Habari?
Wajameni naombeni msaada wa kimawazo. Kuna mwanaume ambaye anaonyesha dalili zote za kunihitaji kwenye mahusiano lakini hawezi kabisa kutamka kuwa ananihitaji anapokuwa hajanywa pombe.
Anapolewa anaweza kuongea chochote na kuahidi kila kitu. Ila pombe zinapomtoka, atabaki kufanya ishara za kawaida, kupiga simu, kutoka out nk ila Hakuna Jambo la kimahusiano mtakaloweza kuongea. Ukimuuliza hata juu ya plan yenu, atatoa ahadi kwamba mtaongea siku ingine ambapo atategemea akilewa ndipo apige sound.
Binafsi nimeshindwa kuelewa. Ninatafsiri kama mtu muongo ndio maana anatafuta confidence kwenye pombe. Ila angekua anatoa majibu toka moyoni, wala asingepata kigugumizi cha kusubiri kuelewa.
Nimeona mambo yasiwe mengi. Nimeamua aachane na Mimi na hadi sasa ameshindwa kuongea lolote. Ila ikitokea amekunywa, anapiga simu na kuanza kujitetea.
Ndugu zangu, mmewahi kukutana na watu wa aina hii? Na je hiki ninachofikiri Mimi kinaweza kikawa tofauti?
Nawasilisha
Wajameni naombeni msaada wa kimawazo. Kuna mwanaume ambaye anaonyesha dalili zote za kunihitaji kwenye mahusiano lakini hawezi kabisa kutamka kuwa ananihitaji anapokuwa hajanywa pombe.
Anapolewa anaweza kuongea chochote na kuahidi kila kitu. Ila pombe zinapomtoka, atabaki kufanya ishara za kawaida, kupiga simu, kutoka out nk ila Hakuna Jambo la kimahusiano mtakaloweza kuongea. Ukimuuliza hata juu ya plan yenu, atatoa ahadi kwamba mtaongea siku ingine ambapo atategemea akilewa ndipo apige sound.
Binafsi nimeshindwa kuelewa. Ninatafsiri kama mtu muongo ndio maana anatafuta confidence kwenye pombe. Ila angekua anatoa majibu toka moyoni, wala asingepata kigugumizi cha kusubiri kuelewa.
Nimeona mambo yasiwe mengi. Nimeamua aachane na Mimi na hadi sasa ameshindwa kuongea lolote. Ila ikitokea amekunywa, anapiga simu na kuanza kujitetea.
Ndugu zangu, mmewahi kukutana na watu wa aina hii? Na je hiki ninachofikiri Mimi kinaweza kikawa tofauti?
Nawasilisha