Mwalimu v/s muuguzi

Twilumba

JF-Expert Member
Dec 5, 2010
11,542
12,404
WanaJf Habari za Mchana kutwa!

Nilihudhuria Sherehe za Mei Mosi, mahala furani kimsingi hapo ilikuwa ni maadhimisho ki-wilaya.
Walimu walikuwa wamepangwa kutumbuiza kwa Mashairi na Ngonjera ki ukweli niliona ubunifu wa walimu wale kwa jinsi walivyopangilia yale mashairi.

Lakini ghafla niliingiwa na huzuni baada ya Beti Mbili za Shairi lile kuweka bayana kuwa kuna gap kubwa sana kati ya walimu na watumishi wa idara ya afya wahudumu wa sekta ya afya na wauguzi.
Ilimiia majonzi jinsi walimu wale walivyoliweka lalamiko hili kiushairi ni kama walikuwa nalia na kujuta kwa nini wamekuwa walimu.

Mathalani wansema mwalimu aliyehitimu Ngazi ya Cheti analipwa Ngazi ya Mshahara TGTS B/1 -Sh 210,000 wakati Mhitimu wa Cheti cha Uhudumu wa Afya (Medical attendant) analipwa ngazi ya Mshahara TGHS B/1- shilingi 415,000 ikiwa na maana kuna tofauti ya shilingi 205,000/=!

Swali langu hapa ni kwa nini hawa wote mwalimu na mhudumu wa Afya wasilipwe kiwango sawa maana mwalimu na mhudumu wa Afya kwa kweli naona wote ugumu wa kazi unafanana!

Je serikali haijaona kama kuna ulazima wa kuondoa gap hili ambalo pengine linachangia kudumaza kiwango cha Elimu Nchini?

NAOMBA KUWASILISHA KWA MJADALA
!
 
Hapa duniani kuna kazi zinaitwa Rare Proffesion,zikiwemo zile za sector ya afya,jeshi,n.k. huwa wanalipwa tofauti na wafanyakazi wengine
 
Tofauti ni kubwa sana kwani medical attendant ni stage ya chini sana kwenye uwanja wa medicine(siwadharau),hivyo kwa maoni yangu wawavute waalimu juu hata wakilipwa sawa ikibidi hata mwalimu alipwe zaidi kwani kazi yao ni ngumu kuliko hata hao M.A
 
Just curious...hivi walimu wana zamu za usiku? wanaenda kazini week end? na siku za sikukuu/holidays je? Hivi walimu wanajiweka katika risk yeyote ya magonjwa kutokana na kazi yao? TB, HIV, bacterial/fungal nfections? Hivi walimu wanathirika kisaikolojia kutokana na kuona watu wakiwa katika hali mbali mbali...maiti, ajali, moto, madonda makubwa yanukayo, wagonjwa taabani, kufiwa mikononi na wagonjwa? Hivi walimu wanadeki matapishi, mavi, damu, usaha n.k za waginjwa mawodini?

Kweli kuna uhalali wa kuwapa mshahara sawa hawa watu wawili sababu tu wote wana level sawa ya certificate au diploma au degree?
 
Basi inatosha! Umemaliza yote
Just curious...hivi walimu wana zamu za usiku? wanaenda kazini week end? na siku za sikukuu/holidays je? Hivi walimu wanajiweka katika risk yeyote ya magonjwa kutokana na kazi yao? TB, HIV, bacterial/fungal nfections? Hivi walimu wanathirika kisaikolojia kutokana na kuona watu wakiwa katika hali mbali mbali...maiti, ajali, moto, madonda makubwa yanukayo, wagonjwa taabani, kufiwa mikononi na wagonjwa? Hivi walimu wanadeki matapishi, mavi, damu, usaha n.k za waginjwa mawodini?

Kweli kuna uhalali wa kuwapa mshahara sawa hawa watu wawili sababu tu wote wana level sawa ya certificate au diploma au degree?
 
lakini tukumbuke kuwa.... Maraisi, mawaziri, Madaktari, Medical attendants na hata ngazi yoyote ambayo mwanadamu anafanya akiwa na professional yoyote ni mwalimu ndie aliyemfundisha.. hebu tujifanye wajinga tuwatoe waalimu woooote duniani halafu tuone itakuwaje... Je tutatibiwa? , Bank kutakuwaje? mawaziri watatoka wapi?

jamani waalimu nao tuwape angalau thamani kubwa tuwathamini tu hatakama hawaingii w/end kazini.
 
Labda mkuu niseme,zamu za usiku haziko kwenye mshahara zinalipwa separate na zinaitwa night calls ,na si kweli holidays zote unaenda kazini labda uwe zamu na unalipwa separate(kiwango sitaji)na hawa watu hawaathiriki kisaikolojia kwani ni sehemu ya training hawatokei wanakotoka na kuanza kazi,mwisho kazi yao si kudeki mavi na damu waombe radhi....ni watu wa kawaida tu.
 
Kwahiyo ni serikari yetu tu haiwathamini waalimu kama wananafasi kubwa katika jamii.....Mimi nam-admire sana mwalimu wangu wa Mwanza sec. kweli alinipa kazi.
 
Back
Top Bottom