Mwamtafuta Mchungaji? Ni Mimi...

Rev Kishoka,
ulivyoweka Rubisi umenikumbusha mbali sana....kuna kisiwa flani hivi ziwa victoria kinaitwa Kome!! story ndefu, lakini huko ndio kuna mambo ya rubisi, genzemu na muramba kwa saaaaana......mambo ya Mzee Mhuyoba na Kapatiko!!!

lakini huchelewi kupata "taenia spp" kwa kunywa kinywaji hicho! so, polepole ndugu yangu na hivyo vinywaji vya kukamuliwa kwa miguu yenye "machacha."

Wewe inabidi uchukue darasa la jinsi ya kujielezea maana huwa hueleweki hata kidogo!!!!
 
...najua kwamba wewe na baadhi ya watu kama wewe hamuwezi kunielewa!!! ni jambo la kawaida na kimsingi ni nia yangu kukukoroga "ndonya" bwiko kama wewe!!....ndio maana kuna wengine kama wewe wanamwona JMushi1 chizi, kumbe wao ndio machizi!!!

Exactly, what is ndonya bwiko? kweli wewe umeshaanza kuwa mwehu
 
Hakuna kitu kiadilifu na makini kwa Binadamu kama Unyenyekevu. Ukiwa ni mnyenyekevu, utakuwa msikivu mzuri, utakuwa mwepesi kujisahihisha, utaongozwa na Busara, Hekima na Baraka nyingi na kamwe hautakaa kusongwa na roho ikiwa imejaa chuki, wivu na inda.

Wengi wa hao wenye shida kumjua Mchungaji, si watu wanyenyekevu. Ni watu wasio na Busara, ni Jeuri, Katili, Majivuno na wenye Tamaa mbaya kutaka kuwa ni wao pekee wanaostahii kuongezewa kibaba kwa kunyang'anya kile kidogo tulichonacho cha ushirika.

Narudia tena, sauti yangu yamwakilisha Mnyonge mnayetaka kumnyonga na kumdhulumu, iweje muwe na woga kwa mtu Mnyonge? Jee nyie si wale wa Miraba minne wenye nguvu na dola? Sasa kwa nini mnababaika? Au mnaanza kugundua kuwa umoja wa Wanyonge ni mkubwa na una nguvu kubwa?

Jee mwamtafuta Mchungaji ili sauti yake isiendelee kuinua roho za Wanyonge? mnata Mchungaji awape tukuzo na sifa ilhali hamstahili hata kutazamwa usoni?

Hamuoni soni kuwa mmevimbiwa na Tamaa, Dharau na Ubabe lakini ni Wababe Uchwara ambao hata kuzipiga kavukavu hamuwezi?

Kama mnajiamini, msipoteze muda kumtafuta Mchungaji. Mchungaji yupo jirani nanyi kila siku. Mwampita barabarani, sokoni, kazini na shambani.

Kilio cha Mnyonge kitazaa matunda bora kutokana na Rasilimali kubwa ya Mnyonge huyu kuwa ni Umoja.

Nawaasa, acheni kiburi, ngebe na majivuno. Jirudini mkaishi nasi vizuri, ndipo hapo mtajua Mchungaji ni nani.

Mlango wangu uko wazi, kama Mwokozi Kristo alivyosema, "njooni enyi wenye mizigo" nami nawaambia njooni mkae nasi sisi Wanyonge, tutawasaidia kuitua hiyo mizigo na tutakaa pamoja mkekani kupata riziki.
 
Mchungaji
huu ujumbe wako ni mzito na umenifanya niurudie twice.
Wakisoma wahusika nina imani mioyo yao migumu italainika kiasi fulani
 
Tumeambiwa, Rais wetu ni mtu mwenye HADHI, hivyo nyumba yake, gari lake, ndege yake na mavazi yake lazima yawe na hadhi ya Kiraisi.

Najiuliza HADHI ya Uongozi ni vitendea kazi au ni mtu mwenyewe ndiye atakaye leta sifa na kuheshimika kwa nafasi hiyo ya Uraisi?

Mnaonitafuta, mwakasirika nikimzungumzia mwajiri wenu, ukweli ni kuwa hana HADHI kuwa Kiongozi Mkuu wa Taifa. Hajafanya kazi yeyote kwa Madaraka yake ambayo yataonyesha kuwa ana HADHI ya kuwa Kiongozi wa Taifa, mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu, kutoa hamasa kwa wananchi, kuamsha na kuweka dira mpya ya maendeleo ili lile Gurudumu la Maendeleo lifikie Tambarare.

Udhaifu wa Rais na Serikali yake, unashusha HADHI ya Taifa letu. Mnakasirika bure kwa Mchungaji na Kondoo wanapolalamika na kubeza kuwa Mfalme yupo Uchi.

Nyinyi mwadhani kuwa Rais na Serikali ni yenu na mali zote na kilichomo ni chenu pekee. Nyinyi si Wateule wa Taifa, ambao ndio wenye haki pekee kula na kunywa tukivunacho.

Rais na Serikali ni mali yetu sote, na hata wale 20% waliompinga Raisi na Serikali kwenye kibanda cha Kura 2005, wana hati miliki na ni halali yao kuhoji mwelekeo wa Taifa na HADHI ya Taifa, Raisi na Serikali.

Mnatembea mkiwa uchi, mkidhani mmevaa kikoi. Ondoeni Upofu wenu, Tamaa na Ujeuri, tambueni kuwa Mchungaji na wenzake wanatetea na wanataka kulinda HADHI ya Taifa.

Jiulizeni ni wapi mlipopotoka? je Umahiri wenu wote wa kufanya mambo na kujibeza kwa vyeti na misifa kibao vina faida gani ikiwa mnashindwa kazi zenu?

Nyie mlio wanaangalizaji ndio mnatia aibu kabisa na kuvunja HADHI za kazi zenu. Kila siku tunagundua uzembe fulani,hujuma fulani, uharamia fulani, mnakuwa wazito kufanya kazi zenu lakini mna nguvu na nyenzo kumtafuta Mchungaji ni nani?

Kalagabaho, endeleeni kunitafuta, mimi najitahidi kusafisha uchafu mnaoupuuzia na msiouona, labda siku mkinipata, macho na masikio yenu yatafunguka na kujua Mchungaji na wenzake, si adui zenu, bali ni wale wanaotaka HADHI ya Taifa irudi.

Angalieni nyote nyie msijekuwa mwafanyia kazi mafisadi na kufanya Maneno ya Mzee Mwinyi kutimilika, "kichwa cha Mwendawazimu"!
 
.... tambueni kuwa Mchungaji na wenzake wanatetea na wanataka kulinda HADHI ya Taifa..

Wa_Tafuta Mchungaji.

Get to read that several time and let it sink down your Heart and Mind. Get it very clearly. when you are about to sleep let it come again and again to your mind...You will dream about it..and you will work for us! I am not jocking...I Have already programed you ..and you have no way out!

And Let your conclusition lead you to do some usefull Job.
 
YournameisMine,
Wewe umeyafahamu vipi haya ya kisiwa cha KOME!....
kumbe mpo wengi humu mnajifichaficha nyuma ya miti.. Kuna kina Masatu wengi tu haya mkuu tutakuja kutana InshaAllah!
 
najiuliza Hadhi Ya Uongozi Ni Vitendea Kazi Au Ni Mtu Mwenyewe Ndiye Atakaye Leta Sifa Na Kuheshimika Kwa Nafasi Hiyo Ya Uraisi?
..
..
..
Udhaifu Wa Rais Na Serikali Yake, Unashusha Hadhi Ya Taifa Letu. Mnakasirika Bure Kwa Mchungaji Na Kondoo Wanapolalamika Na Kubeza Kuwa mfalme Yupo Uchi.
..
..
..

Mnatembea Mkiwa Uchi, Mkidhani Mmevaa Kikoi. Ondoeni Upofu Wenu.

..
..
..
je Umahiri Wenu Wote Wa Kufanya Mambo Na Kujibeza Kwa Vyeti Na Misifa Kibao Vina Faida Gani Ikiwa Mnashindwa Kazi Zenu?
!
Sina Cha Kuongeza!!!
Hakika Tuko Pamoja Katika Hili La Kusikitisha.
amen
 
Rev Kishoka,
ulivyoweka Rubisi umenikumbusha mbali sana....kuna kisiwa flani hivi ziwa victoria kinaitwa Kome!! story ndefu, lakini huko ndio kuna mambo ya rubisi, genzemu na muramba kwa saaaaana......mambo ya Mzee Mhuyoba na Kapatiko!!!

lakini huchelewi kupata "taenia spp" kwa kunywa kinywaji hicho! so, polepole ndugu yangu na hivyo vinywaji vya kukamuliwa kwa miguu yenye "machacha."

YIM,

umenikumbusha mbali na mimi pia...Kome...Nyakasasa...Nyakaliro...genzemu...rubisi...kwi kwi kwi!!!
 
Mliounda genge la Uhujumu wenye Ufisadi, hamjatosheka na mlichokwisha kukikomba? Yaani hata ukoko mnautaka wakati mmesha maliza kila kitu na kutubakizia masizi?

Ni mpaka lini mnaitamani LISHE muendelee kunona na kuvimbiwa? J hamuogopi kuwa matumbo yatapasuka?

Nanyi mwamtafuta Mchungaji ili iwe nini? mnataka mtubu? mnatubu nini? kwa nini mumtafute Mchungaji pekee na si Mchungaji na Kondoo wote ambao wanaishi kwa dhiki na unyonge kutokana na ulafi wenu?

Mwamuogopea nini Mchungaji? Je Mchungaji na wafuasi wake ni tishio kwa "maslahi" yenu? ni "maslahi" gani hayo ambayo ni yenu binafsi lakini yamepewa hati miliki inayoitwa Taifa?

Nyinyi ni watu wabaya, hayawani. Mmeingilia nchi yetu kama kirusi cha ukimwi. Mmeingilia Serikali yetu na kugeuza Viongozi wetu kuwa wafuasi wa Ibada zenu chafu za Ulafi, Uhujumu na Dhuluma. Mmewafanya viongozi wetu wawe Vikaragosi, Wazembe, Wapenda Rushwa, wakosefu wa maadili yote haya mkiyafanya katika jina la Ushindani wa Kibiashara, Utandawazi na Ubepari.

Kwa nini mwatafuta njia fupi kujipatia riziki na kutulazimisha sisi Walalahoi tuvuje jasho la damu kuwatumikia?

Mshikamano wenu ambao una nguvu za Kihalifu umefanya hata ile imani yetu ya Chama kuwa na walakini. Kiapo chetu cha kusema Rushwa ni Adui Haki kimegeuka kuwa ni kituko katika Chama Chetu kilichotupatia Uhuru.

Virusi vyenu vimesababisha nchi kuendeshwa kiharamia na kuburuzwa kwa maslahi ya wachache ambao wengi wenu ni Washihiri na Viongozi wa Chama na Serikali.

Sasa Mchungaji akilonga kweli na kusema fitina kwake ni mwiko, mwakasirikia nini?

Kwa nini mnaendelea kufanya mambo kwa fitina na unafiki? Si mje nje ya boma na kutuamkia wazi kuwa Chama na Ushirika wenu ni kwa manufaa yenu na si kwetu kama Taifa?

Msinichukie kuwa Mjamaa, Ujamaa umenifundisha Utu pamoja na mapungufu yake. Je mlijifunza nini enzi za enzi?

Msisumbuke sana kumtafuta Mchungaji, atakuwa jimboni akiwasubiri mkijileta kujiuza na kutoa hongo zenu ili muendelee kupata siagi na jibini mkanenepa na kupata vitambi, huku sisi funza wakitambaa mwilini.

Nawaomba kama hamtaweza kujirekebisha na kujirudi, ondokeni mtuachie nchi yetu na umasikini wetu. Hizo kasumba zenu za kujenga mipango ya muda mfupi ya kuzuga macho tumeibaini. Hamnalo tena mtakalotuambia tutakaloamini.

Endeleeni kunitafuta, nami nitaendelea kuhubiri.

Hapendwi mtu ila Uzalendo tu!
 
Rev. Its all about time. Keep it up in that comradely sense, and the truth shall prevail. Whoever is looking for you should know that you are always with them everytime, everyday everywhre. What else do they want you for is thier hiden agenda
 
Kumekua na tabia ya wanasiasa kutishia maisha ya wanaharakati hasa pale mafisadi au madalali wao wanapoguswa iwe ni kwenye interests zao au hata pale wanapowekwa hadharani. Kuanza kumfuatafuata Rev Kishoka sio jambo geni kwani yeye amekua ni mwiba kwa mafisadi na madalali wao. Hivi wanamtafta ili iweje? Mbona yuko nao kila siku na kila mahali ingawa wao uwezo wao wa kumuona ni finyu. Basi Rev Kishoka yuko Manzese, Keko, Masaki kwenye mahotel ya kitali na kwenye madampo. Rev yuko kwenye magazeti , TV,redion na kwenye vikao vya bunge, yuko misikitini na mahekaluni, yukonao kila pembe ya nchi hii. WELL DONE REV KISHOKA KEEP IT UP. WAANDIKE MPAKA VIDOLE VIISHE. ukiwaogapa hao utakuwa umewafanyioa ufisadi wa TZ kuanyima dataz
 
Praise The Lord Rev.

Tunaamini Sauti Ya Mungu Inapitia Kwa Watu. Ndivyo Hata Manabii Walikuwa Wana Wakilisha Sauti Ya Mungu. Nalazimika Kusema Hata Sauti Yako Ni Mwito Wa Mungu Kwa Taifa Letu. Wanaokutafuta, Kama Ni Kwa Nia Mbaya Washindwe Kwa Jina La Yesu. Na Walaaniwe Mchana Kweupe Waumbuke.
 
Unanikumbusha kipindi kile wakati mayahudi 'wanamtafuta' Yesu, aliwauliza: 'Mwamtafuta nani?'
Wao wakamjibu: 'Yesu Mnazareti'
Yesu akasema: 'Ndiye mimi'

Kisha wakarudi nyuma, wakaanguka chini......


nadhani nafsi zao zinawasuta kwa kumtafuta mtu wanayemjua, na kumwona, 'akila na kunywa' nao

lakini unabii utatimia kwa sababu wale wote wanaisaliti nchi yetu, watajikuta wanakitamani kitanzi kama alivokitamani Yuda Iskariote baada ya 'kumsaliti' Yesu.

Ole wao ambao andiko hili litatimia juu yao!
 
Mnyonge akichoka, hana hofu ya kifo au balaa. Maana kaishi siku zote kwa unyonge na kwa kupoteza matumaini ya ahueni, mara nyingine Mnyonge hutamani Mola amchukue aachane na adha za dunia na hasa zile za kudhulumiwa.

Sauti ya mnyonge iliayo kutoka nyikani muiogope.

Ndugu yenu Mugabe anatumia Dola kujisimika, nanyi mwatumia nguvu za dola kuficha maovu yenu, ubatili wa Utawala na Dhambi zenu.

Sitaogopa kuwaambia ukweli kama Anna wa Killango alivyofanya! Sitajitafuna tafuna kama Anna Abdallah au Peter Serukamba ambao wamekosa Uzalendo na kukimbilia kutaka kufunika makosa, uzembe na uhujumu wa wazi kisa kuikilindia chama Heshima. NI aibu gani hii kulinda heshima ya Chama na si heshima ya nchi? ni kituko gani hiki? hivi mna akili sawasawa kutuambia na kuaibika kote kama Taifa tukae kimya kisa ni maslahi ya Chama?

Nitawapasha kweli muelewe nyinyi mnaonitafuta.

Mimi ni MwanaCCM, ni mfu na sijakimbia kukimbilia Upinzani. Kadi yangu iko sandukuni mkiitaka njooni muichukue. Mnanihitaji mchango wangu mimi na kondoo zangu kwa dhati kuliko mimi ninavyowahitaji ninyi.

Kama mlikuwa mnafikiri ni wakala wa wapinzani wenu Chadema, CUF, TLP au wenginewe, mmecheza pata potea. Ina maana mmejaa upofu kiasi hamuamini kuwa kuna wana CCM ambao wanaweza kuwa wakali kukiumbua Chama chao kwa Udhaifu wa Uongozi ambao unaozesha si Umaarufu wa Chama tu bali unalipaka Taifa matope na uozo.

Mimi nimeweka maslahi ya Taifa na Utaifa mbele. Kanisani tuliimba Msalaba Mbele, Dunia Nyuma, mimi nawapasha Tanzania Mbele, CCM nyuma!

Mimi ni Mjamaa, mwenye kuamini Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Ninalienzi Azimio la Arusha pamoja na mapungufu yake. Naamini Taifa likiweka nguvu kuushinda Umasikini, Ujinga na Maradhi, safari ya kusukuma gurudumu la maendeleo itafika kwenye ardhi tambarare na mwendo kasi wa safari utakuwa ni kasi ya juu na Watanzania tutaona maendeleo na kufurahia kazi zetu.

Naamini tukiondoa ujinga, tutaongeza juhudi na maarifa, hivyo uzalishaji mali utaongezeka, tija na motisha vitakuwa machoni mwa kila Mtanzania na Umasikini utatutoka taratibu.

Lakini haya hayawezi kufanikiwa kama bado afya zetu zitakuwa na wasiwasi. Si Tiba pekee, bali hata Kinga vinahitajika ili Mtanzania awe mkakamavu na mchapa kazi hodari. Afya haiishi kwenye kwenda zahanati pekee, pia mipango bora ya lishe na kuhakikisha kuwa kila Mtanzania ana pata maji safi, ana chakula na mahali pa kulala kutokana na uwezo wake.

Inashangaza kusikia kuwa miaka 47 tangu tupate uhuru na zile jitihada za UPE na kisomo cha Watu wazima, kuwa 31% ya Watanzania watu wazima (umri kati ya miaka 18-75) hawajui kusoma wala kuandika.

Inasikitisha kusikia kuwa 52% ya wananchi wa Tanzania wanaishi katika dhiki ya hali ya juu na hawana uhakika wa kuiona kesho au ukihimili kesho kutokana na umasikini.

Wakulaumiwa si Mtanzania bali ni nyie mnaojiita Viongozi wa Serikali, mlio na tamaa ya madaraka, wenye kuhangaika kutafuta kuwanayamazisha wanaowapa vidonge vya ukweli kuhusu mapungufu yenu ya kitaaluma, kitendaji na hata tamaa za mwili.

Anzieni kwenye Serikali yenu, Chama chenu na hata jamii zenu. Mnajiona nyinyi ndio bora na wenye hati miliki ya maliasili, rasilimali za Taifa na warithi na Viongozi wa Tanzania Milele. Mmekuwa makuwadi, vikaragosi na watumwa wa Mabepari Uchwara ambao nia yao si kulisaidia Taifa la Tanzania lijitegemee, bali ni kujitajirisha wao wenyewe na kutuacha sisi tukiwa hoi.

Madhambi mengine ni ya kwenu wenyewe na si ya Wageni, wawe Wazungu, Wahindi, Wachina, Waarabu au Waafrika wengine. Mnajaribu kupanda mbegu chafu za kudai Uzawa huku uzawa mnaolilia ni wa haki zenu na familia zenu.

Kama mwanaCCM, nitasema kweli daima, fitina kwangu ni mwiko. Karibu 75% ya nyinyi mnaojiita viongozi wa Taifa na CCM ni watu wabovu na hamfai. Ndio maana mnamtafuta Mchungaji ili asiendelee kuanika uozo wenu.

Mchungaji ameanza vita kumkomboa Mtanzania. Mkiwa kama mafisi waoga wenye kutegemea mkono uanguke mjipatie mlo, Mchungaji anawaasa, jirudini na muanze kulitumikia Taifa.

Msinitafute mimi au kondoo wangu na wafuasi wangu, tafuteni suluhisho kwa Matatizo ya Taifa ambayo yametokana na udhaifu wa Uongozi wenu zilizoandamana na tamaa za Ufisadi na Uhujumu.

Kama mlikosea kwa Uzembe kama binadamu, acheni viburi na jeuri, mkiri mlipokosea na msawazishe makosa na si kutoa ahadi tuu kila siku kutuhadaa Wananchi.
 
Kwa nini mnaendelea kuwa walaghai, wadanganyifu, wajeuri na wenye kiburi?

Hivi mnafikiri mnamdanganya nani? Labda mnajidanganya wenyewe kuamini kuwa mnachokifanya na kutamka, basi ni heri ili kutuziba midomo na kutupofusha.

Mlaaniwe kwa Uongo wenu. Mlaaniwe kwa Kiburi na Majivuno yenu. Laana hizi zikae hata na vizazi vyenu vinne, kama laana za Mungu alizoacha kwa vizazi vinne.

Nyinyi mnaendelea kutufanya na kutufikiria sisi ni mabwege? Ni lipi tulilowakosea mpaka mtudharau kiasi hicho?

Hasira zetu na gadhabu yetu, italipwa na Mungu.

Mnakasirika mnaposikia tukiwadai mtupe ukweli, mnatutafuta si kutushukuru, bali kututakia mabaya na maovu, eti tunawaharibia.

Ni nani kati yetu sisi na nyie waliomharibia mwenziwe?

Laiti mngelijua kuwa kama mngekuwa wanyenyekevu, wasikivu na wenye kujirudi, basi mngekuja mbele zetu na kukiri makosa yenu ya Uzembe na Tamaa, na sisi kama Taifa, Watanzania ambao tunasifika kwa Amani, Mshikamano na Utulivu, tungewasikiliza na kama kawaida ya Watanzania tungewasamehe mliyotukosea.

Lakini mnajikuza na kujitweza kuwa nyinyi ni Miungu, msio na makosa, na kila mlichofanya na mnachoendelea kukifanya ni sahihi na halali, zaidi ni halali yenu kuendelea kuwa wagereshaji, waongo, wazembe, wasaliti, wapenda makuu na msio na hata soni au haya mkaona aibu kwa mambo mliyoyafanya, mnayoyafanya na mnayotarajia kuyafanya.

Nashangaa sana, na tena sana kusikia mwaendelea kumtafuta Mchungaji.

Kosa lake ni lipi? mbona wale ambao ni wahalifu au waliotuhumiwa kuwa wahalifu bado "wanapeta" na kila siku mnatupiga "kiswahili" kuwa "jambo kubwa sana, ushahidi hautoshi"?

Mnatuambia kwa kujikanganya kuwa Hazina yetu pale Benki Kuu imekuwa ikichunwa tangu mwaka 1997 au mapema. Ni miaka kumi sasa bado hamjapata ushahidi wa kutosha kujua kilichotokea na waliohusika?

Mwatamka kuwa Meremeta ni mambo ya Usalama wa Nchi na Jeshi, hata Kagoda nayo mlitamka ni masuala ya Usalama wa Taifa.

Najiuliza, ni lini tulikuwa na hali ya hatari ambayo ilisababisha Jeshi na Usalama kujipatia pesa za uendeshaji kinyemela bila kuhusisha mamlaka husika kama Bunge?

Je anayehatarisha Usalama wa Taifa letu mpaka mkachotewa pesa hovyo bila viambatanishi vya ushahidi, na stakabadhi ni nani? Kama Usalama wa Taifa uko mashakani, mbona hamtuambii ili nasi tuanze kujifunga kibwebwe kujiandaa na hata kujitolea kulilinda Taifa letu kwa umakini zaidi?

Ni lini mlitangaza hali ya hatari?

Je nyie wote hamkuwapo dunia hii siku ile mwaka 1977 wakati Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (naona nywele zinawasiamama mkisikia hili jina) alipotutangazia Taifa la Tanzania na Dunia nzima rasmi kuwa tunaingia vitani, kwenda kupigana na Nduli Iddi Amini ili tukomboe nchi yetu?

Alisema "uwezo tunao, nia tunayo, sababu tunayo" mbona hakufanya siri kama nyinyi mnavyotuzuga kila mara kuwa kuna "Unyeti"?

Mkatuletea miradi hewa ya nishati, rada ya hongo, ndege ya raisi mchoko, mmeuza Shirika la Reli kwa Baniani mbaya, mmekodisha dege kubwa mbalo mnalilipia huku halina mabawa, kisa hadhi ya Taifa.

Ni hadhi gani hiyo na majigambo yenye manufaa gani ikiwa Wananchi bado wako uchi, wanakufa njaa na magonjwa ni kila siku?

Ni hadhi gani, tununuliwe Chandarua na Rais mgeni aliyekuja tutembelea? je tumekosa kabisa mipango na hata fungu kupigana na maradhi?

Siri ya mafanikio yenu tunaijua.

Ni Uroho wa kupindukia kutumia migongo yetu na kuendelea kutudhalilisha kwa kutufanya wote tuonekane omba omba, saidia masikini!

Mmeimarisha misingi ya Unyonge na Umasikini wa Mtanzania kwa kuendelea kuwa omba omba, kuwa na sheria mbovu, mikataba ya kianaharamu na wageni wakazi-wawekezaji, kukosa upeo wa kweli na dhamira ya kweli kutuleta maendeleo kwa kutumia dhamana na hatamu tulizowapa.

Hatuwezi kuendelea kumlaumu Mkoloni au Mwekezaji wakati mla nchi ni wewe, yeye na yule, nyinyi, akina nyie!

Ni nyinyi ambao mnadai mna mwamsho wa kutetea maslahi yetu, lakini ni matumbo, mapaja na matako yenu ambayo yanaendelea kunona mpaka mnashindwa kupumua, huku sisi tukikondeana na kupangusa nzi na mbu, tukifukuzana na mbwa kugombea makombo!

Hamna aibu miaka yote ya Uongozi na Uwakilishi kuwa Asilimia 31% ya Watanzania watu wazima hawajui kusoma na kuandika?

Hamuoni haya Mtanzania kwa wastani anaishi kwa chini ya dola moja ya kimarekani kwa siku?

Haliwasumbui kuwa Asilimia 52% ya Watanzania wanaishi katika Umasikini wa kutupa na hata hawana uhakika wa kesho, licha ya kujua watamalizaje leo na kushangaa waliwezaje jana?

Mmelitia Taifa letu aibu sana, mnatufadhaisha kwa ujasiri wenu kiburi na uchimvi.

Tunapowapigia kelele, au wengine wenu wanaoamka kutoka kwenye limbwata la Utamu na kuhoji kilichootokea, mnapenyeza maneno na kutumia makuwadi wenu kutunyamazisha na kudai eti ni masuala ya Kikundi chenu mkiwa upenuni mmejificha kujadili machungu ya uzazi wetu!

Ndimi zenu, zitawafunga, kama mnavyoendelea kujikanganya kila siku kwa hata kukosa umoja na kutoa kauli moja.

Nimewaasa, hasira zetu zimefika masikioni kwa aliyetupa hii ardhi na maliasili iliyomo.

Endeleeni kutupuuza na kutudanganya, mwisho wa mnayoyatenda hauko mbali sana, kama Usiku wa Kiza, mtashtukia siku moja mkiwa uchi wa mnyama kuwa kilio chetu kimesikika. Ni siku hiyo ambao macho, masikio na midomo yenu viyafunguka na kung'amua siku zote mmekuwa si waadilifu, ni waongo, waroho, wadhalimu wahujumu, wazembe na mafisadi.

Maonyo yetu na hata wema wetu hautakuwa na maana tena saa hiyo itakapowadia. Kaeni chonjo, saa mbaya inakuja, tubuni makosa yenu, tutawasamehe na kuwakaribisha tuanze kulijenga upya Taifa letu na kurutubisha sifa na hadhi ya kweli.

Yaliyowakuta Mobutu, Marcos, Pinochet, Bokassa, Amin, Noriega, Pol Pot, Ceausescu, Saddam, Marie Antoinette na wengine ambao walikuwa ni watawala kama nyinyi, yatawakuta, tena yanaweza kuwa mabaya mno, ombeni Mungu awachukue, kabla ya ghadhabu za Walalahoi, kuamka mithili ya vita vya Maji Maji, Mau Mau na kwingine kote kung'oa wakoloni.

Mnegro mmoja Gil Scott- Heron alisema " Revolution will not be Televised" hamjui siku, wala saa yatakapowafikia, mapinduzi kuondokana na uharamia wenu yanakuja, tunaanza kwa sala na maneno, mkitupuuza, tutafuatia Demokrasia.

Saa ya Ukombozi na Kuokoka ni Sasa, endeleeni kunitafuta, nipo nimejaa tele kama pishi la Mchele!
 
Nasikia nawakosesha usingizi, mwahangaika kutwa kucha na hata usiku mkiota jinamizi la Mchungaji!

Nawasikiliza kauli zenu mnavyojikanganya na kuongopeana.

Je hamkuisikia sauti yangu kwenye Redio Mestini ivi karibuni ikiwaasa muache kunyanyasa kondoo?
 
Asalaam Aleykum wadugu,

Nilikuwa likizo kidogo nikaenda kutalii nikakikimbia kijiwe. Katika kutafakari kwangu wakai wa likizo, ni mengi nimeyafikira, na nitaanza kwa utaratibu kurudi ukumbini na hoja mpya.

Shukran.
 
Back
Top Bottom