Hutaki kujadiliwa kuhusu familia yako???--- swali, wewe huna dada, shangazi, mama mdogo, mama mzazi, binti au hata binti za nguguzo nk???, kama unao je hao sio wanawake???, na kama ni wanawake, je wao hawahusiki kuwa vyombo vya starehe??!!--- au wanawake wa starehe ni vyangudoa tu??---- hao vyangudoa sio mama, dada, shangazi, mabinti nk wa watu kama wewe???.
Safuher, unaposema; mwanamke ni chombo cha starehe, hiyo ni kauli mbaya sana ni kumdhalilisha mwanamke katika kiwango cha "kifaa" kama toilet paper unayoweza kuitumia upendavyo kukidhi haja zako za STAREHE.
Nimekuambia maneno; "mwanamke ni chombo cha starehe" ni sawa na maneno ya kizungu; "A woman is a comforting stuff", Chombo cha starehe ni kifaa cha starehe, hayo maneno yako yanatoa taswira ya vitendo vya watu wa magharibi jinsi wanavyo mtendea mwanamke kama chombo cha starehe, angalia jinsi mabondia wnapokutana katika "face off" pembeni kunakuwa na wanawake walio nusu uchi, angslia wale "ring girls" wanaoshika vibao vya kuonyesha rounds, hutembea nusu uchi, hii yote inatokana na kauli mbovu ya; "mwanamke ni chombo cha starehe".