Mwana FA ft. G Nako - Mfalme [lyrics]

SHOOyaKIBABE

JF-Expert Member
Feb 10, 2014
2,181
1,707
Mwana FA ft G Nako - Mfalme lyrics
[Mwana FA]
Look around brother
Choir Master!
Ghetto Gospel (Yes!)
Keeping the good music alive!

[G Nako]
Kanipa maarifa loloo (nampa sifa)
Yakanipa nyadhifa loloo (nampa sifa)
Kaziba nyufa loloo (nampa sifa)
Olooh! (Mfalmee!)

Kanipa maarifa yakanipa nyadhifa
Ikajipa sifa, kaziba nyufa
Namwiita ye Mfalmeee
Mfaaalmeee

[Mwana FA]
Holla at ya boy!

Sinung'uniki sina viatu wenzangu hawana miguu
Hawalalamiki wanamshukuru Aliyejuu
Siwezi nikamletea makuu maombi ya kibraza du
Mbwembwe za kuomba magari nawaachia son I'm cool
Kama kipande cha kwanza cha mbao kwenye safina
Mimi ni kitu cha Mungu nafanya alichonituma
Kanipa ubongo na misuli na roho ya kitajili
Sina kitu ila sina roho mbaya tunaishi vizuri
Fukara nayeshukuru au tajiri nisiyekufuru
Najua bata najua hustle mi ni njiwa na kunguru
Kuna vingi vya kumuomba Mungu kabla hujamuomba utajiri
Naishi kwa mapenzi yake hakuna kitu naona hatari
Unapata ulichoandikiwa Mungu hakupi kama hataki
Hata ukipora itapotea ili mradi yatimie maandishi
Mi ndo vito wa kolioni vitu vinaisha my way
Nife nikiwa muumini na everything gon' be I man

[G Nako]
Kanipa maarifa loloo (nampa sifa)
Yakanipa nyadhifa loloo (nampa sifa)
Kaziba nyufa loloo (nampa sifa)
Olooh! (Mfalmee!)

Kanipa maarifa yakanipa nyadhifa
Ikajipa sifa, kaziba nyufa
Namwiita ye Mfalmeee
Mfalmeee

Kanipa maarifa yakanipa nyadhifa
Ikajipa sifa, kaziba nyufa
Namwiita ye Mfalmeee
Mfalmeee

[Mwana FA]
Najua anamipango, anafungua milango
Ndo anatoa michongo, namwita Mfalme Wa Jungle
Boss wa dunia yangu kanipa nguvu na ubongo
Mwenye maamuzi ya mwisho angetaka angeniumba fungo
Mafala wana midomo ka vicheche usiwe kati yao
Wanaosema wenzao rudi angalia maisha yao
Wengine hawana hata kalaki wanaita wenzao maskini
Haki nawaombea mabaya kama wanavyoniombea mimi
Ni hata mtoa wa roho ni malaika, na nahisi ataenda peponi
Achia kuhukumu sio kazi yako, we ni mwenzangu na mimi
Na una dhambi kama mimi, na hatujui kubwa za nani
Labda zako labda zangu, sio kazi yetu ni ya Maanani
Usiniwaze sana mi nawaza maisha yangu
Sina hata mia ya urithi vyote hivi ni vya kwangu
Nshaenda shule bila viatu, nshatoa funza kama buku
Na ipo siku utaniheshimu ama utaheshimu hela zangu

[G Nako]
Kanipa maarifa loloo (nampa sifa)
Yakanipa nyadhifa loloo (nampa sifa)
Kaziba nyufa loloo (nampa sifa)
Olooh! (Mfalmee!)

Kanipa maarifa yakanipa nyadhifa
Ikajipa sifa, kaziba nyufa
Namwiita ye Mfalmeee
Mfalmeee

Kanipa maarifa yakanipa nyadhifa
Ikajipa sifa, kaziba nyufa
Namwiita ye Mfalmeee
Mfalmeee

Kanipa maarifa loloo (nampa sifa)
Yakanipa nyadhifa loloo (nampa sifa)
Kaziba nyufa loloo (nampa sifa)
Olooh! (Mfalmee!)
 
Daaaa daaa kuna mistari mitamu sana me nimepanda hapo
"sinung'uniki sina viatu wenzangu hawana miguu,hawalalamiki wanamshukuru aliye juu"

Asante Mwana FA kwa zawadi nzuri sana kwangu mimi huu ni wimbo bora kutoka kwako tangu nimeanza kukufatilia.
 
Keeping good music alive....B..!hii ndio hip hop unasikiliza punch after punch alafu zote kali,nimemuelewa sana kwenye hii joint.
 
Naona Jide kajibiwa kisomi zaidi sana hizo zote falsafa ndio maana anaitwa mwanafalsafa.
Wale mashabiki wa Jide walosema MwanaFa hana hela majibu yenu ni wengi wetu hamna hata laki na mnamwita mwenzenu masikini. Pia Mwanafa anasema sina kitu ila sina roho mbaya tunaishi vizuri kisa show ndio kanuna hii yote roho mbaya jide big up Fa Mfalme watajifunza tu.
 
You real deserve yo name kweli umeimba kifalsafa zaidi waache wasiotumia akili kuropoka maisha ya watu wasiyoyajua.


Ila hivi FA hawezi kuimba wimbo bila kuweka neno kicheche kwenye punchline zake...
 
Naona Jide kajibiwa kisomi zaidi sana hizo zote falsafa ndio maana anaitwa mwanafalsafa.
Wale mashabiki wa Jide walosema MwanaFa hana hela majibu yenu ni wengi wetu hamna hata laki na mnamwita mwenzenu masikini. Pia Mwanafa anasema sina kitu ila sina roho mbaya tunaishi vizuri kisa show ndio kanuna hii yote roho mbaya jide big up Fa Mfalme watajifunza tu.

Na wewe unasapoti bifu la me na ke??? Haina faida kujenga bifu tena kwa mwanamke.Sidhani kama huu wimbo ni jibu kwa jide anyway aliyeimba chorus kaubeba huu wimbo
 
Nice song ila punch haziko nyingi sana sounds like aliandaa wimbo chap chap studio ukarekodiwa mara moja papo kwa papo
 
Nice song ila punch haziko nyingi sana sounds like aliandaa wimbo chap chap studio ukarekodiwa mara moja papo kwa papo

mkuu,huu wimbo umefutwafutwa sana mpaka kufika hapo....aliuanza Nahreal akaenda kuumalizia Marco Chali...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom