Mwanamke unayajua haya

Mwanamke unayajua haya

QEEN ADEMU1

Senior Member
Joined
Dec 24, 2019
Posts
134
Reaction score
324
WANAWAKE

1. Ukiwa Kama mwanamke, pale panapotokea maudhi dhidi ya mpenzi wako, nyamaza kimya, ukimya wa mwanamke humsumbua akili mwanaume. Atahisi kuna jambo fulani kichwani mwako na kama anabusara atatafuta njia ya kusuruhisha. Usiwe mtu wa tit-for-tat.

2. Kama atakutumia ujumbe wa maudhi katika simu, usimjibu kwa maneno ya kuudhi pia. Muandikie "Samahani" au "Asante sana.".

3. Hakuna mwanaume anapenda mwanamke anayemrudishia maneno, kama wewe ni mke uliye na busara, funga mdomo wako. Pale atakapokuwa ametulia ongea nae mmalize mgogoro.

4. Usiringie uzuri wako. Hujawaona wanawake wazuri wengi tu bado wako single, huvaa nguo za kuacha miili yao wazi, ziwa linaonekana wazi bila kujua wanaume hawapendi hivyo nao wanaishia kuwa wezi wa waume za watu na uzuri wao kama wameshushwa toka mbinguni? Tabia yako itakuhifadhi katika moyo wake.

5. Kamwe usimfananishe na EX wako au mwanaume mwingine, huwezi jua huyo mwanaume nae ana mapungufu gani katika mahusiano yake. Binadamu hatuko 'perfect' na hatufanani....Mvumilie muombeee

6. Usiwe wa kupokea tu, mnunulie chochote, haijalishi kama anavyo vingi au ni kidogo sana, ila kilichotoka kwako siku zote kina umuhimu mkubwa kwake...na hii itaamsha hali ya kujaliana

7. Kuwa mwanamke mwenye mawazo 'mtambuka' usifikirie jambo moja tu, mshauri masuala ya maendeleo, miradi, kununua vip-longa na mengineyo. Usiwaze habari za kucha, nywele, mapochi na shopping, nguo za kuacha miili wazi, hayo mambo kwa mwanaume yamepita kushoto. Na ni ya ziada tu...fikiria juu ya kufanya familia yenu iwe bora zaidi

8. Mheshimu yeye pamoja na familia yake, usidharau wadogo zake, dada zake na kaka zake, hana namna hao ndio ndugu zake na kimbilio alilo nalo, hata kama hawana hali nzuri.

9. Mambo madogo ila yana maana kubwa, mpigie simu, kamwe usisubiri yeye ndio akutafute. Mapenzi ni 'two way traffic'....mchokoze hata kwa msg za hapa na pale .

10. Jithamini wewe kwanza na yeye atakuthamini.....usikibilie kuthaminiwa wakati wewe haujithamini una Tshert ya uchaguzi mdogo ndiyo unayonyonyeshea ...ilishabadilika mpk rangi kufua hautaki unasingizia upo busy saa ngapi mumeo atakuthamini

11. Kwa kuwa hana ukwasi leo, haimfanyi kuonekana ndio atakuwa na ukata milele, tizama sana ni nini kinamuendesha kichwani mwake. Tizama sana mawazo yake chanya na njaa ya kutafuta mafanikio. Ila kama yeye awaza ngono na pombe tu, hilo ni jipu uchungu.....fanya kila unaloweza mtenganishe na marafiki zake wapenda ngono na pombe

MAOMBI YANGU KWAKO
Mwenyezi Mungu akufungue macho katika mahusiano yako, na kama bado hujapata akuongoze vema ukampate yule aliye sahihi, maana lengo la mahusiano sio kuumizana kihisia, bali ni kuziunganisha furaha zetu tulizokuwa nazo hapo mwanzoni kabla ya mahusiano na kutengeneza furaha kubwa zaidi.

Like Page

Sent using i phone x
 
wanawake wote wangekuwa hivyo kwa waume zao DUNIA ingekuwa sehemu salama sana kwa kuishi
Umasikini ungepita kando
majanga ya asili yangepungua
Idadi ya watoto wa zinaa ingepungua
ukimwi tungeusikia kwenye bomba
michepuko ingepata tabu sana
Ndoa ingekuwa kitu cha thaman sana 7bu zisingevunjika hovyo
n.k


Sent using Jamii Forums mobile app
 
wanawake wote wangekuwa hivyo kwa waume zao DUNIA ingekuwa sehemu salama sana kwa kuishi
Umasikini ungepita kando
majanga ya asili yangepungua
Idadi ya watoto wa zinaa ingepungua
ukimwi tungeusikia kwenye bomba
michepuko ingepata tabu sana
Ndoa ingekuwa kitu cha thaman sana 7bu zisingevunjika hovyo
n.k


Sent using Jamii Forums mobile app
Wanaume nyinyi wenyew vichaa, halafu mnataka wenzenu wawe timamu....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Si unaondoka kwani baba yako mzazi huyo?

The issue is... je intergrity ipo? Kama unafanya ili tudumu kwenye ndoa ni afadhali usiyafanye.

Kuondoka ni rahisi hivyo??? Ume invest time na pengine mna familia tayari.. watoto?? Wanawake ni wavimilivu sababu wanazaa kwa uchungu,wanatake full responsibilities of offsprings... huwaga najiuliza km wanaume ndio wanazaa .. ndoa zingedumu?????
 
Haya mambo mie naonaga yanakuja automatic tu kama mna mutual feelings and understanding.
Ila yale ya ilimradi hata vya kujilazimisha vinagoma.
 
Kuondoka ni rahisi hivyo??? Ume invest time na pengine mna familia tayari.. watoto?? Wanawake ni wavimilivu sababu wanazaa kwa uchungu,wanatake full responsibilities of offsprings... huwaga najiuliza km wanaume ndio wanazaa .. ndoa zingedumu?????
Kama sio rahisi ina maana yanavumilika yanayokusibu.

Kwa hiyo mwanamke asiye na uwezo wa kuzaa hana uvumilivu mkuu? Full responsibilities... kina baba kuhangaika kote na familia ila hatuonekani tu...ndiyo maana tunakufa mapema na stress kisa tu hatuonekani tunachofanya.
 
Back
Top Bottom