Mwandosya aitwa Dar kwa shughuli maalum

Mwandosya aitwa Dar kwa shughuli maalum

Huyu alipewa muongozo wa kila kitu kinachoendelea!
 
Zingekuwa zinaendelea kiukweli kweli unafikiri Rais angekuwa anasafiri kihivyo!!?? Maamuzi yote makubwa hayafanyiki akiwa nje!!

Ope
ration tokomeza alikua sauzi kina kagasheki, nahodha et al walipoenda na maji
 
Aitwa kwa kazi maalum au lah hayo hayatuhusu, vyovyote vile iwavyo tunamuhitaji mkulu mwenyewe katika sakata hili. Haiwezekani mtoto wa mkulima aka mfalme wa nyuki abebeshwe lawama wakati mkulu alikuwa akijua kila kitu katika hili. JK jiuzulu fastaaa
 
Waziri asiye na wizara maalum Prof. Mark Mwandosya ameitwa Dar kwa ajili ya shughuli maalum, imefahamika.

Kwa sasa habari za uhakika kabisa ni kuwa kama waziri mkuu Mizengo Pinda atalazimika kujiuzulu jumatatu basi Prof. Mark Mwandosya ndiye waziri mkuu mpya.

Aidha bado haijadhihirika kama Pinda atakaangwa ingawa tayari kuna kila dalili ya serikali kuanguka kwa mara nyingine tena.

Bado haijafahamika ni nini hasa Mwandosya alichoitiwa Dar ingawa ameitwa huko!

Wote ni wale wale tu, ni huyo ndiye alisema Jaji Warioba alikuwa anatukanwa bungeni ili katiba ya CCM ipite. Kwa nini mtu asikaimu tu hiyo nafasi hadi uchaguzi. Si lazima wamuite kaimu waziri mkuu, bali kazi zake zinaweza kufanywa na mmoja wa mawaziri walioko kwenye wizara yake. Hatutaki kubebeshwa tena zigo lingine ambali mhusika atakalia hiyo nafasi kwa mwaka mmoja tu.
Tuwahurumie watanzania jamani.
 
mtasema sana mtaandika sana mtaunda uwongo sana hakuna serikali kuanguka wala hakuna chochote

Muda ulipopost coment yako ilikua ni mapema sana ktk uwasilishaji wa riport ya PAC, vipi baada ya riport kusomwa hadi mwisho bado msimamo wako uko palepale kwamba serikali haianguki? Kama unajua mambo ya siasa vizuri, yale mapendekezo ya kamati pekee yake kabla hata wabunge hawajaanza kujadili, yamemaliza kila kitu. Subiri kesho uone tamko la serikali mtoto wa mkulima atakachokwambia.
 
Tumuulize Nape kama ina info zozote za mdingi kuitwa haraka hivyo....:A S 100:
 
Back
Top Bottom