Mwanamke anapobebeshwa yasiyomuhusu!

Mwanamke anapobebeshwa yasiyomuhusu!

Zinduna

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2011
Posts
2,378
Reaction score
3,392
AdamEve.jpeg


Tafsiri ya awali ambayo ni potofu inamhusu Adam na Hawa au Eva zimewaaminisha waumini wa hizi dini mbili maarufu hapa nchini kwamba Hawa au Eva ndiye aliyemhadaa Adam kula tunda lililokatazwa la ule mti wa katikati.

Kwa tafsiri hiyo potofu inaonekana kama vile Hawa ndiye aliyemtongoza Adam hadi kumfikisha mahali ambapo alikubali kumuasi Mungu. Naamini miongoni mwetu tumewahi kusikia baadhi ya wanaume wakisema kwamba, mwanamke ni kiumbe aliyelaaniwa kwa sababu ya kumdanganya Adam.

Nadharia hii ambayo ilipotoshwa imekuwa ikifundishwa hivyo kwenye mafunzo ya dini yenye kuhusu chanzo cha binadamu na dhambi. Kwa jinsi mafunzo hayo yanavyotafsiriwa na wengi yamemfanya mwanamke kuonekana kama mdanganyifu kama nyoka na laghai jambo ambalo si kweli hata kidogo.

Kwa mfano unaposoma Quran, kuna maelezo yanayobainisha ukweli kwamba Adam anahusika mwenyewe kwenye kosa hilo. Ukisoma kwenye Suratu Taha, yaani Sura ya 20: 115 Mungu anasema, “Na tulimpa ahadi (nabii) Adam zamani, lakini alisahau. Hatukuona kwake azma kubwa (kama za wale mitume wengine).” Aya ya 21 Inasema, “ Basi wakaula wote wawili, na uchi waoukawadhihirikia na wakaanza kujibandika majani peponi (humo). Na Adam akamkosea Mola wake, na akapotea kidogo njia.”

Je ni wangapi kati yetu ambao wanaujua ukweli kuhusu huu ushawishi ambao baadhi ya wanaume huutumia kuwakandamiza wanawake?

Ukweli ni kwamba hakuna kwenye vitabu vyote viwili vya hizi dini zetu maarufu hapa nchini ambapo kuna mahali panaonyesha kuwa mwanamke ndiye chanzo au aliyelaanika kwa kumlaghai Adam kula tunda la mti wa katikati. Ni tafsiri tu iliyotengenezwa ili kuupa nguvu mfumo dume na kumkandamiza mwanamke.
 
mwanamke ndiye aliyempa mume wake tunda ale ipo hivyo
 
Wanawake wasingekuwepo duniani, shida na dhambi nyingi zingepungua. Ila ukweli ni kuwa tungemisi kitu kimoja kitamu sana. Wanawake wamesababisha watu wasimwogope Mungu. Ni rahisi sana kumsaliti Mungu kwa sababu ya utamu wa Mwanamke.

Mi penda sana utamu wa mwanamke. Hakika wanawake ndo watanipeleka motoni. Dhambi nyingine ni rahisi sana kwangu kuzikwepa, isipokuwa ile ya utamu wa mwanamke asiye mke wangu.

Kwa kweli dhambi hii hata majogoo na mabeberu hawaikwepi.

Mungu atusamehe tu, manake utamu wenyewe kausababisha yeye.

Amina.
 
Wanawake wasingekuwepo duniani, shida na dhambi nyingi zingepungua. Ila ukweli ni kuwa tungemisi kitu kimoja kitamu sana. Wanawake wamesababisha watu wasimwogope Mungu. Ni rahisi sana kumsaliti Mungu kwa sababu ya utamu wa Mwanamke.

Mi penda sana utamu wa mwanamke. Hakika wanawake ndo watanipeleka motoni. Dhambi nyingine ni rahisi sana kwangu kuzikwepa, isipokuwa ile ya utamu wa mwanamke asiye mke wangu.

Kwa kweli dhambi hii hata majogoo na mabeberu hawaikwepi.

Mungu atusamehe tu, manake utamu wenyewe kausababisha yeye.

Amina.
Sasa wewe kwani Mungu aliwakataza kupata utamu? Mungu aliweka utaratibu wake wa namna ya kupata huo utamu ambao ni Ndo halali kwa mujibu wa Dini lakini sasa ninyi wanaume tamaa zimewazidi
 
Sina uhakika kama umeisoma vizuri Biblia, maelezo yako yana walakini kidogo.

Nitarejea...
 
Mh, unaposema eti hakuna sehemu ambapo vitabu hivi vimesema Eva akamdanganya Adam unakuwa umekosea. Biblia yangu kuanzia Mwanzo 3:1 inasema nyoka alianza kukutana na Eva kwanza then Eva akaongea na Adam kuhusu lile tunda na si nyoka kuongea na Adam. Acha uongo wako Zinduna.
Itabaki kuwa Eva/mwanamke ndiye aliyemshawishi Adam/mwanaume kula tunda.
 
Nakusubiri tena uharakishe

Zinduna soma kwa makini maandishi mekundu...pia elewa maongezi yalianza baina ya nani na nani?

Mwanzo 3

1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?

2 Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;

3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.

4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.

6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.
 
Last edited by a moderator:
Tumjue kwanza aliepotosha nadharia hiyo nakuifanya ifundishwe ndio atakaye kuwa chanzo cha kujenga imani hiyo.
Hapo sasa ndo tutajua hapa mwanamke hakuhusika kudanganya mwanaume.
 
Mods tafadhari naomba uzi huu msiupeleke Jukwaa la Dini maana wengine hatuna access huko..

cc: Pruner, Fang, Moderator
 
Last edited by a moderator:
Mh, unaposema eti hakuna sehemu ambapo vitabu hivi vimesema Eva akamdanganya Adam unakuwa umekosea. Biblia yangu kuanzia Mwanzo 3:1 inasema nyoka alianza kukutana na Eva kwanza then Eva akaongea na Adam kuhusu lile tunda na si nyoka kuongea na Adam. Acha uongo wako Zinduna.
Itabaki kuwa Eva/mwanamke ndiye aliyemshawishi Adam/mwanaume kula tunda.

Hivi Adam hakuumbwa na ubongo na hakuwa na uwezo wa kufikiri
 
Zinduna soma kwa makini maandishi mekundu...pia elewa maongezi yalianza baina ya nani na nani?

Mwanzo 3

1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?

2 Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;

3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.

4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.

6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.

kwa hiyo unataka kutuambia kwamba zamani nyoka alikuwa anaongea?

we huoni kwamba kuna lugha ya picha hapo?
 
Zinduna ukiendelea kusoma kifungu cha 9 na kuendelea bado utaona kuwa mwanamke ndiye aliyeleta kadhia yote...

Soma kwa makini maelezo yaliyo katika rangi nyekundu...


9 Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi?

10 Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha.

11 Akasema, Ni nani aliyekuambia ya kuwa u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale?

12 Adamu akasema, Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala.

13 Bwana Mungu akamwambia mwanamke, Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala.
 
Last edited by a moderator:
Sasa wewe kwani Mungu aliwakataza kupata utamu? Mungu aliweka utaratibu wake wa namna ya kupata huo utamu ambao ni Ndo halali kwa mujibu wa Dini lakini sasa ninyi wanaume tamaa zimewazidi

Tatizo huu utamu hauna kikomo. Kila tunda lina utamu wake na wanaume tunalitaka. Na nyie wanawake hamna hiana. Mnatupa tu tunda lenu. Na sisi tunalila tu. Hatuna jinsi.
 
Quran imewataja wanawake hivi;- "hakika hii ni miongoni mwa vitimbi vyenu wanawake kwani vitimbi vyenu ni vikubwa mno" (surat yusuf). Sio Adam tu alieshawishiwa na mwanamke, umemsahau Yusuf? Mke wa mfamle alimfanyia mengi mpaka akafungwa yusuf bila kosa lolote, wanawake ni viumbe waajabu sana
 
Zinduna soma kwa makini maandishi mekundu...pia elewa maongezi yalianza baina ya nani na nani?

Mwanzo 3

1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?

2 Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;

3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.

4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.

6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.

Bado hujanionyesha mahali ambapo panaonyesha kwamba Eva au Hawa alimhadaa Adam, hapo panasema tu kwamba alimpa mumewe naye akala, hata hivyo Adama alikuwa na uwezo wa kukataa kula na kumkumbusha eva kwamba tulikatazwa kula huo mti wa katikati. Kumbuka hapa sizungumzii swala la Eva kutangulia kula tunda bali napinga kusingiziwa kumhadaa Adam au kumshawishi kama tulivyoaminishwa.

Lakini pia Mungu alimuumba Adam na ndipo akamuumba Eva kutokana na ubavu wa Adam, kama maandiko ya hizo dini mbili maarufu hapa nchini yanavyosema, na pia maandiko hayo yanasema kuwa huyu Adama ni kichwa cha nyumba, yaani ndiye kiongozi, sasa kwa kuwa kiongozi si alipaswa kumuongoza Hawa au Eva. Sasa ilikuwaje akapewa tunda ambalo waliambiwa wasile yeye akajitwalia na kula bila kukataa na kumkataza Eva au Hawa akiwa kama kiongozi wake?
 
Back
Top Bottom