Mwanaume kimbia

Mwanaume kimbia

Anatuvuruga mkuu
Mwanaume unaanzaje kukimbia changamoto?

Kukimbia na kurudi, utaishi hivyo kwa muda gani?

Ukikimbia usipopata ndiyo jumla unawatelekeza?

Nini maana ya kuwa kichwa cha familia?

Aliyesema mwanaume lazima awe nacho muda wote ni nani?


Ulioa ili muishi katika raha tu na ikifika wakati wa karaha mkimbiane?


Unaishije na mtu hawezi kuelewa kuna kupanda na kushuka katika maisha?


Unaishije na mtu anaye kuonyesha kujali wakati ukiwa nazo tu, na usipokuwa nazo hakujali? Huoni unatumika?

Unakubalije kuwa mtumwa wa mtu mwingine?


Humu kuna vijana wadogo wanaposoma thread kama hizi ile spirit ya kuwa mwanaume mwenye kuyakabili majukumu inapungua wakiamini mambo yakiwa magumu wakimbie na siyo kupambana kutafuta suluhisho.

Na SIVYO mwanaume anavyopaswa kuwa.

Uliamua kuyavulia nguo, YAOGE mzee.
 
Vijana Oeni wanawake wanaowapenda pasipo kujali una kitu au hauna kitu.

Mwanamke anaekupenda hawezi kukukimbia kwny shida au Raha.

Hao wenye chura na sura watumieni na wafanyeni michepuko TU,

Ukiishiwa unamkimbia speed 120 kwa usalama wako unarudi kwa mkeo kufarijiwa
Kwani hata wanasikia. Nilikuwa naye wakati anapitia kipindi kigumu sana hata hela ya kula ilikuwa shida. Kafanikiwa kakata mawasiliano na karudi kwa mwanamke aliyemkimbia wakati hana kitu. Huyo mwanamke alikuwa naye wakati mambo super, alipoona jamaa hela imekata akawa hana habari naye. Haya ndio maisha
 
Kila mbuzi ale kwa urefu wa kamba yake, kila mmoja wetu atabeba mzigo wake mwenyewe. Kuoa zama hizi ni adhabu ya kujitakia.
Naam nikweli kabisa nimeshuhudia hayo , kuwa mwanaume halafu ukaoa ni Moja ya adhabu 1 kubwa Sana
 
Ndugu acha kabisaa watoto ni kitu kingine aiseee! Ni dhamana aliotupa Mungu haijalishi nitapita wapi niwaaache.
Haujajibu hoja , Swali --- ukifa hao watoto wataishi katika mazingira gani ,
Ukifungwa jela hao watoto wata hudumiwa na Nani ,!?

Binafsi nilitegemea utoe majibu ya hayo maswali
 
Haujajibu hoja , Swali --- ukifa hao watoto wataishi katika mazingira gani ,
Ukifungwa jela hao watoto wata hudumiwa na Nani ,!?

Binafsi nilitegemea utoe majibu ya hayo maswali
Swala la kufa na kufungwa hiyo ni dharura ilio nje ya uwezo, automatically hapo sita kuwa nimekimbia bali dharura ilio nje ya uwezo imetokea.

Lakini hali nina macho, mikono , miguu, nguvu na maarifa kitu kama hicho hapana aisee!

Na hata kama hivyo havitakuwepo bado haitoshi kuwa sababu ya kukimbia ndugu yangu.
 
Back
Top Bottom