SWEET RIZIKI
JF-Expert Member
- Jul 3, 2017
- 288
- 387
Kifupi Hisia za mapenzi za wanawake wengi huamshwa na KUSIKIA Maneno Mazuri ya Mahaba kutoka kwa mpenzi wake . Awe mwanamke wa umri wowote ule na wala haijalishi umedumu nae kwenye mahusiano kwa muda gani Suala ni kwamba wanawake tunapenda kudeka kwa mabwana zetu ukifaulu hapo Neno kunyimwa unyumba utasikia tu jf au kwenye redio.
Kitandani
ndipo haswa na kuonesha ujuzi wako wa kuchekesha na kufurahisha .Kuwa comedian kwa mkeo usiseme atanichukuliaje ,ndo atasisimka na kukumbuka kila ukisafiri ni Miss you, baby unarudi lini.
Jamani kaka, baba, wajomba na watoto wetu wa kiume jaribu sasa kubadilika ilibTanzania ya Viwanda iende sambamba na Familia zenye Furaha na Watu wenye Furaha. Furaha ya Mwanamke itakuletea faida nyingi ikiwemo
1. Mapenzi moto moto yasiyochuja.
2. Watoto wenye akili na wanaojiamini.
3. Familia bora.
4. Utendaji kazi bora na uliotukuka.
Wanawake wengi kwa asilimia kubwa wameweza kuamsha Hisia za Wanaume kwa Kupitia KUONA , siku hizi karibia kila mwanamke ni mrembo na anavutia haswa hivyo wanaume msituangushe twende sambamba tuijenge Tanzania imara.
Jamani ni kukumbushana tu, ahsanteni.