Mwanza: Basi la Mohammed Trans lapinduka, wawili wafariki

Mwanza: Basi la Mohammed Trans lapinduka, wawili wafariki

n00b

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2008
Posts
1,028
Reaction score
2,731
Watu wawili wamepoteza maisha wengine wakijeruhiwa baada ya basi la Mohammed Trans la Mwanza-Singida kuacha njia na kupinduka eneo la Ukiliguru, Mwanza!
 
Oooh..........habari ya kusikitisha hii,Mungu awajalie majeruhi wapone haraka na awarehemu marehemu,ajali za barabarani zimekuwa zikituondolea wapendwa wetu katika mazingira ambayo mara nyingi tunaambiwa ni uzembe wa madereva, huwa nahuzunika sana nisikiapo suala la ajali.
 
Mungu awasamehe makosa yao marehemu awapumzishe pale panapostahili amin,majeruhi awatie nguvu wapate kurejea salama katika pilika za kujenga nchi.ila haya mabasi yamekuwa na rekodi mbaya sana ya ajali za mara kwa mara tatizo lake cjui au ndio kafara jaman watatumaliza sasa
 
Nilikuwa nasoma hii habari ambayo imetoa takwimu za masaa 24, na sasa imeongezeka hii tena!!!
Watanzania tumepoteza umakini na tutazidi kuumia! Mungu awarehemu hawa waja wake.
Ajali mbaya yaua watu 22 Rufiji
Rufiji: Siku moja baada ya ajali kuua watu 12 wilayani Same, ajali nyingine mbili mbaya zilizohusisha magari matano zimetokea katika eneo moja wilayani Rufiji na kuua watu 22, akiwamo kondakta wa gari aina ya Toyota Hiace ambaye kichwa chake kimetenganishwa na kiwiliwili.
Ajali hizo zilizopishana kwa dakika chache zilitokea juzi saa 1:00 jioni katika Kitongoji cha Mkupuka, Kata ya Kibiti na zilisababisha vifo vingi kutokana na watu 14 waliojeruhiwa katika ajali ya kwanza iliyoua watu saba, kukanyagwa na gari jingine wakati wakisubiri kupandishwa kwenye gari aina ya Toyota Land Cruiser la Idara ya Maliasili ili kupelekwa hospitali.
 
pichaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Nilipita ukiliguru jana jioni basi limegeuka lilikotokea,tbc wameripoti kuwa majeruhi 20 waliruhusiwa,9hali zao mbaya na wamehamishiwa bugando na 10 walilazwa hospitali moja karibu na eneo la ajali
 
pichaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Picha ndo inponya majeruhi au kuzuia ajali nyingine zisitokee?
 
Hii miezi ya Mwisho wa mwaka ,
Hedaru 10
Rufiji 21
Mwanza 2
 
na hizi mvua, leo nilikuwa natoka dar naenda chalinze, nimekutana na ajali kama 5 za fuso na malori, madereva tuwe makini. pole kwa wafiwa na majeruhi.
 
Mohamed imezidi! Sumatra kagueni magari.

Trafic huishia kutoa salamu to mlangoni, hakuna cha zaidi!
 
Wapumzike kwa amani waliotangulia na Mungu awaponye majeruhi . Amen.
 
Jamani Mohamed Trans ni juzi tu wamepata ajali musoma, leo tena ukiluguru!, mbona sumatra hawawagusi? Mie mohamed trans naogopa kuipanda kabisa.
 
Back
Top Bottom