Kamakabuzi
JF-Expert Member
- Dec 3, 2007
- 2,904
- 1,364
Mwanaume mmoja ambaye jina halikuweza kupatikana mara moja, amejifungua mtoto wa kiume kwa operesheni huko Biharamulo.
Maelezo ya awali yanadai kwamba mwanaume huyo ambaye ana mke, alimpachika mimba binti ambaye haikujulikana kama ni mwanafunzi au la. Baada ya hapo alikataa katakata kuwa hahusiki na mimba hiyo, ndipo wazazi wa binti walipoamua kumkomesha wakaenda walikojua wao na mimba ikahamia kwa huyo mwanaume. Ameibeba miezi yote iliyokuwa imebaki na kujifungua. Mke wake ndiye ananyonyesha huyo mtoto.
Kama kuna wana JF walio biharamulo watujuze zaidi.
Je hii si inaweza kuwa suluhu ya wanaowatia mimba watoto wa shule?
Maelezo ya awali yanadai kwamba mwanaume huyo ambaye ana mke, alimpachika mimba binti ambaye haikujulikana kama ni mwanafunzi au la. Baada ya hapo alikataa katakata kuwa hahusiki na mimba hiyo, ndipo wazazi wa binti walipoamua kumkomesha wakaenda walikojua wao na mimba ikahamia kwa huyo mwanaume. Ameibeba miezi yote iliyokuwa imebaki na kujifungua. Mke wake ndiye ananyonyesha huyo mtoto.
Kama kuna wana JF walio biharamulo watujuze zaidi.
Je hii si inaweza kuwa suluhu ya wanaowatia mimba watoto wa shule?