Mimi kwa kweli hata wanaume wanaovaa nguo za kubana, iwe jeans, suruali ya kipapa n.k. uwa siwaelewi. Huku kuiga uzungu huku. Wao wanavaa nguo za kubana kutokana na hali ya baridi. Sasa siye nasi tunajitikwa tu na joto la bongo!
Of course, hii ya nguo za kubana linaenda hata kwa wanawake, ndiyo maana magonjwa ya ajabu ya sirini yamezidi. Badala ya kuvaa nguo za kupwaya ili mpunge upepo mnajivisha skinny! Halafu unakuta mwanamke ndani ya skinny akiswampa kwenye jua kali!