Binti Msichana
Senior Member
- Oct 9, 2016
- 109
- 247
Nimesikitishwa kupata habari kuhusu mwalimu anayefundisha shule ya sekondari Dunda iliyopo Bagamoyo mkoa wa Pwani kukimbia kazi ya ualimu baada ya kulipwa 34000 kwa mwezi.
Hii inatokana na adhabu ya kushushwa cheo na kulipwa nusu mshahara na Tume ya Utumishi wa Walimu kwa kosa la utoro kazini.
Mwalimu huyo wa kike aliishi maisha magumu sana hapo hapo shuleni ,alikosa mpaka hela ya kula ilimlazimu auze miwa na maembe aliyoyaokota hapo shuleni ili apate pesa ya kula.
Uzalendo ukamshinda baada ya mazingira magumu ya kazi aliamua kuondoka kazini bila ya taarifa kwa muajiri.
Habari nilizozipata mwalimu huyo yupo Mlandizi akifanya kazi ya kuhudumia wateja bar.
TSC mnapotoa adhabu ya kupunguza mishahara kwa walimu mzingatie iwapo kama mtuhumiwa ana mikopo benki, isitoshe adhabu ya kupunguza mshahara ni ya kikatili maana mshahara wenyewe hautoshi hapo hapo mnaupunguza.
Habari nilizozipata huyu mwalimu alikuwa na madeni benki na taasisi za fedha hapo Bagamoyo.
Kutokana na mazingira magumu ya kazi mwalimu huyo kaamua kutelekeza kazi yake.
Hii inatokana na adhabu ya kushushwa cheo na kulipwa nusu mshahara na Tume ya Utumishi wa Walimu kwa kosa la utoro kazini.
Mwalimu huyo wa kike aliishi maisha magumu sana hapo hapo shuleni ,alikosa mpaka hela ya kula ilimlazimu auze miwa na maembe aliyoyaokota hapo shuleni ili apate pesa ya kula.
Uzalendo ukamshinda baada ya mazingira magumu ya kazi aliamua kuondoka kazini bila ya taarifa kwa muajiri.
Habari nilizozipata mwalimu huyo yupo Mlandizi akifanya kazi ya kuhudumia wateja bar.
TSC mnapotoa adhabu ya kupunguza mishahara kwa walimu mzingatie iwapo kama mtuhumiwa ana mikopo benki, isitoshe adhabu ya kupunguza mshahara ni ya kikatili maana mshahara wenyewe hautoshi hapo hapo mnaupunguza.
Habari nilizozipata huyu mwalimu alikuwa na madeni benki na taasisi za fedha hapo Bagamoyo.
Kutokana na mazingira magumu ya kazi mwalimu huyo kaamua kutelekeza kazi yake.