Mwarabu wa Dubai, Emirates National Group (ENG) wapewa kazi ya kuendesha Mabasi ya Mwendokasi

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
Serikali imedhamiria kusaini mkataba wa ubia na Shirika la Emirates National Group (ENG) lenye makao yake makuu Dubai ili kuendesha usafiri wa mabasi yaendayo haraka Dar (DART) awamu ya 1 mwezi ujao.
28272197 (1).jpg

ENG chini ya Mkurugenzi Bw. Ahmed Abood Al Boasy (Pichani) inamiliki na kuendesha makampuni ambayo yanashughulika na njia zote za usafiri wa kibinafsi na wa umma, pamoja na huduma zao za ziada.

Kamishna wa Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), David Kafulila amesema kuwa ENG ilishinda zabuni hiyo.

Serikali imechukua hatua ya kukaribisha sekta binafsi kuendesha DART ili kuboresha huduma za usafiri mijini kutokana na kasi kubwa ya mabasi kuharibika, kuruka abiria kwenye stendi nyingi za mabasi mbali na vituo vikuu na mabasi mazima kubaki machache.
mwendo-kasi-pic.jpg

Mwekezaji huyo atapewa nafasi ya kupewa ruti kwenye awamu ya pili ya mradi iwapo itathibitika kuwa ameweza kuboresha huduma kwa kiasi kikubwa.

Kafulila aliongeza kuwa kuwa mwekezaji mpya anatarajiwa kuleta idadi ya kutosha ya mabasi ili kumaliza msongamano huo.

Kafulila alisema pia kuwa utiaji saini unatarajiwa kufanyika wiki mbili zijazo, huku ENG ikitarajiwa kununua mabasi na kutoa huduma za usafiri “wakati jukumu la DART litakuwa ni kusimamia mapato.”
 
Nyerere aliwaamini Wachina kwenye uwekezaji
Mwinyi aliwaamini Wananchi wake/sekta binafsi kwenye uwekezaji
Mkapa aliwaamini Makaburu kwenye uwekezaji
Kikwete aliwaamini Wazungu kwenye uwekezaji
Magufuli aliwaamini Wahindi na Mawaziri na Ma RC wake waongo uanzishwaji viwanda
Mama Samia anawaamini Waarabu kwenye uwekezaji

Ngoja tuone!
 
Nyerere aliwaamini Wachina kwenye uwekezaji
Mwinyi aliwaamini Wananchi wake kwenye uwekezaji
Mkapa aliwaamini Makaburu kwenye uwekezaji
Kikwete aliwaamini Wazungu kwenye uwekezaji
Magufuli aliwaamini Wahindi na Mawaziri na Ma RC wake waongo uanzishwaji viwanda
Mama Samia anawaamini Waarabu kwenye uwekezaji

Ngoja tuone!
Wewe unawaamini wepi kati ya ukiowataja?
 
Serikali imedhamiria kusaini mkataba wa ubia na Shirika la Emirates National Group (ENG) lenye makao yake makuu Dubai ili kuendesha usafiri wa mabasi yaendayo haraka Dar (DART) awamu ya 1 mwezi ujao.

ENG chini ya Mkurugenzi Bw. Ahmed Abood Al Boasy (Pichani) inamiliki na kuendesha makampuni ambayo yanashughulika na njia zote za usafiri wa kibinafsi na wa umma, pamoja na huduma zao za ziada.

Kamishna wa Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), David Kafulila amesema kuwa ENG ilishinda zabuni hiyo.

Serikali imechukua hatua ya kukaribisha sekta binafsi kuendesha DART ili kuboresha huduma za usafiri mijini kutokana na kasi kubwa ya mabasi kuharibika, kuruka abiria kwenye stendi nyingi za mabasi mbali na vituo vikuu na mabasi mazima kubaki machache.

Mwekezaji huyo atapewa nafasi ya kupewa ruti kwenye awamu ya pili ya mradi iwapo itathibitika kuwa ameweza kuboresha huduma kwa kiasi kikubwa.

Kafulila aliongeza kuwa kuwa mwekezaji mpya anatarajiwa kuleta idadi ya kutosha ya mabasi ili kumaliza msongamano huo.

Kafulila alisema pia kuwa utiaji saini unatarajiwa kufanyika wiki mbili zijazo, huku ENG ikitarajiwa kununua mabasi na kutoa huduma za usafiri “wakati jukumu la DART litakuwa ni kusimamia mapato.”
hao ENG walishindana na akina nani hadi wakashinda zabuni mu waweke hapa tuone profile zao
 
Nyerere aliwaamini Wachina kwenye uwekezaji
Mwinyi aliwaamini Wananchi wake kwenye uwekezaji
Mkapa aliwaamini Makaburu kwenye uwekezaji
Kikwete aliwaamini Wazungu kwenye uwekezaji
Magufuli aliwaamini Wahindi na Mawaziri na Ma RC wake waongo uanzishwaji viwanda
Mama Samia anawaamini Waarabu kwenye uwekezaji

Ngoja tuone!
pote alikopita Mwaarabu hajawahi mwacha mtu salama
 
Nyerere aliwaamini Wachina kwenye uwekezaji
Mwinyi aliwaamini Wananchi wake kwenye uwekezaji
Mkapa aliwaamini Makaburu kwenye uwekezaji
Kikwete aliwaamini Wazungu kwenye uwekezaji
Magufuli aliwaamini Wahindi na Mawaziri na Ma RC wake waongo uanzishwaji viwanda
Mama Samia anawaamini Waarabu kwenye uwekezaji

Ngoja tuone!
Kila zama na kitabu chake
 
Nyerere aliwaamini Wachina kwenye uwekezaji
Mwinyi aliwaamini Wananchi wake kwenye uwekezaji
Mkapa aliwaamini Makaburu kwenye uwekezaji
Kikwete aliwaamini Wazungu kwenye uwekezaji
Magufuli aliwaamini Wahindi na Mawaziri na Ma RC wake waongo uanzishwaji viwanda
Mama Samia anawaamini Waarabu kwenye uwekezaji

Ngoja tuone!
mwarabu hana hasara
 
Serikali imedhamiria kusaini mkataba wa ubia na Shirika la Emirates National Group (ENG) lenye makao yake makuu Dubai ili kuendesha usafiri wa mabasi yaendayo haraka Dar (DART) awamu ya 1 mwezi ujao.

ENG chini ya Mkurugenzi Bw. Ahmed Abood Al Boasy (Pichani) inamiliki na kuendesha makampuni ambayo yanashughulika na njia zote za usafiri wa kibinafsi na wa umma, pamoja na huduma zao za ziada.

Kamishna wa Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), David Kafulila amesema kuwa ENG ilishinda zabuni hiyo.

Serikali imechukua hatua ya kukaribisha sekta binafsi kuendesha DART ili kuboresha huduma za usafiri mijini kutokana na kasi kubwa ya mabasi kuharibika, kuruka abiria kwenye stendi nyingi za mabasi mbali na vituo vikuu na mabasi mazima kubaki machache.

Mwekezaji huyo atapewa nafasi ya kupewa ruti kwenye awamu ya pili ya mradi iwapo itathibitika kuwa ameweza kuboresha huduma kwa kiasi kikubwa.

Kafulila aliongeza kuwa kuwa mwekezaji mpya anatarajiwa kuleta idadi ya kutosha ya mabasi ili kumaliza msongamano huo.

Kafulila alisema pia kuwa utiaji saini unatarajiwa kufanyika wiki mbili zijazo, huku ENG ikitarajiwa kununua mabasi na kutoa huduma za usafiri “wakati jukumu la DART litakuwa ni kusimamia mapato.”
DART wakibaki kusimamia mapato mambo yatakuwa yale yale.Hiyo haki nayo apewe mwekezaji.DART wabaki kuchunga kupokea fungu lao basi.
 
Kwa lugha nyepesi kabisa ni kwamba ''Watanzania tumeshindwa kuendesha mradi wa Mwendo kasi''

Inashangaza kiasi, inawezekanaje watu binafsi wanaweza kumiliki mabasi na kuendesha huduma za usafirishaji tena ikitumia watu wa kawaida kabisa lakini serikali na taasisi zake na wake wake wasomi wanashindwa kuendesha usafirishaji wa abiria kwenye mji mmoja, tena kwenye njia chache kati ya nyingi za mji huo.
Route:
Mbezi - Kivukoni
Mbezi - Kkoo
Mbezi - Kibaha
Mbezi- Kimara
Mbezi - Morocco
Kkoo - Morocco
Morocco - Kivukoni

Hizi route ni chini ya asilimia kumi ya route za usafirishaji wa abiria hapa Dar.

Nini tunaweza kukifanya kwa ufanisi?
Ni wizi, rushwa, soga, chuki, uongo, uzushi, ngono..............
 
Back
Top Bottom