamini cdm inakufa kabla ya mwisho wa 2012 lakini sptember 2013 ni imara zaidi ya kipindi walichodhania itakufa, kesi zote za ugaidi sio zimeisha tu bali kwa aibu. Na moja ya misumari ya mwisho ni mbinu ya Ndugai juzi bungeni alidhani 'wanamaliza mchezo' lakini hadi ninavyoandika hivi kila Mtanzania anawacheka na kuwadharau juu ya kilichotokea pale.2015 ccm itashinda labda kwa kuiba kura au kutumia jeshi, nje ya hapo ccm inaelekea kubaya mwaka 2015...
kinachonishangaza kila siku wakiitisha mikutano wanadai wanachama wa cdm wamehamia ccm je wanachama wa ccm ni wapi? je hawana staili nyingine ya kuongea zaidi ya hiyo?
kwa hiyo kazi ya vyombo vya dola ni kulinda chama tawala? Kama ni hivyo basi ccm ni zaidi ya janga!
mkuu hilo unalosema huenda ni sahihi, suala la bungeni limeongeza umaarufu kwa chadema kuliko ccm, kuna wananchi wanatamani ngumi zipigwe bungeni kati ya ccm na chadema, wakiamini chadema ndo mkombozi wao! Lakini tuwe na tahadhari ccm wanaweza wakalazimisha watangazwe washindi mwaka 2015 kwa kutumia jeshi!Possibly lakini mpaka 2015 hali itakuwa ngumu sana kwa ccm. Kwanza walishaamini cdm inakufa kabla ya mwisho wa 2012 lakini sptember 2013 ni imara zaidi ya kipindi walichodhania itakufa, kesi zote za ugaidi sio zimeisha tu bali kwa aibu. Na moja ya misumari ya mwisho ni mbinu ya Ndugai juzi bungeni alidhani 'wanamaliza mchezo' lakini hadi ninavyoandika hivi kila Mtanzania anawacheka na kuwadharau juu ya kilichotokea pale.
Kwa hiyo hao askari, uwt, jeshi (kama Simbo alivyofanya 2010) huenda isiwe msaada wa maana.
Tutachoma mahirizi yooooote mpaka kieleweke....chadema ni sawa na mgonjwa ambaye ugonjwa wake unapanda na kushuka na ndivyo kilivyo chadema.
kwani huo mkate unatoka wapi? Je si kwamba unachangiwa na wananchi wote? Bila kujali vyama vyao?we ulikuwa hujui? watamlinda nani zaidi ya yule anayewapa mkate wa kila siku
mkuu ccm bila rushwa, polisccm, Tissccm,tbccm, hakuna ushindi!
Tatizo manfikir kura wanapiga wana propaganda wa JF, kura zinapigwa na wananchi wanaojua CCM inafanya nini majimboni mwao.
Mkuu, hivyo ni vyombo vya dola na vina haki ya kuilinda serikali ya ccm. hata mngekuwa nyie mngevitumia
Watu tuna mitazamo tofauti kweli, wakati Watanzania wengi wanaamini Katiba mpya ndiyo ilikuwa karata ya mwisho kwa CHADEMA , kumbe bado wanaojifariji kuwa CHADEMA wana nguvu? kazi kweli kweli.
Nyie hangaikeni, 2015, ndo mtawajuwa CCM ni akina nani, si mnahangaika na M4c, Mara kunadi Katiba wao kimya, na uzuri CCM bwana wafuasi wao hawana papara kabisa siku wakianza kuwanyeshea mnaanza kumtafuta mchawi.