Mwanaharakati wa Gesi Mtwara afariki Dunia!

Mwanaharakati wa Gesi Mtwara afariki Dunia!

MMAHE

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2012
Posts
815
Reaction score
420
Mwanaharakati mmoja anayefahamika kwa jina la Mohamed Namtande anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 35, mkaazi wa kijiji cha Mihambwe kilichopo halmashauri ya Tandahimba mkoani Mtwara, amefariki dunia katika hospitali ya Ligula mkoani Mtwara.

Akizungumza na Pride fm Katibu wa Chama cha Wananchi CUF wilaya ya Mtwara, Said Issa Kulaga amesema kuwa, Mohamed Namtande maarufu kama Awilo amefariki leo majira ya saa 11 alfajiri katika hospitali ya Ligula baada ya kuwa hapo kwa takriban siku 3 kufuatia kujeruhiwa katika ajali ya gari akiwa katika harakati za kupinga gesi kusafirishwa kuelekea jijini Dar es Salaam.

Kulaga amesema kuwa, anatoa taarifa kwa wananchi wa mkoa wa Mtwara, Lindi na Tanzania kwa ujumla kufuatia kifo hicho cha Awilo ambaye alikuwa mstari wa mbele katika kupinga gesi asilia kupelekwa jijini Dar es Salaam.

Mwili wa marehemu Mohamed Namtande unatarajiwa kuhifadhiwa katika makazi ya milele, hapo kesho majira ya saa nne asubuhi katika kijiji cha Mihambwe.

Kuhusu utaratibu wa kuhudhuria mazishi hayo, mwananchi mmoja amejitolewa usafiri huku mtu anayetaka kushiriki katika mazishi hayo anatakiwa kuchangia mafuta shilingi 3,000 huku mchango huo ukiwasilishwa katika ofisi za CUF, kituo kikuu cha mabasi dukani kwa Ndinda na soko kuu kwa Namdimba na waweza kutuma mchango kupitia 0653 183 169. Safari kuelekea mazishini itaanzia kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani majira ya saa 10 alfajiri na magomeni.

Inna lillah wa Inna Illah Rajiun!
 
Ule mkakati wa CCM ndo umeanza mapema hivi? Kuna mtu alileta uzi hapa wa kuua ili kutisha watu
 
Mazingira ya ajali yalikuwaje? Ajali inaweza kutengenezwa
 
RIP Mwanaharakati wa Mtwara, kumuenzi huyu jamaa inabidi mapambano ya kudai mgawanyo wa haki wa rasilimali na kuzuia mafisadi wasiibe dola milioni 532 za maradi wa bomba la gesi, yaongezwe kasi.

Weka namba ya Mpesa hapo...
 
RIP Mwanaharakati wa Mtwara, kumuenzi huyu jamaa inabidi mapambano ya kudai mgawanyo wa haki wa rasilimali na kuzuia mafisadi wasiibe dola milioni 532 za maradi wa bomba la gesi, yaongezwe kasi.

Weka namba ya Mpesa hapo...


Hakika damu yake haiwezi kupotea bure.
 
kazi kwa familia nilisema haya mambo mtu awe makin na aangalie maisha yake .ges ges
 
mwanaharakati mmoja anayefahamika kwa jina la mohamed namtande anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 35, mkaazi wa kijiji cha mihambwe kilichopo halmashauri ya tandahimba mkoani mtwara, amefariki dunia katika hospitali ya ligula mkoani mtwara.

Akizungumza na pride fm katibu wa chama cha wananchi cuf wilaya ya mtwara, said issa kulaga amesema kuwa, mohamed namtande maarufu kama awilo amefariki leo majira ya saa 11 alfajiri katika hospitali ya ligula baada ya kuwa hapo kwa takriban siku 3 kufuatia kujeruhiwa katika ajali ya gari akiwa katika harakati za kupinga gesi kusafirishwa kuelekea jijini dar es salaam.

Kulaga amesema kuwa, anatoa taarifa kwa wananchi wa mkoa wa mtwara, lindi na tanzania kwa ujumla kufuatia kifo hicho cha awilo ambaye alikuwa mstari wa mbele katika kupinga gesi asilia kupelekwa jijini dar es salaam.

Mwili wa marehemu mohamed namtande unatarajiwa kuhifadhiwa katika makazi ya milele, hapo kesho majira ya saa nne asubuhi katika kijiji cha mihambwe.

Kuhusu utaratibu wa kuhudhuria mazishi hayo, mwananchi mmoja amejitolewa usafiri huku mtu anayetaka kushiriki katika mazishi hayo anatakiwa kuchangia mafuta shilingi 3,000 huku mchango huo ukiwasilishwa katika ofisi za cuf, kituo kikuu cha mabasi dukani kwa ndinda na soko kuu kwa namdimba na waweza kutuma mchango kupitia 0653 183 169. Safari kuelekea mazishini itaanzia kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani majira ya saa 10 alfajiri na magomeni.

Inna lillah wa inna illah rajiun!
poleni sana wafiwa...........mie sijaelewa.kuna uhusiano wowote kati ya kifo na harakati za kupinga gesi kwenda dsm?
 
poleni sana wafiwa...........mie sijaelewa.kuna uhusiano wowote kati ya kifo na harakati za kupinga gesi kwenda dsm?

Marehem alipata ajali akielekea kwenye mkutano wa kupinga Gesi ghafi isisafirishwe kwenda dsm, alitoka kijiji cha Mihambwe wilayani Tandahimba kuja kwenye mkutano Mtwara mjini ambako bahati mbaya gari yao ikapata ajali,alilazwa Hospitali ya Mkoa Ligula kwa matibabu hadi leo alfajiri Allah alipomchukua.
 
kazi kwa familia nilisema haya mambo mtu awe makin na aangalie maisha yake .ges ges

Utakuwaje na maisha ikiwa upo katika hali hii hapa chini:-

Skeleton.jpg

Pambana tu usiogope kufa, hata katika vita ya maji maji wazee wetu walikubali kufa ili kupinga unyanyasaji wa mkoloni.

Sasa leo tumepata uhuru bado tunanyanyasana wenyewe.

RIP MAREHEMU AWILO



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
marehem alipata ajali akielekea kwenye mkutano wa kupinga gesi ghafi isisafirishwe kwenda dsm, alitoka kijiji cha mihambwe wilayani tandahimba kuja kwenye mkutano mtwara mjini ambako bahati mbaya gari yao ikapata ajali,alilazwa hospitali ya mkoa ligula kwa matibabu hadi leo alfajiri allah alipomchukua.
asante,sasa nimekuelewa.
 
Mwili wa marehemu MUNGU ailaze shambani mwa Bwana wetu milele, Aaaamen!
 
Mbona wanaochangisha ni wanaCUF kwa hiyo kupinga kusafirisha gesi Dar imekaa kichama ama imekaa kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa kusini kujikomboa katika ufukara kwa kuanzaisha miradi mabli mbali mikoani mwao
 
Back
Top Bottom