Kuna uvumi (binafsi naziita propaganda) kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum na Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M.Lissu 'amemtukana' Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 'Matusi' husika yanadaiwa kuporomoshwa na Tundu Lissu alipokuwa akiwasilisha Maoni ya Wachache katika Kamati Nambari Nne ya Bunge.
Inasemwa kuwa Tundu Lissu amemtukana na kumdhalilisha Baba wa Taifa. Propaganda hizi zinazosambaa haraka na kwa kishindo zimemkumba hadi Mzee Edwin Mtei ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA. Nikumbukacho ni kuwa Lissu alipokuwa akitetea na kufafanua Maoni ya Wachache,alitoa mifano minne akiwataja watu mbalimbali wakiwemo Mwalimu Nyerere,Profesa Issa Ghulamhussein Shivji na Dr.Harrison Mwakyembe.
Kwanza,tufahamishane hasa matusi yaliyoporomoshwa na Wakili Lissu dhidi ya Mwalimu Nyerere. Tukiyajua na kutambua kuwa ni matusi na dharau kweli,tuungane kumkemea Wakili Lissu na kumuonya asirudie tena. Karibuni tutaje matusi au dharau za Wakili Tundu Lissu kwa Mwalimu Nyerere. Halafu,kwanini wengine waliotajwa hawaonekani kama wametukanwa au kudhalilishwa?
Umenena mkuu, lakini umemsahau pia Lyatonga Augustine Mrema mzee wa Kiraracha ambaye aliimarisha usafi wa jiji la DSM na kuleta vivuli vya miti na pavements katikati ya jiji kwa amri ya siku 7, ingawa fadhila za JK zimemfanya aonekane kutikiswa siku hizi kimsimamo na kuegemea lolote la ccm hata bila kuchuja kama zamani. mnyonge myongeni lakini haki yake mpeni. Kaifanyia nji hii mambo mengi sana mazuri ambayo hapaswi kusubiri afe ndo tumsifu.
mkuu big up sana mkuu,nawashangaa sana ccm jk alipokuwa hai hawakutimiza wala kuyaishi yale sahihi aliyosema..walisema yamepitwa na wakati,leo ni marehemu wanajifanya kumtumia kama nukuu za biblia,wanafiki hawa tulione hili...wanatafuta tonge tu
Hicho kibabu cha chadema kimevurugwa
TUNDU LISSU namfananisha na "tanganyika jeki"
sifa kuu ya hii jeki ni kuwa hunyanyua gari pamoja na mzigo wake.
JK alinyanyuliwa pamoja na mizigo ya majaji wake.
Nyerere kanyanyuliwa na mizigo ya uongo wake.
Jk aliteua baadhi ya majaji ambao hawakuwa na sifa za uteuzi ndio maana kuna baadhi ilibidi wajiunge open university kuchukua LLB ili wakidhi matakwa ya sheria waliyokwisha ikiuka. "tanganyika jeki imewanyanyua"
Huyu Nyerere sasa kanyanyuliwa juu zaidi muuone uongo wake, kwa kuthibitisha uongo wake jiulize,
uko wapi ujamaa na kujitegemea!!!!!
Liko wapi azimio la arusha!!!!!!
muungano nao magumashi.
Msipanick huu ni ukweli hamkuujua kabla.
Mkuu Ogah, tunaomba utoe jibu la swali la aliyeanzisha uzi. Vinginevyo utakuwa unaendeleza uzushi kama hutaweka hizo kauli za Lissu mnazodai ni mbovu.
Hayo matusi ni yepi?
Mkuu Kichuguu, mbona hutaji hizo kauli? Tunawashukuru kwa kutukumbusha ya Zitto, Kilita, Majaji n.k. Ila unaendelea kuharibu badala ya kusaidia kwa kushindwa kuandika hizo kauli. Kama huwezi kufanya hivyo ni bora ukakaa kimya.
Lissu hakuwa anaiwakilisha JF bali alikuwa anawakilisha maoni wa Wachache katika kamati yake kwa hiyo waliyoyaleta hapa JF ndio wanatakiwa watuletee uchambuzi wa kina ni katika maneno yapi au maandishi yepi yanayoonyesha LISSU amemtukana Nyerere (R.I.P) tofauti na hayo mtakuwa bado mnaimba ngonjera na hamjajibu kinachotakiwa kujibiwa na mleta mada.
Maziwa Lala kwelikweli wewe na uanasheria wako wa kwenye JF...yaani matusi kwako ni yale ya nguoni tu...kama baba yako ni marehemu akatokea mpuuzi miaka kadhaa baadaye akasema baba yako alikuwa gaidi wewe hutaona kuwa ni matusi...acha ushabiki wa pesanane...
Maneno ni upanga wenye ncha mbili zinayokata pande zote. Maneno yako yanaweza kukufanya uwe na hatia na vile vile yanaweza kukuondoa kwenye tuhuma za hatia. Yote inategemea na jinsi unavyotumia maneno yako.
Sidhani kama Lisu alitumia maneno yake vizuri, na ndiyo maana nimekuwa na wasiwasi na uhakika wa maneno yote aliyowahi kutuambia kuhusu Zitto na Kitila huko nyuma.
Nikisema OSAMA gaidi ni tusi au sifa?
Tundu Lissu amemsifu hayati J.K.Nyerere kwamba aliongoza nchi
1.Kibabe
2.Kiujanjaujanja
3.Kidikiteta
4.Uongouongo
Sasa hizo zote ni sifa za Baba wa taifa. Tusi hapo ni lipi mbona ccm munakuwa wanafiki. hata mukisifiwa kwa natendo yenu bado munanuna!!!.
Lissu n mwanasheria anajua kitendo cha kutoa lugha inayoashiria kumdhalilisha mtu n makosa.
kumwita mtu muongo kisheria n kumdhalilisha.
kumwita mtu dikteta kisheria n makosa( defamesheni).
Kwa vile kauli kaitolea bungeni hakuna chombo chochote kitahoji kasoro bungeni tu.(kinga ya bunge kwa mbunge) .
Nje ya bunge anajua madhara yake hawezi kuyasema hayo.
Hata kama sio nyerere, sio busara kutamka" nyerere ni muongo, alizoea vya kunyonga, alitawala kijanjajanja. laghai nk" hayo sio matusi ni kashfa.
Wewe husiyejielewa ndio hauna adabu kwani una laana ya kuishabikia CCM huku hiyohiyo CCM ikinyanyasa wazazi na ndugu zako.tundu lisu hana adabu..kichaa chake hakijapona bado
sidhani kama Lisu katukana ila naona kuna upotoshwaji wa hali ya juu kwani nyerere ni binadamu lazima kuna sehemu amekosea na hatutakiwi kurudia yale yale makosa tunapoelekea kuandaa hatma ya vizazi vya leo,kesho na kijacho.Kuna uvumi (binafsi naziita propaganda) kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum na Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M.Lissu 'amemtukana' Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 'Matusi' husika yanadaiwa kuporomoshwa na Tundu Lissu alipokuwa akiwasilisha Maoni ya Wachache katika Kamati Nambari Nne ya Bunge.
Inasemwa kuwa Tundu Lissu amemtukana na kumdhalilisha Baba wa Taifa. Propaganda hizi zinazosambaa haraka na kwa kishindo zimemkumba hadi Mzee Edwin Mtei ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA. Nikumbukacho ni kuwa Lissu alipokuwa akitetea na kufafanua Maoni ya Wachache,alitoa mifano minne akiwataja watu mbalimbali wakiwemo Mwalimu Nyerere,Profesa Issa Ghulamhussein Shivji na Dr.Harrison Mwakyembe.
Kwanza,tufahamishane hasa matusi yaliyoporomoshwa na Wakili Lissu dhidi ya Mwalimu Nyerere. Tukiyajua na kutambua kuwa ni matusi na dharau kweli,tuungane kumkemea Wakili Lissu na kumuonya asirudie tena. Karibuni tutaje matusi au dharau za Wakili Tundu Lissu kwa Mwalimu Nyerere. Halafu,kwanini wengine waliotajwa hawaonekani kama wametukanwa au kudhalilishwa?
[h=2]Edwin Mtei asikitishwa na alaani kitendo cha Tundu Lissu kumtukana Baba wa Taifa, Mwl. Nyerere[/h]Nilimsikiliza Mheshimiwa Tundu Lissu na nasikitika kwamba sikubaliani naye jinsi alivyoeleza shutma juu na dhidi ya Mwalimu Julius Nyerere, Baba na Muasisi wa Taifa letu.
Inajulikana na umma wa Watanzania, kwamba mimi binafsi, kama Waziri wa Fedha, nilitofautiana na Mwalimu, nikajiuzulu Uwaziri Decemba,1979, nikimwomba ateuwe Mtanzania mwingine atakayeshauri mambo ya Uchumi na Fedha. Lakini tuliendelea kuwasiliana kwa maelewano bila chuki, na hata aliniteuwa niwe Mwakilishi wa Tanzania na Afrika inayoongea Kiingereza katika IMF (Shirika la Fedha Duniani) chini ya miaka mitatu baadaye Novemba, 1972.
Nimekuwa na mawasiliano na maelewano mazuri sana na Mwalimu hata baada ya kuasisi CHADEMA, Julai 1992 na tulipokamilisha Katiba na Sera za Chadema, nilimtembelea Nyumbani kwake Butiama nikampa azisome ajionee jinsi tulivyonuia kuwahudumia Wananchi wetu. Hata siku moja siwezi kumtusi Muasisi wa Taifa letu. Iwe ni mwiko pia kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo kumtusi Baba wa Taifa.
Ningewashauri uongozi wa Chadema na hasa Vijana wa M4C (Vuguvugu la Mabadiliko) tuendelee na uhamasishaji : kwa umakini, tukiwa na huruma kwa wanyonge maskini wa kutupwa, tukijiandaa kwa umakini na kiutaalamu Sera na Mikakati ya kuwakomboa toka katika umaskini wa kutupwa kwa kutumia nguvu ya umma (Peoples Power) tukitumia mikakati sahihi: kwani Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke:
Mikakati na Sera sahihi ikiwa ni kutumia misingi ya Uchumi na Miundombinu tulionayo licha ya uhalisia dhoofu tulioridhi; tukiwaenzi walioijenga na kuturidhisha kwa unyofu wao.
Roho ya Julius Nyerere ilale mahala pema Peponi. Amen!
With all due respect to Hon. Tindu Lissu, this smacks BAD TASTE.
Edwin Mtei,
Founder Chairman of CHADEMA.
nadhani wewe ndio huna akili timamutundu lisu hana adabu..kichaa chake hakijapona bado
Kuna uvumi (binafsi naziita propaganda) kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum na Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M.Lissu 'amemtukana' Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 'Matusi' husika yanadaiwa kuporomoshwa na Tundu Lissu alipokuwa akiwasilisha Maoni ya Wachache katika Kamati Nambari Nne ya Bunge.
Inasemwa kuwa Tundu Lissu amemtukana na kumdhalilisha Baba wa Taifa. Propaganda hizi zinazosambaa haraka na kwa kishindo zimemkumba hadi Mzee Edwin Mtei ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA. Nikumbukacho ni kuwa Lissu alipokuwa akitetea na kufafanua Maoni ya Wachache,alitoa mifano minne akiwataja watu mbalimbali wakiwemo Mwalimu Nyerere,Profesa Issa Ghulamhussein Shivji na Dr.Harrison Mwakyembe.
Kwanza,tufahamishane hasa matusi yaliyoporomoshwa na Wakili Lissu dhidi ya Mwalimu Nyerere. Tukiyajua na kutambua kuwa ni matusi na dharau kweli,tuungane kumkemea Wakili Lissu na kumuonya asirudie tena. Karibuni tutaje matusi au dharau za Wakili Tundu Lissu kwa Mwalimu Nyerere. Halafu,kwanini wengine waliotajwa hawaonekani kama wametukanwa au kudhalilishwa?