Mwanangu mkorofi, anajikojolea kitandani

japhete robert

New Member
Joined
Jul 30, 2019
Posts
3
Reaction score
0
Hii wanajamvi natumaini ni wazima wa afya.

Nina mtoto ana umri wa miaka 6, wa kiume ni kiboko kwa kukojoa kitandani yani hata kama nikimuamsha usiku bado atakojoa tu nimewaza hadi nikaona niandike hii thread lakini pia ni mtundu sana ukimwambia kitu dakika sekunde 30 anakuwa kasahau. Pia hata akifundishwa shuleni anavofika tu nyumbani anakuwa kasahau tayari ila art zake za mwandiko ni nzuri sana, ninaomba msaada wa hali na mali nifanyaje jamani, zamani nilkuwa namuadhibu lakini hadi sasa hivi nimepoa.Hi hali inanikera sana yani.

Lakini pia mchana anacheza sana na usiku analala fofo.
 
pole sana kwa matatizo yanayokukabili.
kuna baadhi ya watoto huwa wanachelewa kuacha kukojoa, lakini wengine huwa ni tatizo la hospital, wengine hupata tiba za dawa za miti shamba. pia kuna maradhi ambayo hata watu wazima huwa wanayo ya kukojoa mpaka ukubwani.

la muhimu la kuanza kufanya ni kuwa na ratiba maalum za saa za kula huyu mtoto, yaani ale milo yake yote pamoja na maji ya kutosha. ikifika saa moja usiku haruhusiwi kula tena mpaka siku ya pili.

Pia jitahidi sana kumuachisha juice kabisa za kutengeneza, badala yake ale matunda. linalofuatia awe analala wakati maalum siku zote, kama analala saa tatu iwe hiyo hiyo haibadiliki.

Sasa kama atalala saa tatu, itabidi saa sita kumuasha kwenda kujisaidia. na ikifika saa tisa hivyo hivyo, Na saa kumi na mbili, huku ukiangalia wakati gani huwa ndio mara nyingi hujikojolea. Watoto wengi hukojoa alfajiri.

Baada ya ratibu kuizoea ya kumuasha muda huo siku zote, sasa akili itaaanza kuzoea na kuamka mwenyewe kwenda chooni, au kama ukiona haamki, jaribu kumuwekea alarm umwambia ukisikia inalia basi lazima uamke uende chooni kama hujaamka nitakupa adhabu. Jengine hakikisha anakoga siku zote kabla ya kwenda kulala.

Kuhusu suala la kusahau, Ni wewe kutenga muda maalum wa kuanza kumsomesha vitabu vidogo vidogo, ikisha unamuuliza masuala kuhusiana na kile ulichomfundisha. inabidi uende taratibu sana, sio kuweka hasira mbele.

Yeye ni mtoto umeamua kumsaidia kwa hivyo inabidi uwe na subra sana. Hapo ndio utaanza kumpima kama akili yake ni nzito au ni mchezo mwingi tuu hata tatizo lolote. usiache pia kumuombea dua wewe na mama ake.
ahsante/
 


Sasa mipicha ya nn humu na moka white?
 
Mpe mtoto samaki wa kutosha,achana na vyakula vya makopo.Lakini pia suala la kusahau inawezekana jinsi unavyuomkabili,kama wewe ni mkali sana kwake usitegemee abadilike.
 
We jamaa uko vizuri sana,haya ni MADINI matupu. Ubarikiwe
 
Mmefanana sana, usimlaumu kachukua tabia zako. Akikua ataacha.
 
Pole ni tatizo kwa watot wengi.
Hata mimi nina wa kwangu ten yrs.
Ni kikojzi vibaya.
Nafanya hivi kuanzia sa moja asinywe
Juis wala maji namuasha mara 2
Ana miez2 hajakojoa.
Uzito wa kuelewa linawapata vikojoz wengi
Ila wa kwangu amebadlika sas ameanza na kupata A darasani.na pia kusinzia darasani ni limpeleka pia kwnye maombi.
Usimpige wakati mwingine adui
 
Akili za bavicha mnazifamu wenyewe!

Sasa picha za nini sasa na kipozi kiboya chako!?
 
Kwahiyo huyo ndio wewe na huyo ndio mtoto wako? [emoji3]
Kwa swala la kukojoa kitandani jitahidini sana asiwe anakunywa maji au soda usiku na mjenge mazoea ya kumuamsha usiku kukojoa mpaka atakavyozoea. Huyo bado mdogo sana si ajabu akikojoa.
Na hilo la kusahau anachofundishwa shule sio kwamba hana akili hapana, ni michezo imemzidi yeye anawaza mchezo tu muda wote. Limit muda wake wa michezo kwa kumuanzishia tution akitoka shule anapita tution akija jion anacheza kidgo mnamuita anakula anaingia kulala. Kulala fofofo ndio kunamfanya anakojoa kitandani kwa sababu anakuwa kachoka sana.
Na wewe kama mzazi tenga muda wa kuwa na mwanao sio tu unamuacha anacheza huko hovyoo. Ndio mwanzo wa kujifunza tabia za ajabu.
Tatu anaweza kuwa karithi vitabia vyako [emoji23][emoji23]
 
Utafiti wa twaweza unaniambia mapigo hayo na mapozi hayo wewe ni muimba kwaya....alafu unautindio wa ubongo Sasa hilo limpicha La nini.... Au unadhani huku ukurasa kitabu....huku maelezo tu picha zibakize kwnye Tecno yako y3.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…