Mwanamke wa kupanga mahali

Mwanamke wa kupanga mahali

kubwa sana na saizi nimenunua bati za msouth kwa ajili ya kuweka kwenye nyumba yangu

Dah!! Umenichekesha sana mkuu... goma kabisa jenga nyumba yako weka na Italian tiles. ..mambo ya kumgharamia mtu anaekuja kunenepea kwako kwa chicken wings zako tupa kuleeee
 
Sasa mdau calculation ya mahari ulitegemea upigiwe na TRA kama unavyonunua used car?
 
Mshiko mdogo sana huo...jipange tu
 
Mbn mahari ya kawaida hiyo jamani.we toa tu uchukie jiko
 
Pesa ndogo hiyo..km hitaki kuoa acha...hulazimishwi..wenzio ht wakiambiwa bei gani wanatoa..only bcoz hataki kukipoteza chombo
 
Toa hela wewe nimemwambia kabisa huyo mpwa wangu kiwango hicho, tena ni kidogo kulingana na tulivyopata historia yako kwamba una hali ngumu. Muulize mtwasi mwenzio tulimpangia sh ngapi tena ni mwaka juzi. Yaani hako ka million moja ndio uje ututangaze humu Nyambafuuuuu!!!!!
 
Niliposoma nikadhani ni mwanamke amepanga nyumba mahali.Kumbe ni mahari
 
Jamani kuna vituko sana nina mwanamke ambaye ndio nataka kumuoa lakini anapanga mahali kuwa
1.hela ya uchumba nitoe tsh100000 na hela ya vinywaji tsh 80000
2.mahali ni tsh 1000000
Hivi jamani hii nayo imekaaje kwa waliooa ndio mwanamke unayemuoa anapanga mahali au wazazi ndio jukumu lao

Watu wanaoa m1 mpaka m2 wackitika 280000
 
kwanza kuliko yote swala la mahali sio la wazazi tu wanalipanga.
Inategemea na madhehebu aliotokea.
Kuna makabila mengine mtoto mwenyewe ndio anapanga mahali.
Kuna makabila mengine baba anapanga mahali.
Na kuna makabila mengine mama ndio anapanga mahali.
Na mengine yule aliekupa jina siku unazaliwa, na wengine yule alie kulea.
Na kuna makabila mengine ukoo mzima unapanga mahali.

So kwanza inabidi ufuatilie madhehebu ya kwao huyo mchumba wako.
Labda kwao anaetaka kuolewa ndio mwenye haki kupanga mahali je?
Watu wanaweza kukuambia mengi, so kuwa makini kabla hauja amua kufanya lolote juu ya mchumba wako.



Kuna watu wanaolewa bila mahali,
Na wengine ujipangia mahali wenyewe,
Na wengine uolewa na mahali kubwa
Na wengine uolewa na mahali ndogo
Na wengine uolewa na mahali nusu.
So usipende kujifananisha na wengine, hayo ni maelewano yako na mchumba wako na wazazi wenu.

Fuatilia madhebu ya kwao, na fuata masharti.


Kama uwezo wako mdogo na yeye anataka mengi muambie hauna uwezo uwo, basi bora musioane, hakika kama anakupenda uwo ushangingi wa vinywaji utamtoka kichwani.


Mwanamke akikupenda kweli unaweza kumuoa bila mahali au mahali ndogo sana.

JUU YA WANAWAKE WA SASA
Wanawake wa sasa wengi wanataka sifa, waoneshe kwa marafiki zao kuwa wameolewa na mahali kubwa, na sherehe kubwa.
Na hata mama zao ndio hivo hivo, uswahili.

Kuna kaka mmoja alisema yeye hataki kuoa, sababu gauni ya harusi laki 2, madhahabu, viatu, saloni na vipambo, anakadilia laki 5 kwa pamoja. matarumbeta, baikoko, taarabu, nk. vyakula na vinywaji.
Anakadilia ni milion 10.

Baada ya miezi sita anadai talaka, kisa uwezo wa kununua gari kama mume wa rafiki yake hauna.

Nawapa pole wanaume.


Mungu akusaidie uoe kwa gharama sahihi na udumu nae ktk ndoa.
 
Jamani kuna vituko sana nina mwanamke ambaye ndio nataka kumuoa lakini anapanga mahali kuwa
1.hela ya uchumba nitoe tsh100000 na hela ya vinywaji tsh 80000
2.mahali ni tsh 1000000
Hivi jamani hii nayo imekaaje kwa waliooa ndio mwanamke unayemuoa anapanga mahali au wazazi ndio jukumu lao

Hii mbona ya kawaida sana sana....
Mahali mnapanga wote wewe na yeye ili kujua uwezo wako,then ndipo yeye anaenda kumtaarifu wajomba zake/baba wadogo kulingana na tamaduni zao,very normal hii..
 
Ya kwangu mimi na ndio maana nataka nijibane ili tutakapooana afikie kwenye nyumba yangu niachane na maisha ya kupanga yana shida sana
 
Mkuu yeye ni lutherani ndio kanisa analosali
kabila ni mnyamwezi
elimu diploma
kazi ameajiliwa serikarini
na mimi msukuma elimu degree
nimeajiliwa serikarini lakini yeye anataka tufunge ndoa ya kifahari pamoja na mahari hiyo huku mimi nikiparangama na ujenzi wangu na hali ya maisha ni ngumu sana nina duka anasema tulifunge ili mtaji huo tufungie ndoa tukimaliza tutafungua jingine mimi nimekataa jana kaniambia nikamwambia mimi uwezo wangu huo sina nikamwambia anichangie akasema kishika uchumba atatoa tsh 20000 na mimi nitoe tsh80000 na hela ya vinywaji na mahali atatoa tsh 50000 na mimi nitoe 950000
 
katika mila zetu waislam, bi-harusi ndio anataja mahari. so usishangae. alaf naona yupo fair tu wala hajataja nyingi. kama unajenga maliza kwanza kujenga ndo uanze mpango wa kuoa.
 
Mi nafikiri ungeomba msaada uchangiwe hapa jamvini,hapo bado hujaoa,ukiwa nae ndani matumizi yakakuzidia utakuja kuuliza.Tafuta hela bhana!
 
Huyo kwao ndio ana sauti. Wamelelewa na mama kwa sababu ndingi alisepa. Madem wa hivo ni wengi tu na hata ukimuoa atataka yeye ndio awe na say kwenye kila kitu. Utakuja ishia kutelekeza familia au ukubali kuwa mume bwe-ge a.k.a MBWA.
 
Back
Top Bottom