Mwanangu amegongwa na Pikipiki

Mwanangu amegongwa na Pikipiki

Wamenigongea mtoto wangu asubuhi hii anavuka kwenda shule akiwa kwenye Zebra, magari yote yamesimama lakini yeye akajifanya ana haraka sana akaunga na baada ya kumgonga akataka kukimbia.

Sasa hapa tupo Hospitali, tukitoka hapa huyo jamaa nitamshughulikia mi mwenyewe, nna hasira nae sana.
Mkuu punguza hasira, usije 'jinunulia' murder case.

Tumia taratibu za kawaida za kisheria, ingekuwa vyema uripoti tukio hilo kwenye Police Station ilyo jirani na hilo tukio lilipotokea.
 
Pole sana mkuu, hawa jamaa wajinga sana, ule upepo unapowapuliza unaondoka na akili zao
 
unataka kumshugulikia mpiga kura wa Lowassa...Bodaboda Republic
Inawezekana ikawa huyo boda boda akawa miongoni ya wale boda boda waliotoka Mbarali na kusafiri kilomita 600 kwenda Dom, kwa lengo la kumshawishi mzee wa mamvi agombee Urais, na si ajabu akawa miongoni ya waliomchangia EL ile laki 6 ya kwenda kuchukulia fomu ya kugombea Urais.
 
Tunamuombea mtoto apone!! Na wewe japo una hasira sana nakuombea pia ukianza kushugjulika na huyo mjinga akili zako ziwe zimesharudi kichwani.
Umebahatika sana kupata muda kuvita pumzi. Otherwize unaweza kuua. Inauma sana.
 
Ndg zangu wana Jf mi nawashukuru wote mliomuombea mwanangu apate ahueni, ametibiwa......ndg wa aliyemgonga nao wamekuja, kwa kuwa hakuumia sana mtoto nimewaambia wanirudishie tu gharama zangu zote nilizotumia.

Kasheshe iliyopo sasa..... Kumbe aliyemgonga mtoto siyo anaetambuliwa kwa tajiri, yeye alipewa deiwaka tu na kibaya zaidi hana leseni, na yule anaetambulika kwa tajiri (aliyetoa deiwaka) nae pia hana leseni...... Kwa hiyo wote wamewekwa ndani kituo cha police kumsubiri mmiliki wa pikipiki
 
Pole Sana bora kama hajavunjika sehemu, yawe maumivu ya nyama tu.
 
Pole sana, tunamwombea mtoto apone upesi. Safi sana kwa kumkamata huyo aliyemgonga.
 
Pole sana na Mungu atamponya upesi,yani hawa Bodaboda akili zao sijui zimekaa wapi?.
 
Pole sana kaka yangu, shukuru Mungu mwanao anaendelea vizuri. Mi huku jana bodaboda kaua mtoto wa jirani yangu, hivi tunazika leo...........inauma sana jamani.
 
Ndg zangu wana Jf mi nawashukuru wote mliomuombea mwanangu apate ahueni, ametibiwa......ndg wa aliyemgonga nao wamekuja, kwa kuwa hakuumia sana mtoto nimewaambia wanirudishie tu gharama zangu zote nilizotumia.

Kasheshe iliyopo sasa..... Kumbe aliyemgonga mtoto siyo anaetambuliwa kwa tajiri, yeye alipewa deiwaka tu na kibaya zaidi hana leseni, na yule anaetambulika kwa tajiri (aliyetoa deiwaka) nae pia hana leseni...... Kwa hiyo wote wamewekwa ndani kituo cha police kumsubiri mmiliki wa pikipiki

Mkuu pole sana kwa kufikwa na jaribu ili ukiweza ukumbuke maandiko yanasemaje.

Naomba nikukumbushe maandiko kupitia Biblia takatifu.

Yesu akawaambia nyinyi msalipo msali hivi:-
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe,.................. UTUSAMEHE MAKOSA YETU KAMA SISI TUNAVYOWASAMEHE WALIOTUKOSEA................ Kwa kuwa ufalme ni wako na nguvu na utukufu hata milele AMEN.

Jipime katikati ya mistari hiyo utajikuta uko huru, wala damu ya mwanao usiibebeshe gharama ulizotumia, bali fuata walifanya nini enzi za Musa kwa matukio yaliyosababisha kutoka ngeu.
 
Pole sana. Ninakuunga mkono katika kumshughulikia wewe mwenyewe kwani serikali imelala!!
 
Pole sana Galadudu kwa yaliyokupata, tunaomba Mungu amponye mwanao haraka. As for the bodabodas hilo ni janga, serikali inapaswa iwaze mara mbili juu ya uamuzi wa kuruhusu bodaboda nchini

Nashukuru mkuu dogo sasa hivi yuko vizuri
 
pole sana,hawa jamaa hawana hakili kabisa ..jana wameua mwanajeshi mmoja pale lugalo,zebra kama kawaida na boxer zao wakamfyatua mjeshi akafa hapo hapo.

Duh..... Wape pole familia ya mwanajeshi
 
Mkuu punguza hasira, usije 'jinunulia' murder case.

Tumia taratibu za kawaida za kisheria, ingekuwa vyema uripoti tukio hilo kwenye Police Station ilyo jirani na hilo tukio lilipotokea.

Baaada ya dogo kugongwa tulienda kwanza kuchukua Pf3 na jamaa akawa kawekwa ndani, kwa hiyo imebaki kuwa kesi ya polisi maana hata jamaa hana leseni ya kuendeshea
 
Back
Top Bottom