Mwanamke wa kupanga mahali

Mwanamke wa kupanga mahali

iphone 18 promax

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2012
Posts
2,917
Reaction score
2,142
Jamani kuna vituko sana nina mwanamke ambaye ndio nataka kumuoa lakini anapanga mahali kuwa
1.hela ya uchumba nitoe tsh100000 na hela ya vinywaji tsh 80000
2.mahali ni tsh 1000000
Hivi jamani hii nayo imekaaje kwa waliooa ndio mwanamke unayemuoa anapanga mahali au wazazi ndio jukumu lao
 
yeye ndio kwao atakuwa na sauti aka msemaji wa familia mtegemewa wao lazima akuambie hivyo mkuu huna huo mpunga nini? maana usitegemee kitu tofauti mkuu..
 
mbona ela ndogo sana hiyo. sijaelewa unalalamika ela ni ndogo sana au kubwa?
 
kubwa sana na saizi nimenunua bati za msouth kwa ajili ya kuweka kwenye nyumba yangu
 
. Mbona ndogo hiyo?
Maana makabila mengine utaambiwa mablanketi ya babu na bibi, hela ya bibi, mkaja wa mama, mashangazi, za wajomba, halafu ndo mahari na uombe kusiww na mbuzi au ng'ombe

Ila huyo mwanamke kama ana busara angepanga kiwango ambacho anajua kiko ndani ya uwezo wako ( ila mahari wanapanga wazazi banaaaa)
 
^^
Ha ha! Haki za wanawake-kusikilizwa na kuamua
^^
 
Bora Mpemba anakuambia umnunulie Kitanda na Kabati lakini vyote mnaenda kutumia nyie.
 
Jamani kuna vituko sana nina mwanamke ambaye ndio nataka kumuoa lakini anapanga mahali kuwa
1.hela ya uchumba nitoe tsh100000 na hela ya vinywaji tsh 80000
2.mahali ni tsh 1000000
Hivi jamani hii nayo imekaaje kwa waliooa ndio mwanamke unayemuoa anapanga mahali au wazazi ndio jukumu lao
Ni MAHARI na sio "mahali'
 
ndogo sana. Halaf inategemea na utamaduni, kuna baadhi ya makabila mwanamke anaruhusiwa kutaja mahari yake. . .especially hizi matrilinear societies za huku kusini, mwera, yao, makonde kama sijakosea.
 
Nyumba yako ama yenu wewe na mkeo? Ulitakiwa udaiwe mahari billioni moja wewe!

Unajuaje huyo mchumbao kauliza kwao ndio wakamuambia ujiandae kihivyo? Ukienda kuoa na hiyo attitude mtatesana na mwenzio badala ya kupeana raha. Utajisikia kama umenunua kwa bei ambayo sio halali. Mna shida ya mawasiliano, natamani ungeinshughulikia kabla ya kuoana.
kubwa sana na saizi nimenunua bati za msouth kwa ajili ya kuweka kwenye nyumba yangu
 
Exkidumu, sijui kama niko sahihi. Lakini nadhan8 hata baadhi ya imani mahari anataja bi harusi na anaipewa mwenyewe?
ndogo sana. Halaf inategemea na utamaduni, kuna baadhi ya makabila mwanamke anaruhusiwa kutaja mahari yake. . .especially hizi matrilinear societies za huku kusini, mwera, yao, makonde kama sijakosea.
 
Hahaha usitishike na hizo bati za kizulu. Inawezekana kajenga room 2 zimejipanga mstari anaita nyumba. Manake mjini mtu akikuambia naenda 'nyumbani' anaweza kumaanisha 'chumbani'
By mwanakungumbala
kubwa sana na saizi nimenunua bati za msouth kwa ajili ya kuweka kwenye nyumba yangu
1,180,000/= siyo pesa ya kuja kulalamika hapa, dogo. Zaidi, naona unataka tujue unajenga na umenunue bati la Msouth.
 
Jamani kuna vituko sana nina mwanamke ambaye ndio nataka kumuoa lakini anapanga mahali kuwa
1.hela ya uchumba nitoe tsh100000 na hela ya vinywaji tsh 80000
2.mahali ni tsh 1000000
Hivi jamani hii nayo imekaaje kwa waliooa ndio mwanamke unayemuoa anapanga mahali au wazazi ndio jukumu lao

Kuna baadhi ya makabila/dini; mpangaji wa mahari huwa ni muolewaji. Then wazazi/wanandugu huongezea garama zingine za kimila n.k. Kama huyo mrs wako mtarajiwa anatokea huko nadhani anapaswa kutamka kiasi kidogo sana na ziada (hata kama unayo) ije isaidia kujenga maisha yenu kiuchumi n.k) Tofauti na hivo labda anamalengo ya tofauti zaidi ya kitu-mahari.
 
Back
Top Bottom