Mwana"mme" kwa mwana"mke" sawa, mwana"ume" kwa mwana"uke" sawa?

Mwana"mme" kwa mwana"mke" sawa, mwana"ume" kwa mwana"uke" sawa?

chameleon

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2013
Posts
555
Reaction score
170
Naomba kuuliza kama neno "mwanaume" ni la kiswahili na kwanini neno pacha "mwanauke" halitumiki sambamba nalo?
 
Ni muendelezo wa mfumo dume, lakini ni kuwasitiri mama na dada zetu maana neno mwanauke kidogo linaleta ukakasi.
 
Kama unatoa hayo maneno kwenye maneno "uke" na "ume" si sahihi maana kwa kiswahili hatuna neno "ume" lunalojitegemea ila tuna neno "uume" na neno "uke" linajitegemea likimaanisha sehemu za siri za kike hivyo hatuwezi kuwa na "mwanauke".
 
Kama unatoa hayo maneno kwenye maneno "uke" na "ume" si sahihi maana kwa kiswahili hatuna neno "ume" lunalojitegemea ila tuna neno "uume" na neno "uke" linajitegemea likimaanisha sehemu za siri za kike hivyo hatuwezi kuwa na "mwanauke".

Lakini hapo hajasema hv, anachotaka kujua n kwann huyu aitwe mwanaume na yule asiitwe mwanauke aitwe mwanamke?
 
Kama unatoa hayo maneno kwenye maneno "uke" na "ume" si sahihi maana kwa kiswahili hatuna neno "ume" lunalojitegemea ila tuna neno "uume" na neno "uke" linajitegemea likimaanisha sehemu za siri za kike hivyo hatuwezi kuwa na "mwanauke".

pia hatuna mwanauume
 
Mwanaume
Mwanamke
Mwanauume Na mwanauke ndio nalisikia kwako.
Nalog off
 
Lete wingi wake (plural) ya maneno hayo na udadavue kama ulivyodadavua umoja
 
"mwa" hutumiwa sana na watu wa Pwani ya Tanga na maeneo kadhaa ya mkoa huo ukichanganya na Zanzibar. Kiuhalisia kuna "mwanamume" na "Mwanamke"
 
Ni muendelezo wa mfumo dume, lakini ni kuwasitiri mama na dada zetu maana neno mwanauke kidogo linaleta ukakasi.

Katika lugha yoyote kila neno lina maana yake halisi kiletacho ukakasi ni matamshi kutokana na mahali au hadhira inayosikiliza.
 
Yote mawili yanatumika maeneo na mada tofauti tofauti ndio maana imeulizwa.

Ndio, yanatumika katika mada tofauti kama unavyo sema nisawa. Ukitaka
kuongelea jinsia kwamaana ya aina nilazima umtaje mwanamme kama nilivyo andika mimihapa yaani "mwanamme" ukianza kutaja maumbile ndio kunakuja hiyo "ume" yani kama ulivyo andika wewe mwanaume which's not correct kwa kutaja jinsia ya mtu, kama ulivyo uliza kuhusu mwanauke,ukishataja hilo neno uke manayake unazungumzia maumbile nasio jinsia "aina". Ukitaja jinsia inabidi useme mwanamke.

Kwahiyo usiwaze kwamba eti kwanini neno mwanamke lisitamkwe "mwanauke" it's impossible.

Otherwise rudi kwenye post ya Ilu amekuelewesha vizuri sana.
 
Back
Top Bottom