Mwanza: Mangula azomewa kwa aibu

Mwanza: Mangula azomewa kwa aibu

ina maana maenedeleo ni magorofa? Na hayo magorofa yamejengwa na serikali? Vilaza wa ccm ni wengi sana, sehemu kuna weza kukawa na nyumba zilizo ezekwa kwa majani lakini kukwa na maendeleo,
kwani wewe unavyojua maendeleo ni nini?
 
Babu alikimbia usiku usiku kule au mmesahau.Kumbe Mwananchi gazeti zuri ehh
 
hahahahaha...mwananchi mara mnaamini stori zao mara mnaponda

Si suala la kuliamini mwananchi ama la bali huo ndio ukweli8 wenyewe. Jana imerushwa thread hapa kwamba Mangula, Nape na Mwakyembe wamezomewa Mwanza. Kwahiyo walichofanya mwananchi ni kupigilia msumari kwenye kidonda.
 


...

CC LUMUMBA
nyumba ya majangili

Ha ha ha ha! Mkuu hiyo kali. Yaani unataka kutuambia wakati wengine wana "House of Commons" ambapo ni kimbilio la walalahoi na wanyonge wao ni "House of Poachers"; kimbilio la majangili na mafisadi? Teh teh teh teh!
 
hii ya mabungando mengi imenichekesha kweli yaani ndiyo uwezo wao wa kufili umekomea hapo, watu wanataka maendeleo ya moja kwamoja unawaonyesha mabugando wakati milo mitatu tabu, elimu duni, afya duni, mahakamani hakuna haki, polisi wanatuwinda watuue badala ya kutulinda...

Mkuu yegella Nadhani alikuwa hana hoja ndiyo maana alihutubia kwa dakika 5 tu.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu ni muhimu sana kurecord video za zomea zomea na kuziweka humu kuwanyamazisha wakina chama na Ritz
 
Last edited by a moderator:
Iringa mjini walikimbia nape akaenda sokoni kuhutubia wanunua bidhaa na wapita njia aibu tu,alipokuja Tundu lissu tulimbeba juujuu kwa maandamano makubwa vigeregere na furaha sambamba na msigwa ccm haipo tena nchi hii
 
watanzania wa leo wameelimika. Huwezi kuwadanganya kwa kuongezeka kwa idadi ya maghorofa ambayo mengi yanamilikiwa na hao hao mafisadi.
hivi ndugu yangu, wewe ujuavyo maendeleo ni nini? Hebu tupe muongozo wa maana ya maendeleo maana inaonekana unafahamu vizuri juu ya hili!
 
Makamu Mkiti wa CCM Philip Mangula alionja joto ya jiwe mkoani Mwanza pale msafara wake ulipozomewa vibaya njia nzima tokea alipotoka uwanja wa nyamagana kwenye mkutano wa hadhara.

Aibu hiyo ya zomeazomea iliwakumba pia Waziri wa Uchukuzi Dr Harrison Mwakyembe na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye.

Wananchi walijipanga njia nzima msafara huo ulipopita huku wakionyesha ishara ya vidole viwili na zomeazomea ikishika kasi.

Awali Mangula alihutubia kwa dakika 5 tu kitu kilichowashangaza wengi na swala la msingi alilosema ni kwamba CCM imeleta maendeleo katika kipindi cha miaka 50 kwani zamani Mwanza ilikuwa na ghorofa moja tu la Bugando lakini sasa kuna 'Mabugando' mengi.

Source:Mwananchi Jumatatu.

Aisee, this is very serious. Maendeleo = Mabugando? Hawa Magamba wameishiwa sera. Kama hawana cha kuhutubia, wanyamaze kimya kabisa. Watulie kimya. Sio kuhutubia mambo ya kipuuzi kama yale. Sasa hapo Mangula ndio amehutubia kitu gani? Amewaabisha Magamba wenzake.
 
hivi ndugu yangu, wewe ujuavyo maendeleo ni nini? Hebu tupe muongozo wa maana ya maendeleo maana inaonekana unafahamu vizuri juu ya hili!
Kwahiyo maendeleo ni watu wachache wajenge maghorofa kwa hela za EPA MEREMETA na RICHMOND?
 
Mkuu Molemo huyu babu anafikiri hizi ni zile enzi zake za Analogy na propaganda za Urusi na Bulgaria sasa hivi watu wanampa za uso tu

Mkuu Precise pangolin huyu babu alidhani hizi ni zile zama za propaganda ya vita baridi na mataifa yasiyofungamana na upande wowote.
 
Last edited by a moderator:
Aisee, this is very serious. Maendeleo = Mabugando? Hawa Magamba wameishiwa sera. Kama hawana cha kuhutubia, wanyamaze kimya kabisa. Watulie kimya. Sio kuhutubia mambo ya kipuuzi kama yale. Sasa hapo Mangula ndio amehutubia kitu gani? Amewaabisha Magamba wenzake.
Halafu Ma DR kama wakina Mwakyembe na Magufuli wanamsikiliza!!! Huoni CCM ilivyo na Vichaa pamoja na DR wao?
 
hivi ndugu yangu, wewe ujuavyo maendeleo ni nini? Hebu tupe muongozo wa maana ya maendeleo maana inaonekana unafahamu vizuri juu ya hili!

Kiashirio cha kwanza na cha msingi ni kuboreka kwa maisha ya mwananchi wa chini kabisa.
 
Makamu Mkiti wa CCM Philip Mangula alionja joto ya jiwe mkoani Mwanza pale msafara wake ulipozomewa vibaya njia nzima tokea alipotoka uwanja wa nyamagana kwenye mkutano wa hadhara.

Aibu hiyo ya zomeazomea iliwakumba pia Waziri wa Uchukuzi Dr Harrison Mwakyembe na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye.

Wananchi walijipanga njia nzima msafara huo ulipopita huku wakionyesha ishara ya vidole viwili na zomeazomea ikishika kasi.

Awali Mangula alihutubia kwa dakika 5 tu kitu kilichowashangaza wengi na swala la msingi alilosema ni kwamba CCM imeleta maendeleo katika kipindi cha miaka 50 kwani zamani Mwanza ilikuwa na ghorofa moja tu la Bugando lakini sasa kuna 'Mabugando' mengi.

Source:Mwananchi Jumatatu.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Taifa Philip Mangula jana alionja machungu aliyowahi kupata Waziri Mkuu Mizengo Pinda baada ya msafara wake kuzomewa jijini Mwanza.

Msafara huo wa Mangula ulizomewa jana muda mfupi baada ya kumaliza mkutano wake katika uwanja wa michezo Nyamagana.
Katika msafara huo mbali na Mangula pia walikuwapo Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, Naibu Waziri wa Ujenzi, Grayson Lwenge na Katibu Itikati na Uenezi, Nape Nnauye.

Mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo, baadhi ya wananchi waliokuwa katika mkutano huo ambao hawakuwa wamevalia sare za CCM, walijipanga kando ya barabara ya Posta na wakati viongozi hao wakipita waliwazomea huku wakionyesha ishara ya vidole viwili.

Kutokana na hali hiyo, vijana wa CCM maarufu kama Green Guard walianza kuvamia wazomeaji hao na kuanza kutembeza kipigo ambapo vijana wawili ambao majina yao hayakufahamika walijeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili.

Septemba 17, mwaka jana, ndani ya uwanja wa Sahara, Pinda alizomewa na wananchi wakati akihitimisha ziara yake jijini Mwanza, kutokana na kero nyingi zinazowakabili wakazi wa jiji hilo, huku kiongozi huyo akiwataka waachane na ushabiki wa kisiasa.

Awali, akihutubia mkutano huo, Mangula alisema pamoja na kwamba wapinzani wamekuwa wakibeza mafanikio ya ya CCM lakini ukweli utabaki palepale kwamba katika kipindi cha miaka 50 ya utawala huo nchi imepiga hatua za maendeleo.

Mangula alitoa mfano kuwa wakati wa miaka ya nyuma kulikuwa na ghorofa moja la hospitali ya Bugando na sasa yapo ‘mabugando’ mengi.

Mbali na kuelezea mafanikio hayo pia aliwataka wanachama wa CCM kutumia vikao katika mashina kuzungumza na wanachama kubainisha matatizo yanayowakabili badala ya kuzungumza nje ya vikao, jambo ambalo limekuwa likikigawa chama.

Hata hivyo, Mangula ambaye alikuwa akisubiriwa kwa hamu katika mkutano huo, tofauti na matarajio ya wengi hakuzungumza zaidi ya dakika tano.
Wakati akiondoka baadhi ya wananchi hao walisikika walilalamika kuwa walitarajia kusikia mengi lakini hakuna walichosikia.

Kutokana na hali hiyo wananchi hao waliamua kukaa kando ya barabara ya Posta, nje ya uwanja huo na kuanza kuwazomea viongozi waliokuwa wakipita.

Mwananchi
 
Ina maana maenedeleo ni Magorofa? Na hayo Magorofa yamejengwa na Serikali? Vilaza wa CCM ni wengi sana, sehemu kuna weza kukawa na Nyumba zilizo ezekwa kwa majani lakini kukwa na maendeleo,

ndo vichwa vya ccm hivyo!
 
Mabugando mengi yasiyopimwa, yaliyojengwa viwanjani mwa watu ni maendeleo uh?
 
Back
Top Bottom