Mgoda simtwange
Senior Member
- Sep 7, 2012
- 168
- 64
Mke wangu ni mwalimu wa shule ya msingi ambaye kwa muda mrefu amekuwa na wazo la kuanzisha biashara ya stationary hapa mjini Iringa. Chumba cha kufanyia hiyo biashara amepata nje ya geti la chuo kikuu kimojawapo kilichopo hapa iringa mjini kwa sh 50,000 kwa mwezi. Computer na printer amenunua tayari. Anataka akope benk milion 5 ili anunue photocopy mashine ya milion 1, na zingine ziwe mtaji wa kuanzia. Biashara itahusisha kutoa photocopy, typing and printing, na kuuza vifaa vingine kama madaftari, vitabu vya shule ya msingi, pen, nk. Lakini pia anategemea kuajiri mfanyakazi (msichana au mvulana) wa kuuza hili duka la stationaries. Kwa upande wangu mimi nimekuwa na wasiwasi juu ya uendeshaji na faida ya hiyo biashara hasa ukizingatia stationaries eneo hilo na Iringa kwa ujumla ni nyingi sana na mtaji ni mkopo. Tafadhalini sana wataalamu na wazoefu wa biashara mbalimbali ikiwemo stationaries nawaombeni ushauri wenu kuhusiana na mradi huu. Je, ni biashara nzuri au haina maslahi? Je ni mambo gani ayazingatie ili apate maslahi?