Mwanamke kakimbia na akili yangu

Mwanamke kakimbia na akili yangu

Duniani Kuna vituko hiki chako ni zaidi ya hivyo mkuu

Huyo ni mkeo Chagua moja kusuka au kunyoa kwa kuwa na maamzi ya kiume juu ya hatima ya family yako

Kama hapo ni kwako mtimue huyo mwanamke aende akaishi na huyo mwanaume maana huko ni kuvuana nguo hadharani
 
Hii ni dharau kubwa Mkuu. Nimemfanyia mengi mabaya lkn kwa hili analolifanya linanipa akili mpya sio ile niliyokua nayo mwanzo
Dah, mkuu, yaani mkasa wako nimeubeba kama wangu, nikauchukulia kama ni Mimi, hakika machozi yamegonga hodi kwenye mboni zangu ila sijafungua. Inauma, inauma mno, lkn mkeo hakupaswa kufanya yote hayo. Pole mkuu, ushauri wangu, jipange upya, Anza upya maisha yako, tubu kwa muumba wako, muombe msamaha na ondoka hapo nyumbanikapange hata Chumba uanze upya. Hakika utaona tofauti maishani mwako.
 
Umemkosea sana mwanamke ila iyo revenge siooo. Ia kufanya. Ongea na boss wako akupe siku 3 usitoke kwako.siku ya kwanza ona kama atakuja na ya pili. Ya tatu.asubuhii ukiwa na akiri timamu. Toa vitu vyote vya mke wako vitoe njee mwambie "nenda kaishi na mmeo"

Option ya pili, ndani ya hizo siku 3 Waite wazazi wa mkeo.wakabidhi mtoto wao.

Tatu achana na nawaza ya kuchoma nyumba itakucost maisha yako.

N.b nyie mlipo fikia no need of reconciliation seperation is the best option. Ukikaa mwenyewe utajitathimini upya na akiri itakaa sawa.watoto peleka boarding.

Awe mme au mke kuleta malaya ndani ya hiyo dhambi hata kwa mungu haisameheki.

Machungu ya mwanamke kumtesa ni zaidi ya kuchomwa mkuki hicho alichofanya ni last option maana yake anataka umfukuze wewe mwenyewe. Then do it.

Lastly. Usisahau kuwa kuna procedure za Mahakama in case akitaka mgawane mali. Tho anaweza akuachie kila kitu aondoke na mr pradooo
 
We jamaa kama mpaka sasa hujaenda kulewa.... Naona una mpango wa kuwachomea ndani... Sio kawaida yako kuwa timamu hadi mida hii...
 
Aiseee kweli naona uchungu ktk maandishi yako hujaandika ilimradi kuandika ,,, mtu mzm anapolia ujue kuna mawili either kaumia sana au anafuraha sana .

Kuhusu Mdigo sio kwamba kaondoka na akili yako ,maana mpaka mnaachana na mdigo nikithibitisho tosha kua akili yako ipo,,, kinachokumaliza nafikra juu yanhuduma alokupa hususan kupewa kisichopewa ,,,hii kitu ukishaipata kiukweli inavuruga sana akili naunaweza kuitelekeza familia .

Kuhusu Mkeo ,, kwatabia alofikia nimbaya sana haiwezekan afanye ubaya eti kisa naww ulifanya baya,, Kama Huyo mama angekua anajielewa namwenye Hofu na Mungu yeye ndo angekua mstari wambele kukuokoa wewe mume wake kwaajili ya familia yenu ,, lkn sio kufanya huo ujinga ambao mwisho wasiku utawamaliza wote. HAPA MKEO NAWEZA SEMA SIO MKE BORA.

Kuhusu Afya yako ,,,, Kwanza nakuomba nipo chini ya magoti yako ,,Ondoa mawazo mabaya yakuhisi Una HIV aiseee utakonda Sana'a sanaaa , kuzorota Kwa afya yako nisababu ya Msongo mkubwa was mawazo ulopitiliza ,,kukoswa usingizi wakutosha ,,,Unywaji wapombe ulopitiliza ,, Kwaufupi upon na emotional stress ambayo itakupa physical complications kama vile ulcers ,,mawazo heartache n.k .... Mkuu kwaiyo ndio maana unazota .

TIBA

Jaribu kujipa muda wa kuongea tatizo lako na marafiki unaowaamin .

Kula balanced diet ,,,na kunywa maji mengi kila Mara ,,,plz plz make sure muda wote unachupa ya MAJI YA KUNYWA Kilimanjaro..Maji yanaondoa stress ,,maji yanang'arisha mwili ,,maji ni kiungo muhimu ktk ubongo ,,maji yansongeza mzunguko wadamu mwilin na volume ya dam mwilin,,AISEEEE KULA NA KUNYWA MAJI .

Make Sure unakua Positive Muda wote Yaan hapa MKUU NAKUITAJI UWE POSTIVE KIMWILI NA KIMAZINGIRA MAKE SURE UNAEPUKANS NSMAMBO YANAYOKUPA JAZIBA AU KUFIKIRIA VISIVOFIKIRIKA .

ACHA KABISA KUNYWA POMBE ,,IYO MIPOMBE NDO INAONGEZA MATATIZO NA AT THE SAME TIME INAKUYUMBISHA KIUCHUMI ,,,Aiseee Mkuu IVI UNAJUS WEWE NI MWANAMME BORA SANA ?? IVI UNAJUA WATU WENGI WANATAKS KUA KAMA WEWE ??? YOU ARE GENTLEMAN ,,WISE SASA KWANN UJIONE MKOSAJI KIASI IKO ????KWANN UJIHISI USIYEFAAA ???? BINAFSI SIKUJUI MKUUU ILA DAAAH KTK MAANDIKO NMEKUONA KAMA MWANAMME MWENZANGU AMBAYE UNAUPEKEE WAHALI YA JUU NA MWENYE BAHATI USIYE MAKUU ,,SASA KWANN UJIHISI MWENYE DHAMBI KIASI IKO ???? CAMOOOON AISEEEEE UNGEKUA KARIBU YANGU NINGEKUPIGA MINGUMI YA URAFIKI AISEEE( kidding).

SASA MKUUU NATAKA TUIBADILISHE FAMILIA HUSUSANI MKE ,,NA MUISHI KAMA ZAMANI NAJUA UPO TAYARI ,, UNGANA NAMI SASA .


KWANZA SUALA LA KWENDA KUPIMA KWASASA ACHANA NALO.

USISHIRIKIANE KIMAPENZI NAMKEO KWA MUDA .

BADILIKA ,,IKIWEZEKANA OMBA KIJILIKIZO CHA MWEZI .

MAKE SURE UNAANZA KUJIFANYIA USAFI WAKO BINAFSI NA IKIWEZEKANA FANYA USAFI WANYUMBA WATOTO ,,,HAPA USICHOKE ( mfulie mkeo nguo zake ,,,ningumu ila Fanya ivo ) make sure wewe ndo unajifanya kua mama wa nyumba ,,,HII ITASAIDIA SANA KUMSHINDA MOYO NAKURUDISHA MOYO WAKE KWAKO ,,,,ATAKUA ANAJIULIZA ( "" KWANN HUYU MWANAMME AMEBADILIKA NA KUANZA KUA MWEMA NAMNA HII ??????) ILI SWALI HATOLIPATIA MAJIBU NAMWISHO ATAAMUA KUJIRUDI. ..N.B hapa tunamtesa akili Kwa faida ya familia .

HAYO UWE UNAYAFANYA HUKU KILA SIKU YA KUSALI UNAENDA KANISANI ,,,AISEEE NASISITIZA FANYA HAYO UKU UKIENDELEA KUSALI ,,TENA IKIWEZEKANA HAKIKISHA UNAANZISHA IBADA YAUSIKU NYUMBAN ,,UNAWAITA WATOTO UNAMKARIBISHE NAYEYE ,,HATA AKIKATAA KILE KITENDO KITAANZA KUMSUTA MWENYEWE SO NI AMA AKUBALI YAISHE AU AENDELEE KUUMIA ,,NAKWAMOYO WA WANAWAKE NIWADHAIF HAWAIMIL KUUMIA.

BADAE SASA PIGA HATUA KWENDA KUPIMA DAMU PEKE YAKOOOOO.

ENDELEA KUISHI KAWAIDA N.B KWAUO MUDA USIRUHUSU KUMGEGEDA ,,YAAAN WEWE MFANYIE WEMA BILA KUOMBA KITU IN RETURN.

UTAJIKUTA SIKU MOJA ATAANZA KUJISOGEZAAAAAAA HUYOOOOOOO MARA KUJISEMESHAAAAA MARA CHUNGWAAAAA MARA AHITAJ KUKUNYOA NDEFU NAMWISHOOO ATAKUJA KUTAKA MCHEZO ,,,, NGUVU YA KUSAMEHEWA KWA MWANAMKE WAO HUA WANAAMINI AKIKUOMBA MSAMAHA ALAFU UKAFANYA NAYE MAPENZI NDIO UNAKUA UMEMSAMEHE ,,, SASA IKIFIKA HAPO ,,USIMKATALIE IA MWAMBIE """ MKE WANGU SOTE TUMEFANYA MAKOSA ,NIVEMA TUSIENDELEE KUFANYA MAKOSA , NAITAJI KUFANYA IKI KITENDO TUKIWA HURU ,NAOMBA TWENDE TUKAPIME KWANZA ILI TUANZISHE MAISHA MAPAYA "" n.b wewe utakua umeshajifaham sasa ule ujasiri ulouonyesha kwake unazidi kukupa nguvu ya kumshinda nayeye kuamin sasa umerudi ..


Yaaan ukijiua ,,SIKU namimi nikifa kama rafiki Nitakutafuta popote ulipo alafu nikutie bakora kila siku kwahuo ujinga wako.

Mkuu all in all Mwenyezi Mungu akusaidie ,, muwe wote naafya njema nazaidi ,,mrudi kuisha maisha yen mtunze familia . napenda kuona unarudi ktk mstari ,,mambo mazur yapo mbele ,,,usiruhusu yalopita kukuumiza..


Mche Mungu kwakua ktk yeye utayaweza yote.
 
Boss sijawahi kuishi maisha ya ndoa, kwahiyo sijui sana huko kuna nini.

Lakini maisha ya mapenzi, visasi, maumivu na karma nimeyaishi na yamenifanya niwe niliye Leo na namshukuru Mungu naishi kwa Amani sana.

Mkuu nilifindishwa kutotumia mabavu wala kilevi kama suluhisho la ugomvi na machungu (Haswa ya mapenzi). Na Leo nafurahia sana, me nawaangalia tu wengine kama senema tu.

Nakushauri, kwanza kwa sasa achana na pombe (Kama unaipenda sana utainywa mbeleni kwa starehe), Pili achana na hilo wazo la kuwachomea ndani na ukafie mbali. Kwa kufanya hivyo utakuwa mbinafsi na mchoyo sana, tena sio mchoyo kwa mwingine Bali mtoto/watoto wenu. Hawatakuwa na both mom and dad, je unataka waje wakuwe na kuwa kama MDIGO? I hope not.

Chill boss wangu. Wasihi kabisa kistaharabu wakupishe kwako wakaendeleze upendo mbali. Kumbuka huyo mwanamke anachofanya Leo sio akipendacho anaongozwa na Trauma tu ya kubakwa na aliemuamini ambae ni wewe.

Kama muda ulivyokufundisha wewe, na yeye pia in time atatulia tu. Mtalea matunda yenu mkiwa hai na kila mmoja akiwa amejifunza.

Kwa sasa wasihi tu wakupishe sio picha nzuri kwa mtoto.

Pole mkuu, I can't say najua ni kiasi gani unaumia, ila niamini mimi Nina idea

Hii Simu Sio Ile, Hii Ni Hii
 
Pole sana mkuu, ni kweli dunia imeharibika na naskitishwa sana na kosa hilo ulilolifanya, mkuu unastahili sehemu ya lawama katika hili, na mdigo pia ana sehemu yake. Ukirejea wakati unataka umuoe mama Yasi nina uhakika ulikosea katika vigezo. Kama unge-search vizuri katika jamii basi ungempata mdigo tangu kipindi hicho na haya yote pengine yasingetokea. sasa ona mkuu unamtia mwanao Yasi kwenye matatizo mazito sana, anaelekea katika kukosa malezi yenu. Ki ukweli mkuu umemuone mama yasi na unastahili kumuomba msamahaa katika hili, nachukua kumuona mwanamke analia. Hawastahili kulizwa hawa viumbe, sote tuna vimeo vyetu huko mitaani lakini wadau iweje mpaka ifikie tunawaliza. Hii ni mbaya kabisa mkuu, kwa upande wa pili mimi nahisi ulabu hautakusaidia katika kurudi katika hali yako ya mwanzo ukizingatia mdigo amezingua tayari, sote tunafanya makosa lakini mbora wa wanaofanya makosa ni yule mwenye kuomba msamaha. Sijui kama member wengine wa JF tunachukulia hii kama paukwa pakawa au kama funzo.
 
Hapo mi naona umebaki wewe Kutoa tamko la kuanza kuishi maisha chanya na kuachana maisha hasi ambayo yamekufikisha hapo so Amua kubadilika achana na mentality ya mdigo kuchukua akili yako maana nimeangalia ulivyoipresent mada yako vizuri then nashindwa kushawishika kuwa mtu aliyechukuliwa akili anawezaje kueleza kitu kwenye mtiririko mzuri kama ulivyoandika

Post sent using JamiiForums mobile app
 
In short aliyechukuliwa Akili hawezi kuandika mada ikaeleweka wewe achana na hiyo mentality anza kwenda hata church ubadili maisha hayo ya kuelekea kuzimu

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Ukishaamua kuwa na familia kona kona za pembeni achana nazo...

Unajiingiza kwenye comparison za kijinga na kuiona familia yako siyo chochote mwisho wa siku unapoteza dira na muelekeo...



Cc: mahondaw
 
Ukipata mpenzi/ mke/mume anayekujali chunga sana. Utajidanganya nimepata kitu kingine kitamuu sura, six pakii, pesa ila muda haudanganyi utakuja kumbuka baadae utalia tu moyoni hata kama umeoa au kuolewa
 
OK nimekuelewa aiseee.

Post sent using JamiiForums mobile app


Na wewe tafadhali naomba ufute hiyo comment yako tofautisha hadithi ya kutunga na hadithi inaytoka moyoni. Hii ni tofauti na porojo zangu za kila siku, usiniharibie uzi chonde kijana.
 
Ni kweli kabisa afya yangu imezorota kupita kiasi. Lakini sidhani kama kurudiana naye itawezekana tena. Kinachoniuma sio yeye kua na mtu mwingine lkn kumleta ndani kwangu ndo kunakonifanya nifikirie siku moja nirudi nimelewa niwangojee waingie ndani nichome nyumba moto nitokomee nikafie mbali .
fanya hivyo mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom