Mokaze
JF-Expert Member
- Aug 3, 2018
- 14,370
- 14,945
Kwa nini neno starehe linaleta ukakasi ?
Linaleta ukakasi kwa mujibu wa fikra za nani ?
Kwa sababu kama umekubali neno chombo ni sifa nzuri ya kumpa mwanamke manake unataka kutuambia kuwa neno starehe ni baya na halina maana ni udhaliloshaji.
Sasa naomba uniambie neno starehe kama ni udhalilishaji ni udhalilishaji kwa mujibu wa nani ?
Kwa sababu neno chombo tumeona kuwa halina tatizo ni sifa nzuri.
Sasa kusema chombo cha starehe inakuwaje neno zuri hilo chombo likiungana na neno starehe inageuka iwe sifa mbaya ?
Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa hatuzungumzii neno; Chombo wala hatuzungumzii neno; mwanamke na wala hatuzungumzii neno; starehe, Tunazungumzia maneno yanayojenga hii sentensi kwamba; " Mwanamke ni chombo cha starehe".
Ni hiyo sentensi nzima kwa ujumla ndiyo inayomfanya leo mwanamke awe dhalili duniani, na mimi nashangaa eti wewe Safuher inakuaje unaunga mkono kauli zinazowatia utumwani wanawake (mama zetu), hivi ni wewe huyo Safuher ninayekujua ndani ya jf au mwingine???, umekumbwa na kitu gani kuunga mkono kauli za "kitwaghuti"??!!

