figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Serikali imedhamiria kusaini mkataba wa ubia na Shirika la Emirates National Group (ENG) lenye makao yake makuu Dubai ili kuendesha usafiri wa mabasi yaendayo haraka Dar (DART) awamu ya 1 mwezi ujao.
ENG chini ya Mkurugenzi Bw. Ahmed Abood Al Boasy (Pichani) inamiliki na kuendesha makampuni ambayo yanashughulika na njia zote za usafiri wa kibinafsi na wa umma, pamoja na huduma zao za ziada.
Kamishna wa Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), David Kafulila amesema kuwa ENG ilishinda zabuni hiyo.
Serikali imechukua hatua ya kukaribisha sekta binafsi kuendesha DART ili kuboresha huduma za usafiri mijini kutokana na kasi kubwa ya mabasi kuharibika, kuruka abiria kwenye stendi nyingi za mabasi mbali na vituo vikuu na mabasi mazima kubaki machache.
Mwekezaji huyo atapewa nafasi ya kupewa ruti kwenye awamu ya pili ya mradi iwapo itathibitika kuwa ameweza kuboresha huduma kwa kiasi kikubwa.
Kafulila aliongeza kuwa kuwa mwekezaji mpya anatarajiwa kuleta idadi ya kutosha ya mabasi ili kumaliza msongamano huo.
Kafulila alisema pia kuwa utiaji saini unatarajiwa kufanyika wiki mbili zijazo, huku ENG ikitarajiwa kununua mabasi na kutoa huduma za usafiri “wakati jukumu la DART litakuwa ni kusimamia mapato.”
ENG chini ya Mkurugenzi Bw. Ahmed Abood Al Boasy (Pichani) inamiliki na kuendesha makampuni ambayo yanashughulika na njia zote za usafiri wa kibinafsi na wa umma, pamoja na huduma zao za ziada.
Kamishna wa Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), David Kafulila amesema kuwa ENG ilishinda zabuni hiyo.
Serikali imechukua hatua ya kukaribisha sekta binafsi kuendesha DART ili kuboresha huduma za usafiri mijini kutokana na kasi kubwa ya mabasi kuharibika, kuruka abiria kwenye stendi nyingi za mabasi mbali na vituo vikuu na mabasi mazima kubaki machache.
Mwekezaji huyo atapewa nafasi ya kupewa ruti kwenye awamu ya pili ya mradi iwapo itathibitika kuwa ameweza kuboresha huduma kwa kiasi kikubwa.
Kafulila aliongeza kuwa kuwa mwekezaji mpya anatarajiwa kuleta idadi ya kutosha ya mabasi ili kumaliza msongamano huo.
Kafulila alisema pia kuwa utiaji saini unatarajiwa kufanyika wiki mbili zijazo, huku ENG ikitarajiwa kununua mabasi na kutoa huduma za usafiri “wakati jukumu la DART litakuwa ni kusimamia mapato.”