Mwanza: Mwanamke amuua mwanae wa miezi 9 kwa khanga ili aolewe

Johnny Sins

JF-Expert Member
Nov 4, 2019
2,538
3,832
Helena Washera (19) mkazi wa Nyamilamba, wilayani Kwimba, jijini Mwanza anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza akidaiwa kumuua mtoto wake, Abdalah Simon mwenye umri wa miezi tisa kwa kumnyonga kwa kanga ili aolewe.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Machi 14, 2020 kwa vyombo vya habari na Kamanda wa polisi Mkoa huo, Jumanne Muliro amesema mama huyo alishirikiana pamoja na mpenzi wake, Lucas Jackson (24) akimlaghai wamuue mtoto huyo ili amuoe.

Kamanda Muliro amesema tukio hilo lilitokea kijiji cha Bugembe Februari 25, 2020.

"Baada ya mama wa mtoto kuelezwa na mpenzi wake (Jackson), kuwa amuue mtoto huyo ili amuoe ndipo walifanya hivyo na kuendeleza uhusiano japo walikuwa hawajaona kama walivyokubaliana," amesema Kamanda Muliro

Amesema baada ya muda kupita baba wa marehemu, James Simon alienda kwa mzazi mwenziye (Helena) kumsalimia mtoto wake lakini aliambiwa kwamba mtoto huyo yupo kwa bibi yake na hata alipokwenda kwa bibi hakumuona ndipo alitoa taarifa polisi.

Amesema baada ya polisi kufuatilia jambo hilo na kuwahoji watuhumiwa wote wawili Machi 12, 2020 walikiri kutenda kosa hilo na kuwapeleka ulipofanyikia unyama huo ambapo walikuta mifupa inayosadikiwa kuwa ya mtoto huyo.

Muliro amesema mifupa hiyo imepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya uchunguzi zaidi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanza.

Helena Washera (19) mkazi wa Nyamilamba, wilayani Kwimba, jijini Mwanza anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza akidaiwa kumuua mtoto wake, Abdalah Simon mwenye umri wa miezi tisa kwa kumnyonga kwa kanga ili aolewe.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Machi 14, 2020 kwa vyombo vya habari na Kamanda wa polisi Mkoa huo, Jumanne Muliro amesema mama huyo alishirikiana pamoja na mpenzi wake, Lucas Jackson (24) akimlaghai wamuue mtoto huyo ili amuoe.

Kamanda Muliro amesema tukio hilo lilitokea kijiji cha Bugembe Februari 25, 2020.

"Baada ya mama wa mtoto kuelezwa na mpenzi wake (Jackson), kuwa amuue mtoto huyo ili amuoe ndipo walifanya hivyo na kuendeleza uhusiano japo walikuwa hawajaona kama walivyokubaliana," amesema Kamanda Muliro

Amesema baada ya muda kupita baba wa marehemu, James Simon alienda kwa mzazi mwenziye (Helena) kumsalimia mtoto wake lakini aliambiwa kwamba mtoto huyo yupo kwa bibi yake na hata alipokwenda kwa bibi hakumuona ndipo alitoa taarifa polisi.

Amesema baada ya polisi kufuatilia jambo hilo na kuwahoji watuhumiwa wote wawili Machi 12, 2020 walikiri kutenda kosa hilo na kuwapeleka ulipofanyikia unyama huo ambapo walikuta mifupa inayosadikiwa kuwa ya mtoto huyo.

Muliro amesema mifupa hiyo imepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya uchunguzi zaidi.


Sent using Jamii Forums mobile app
Tuliza kichwa unapoleta taarifa jamvini.Nyamilamba wilayani Kwimba jijini Mwanza kijiji Bugembe ndio wapi huko?

Hongera,umekuwa wa kwanza kuleta hii taarifa jamvini lakini ukaedit hasa kuhusu maeneo lilipotokea tukio.
 
Tuliza kichwa unapoleta taarifa jamvini.Nyamilamba wilayani Kwimba jijini Mwanza kijiji Bugembe ndio wapi huko?

Hongera,umekuwa wa kwanza kuleta hii taarifa jamvini lakini ukaedit hasa kuhusu maeneo lilipotokea tukio.
............................Wewe tusipotoshane acha kutupotosha,kama ulikuwa unaijua hii habari mbona hukuileta zaidi umebaki kama unaijua sana?

Mimi naamini alichokiandika mleta mada ndicho kilichotokea.


Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Mwanamke akisikia neno NDOA anachanganyikiwa,unaweza fikiri ni tiketi ya kwenda peponi
 
Pumbavu Hawa Aliyenyonga Na Aliyeshawishi Wapewe Adhabu Stahiki Kisheria,laana Hii Duh Naogopa
 
Back
Top Bottom