Mwana FA hajui mnyororo wa thamani katika sherehe za harusi, aelimishwe...

Kuna mambo mengine kwenye jamii hayaepukiki moja wapo ni hili la kuchangia mambo ya kijamii.
 
Nitoe pesa ya mchango,
Nitoe pesa ya nguo sijui sare,
Nitoe pesa ya zawadi,
Bado sijafanya make up,
Hehehehe

Tena usiombee waoane wakiwa washatiana mimba, hujakaa sawa kidogo mtoto kazaliwa upeleke zawadi bado arobaini ya mtoto ukinusurika kuchangishwa basi zawadi lazima, looooh!
Bora hiyo harusi ifanyikie hapo inafanyikia mbaaaliiiiii nauli ya kwenda kurudi malazi, unanunua ng'ombe
 
Kuna mambo mengine kwenye jamii hayaepukiki moja wapo ni hili la kuchangia mambo ya kijamii.
Sio harusi, showers, birthday maana siku hizi hadi vipaimara tunaletewa kadi..hii jamii imekujankuwaje ... Yaaani mtoto aende mafundisho miezi 6-8 usijipange uje uchangishe watu !!??
 
Kuhusu kuhusisha mchango na ajira naona umepotoka...Mwana fa alisisitiza ishu ya maandalizi kwa mlengwa mwenyewe. Hilo haliondoi watu kupata ajira kama unavyotaka.Mf. Kama harusi yako ni milioni kumi,muoaji jichange mwenyewe upate milioni kumi (ajira ulitotaja zitapatikana)...Hata watu wakikuchangia itakuwa milioni kumi (ajira ulizotaja zitapatikana) huo ndio nadhani mtazamo sahihi. Labda kama unataka harusi ya mil.10 wewe unayo laki mbili….unataka michango ndio ijazie hapo kweli tutafeli; na ndio wengi wanataka hiyo kitonga Mtizamo
 
Kwa point zako bado Hamisi yupo sahihi...kuna njia nyingi za kudumbukiza hela zako kwenye mzunguko...kafanye hata shopping kwa machingaz
 
Najua Hamisi Mwinyijuma au Mwana FA ni miongoni mwa wasanii wachache wasomi tulionao hapa Tanzania.

Ukiwa msomi, tunatarajia uwe na fikra pana na za kina kwenye masuala mbalimbali ya kijamii na mazingira yanayokuzunguka, ukiachana na yale ya fani uliyosomea.

NATAKA KUSEMA NINI?

Nimeona video fupi ikisambaa inayomuonesha MwanaFA akizungumzia suala la michango ya harusi. Kwamba, yeye hachangii harusi kwani ni suala la mtu binafsi na linahitaji maandalizi. Yuko tayari kuchangia Msiba, si harusi.

Kwanza, huo ni mtazamo unaofikirisha lakini pia ni mtazamo wa watu wengi. Watu wamechoka na utaratibu wa kuchangia harusi. Mimi ni mmojawapo

Hata hivyo, nikiangalia mnyororo wa thamani uliopo kwenye hizi sherehe na ajira zilizozalishwa, nabaki kuona ni jambo zuri na lenye tija.

Ukichangia harusi, unatoa ajira kwa watu wengi sana. Kuanzia MC, watu wa mapambo, chakula, wapiga picha, maids, watoa burudani n.k.

Faida nyingine ni mzunguko wa fedha kuchochea uchumi wa eneo husika, kuimarisha undugu na ujamaa, kutengeneza kumbukumbu na mengine mengi.

Wapo wasiochangisha watu kwenye mambo ya sherehe, lakini hao ni wale wanaojiweza, vipi wale wasiojiweza?

USHAURI WANGU

Tusiache kuchangiana kama tunapendana na kushirikiana. Umoja ni nguvu. Sherehe za harusi sio suala binafsi tena, ni suala la kiuchumi na maisha ya watu wengi yanategemea hapo.

Mwezi wa 6 mwakani nafunga ndoa. Nitatoa kadi za michango. Mnichangie. Puuzeni maneno laini laini ya Hamisi.
Nakubaliana na MwanaFA, ajira sio lazima utegemee michango yetu. Hebu tupumzisheni, hapa Nina kadi za ndoa sita harusi kabla ya xmas ambazo naona moja ndio labda watavuka miaka mitano.

Hebu niacheni sichangi hata moja BTW yangu nikibahatika kaurithi na pesa yangu flani nikapiga bila kuchangisha 13 years ago sitaki usumbufu kwa sasa kila mtu apambane na mkewe.

Imagine juzi natumiwa msg sasa Hadi kipaimara watu eti wanachangisha huu upuuzi zamani haikuwepo, mzee alikuwa anajipanga anapigansherehe mwenyewe anaalika watu wake kadhaa mnapiga kipaimara Mambo kwisha.

Huu utaratibu wa michango uwepo kwa vijana wenye projects zilizosimama na wakiwa wanataka funds zaidi au kusoma (elimu) , hospital (maradhi) Ila starehe yenu chumbani siwezi kuichangia No thank you.
 
Nitachangia msiba na maradhi tu kwa sababu sio utashi binafsi wa mhusika.Vinatokea tu havipangwi.
Arusi upange mwenyewe halafu gharama nichangie?Ni ujinga ambao sitafanya hata siku moja.Sijachangiwa wala sichangii.
 
Back
Top Bottom