Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 5,174
- 17,635
Changamoto ya Wanafunzi wa Kijiji cha Misufini, Kata ya Magoroto, Wilayani Muheza, kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 7 kila siku huku wakipanda na kushuka vilima na misitu kufuata shule imekwisha sasa. Hii ni baada ya kukamilika kwa ujenzi wa madarasa ya shule ya msingi karibu na kijiji hicho.
Hatua hiyo imechochewa na juhudi za Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Muheza, Mhe. Hamis Mwinjuma baada ya kufika katika Kijiji hicho kwa mara ya kwanza ambapo alikumbana na hali ya kusikitisha ambayo ilimlazimu kuahidi kujenga shule hiyo hata kwa kutumia fedha za mfukoni mwake. Watoto wadogo walimfuata huku wakikabiliana na milima na misitu, wakisema, "Haya ndio maisha yetu ya kila siku.
Pia, Soma: Mwana FA azindua mradi wa Maji Kwatango wenye thamani ya TSh. Milioni 679
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Bi. Miranda Mpogolo, amekabidhi madarasa hayo kwa Mhe. Mwinjuma ambapo amesema benki hiyo inajivunia kuwa mdau wa maendeleo na inatekeleza sera yake ya uwekezaji katika jamii kwa kutoa asilimia moja ya faida yake kwa miradi ya kijamii.
Hatua hiyo imechochewa na juhudi za Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Muheza, Mhe. Hamis Mwinjuma baada ya kufika katika Kijiji hicho kwa mara ya kwanza ambapo alikumbana na hali ya kusikitisha ambayo ilimlazimu kuahidi kujenga shule hiyo hata kwa kutumia fedha za mfukoni mwake. Watoto wadogo walimfuata huku wakikabiliana na milima na misitu, wakisema, "Haya ndio maisha yetu ya kila siku.
Pia, Soma: Mwana FA azindua mradi wa Maji Kwatango wenye thamani ya TSh. Milioni 679
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Bi. Miranda Mpogolo, amekabidhi madarasa hayo kwa Mhe. Mwinjuma ambapo amesema benki hiyo inajivunia kuwa mdau wa maendeleo na inatekeleza sera yake ya uwekezaji katika jamii kwa kutoa asilimia moja ya faida yake kwa miradi ya kijamii.