Sam82
JF-Expert Member
- Feb 11, 2013
- 295
- 193
Ndugu napenda kukuambia ukweli kuwa ni aghalabu sana kukuta mwanamke mwenye mtoto akavunja mahusiano ya moja kwa moja na baba mtoto wake. Mimi binafsi nimeona mifano mingi sana, hakika sikushauri kuoa mwanamke mwenye mtoto wakati mabinti wamejaa.
Mtoto ni kiunganishi kikubwa sana kwa wazazi hao wawili hata kama si leo bali hata kesho. Siku mtoto akiwa mkubwa mwenye uwezo akaamua kumuita Baba yake kisha akamuita mama yake, je unahisi utakuwa katika hali gani? Mapenzi ya waliozaa huwa kuisha ni ngumu sana hata kama waliachana katika hali mbaya, msamaha huwa upo japo kuoana itashindikana.
Ingia ukijua kuwa kuwa unaenda kukabiliana na changamoto nyingi katika familiya mbili tofauti, nikimaanisha mtoto wa mkeo na watoto wako ambako kote mkeo atacheza kama mhusika mkuu.
Mtoto ni kiunganishi kikubwa sana kwa wazazi hao wawili hata kama si leo bali hata kesho. Siku mtoto akiwa mkubwa mwenye uwezo akaamua kumuita Baba yake kisha akamuita mama yake, je unahisi utakuwa katika hali gani? Mapenzi ya waliozaa huwa kuisha ni ngumu sana hata kama waliachana katika hali mbaya, msamaha huwa upo japo kuoana itashindikana.
Ingia ukijua kuwa kuwa unaenda kukabiliana na changamoto nyingi katika familiya mbili tofauti, nikimaanisha mtoto wa mkeo na watoto wako ambako kote mkeo atacheza kama mhusika mkuu.