Ertugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 13,620
- 27,508
My people hope mko poa kabisa ni mwendo wa VPN tu nikisomeka hapa France.
Kuna kisa kimoja nimekipata leo asubuhi nikiwa ndani ya public transport kuelekea job, ni mwanamama ambaye anaongea kwenye line baada ya kupigiwa call kutoka kwa ndugu zake
Bimkubwa huyu analalamika kwamba mumewe daily husema kwamba hana hela,na hivyo majukumu yote ya familia anabeba yeye
Sasa Mungu sio Bey, bimkubwa si akaamua kusachi nguo ya mumewe akakuta shilingi Milioni Mbili [2,000,000/=]
Akasema yeye akachukua shilingi laki Moja [100,000/=] na lengo sio kutumia ila kumfanya mumewe ajue kwamba bimkubwa ameshtukia mchezo.
Na kweli mkulungwa akaingia kwenye line,akauliza wife vipi umechukua hela yangu? Wife akajibu ndio,kwahiyo hapo akauliza si unasemaga huna hela je,hizi ni nini?
Mwamba akajibu ana mahesabu nazo! Hapo nyuma kidogo bimkubwa baada ya kuona mzigo ule aliwaonyesha watoto wake,mnamuona baba husema hana hela je, hizi ni nini?
Baadae kilichofuata ni mwamba akalazimishwa kulala chini,kwasababu vitu vya ndani alinunua wife
Kwahiyo juzi mwamba kalala chini na jana kuamkia leo kalala chini,na bimkubwa akasema ingawa wana nyumba wamejenge wote,ila akimaliza kibanda chake anaondoka
Bimkubwa akasanuka kwamba hata pale mtaji wake unapokata akimuomba mumewe hata 20,000/=, huyu mwamba huwa hatoi
Huyu mwanaume mwenzetu katuangusha sana,kwanini hawajibiki kwa familia yake,kama watu kama nyie mpo humu ebu badilikeni,mwanaume ni kubeba majukumu
Ila kibaya ni Muongo Muongo halafu kaweka mzigo mfukoni mwake,je hajui kuna wake zetu ambao ni majasusi?
Kutoka France kwa mujibu wa VPN mimi expert wako Bey
Ni hayo tu!