Mwalimu Mkuu amfungia mwanafunzi darasani kwa Mnyororo

Mwalimu Mkuu amfungia mwanafunzi darasani kwa Mnyororo

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Mwanafunzi wa darasa la saba (13) shule ya Msingi Ngarenaro Jijini Arusha amefungwa na mnyororo na kufungwa kwenye dawati Darasani na Mwalimu mkuu wa shule hiyo kwa kile kilichoelezwa kuwa kuwa ni mtoro.

Wakizungumza wazazi wameleza kuwa walipigiwa simu na mlinzi wa shule aliyekuwa zamu mchana kwamba mtoto wao amefungiwa darasani na Mwalimu mkuu hivyo waende wakamsaidie kwasababu anakohoa sana na hana msaada

Baada ya Time TV kufika shuleni hapo ilishuhudia mwanafunzi huyo akiwa kwenye dawati na raia waliokuwepo walitamani kumsaidia lakini mlinzi aliyekuwa zamu usiku huo alikuwa amefunga geti kwa kile alichoeleza kuwa kufanya hivyo ni magizo ya boss wake ambaye ni mkuu wa shule hiyo.

Baada ya tukio hilo taarifa zilitolewa na alifika mkuu wa kituo cha polisi ngarenaro na baadhi wa walinzi wakaruka geti kwa na Kwenda kuingia darasani na kuvunja mnyororo huo ili kumsaidia mwanafunzi huyo.

Hata hivyo mlinzi wa shule hiyo amekiri kuwa shuleni hapo wanafunzi huwa wanafungwa nyororo na Mwalimu mkuu kama ni watoro na kulala darasani mpaka asubuhi huku wamavaliwa nyororo ikiwa imefungwa na kufuli ambapo kazi yao ni kulinda kutokana na maelekezo ya Mwalimu mkuu wa shule hiyo Bwana Mussa

 
Huyo fal,a wakuitwa mwalimu mkuu afikishwe mbele ya vyombo vya dola akajibu tuhuma za udhalilishaji na kutweza utu wa mtoto.

Yaani mambo ya kufungana minyororo kama zama za utumwa zinafanywa karne hii ya utandawazi?

Nitakuwa wa mwisho kuamini kama huyo mwalimu mkuu atakuwa bado yupo ofisini hadi muda huu.

Wazazi hakikisheni mnafuatilia maendeleo ya watoto wenu wanatendewa unyama mwingi sana.
 
Tunaposema walimu ni kundi linaloongoza kuwa na shida ya afya ya akili muwe mnaelewa.

Sasa kweli kumfunga mtoto kwa mnyororo tena unamlaza usiku kucha na baridi kali vipi akipatwa na mauti atajiteteaje?

Mfano hapo tunaambiwa mtoto anakohoa sana maana yake afanyiwe vipimo ili kama ana shida yoyote basi msalaba huo abebe huyo mwalimu kilaz,a.

Hii habari imeniharibia sana siku yangu huwa sipendi manyanyaso ya aina yoyote dhidi ya binadamu.

Wanasheria mliopo Arusha msaidieni huyo mtoto apate haki yake maana kazi za sheria ni pamoja na kulinda haki za watu.
 
Back
Top Bottom