Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Leo gazeti la MwanaHalisi limeanika madudu yaliyofanywa na Tume ya Uchaguzi (NEC) katika daftari la wapiga kura wakati wa uchaguzi mdogo wa Igunga.
Sehemu husika (relevant paragraphs) za habari hiyo ni kama ifuatavyo:
Tume ya uchaguzi (NEC) yaweza kutiwa kitanzini iwapo itathibitika kuwa ilichakachua daftari la wapiga kura katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimboni Igunga, MwanaHalisi limeelezwa.
Taarifa kutoka ndani ya serikali, NEC na mashirika huru ya uangalizi wa uchaguzi nchini, zinaonyesha kwamba idadi ya wapigakura waliomo katika daftari la mwaka 2010 na wale waliotajwa katika uchaguzi mdogo wa Igunga inapishana, tena kwa mbali .
..Kuna taarifa za kuondoa majina ya wapiga kura, kuongeza majina yaw engine na kuonekana, angalau kwa namba moja ya shahada isiyokuwa na jina mbele
..MwanaHalisi limetarifiwa kuwa kazi ya kuingiza wapigakura hewa na kuondoa baadhi ya majina imefanyika kwa ustadi mkubwa, kwa kuhusisha NEC na wataalam wenye ujuzi katika mawasiliano ya kompyuta (IT).
Taarifa zinaonyesha kwenye Kata ya Mbutu peke yake, wapigakura zaidi ya 2500 waliongezwa kwenye daftari hilo kwenye uchaguzi mdogo wa Igunga. Jimbo hilo lina jumla ya kata 26.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa MwanaHalisi, daftari la wapiga kura lilitumika kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka jana (2010) linaonyesha wapigakura waliopo kwenye kituo cha Shule ya Msingi Mwakabima C, kata ya Mbutu, ni 382, lakini daftari lililotolewa na NEC kwa vyama vyote vya siasa katika uchaguzi mdogo wa Igunga, limetaja wapigakura 393 kwa kituo hicho.
Daftari hilo la wapiga kura 382 lilitolewa na NEC 18 Oktoba 2010.
Kwenye kituo hiki peke yake, daftari linaonyesha ongezeko la wapigakura 11, wakati ambapo NEC haikuwahi kufanya marekebisho yeyote kwenye daftari la wapigakura kati ya 23 Septemba 2010 na 10 2010, wala wakati wa kuelekea uchaguzi mdogo wa Igunga.
NEC inasema katika maelezo yake yaliyo mbele ya daftari hilo, Daftari hili litatumika kuanzia 15 Oktoba 2010 hadi itakapotangazwa vinginevyo na Tume ya Uchaguzi.
Kati ya wakati huo na sasa NEC haijatangaza kusitishwa kwa matumizi ya daftari hilo.
Aidha kwenye kituo cha Mwambakima Shule ya Msingi 3 chenye Na. 00015059, idadi ya wapigakura imeongezeka kutoka 393 waliotajwa na NEC 18 Oktoba 2010 hadi wapigakura 419 waliotajwa kwenye uchaguzi mdogo wiki iliyopita .
Habari zaidi katika MwanaHalisi la leo.
My take:
Jee NEC wataeleza nini hapa? NEC ni taasisi inayotaka kuleta machafuko hapa nchini, maana haikujifunza kutoka kwa ile Tume ya Kenya mwaka 2007.
Ewe Mwenyezi Mungu tunusuru tunakokwenda.
Sehemu husika (relevant paragraphs) za habari hiyo ni kama ifuatavyo:
Tume ya uchaguzi (NEC) yaweza kutiwa kitanzini iwapo itathibitika kuwa ilichakachua daftari la wapiga kura katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimboni Igunga, MwanaHalisi limeelezwa.
Taarifa kutoka ndani ya serikali, NEC na mashirika huru ya uangalizi wa uchaguzi nchini, zinaonyesha kwamba idadi ya wapigakura waliomo katika daftari la mwaka 2010 na wale waliotajwa katika uchaguzi mdogo wa Igunga inapishana, tena kwa mbali .
..Kuna taarifa za kuondoa majina ya wapiga kura, kuongeza majina yaw engine na kuonekana, angalau kwa namba moja ya shahada isiyokuwa na jina mbele
..MwanaHalisi limetarifiwa kuwa kazi ya kuingiza wapigakura hewa na kuondoa baadhi ya majina imefanyika kwa ustadi mkubwa, kwa kuhusisha NEC na wataalam wenye ujuzi katika mawasiliano ya kompyuta (IT).
Taarifa zinaonyesha kwenye Kata ya Mbutu peke yake, wapigakura zaidi ya 2500 waliongezwa kwenye daftari hilo kwenye uchaguzi mdogo wa Igunga. Jimbo hilo lina jumla ya kata 26.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa MwanaHalisi, daftari la wapiga kura lilitumika kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka jana (2010) linaonyesha wapigakura waliopo kwenye kituo cha Shule ya Msingi Mwakabima C, kata ya Mbutu, ni 382, lakini daftari lililotolewa na NEC kwa vyama vyote vya siasa katika uchaguzi mdogo wa Igunga, limetaja wapigakura 393 kwa kituo hicho.
Daftari hilo la wapiga kura 382 lilitolewa na NEC 18 Oktoba 2010.
Kwenye kituo hiki peke yake, daftari linaonyesha ongezeko la wapigakura 11, wakati ambapo NEC haikuwahi kufanya marekebisho yeyote kwenye daftari la wapigakura kati ya 23 Septemba 2010 na 10 2010, wala wakati wa kuelekea uchaguzi mdogo wa Igunga.
NEC inasema katika maelezo yake yaliyo mbele ya daftari hilo, Daftari hili litatumika kuanzia 15 Oktoba 2010 hadi itakapotangazwa vinginevyo na Tume ya Uchaguzi.
Kati ya wakati huo na sasa NEC haijatangaza kusitishwa kwa matumizi ya daftari hilo.
Aidha kwenye kituo cha Mwambakima Shule ya Msingi 3 chenye Na. 00015059, idadi ya wapigakura imeongezeka kutoka 393 waliotajwa na NEC 18 Oktoba 2010 hadi wapigakura 419 waliotajwa kwenye uchaguzi mdogo wiki iliyopita .
Habari zaidi katika MwanaHalisi la leo.
My take:
Jee NEC wataeleza nini hapa? NEC ni taasisi inayotaka kuleta machafuko hapa nchini, maana haikujifunza kutoka kwa ile Tume ya Kenya mwaka 2007.
Ewe Mwenyezi Mungu tunusuru tunakokwenda.