Elections 2010 Mwamunyange jiuzuru!

Mvaa Tai

JF-Expert Member
Aug 11, 2009
6,159
4,442
Hivi najaribu kujiuliza Ki-protokali Matamshi ya Shimbo yana mhusisha vipi Mkuu wa Majeshi Mwamunyange?

1. Kama Shimbo anaagizwa afanye nini na Mkuu wa Majeshi, je Mwamunyange haoni kwamba umefika wakati wa yeye kujiuzuru?, Maana kawakosea sana wananchi maana ndo wenye jeshi(Jeshi la wananchi wa Tanzania), na siyo la Rdhiwani na baba yake.

2. Kama Shimbo aliagizwa na Jk/Chama atoe hilo tamko, pia Mwamunyange ajiuzuru, kama alivyotaka kufanya pindi swahiba mmoja wa JK (mwanajeshi) alipojitwalia eneo la jeshi na hata alipoagizwa na mkuu wake alirudishe alikataa, mpaka Mwamunyange alipotaka kujiuzuru na Jk kumuomba asifanye hivyo lile eneo likarudishwa.

Mwamunyange jiuzuru usisubiri uendelee kuchafuliwa na hawa wapuuzi, unaheshimika sana katika jamii hasa kwa misimamo yako, na mbaya zaidi baada ya wananchi kuonyesha kuchoka kuburuzwa na familia ya JK, Jk anajaribu kuangalia uwezekano wa kuubeba urais kwa influence ya jeshi.
 
Kiprotokali Mshimbo alitakiwa awajibishwe kijeshi maana ameact Ultravires. (out of powers) na hii ni insurbodination. Mpuuzi kama huyu anaweza kuamrisha kikosi bila bosi wake kujua na ndio maana tunamtaka yeye Shimbo ajuizulu haraka iwezekanvyo. BTW mtoa hoja ..ni kujizulu na sio kujiuzuruuuuu............
 
Nina imani Luis Moreno Ocampo ameshamuweka Shimbo kwenye list of ring leaders in case...................!
 
Jamani angalieni akili mbovu za Jk na CCM yao watamtumia Shimbo kuleta maafa ikiwa Chadema itakomboa nchi. Alivyokuwa anaongea huku anakenua kenua mijimeno nilihisi hatari maana nadhani huyu jamaa ni Idd Amin fulani hivi. Hivi huyu Shimbo shule kasoma kweli? Maana elimu pia inaweza mfanya mtu awe sensible.
 
Someni gazeti la mtanzania leo tarehe 6 Oktoba 2010 ukurasa wa 14 jeshi linasisistiza kwa kutoa tamko lenye kichwa cha habari " tamko la vyombo vya ulinzi na usalama kuhusu amani wakati wa kampeni na uchaguzi"

Aya ya pili wanasema "wajibu wa jeshi ni kwa wananchi na serikali iliyoko madarakani"


Kama ndio hivyo kura za CHADEMA zitapona kweli iwapo wajibu wao ni kwa serikali iliyopo madarakani????????
 
Jamani angalieni akili mbovu za Jk na CCM yao watamtumia Shimbo kuleta maafa ikiwa Chadema itakomboa nchi. Alivyokuwa anaongea huku anakenua kenua mijimeno nilihisi hatari maana nadhani huyu jamaa ni Idd Amin fulani hivi. Hivi huyu Shimbo shule kasoma kweli? Maana elimu pia inaweza mfanya mtu awe sensible.

Ndiyo maana napenda kabila au watu wa maeneo fulani kuongoza jeshi. Nonsense kama hizi huwezi kuziona. shimbo anaona jeshi ni sawa na bendi ya taarabu. hafai hata kuwa mkuu wa mgambo wa wilaya. amelidhalilisha jeshi na nchi kwa ujumla.anapaswa kujiuzulu.
 
"Ndiyo maana napenda kabila au watu wa maeneo fulani kuongoza jeshi. Nonsense kama hizi huwezi kuziona. shimbo anadhani jeshi na kama bendi ya taarabu."

Kweli bro, bora kina MURAAAAA!!!! washike jeshi......... They know the true meaning of military....Hata mkoloni wa kiingereza aliliona hilo....Pamoja na umahiri wao wa kijeshi, nchi haijawahi kuwa na military upset za ajabu ajabu (ukiondoa ile ya Nyerere ya 1964)
 
Leo nilipofungua Jf nimekutana na email inahoji kwa nini ninekuwa member wa muda mrefu lakini sichangii mada wala kuanzisha thread. Ni kwamba nilikuwa bize sana na shule ila nimeitimu sasa. Muda wote nilifika hapa jamvini na kusikiliza utamu wa JF ila baada ya kupata ujumbe wa wanaJf nilirudi nyumbani ili nkasome maana nilikuwa nasoma IFM uhasibu,jamani ifm wanasumbua si kawaida kuna mwalimu anaitwa Zawadi Ally/gift nitamleta kwenu wanajamii mukamshauri. Baada ya machache ayo, naungana na wanaJF kuyashangaa majeshi yetu yaliyoanza kufanya kazi ya Mahita kwa chaguzi ziliopita. Binafsi nashangaa kuona vitisho wakati ata watu hawana mawazo ya vurugu. Ukiona mtu ameanza kubashiri tatizo ujue hapo kuna tatizo. Hii ni sawa na kupanda ndege ukiwa mwl Nyerere airport dar ukaanza kung'aka kwa rubani ukimweleza kuwa ajali ikitokea atakoma. Inaleta maana ukitambua kuwa pale rubani akianza kufanya masihara ndo anaelezwa aache na sio wakati amekaa anafikiri jinsi ya kufika na kutua salama wewe unaanza kushika tai inauma sana. Binafsi najua wanamajeshi hawana chama lakini tukiona wanaendekeza kutumwa na wajanja haikubaliki. Mi napenda sana kama tarehe 31 mwezi huu tutamweka ikulu mtu asiye na ghilba,mwenye akili za kuchangua. Kwa ukweli wangu kura yangu ni ya Dr. nkisema dr. namaanisha dr. Slaa. Hii haimaanishi ushindi ni lazima ila natumia haki yangu. Siasa kweli ni siasa. Naomba kutoa maoni yangu.
 
Kweli madaraka matamu katika hali mbaya sasa CCM wanatumia jeshi kuwatisha wananchi!!!!
 
tangu tunyang'anywe jwtz{jeshi la wakurya tangu zamani} na huyu mkwere mambo yanaenda kisanii sanii tu :hand:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom