Nchi zingine watu walioliwa kwa mamilioni na nchi zilikuwa in a state of emergency 24/7. Anyway ni kweli alikua na mapungufu yake na aka kiri. Je ni viogozi wangapi leo wana weza kutamka hadharani kuwa wana kubali kukosa? Hata Mwinyi na Mkapa leo hii hawa kubali makosa yoyote. Let's just admit if, looking at African leaders of the time tuli bahatika. He wasn't perfect but he was no Iddi Amin, Mobutu Sese Seko or Bokasa.
Jamani hata kipofu kwa hili anaona jamani, chukua hii logic ni yupi Kidume kwenye mafanikio ya maisha, kati ya hawa vijana wawili, aliyemaliza chuo akakuta Baba yake keshamfungulia Kampuni,au mwenzie aliyemaliza chuo nae yeye baada ya kumaliza chuo anakwenda kuanza moja kuhangaika kufungua kampuni ya kwake kwa bidii zake binafsi bila msaada wa wanafamilia yake kama yule wa awali.Yupi kati ya hawa anastahiki heshima ya kuwa amefanikiwa katika Maisha.
Natumaini daima tumtendee haki Mwalimu, kama
ANGEKUWA MLAFI NA MLEVI WA MADALAKA YEYE na
Wafuasi wake waaminifu,nahakika ingezaliwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yenye
uwozo zaidi ya Kongo ilivyo sasa.Na kwa kuwa ndio nchi yenye makabila mengi kusini mwa jangwa la Sahara vita vya wenyewe vingekuwa ni sehemu ya utamaduni wetu.Na wenzetu wanavyopenda kufanya Biashara ya kuuza siraha. Sehemu zenye maliasili kama madini zingekuwa ni nchi zinazojitegemea.
Kunakotoka Almasi na Dhahabu jamaa wangenyonya mpaka basi kwa kuwa mtawala ni
MROHO NA MLAFI,na wao wanajua jinsi ya
kuwachezea [Handling] watawala aina hiyo.Wangeivuluga nchi hii vibaya sana, na sasa hivi hata hicho kidogo ambacho tunacho tunaendelea
kukigawa bule [kwa vigezo vya uwekezaji] kingekuwa kimekwisha kwisha zamani sana.
Waliwarubudi Viongozi wachache kama wakina Marehemu
Kambona wakafanikiwa,lakini Mwalimu kwa kulijua hilo akasimama
kidete akawa tayari kuwatosa wakina Kambona hili atufikishe hapa tulipo ingawa akiamshwa leo hii,jamani mzee wa watu I hope itabidi azimie.
Tena wengi wa Viongozi wetu wasivyo na ADABU kwa Mzee yule wakisikia watanzania wanamlilia
Baba wa Taifa, kupitia makongamano, maandamano,mikutano ya hadhara na vyuoni, wao
ukejeri na kusema marehemu ahaongei.Na ndio maana kwa kuwa wengi wao si watu wa imani ya kuwa kunauwepo wa Mungu [ambalo pia ni kosa letu Watanzania kuchagua viongozi wasiokuwa na
hofu ya Mungu].Na hivyo kwa kuwa Kiongozi hana uhusiano na Mungu,umpelekea kutopata maarifa [
Kumcha Mungu ni Chanzo cha Maarifa].
Kwa kutokumjuha Mungu hawatambui ni kwanini vijana wadogo ambao hawakupata kumuona
Baba Wa Taifa lakini leo hii wanaamini na kumtaja kwa kutambua uwezo wake kuwa alijibidiisha kujenga TAIFA kwa faida ya Watanzania wote na sio kundi fulani la watu.
Hawaoni uwezo wa Mungu na hawatambui mausiano ya kiroho kati ya
Taifa na
Wananachi wa Tanzania, huyo
Raia Mwenzao [
Baba Wa Taifa] ambae aliwaongoza kuwa
Taifa Huru,na hatimae baada ya kifo chake wote kwa pamoja wakakubali kumpa jina kuwa anastahiki kuitwa
Baba Wa Taifa La Watanzania.[daima hatatoke mtu mwingine kupokea jina hilo ndani ya Taifa] zaidi yake kutakuwa na mababa wadogo wataifa kama Baba wa Demokrasia.
Nani asiyejua Baba alishapata kuwaonya baadhi ya watoto wake kuwa hawafai, lakini matokeo yake aliyoyasema yametokea na wananchi wamedhihili usemi wake.Wasemwa wamekuwa vinganganizi na hawataki kusikia kuna
Baba wa Taifa, ambaye kwa dhahili wanajua hawawezi na hawoteweza kutembea ndani ya nyayo zake sembuse na kuvaa viatu wapishe wawaachie wenye uwezo wa kuvaa viatu vya Mwalimu.Wanachokifanya ni kufuta yale yote aliyoyasisi ili wajenge ndani ya
uovu wao [Ufisadi].Wakasahau kuwa Baba ni nguzo na Msingi wa familia hata kama alishakufa kuna yale aliyowaachia kama
wosia daima yatabakikuwa nguzo na kinga inayofanya kazi kuwatatulia matatizo yenu ya kila siku katika maisha yenu.
Tanzania bila maono [
Vision] ya
Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kuwa kila mtu anastahiki keki ya Taifa na haki ya utu wake kuheshimika kwa wanajamii wenzake. Tanzania tumeiona chungu sote,hatimae uchungu huo ambao wananchi walishaupitia utatoka utaamia kwa mafisadi, kwa kuwa muda utafika wa mwenye haki kudai haki yake itabidi mafisadi wamludishie mwenyenacho mali yake ambae ni raia wa Tanzania.