Lutala
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 848
- 103
Demu wangu kila tukikwaruzana kidogo anasema mi sio mwanaume ila ni mwanaume suruali.
Tukitulia ananiomba msamaha na kusema kuwa alipitiwa na alikuwa hamaanishi kitu.
Hali hii imejitokeza zaidi ya mara sita sasa kwa nyakati tofauti tofauti.
Je kuna haja tena ya mimi kuendelea kumvumia na msemo wake huo au nimwache aende akatafute wanaume ambao sio suruali ila sketi?
Kaka cha msingi anza mbele. Kwa sisi tuliokulia uswahilini maneno yake yana maanisha kuwa mzee hupigi mashine sawa sawana hivyo kuna jamaa wanakusaidia. Au kama alivyo zungumza mwenzangu, kuwa wewe ni super tegemezi.
Hiyo dhambi haiwezi kwisha au la sivyo wewe ubadilike.