Mwanza: Fisi anyofoa kipande cha mkono wa mwanafunzi wa darasa la pili na kuondoka nacho

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Deus.jpg
Mwanafunzi wa Darasa la Pili katika Shule ya Msingi Kasomeko iliyopo Kata ya Katunguru, Deus Dalama (8) mkazi wa Wilayani Sengerema amejeruhiwa na fisi sehemu mbalimbali za mwili ambapo madhara makubwa aliyoyapata ni mnyama huyo kuondoka na mkono wa Deus.

Tukio limetokea Agosti 2, 2023 wakati Deus alipokuwa akicheza na wenzake ambapo fisi huyo aliwavamia.

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Mkuu wa wilaya hiyo ya Sengerema Senyi Ngaga amewataka Wananchi hao kuchukua tahadhari dhidi ya wanyama wakali.

Naye, Sadick Jimola ambaye ni Diwani wa Kata ya Katunguru ameiomba Serikali kumpa fidia mtoto Deus kwa kupoteza sehemu ya mkono.

Upande wa Mhifadhi wa Wanyamapori Mkoa wa Mwanza, Godfrey Baisi amesema tayari wametuma kikosi kazi kwenda katika kata husika kwa lengo la kuwaangamiza fisi hao.
 
Pole kwake.
Hyo fidia kwa nchi nyingine ingembeba hadi utu uzimani pamoja na kupewa mkono wa bandia n.k.
Lakn huku kwetu pa kithenge sana, hapo watajitahd saaaana watampa laki 5 na wataita waandishi wa habari juu kujarb kujionyesha wanajali.
Hii nchi ya kisenge sana kumamaqe..
Kwanza nna hasira subr nkajichome nipoze wenge
 
Aisee maliasili waache zao picha risasi hao fisi waogope kuja kwenye makazi ya watu.
 
SERIKALI INAYOJALI WANYAMA KULIKO WATU WAKE...

ASSUME HUYO MNYAMA ANGEUAWA NA WANANCHI...WANGEFANYA BONGE LA MSAKO...

ALAFU WANAIOMBA SERIKALI GANI FIDIA...HII HII YA SAMIA...AU SERIKALI IJAYO..?

SERIKALI HII INA WATU WAKE...SIO NYIE MASKINI.
 
Back
Top Bottom