JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Tukio limetokea Agosti 2, 2023 wakati Deus alipokuwa akicheza na wenzake ambapo fisi huyo aliwavamia.
Akizungumza kuhusu tukio hilo, Mkuu wa wilaya hiyo ya Sengerema Senyi Ngaga amewataka Wananchi hao kuchukua tahadhari dhidi ya wanyama wakali.
Naye, Sadick Jimola ambaye ni Diwani wa Kata ya Katunguru ameiomba Serikali kumpa fidia mtoto Deus kwa kupoteza sehemu ya mkono.
Upande wa Mhifadhi wa Wanyamapori Mkoa wa Mwanza, Godfrey Baisi amesema tayari wametuma kikosi kazi kwenda katika kata husika kwa lengo la kuwaangamiza fisi hao.