Mwandosya ajiuzulu?

Kabla hajaondoka tunaomba atupe maelezo kuhusu bwawa lilojengwa kule musoma chini ya kiwango likabomoka.
<br />
<br />
USHAJIAMBIA MWENYEWE CHINI YA KIWANGO SASA AELEZE NINI? NA HELA ALOPIGA PANGA NDO ANATIBIWA NAYO HUKO APOLLO HIHIHIIII
 
tatizo baraza la mawaziri lina vizee kibao vilivyojichokea sasa vinatutia gharama za matibabu wazee muwapumzishe wacheze na wajukuu wamalizie vizuri siku za uhai wao duniani lakini utashanga Rais ajae anamteua KINGUNGE kuwa waziri mkuu hivi mnawaogopa hawa wazee ni wa BUSARA nini!!? MAGAMBA badilikeni
 

Hii nchi ina wenyewe bwana ...sisi watu wa pembezoni ni wasindikizaji tu..ukisema hivyo basi hii nchi tutaikata vipande vipande ..vumilia tu....la muhimu katiba mpya ikija iruhusu serikali za majimbo..maana watu wengine tunarudishwa nyuma kwa kuongozwa na watu wenye akili hafifu.....kwa kunyimwa fursa za kuwa viongozi wa juu.....

Kama watu wa Mbeya wakilalamika kwa wana wao wenye dalili za kuwa watawala kuwa eliminated ...kaskazini wasemeje.....Wananchi wa kawaida wanaamini hivi...alikuja Sokoine ....wakampa za uso,akaja Mrema wakasema hana Degree,akaja Sumaye wakasema ameiba mashamba,akaja Lowassa wakasema ni fisadi ..na mwaka 2025 tutamleta January ...sijui watasemaje.....all in all TUNATAKA SERIKALI ZA MAJIMBO ..ILI TUSHINDANE KWA MAENDELEO BADALA YA KUWEKEANA VIGINGI...NA KURUDISHANA NYUMA.........SIO KWAMBA NINI NAAMINI KANDA YA KASKAZINI IKIWA JIMBO ...INAWEZA KUWA KITOVU KIKUU CHA KIUCHUMI ..,TEKNELOJIA,ELIMU,KILIMO NA UTALII.....NA HATUTAJALI NANI RAIS HATA TUKIENDELEA KUONGOZWA NA ZEZETA MIAKA 100 ....KATIBA MPYA ITAAMUA....NA KUONDOA HII HALI YA KURUDISHANA NYUMA KWA KUONGOZWA NA WATU WAVIVU!!
 
Yaani yuko nje ya kazi zaidi ya Miezi 6 na bado ni Waziri? Jamani nchi yetu, Hawezi kusema anajiuzulu Uwaziri kwa sasa mpaka apone?

Angalia Kenya Mawaziri wana jiuzulu kwanini wakwetu mpaka waondolewe??
 

Are you serious? Visije vikaishia kuwa ni vita vya mdomoni ndugu yangu.
 

Wewe ni nani kakuuliza chama unachoshabikia? Wewe kuwa chadema kuna uhusiano gani na suala la ugonjwa wa Profesa Mark Mwandosya?
 
Vipi TTCL nasikia walimdhamini mtoto wake SA

Yule aliyekuwa anafanya PhD? he kale kasichana nako kamezidi na kusoma bwana! roho inauma kweli aisee! kumbe ndiyo aliua Ttcl mpaka sasa inazidi kufa? ni yeye dah! kazi kwelikweli, alipindisha maamuzi baraza la mawaziri la kutokuuza ttcl? inamaana alipo wahi kuliambia bunge kwamba wale ni wababaishaji, halafu tena akabadilika ghafla kumbe ilikuwa hongo ya mwanae du!na baraza la mawaziri chini ya makapa nao wakamsikiliza ili mwanae apelekwe south Africa?

Sasa kwanini tena alitaka kujiuzulu sababu ya kashfa ya Ttcl halafu akaambiwa akifanya hivyo baraza lote la Mkapa inabidi lijiuzulu? au labda tatizo ni CCM? kwahiyo Ttcl imekufa sababu ya mtoto wake kupelekwa south africa? kama ndivyo hivyo basi hata ndege ya rais ni yeye, rada ni yeye pia hata kama swala la ndege alipewa nakala ya barua ya waziri mramba huku yeye akiwa ni waziri mwenye dhamana hiyo kwa mujibu wa gazeti la Rai enzi hizo nayo tutasemaje?

Na maokola majogo waziri wa nishati na madini aliye sema swala la Tanesco maamuzi ya kuleta management ya matapeli wa South africa haikuwa maamuzi yake bali ni ya baraza la mawaziri, akatolewa wizara hiyo baada ya kusema hivyo akapewak Daniel yona Mnunuzi wa kiwira coal mine kwa bei ya kitapeli nalo unasemaje?

Tatizo ni CCM,IMEOZA KABISA,KUNA VIONGOZI WACHACHE SANA AMBAO WAO WAKIAMUA BASI,HALAFU KUNA MWINGINE HUYO DU YEYE NDIYO HAGUSWI MAANA YUPO JUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU! anaweza hata kukusamehe kama umehujumu nchi,atakuambia rudisha na hakuna wakukuliza wala kusema!

TANZANIA BILA UMEME INAWEZEKANA!
 
<br />
<br />
 
dira ya mtanzania= clouds fm = entertainment media= not reliable source
jamani nilipa nyembamba kwamba mkwele anataka kuwamwaga wote wenye ndoto za uraisi sasa mnyachusa ame pre empty hiyo ni nzuri vilivile kwani ametunza cv.
 
si amini kama mwana JF anaweza fikiri na kuamini eti Prof ktk capacity yake anashindwa somesha mtoto wake ati anahongwa kusomeshewa mwanae,mtoto yule ni msomi wala siyo mbabaishaji wala siyo mzembe kama coconuts tusemee mengine yenye tija kwa taifa kama hamna tukae kimya tusikilize kwa wanaojua.NAONA WENGINE HUMU MA AGENT WA WALE WENYE MAJINI,MSHINDWE NA MLEGEE KABISA,YOTE HAYA MWISHO WAKE UTAFIKA.GET WELL SOON PROF. MWANDOSYA AND STAY BLESSED
 
 
SIRLIMU IBWE;
Naye pia ni gamba??????


Kuna ubadhilifu katika wizara yake wa takriban bil. 63. Ndio maana MH. Kiwia katika hotuba ya upinzani kataka huyu Prof. Mark apishe ofis na uchunguzi ufanyike.
Gamba huyu. Hakwepi hapo.
 
Itakua la maana. Mtu huwezi kuwa waziri halafu ukawa nje ya ofisi miezi yote hiyo. Itakua la maana kwake kujiuzulu maana hata akirudi Mungu akimjalia bado atahitaji recovery period.

Pia saa nyingine hizi stress za kazi haziendani na umri za hawa waheshimiwa kwa hiyo unakuta kubaki madarakani kuna waumiza tu.
 
Hapa nasikiliza katika vyombo vyetu jamaa ana ugonjwa kama wa mwalimu, pia inasemekana ana saratani ya damu, kila kuumwa hakutokani na nguvu za giza
 
Mimi nashangaa wanayofurahia Prof kuumwa na wanayomtakia mabaya. Kila mtu hapa duniani atakufa na Mungu pekee ndio anajua siku na saa ya kila mtu.

Mtashangaa wengine mnatangulia yeye anapeta. Tusitumie siasa juu ya ugonjwa wa mwenzetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…