Mwaka mpya wa 2012: Tuimarishe ndoa zetu…

Hata mie imeniuma sana na kunikumbusha kisa nilichokutana nacho jana,

Dada mmoja jirani yetu jana alipewa kipigo kama kibaka...

Wakati tunatoka kanisani tukakuta majirani wanaamulia ugomvi. Dada huyo alitumia simu ya mume wake kuwasiliana na dada yake (wana simu moja ambayo wanaichangia wote mume na mke). Bahati mabaya hakumpata dada yake kwenye simu. Baadaye kidogo, dada yake akapiga na simu kupokelewa na shemeji yake. Dada wa huyo mke alimweleza shemeji yake kuwa amekuta missed call. Mume akamvaa mke wake na kumuuliza kuwa, kwa nini anabeep watu kwa simu yake? Dada wa watu akajaribu kujieleza kuwa hakubeep bali alipiga lakini akamzidishia hasira mume wake na kuanza kupata kipigo. Yaani alipigwa ngumi, mateke na vibao kama vile ni kibaka kaiba cheni!!

Basi tena, sikutaka kuongelea haya mambo ya kupigana kwa sababu yananikera sana!1

huyu dada anahitaji awe na kaka kama Asprini....
lakini kwanini na nyie hamkuamulia bana? aisee ugomvi wa mke na mume kiasi cha majirani kusikia hii haijanikalia sawa aisee...nimejiskia uchungu sana.
 
Wala usiogope Lizzy,

Kama wote tungeweza ku-predict kitakachotukuta, hakika wengi wetu tusingeoa/olewa..Ila kwa vile hatukujua tumekubaliana na kila kitu ambacho kimetukuta.

You package is on the way but even the sender doesn't know what it contains!!

Uwe na amani tu!!

Babu "lisilojulikana" linatisha. Waweza kudhani umepata kumbe umepatikana. . . au ukapata na usijue ukaishia kuchezea shilingi karibu na shimo la choo. Tabu tupu.
 
Hahahahaha. . . .
Haki ya nani kesi ntakua nazileta kivingine. Sitaki madongo ya "siulisemaga hivi na vile? Iko wapi jeuri yako sasa??"
Au nakuja na "Rafiki yangu anahitaji ushauri. . . . . " hapo hamtaniweza ng'o.

...amaaaa? usifanye hivyo bana, utakosa huruma yangu dearie...pls dont
ukishatendwa huko we njoo tu hapa na jina hili hili, labda na avatar yenye manundu...
si unakumbuka sympathy aloipata makaburini na yule mke aloishiwa mafuta?
 
Babu hapo kwenye suala la kipato ukijumuisha na watoto wa nje ya ndoa (yaani waliozaliwa nje but wakati mume tayari yu ndoani) bado ina ugumu.
I was once asked na mmama ambaye yeye ndo breadwinner na mhimili wa familia. Mumewe akafariki pasipo kuandika urithi. Mali yoooote (ambayo technically amechuma mwanamke) ikatiwa kwenye mirathi.... Mtoto wa nje akapewa nyumba Kunduchi (ambayo iloinunuliwa lwa juhudi na pesa za mama) naye kijana amemvuta mamake wanaishi pamoja!

Huyu mmama anakaribia kupasuka kwa hacra.

Hapana dada,

hapo kuna makosa ya kisheria...Mtoto wa nje hawezi kurithi mali ya ndoa labda kama baba yake aliandika hivyo kwenye wosia na kuspecify kitu gani apewe. Kama baba hakuandika basi waliompa nyumba huyo mtoto walikosea. Mwambie mama atafute washauri wa sheria wampatie msaada. Vitoto kama huwa hata adabu havina, kitakuwa hapo kinamporomoshea matusi huyo mama utadhani ni kuli!!

...lahaula wala quwwata,... tuseme mie nimezaa watoto wawili nje ya ndoa, kwa nyakati tofauti, na wanawake tofauti...halafu baadae maishani nije nioe mwanamke nizae nae...how can i exclude my blood bana kwenye urithi?

tusitishane mzee, kwangu mie nitaendana kinyume na maandiko ya kidini, na ya kiserikali...wanangu lazima wanirithi bana, ...kwangu mimi mwana wa haramu msemo huo hau apply... kosa la wazazi halimhukumu mtoto bana..

...hapa ndoa yangu lazima iyumbe kwa msingi huu mkuu DC.
 

...amaaaa? usifanye hivyo bana, utakosa huruma yangu dearie...pls dont
ukishatendwa huko we njoo tu hapa na jina hili hili, labda na avatar yenye manundu...
si unakumbuka sympathy aloipata makaburini na yule mke aloishiwa mafuta?
Hahahaha. . . yale ya Makaburini yalikua mepesi. Nikija na yangu mtaogopa kunisema kweli, mtabaki kunipa pole hata kama "nilijitakia".
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Katika thread mbali mbali ambazo tumechambua mwaka huu wa 2011, binafsi nimefarijika na kufaidi michango ya wadau kuhusu taasis ya ndoa. Ndoa ni taasisi ni muhimu sana na kila mmoja wetu analo jukumu la kulinda ndoa yake na pia kutoa support kwa ndoa za marafiki zake. Ili ndoa idumu, kuna vitu ambavyo ni muhimu sana kuvipa kipaumbele. Hivi ni pamoja na,

1. Upendo….Ni muhimu kuonesha kwa maneno na vitendo kuwa unampenda mwenzio na kumthamini. In short, mke au mme anatakiwa awe nambari one siku zote…
…Kwenye hili suala huwa sitaki utani…my wife is always nambari one and I can give anything including my life to protect her!!

2. Heshima na uvumilivu…Bila kuyaonesha haya kwa vitendo lazima ndoa itayumba

3. Kujitoa (sacrifice)…Kama hauko tayari kujitoa kwa ajili ya mwenzi wako ni bora ubaki single au ukapursue line nyingine za maisha ikiwemo utowashi!!

4. Uaminifu….Hapa ni pagumu sana ila ni eneo nyeti…Ukishindwa basi tumia kanuni ambazo wadau walileta na kujadili hapa….Cheating should be avoided but doing it responsively ni sehemu ya uungwana kwenye ndoa

5. Consensus .. ni muhimu sana kukubaliana katika vitu vya msingi na kutekeleza hayo makubaliano kwa vitendo! Kuacha kila mtu afanye mambo yake kwenye ndoa ni sawa na kuwa na jeshi lisilo na kamanda…Lazima litasambaratika tu!

Yapo mambo mengine mengi na wadau wanaweza kuyaongeza. Hata hivyo kuna changamoto nyingi ambazo zimejitokeza hivi karibuni na wadau wanatakiwa kupambana nazo.

1. Uzoefu wa wanandoa unaotokana na kuwa na mahusiano ya ki-ngono kabla ya ndoa…
……Enzi zile watu walikuwa wanakutana wakiwa mabikra…hawakuwa na kitu chochote cha kufanyia reference. Je tunafanyaje kudeal na historia zetu za nyuma katika ndoa zetu ili zisituyumbishe?

2. Watoto waliopatikana kabla ya ndoa….Hili ni gumu sana especially kwa wanawake kuliko kwa wanume….Linachangiaje ku-destabilize ndoa??...Naomba michango ya wadau!!

3. Tofauti ya kipato…Hili ni janga jingine especially mwanamke anapokuwa na uwezo zaidi ya mwanamume. Hapa couples zinatakiwa kukubaliana jinsi ya kuhandle mambo ya pesa!

4. Infidenlity inayopata support ya technology mpya….Siku hizi ni rahisi sana kukutana na watu wapya na kuweka mambo sawa bila hata kutakiwa kusafiri…!! Wanandoa wanatakiwa kukwepa haya mambo ili kutowaumiza wenzi wao!

Naamini kuwa, tunatakiwa kuelewa kwamba kuna mabadiliko makubwa yaliyotokea hivi karibuni na hivyo tuchukue hatua mathubuti ili kuimarisha ndoa zetu,

Nawatakia heri ya mwaka mpya wa 2012!!

Babu DC (1947)

yani kwakweli maelezo yamejitosheleza da!
 

...lahaula wala quwwata,... tuseme mie nimezaa watoto wawili nje ya ndoa, kwa na Nyakati tofauti, na wanawake tofauti...halafu baadae maishani nije nioe mwanamke nizae nae...how can i exclude my blood bana kwenye urithi?

tusitishane mzee, kwangu mie nitaendana kinyume na maandiko ya kidini, na ya kiserikali...wanangu lazima wanirithi bana, ...kwangu mimi mwana wa haramu msemo huo hau apply... kosa la wazazi halimhukumu mtoto bana..

...hapa ndoa yangu lazima iyumbe kwa msingi huu mkuu DC.

Hii mada tulishaichambua sana hapa hapa kwenye MMU,

https://www.jamiiforums.com/mahusia...-na-umiliki-wa-mali-kizungumkuti-kingine.html


Mtoto wa nje ni yule ambaye amezaliwa nje ya ndoa husika. Na mali za ndoa (marrital property) ni zile ambazo zimechumwa wakati mko pamoja. Hata hivyo mali zako za awali unaweza kuziandikisha kuwa zitakuwa zako peke yako na kwake vile vile.

Suala la watoto ambao uko nao kutoka kwenye ndoa ya awali nadhani ni tofauti. Nitauliza wataalamuu wanisaidie kwenye hili. Hata hivyo, dawa yake ni wewe kuandika wosia na kuwapa mali zao upfront!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu

...lahaula wala quwwata,... tuseme mie nimezaa watoto wawili nje ya ndoa, kwa nyakati tofauti, na wanawake tofauti...halafu baadae maishani nije nioe mwanamke nizae nae...how can i exclude my blood bana kwenye urithi?

tusitishane mzee, kwangu mie nitaendana kinyume na maandiko ya kidini, na ya kiserikali...wanangu lazima wanirithi bana, ...kwangu mimi mwana wa haramu msemo huo hau apply... kosa la wazazi halimhukumu mtoto bana..

...hapa ndoa yangu lazima iyumbe kwa msingi huu mkuu DC.
Ni kweli usemayo Mbu but kesi ya huyu mama ni kuwa mumewe alichetuka somewhere in between!!
Na hapa inachukuliwa ni kosa la mme na adhabu yake ni kumtafuti urithi wake lakini si kumpatia kile alichotafuta mama ?
 
Ni kweli usemayo Mbu but kesi ya huyu mama ni kuwa mumewe alichetuka somewhere in between!!
Na hapa inachukuliwa ni kosa la mme na adhabu yake ni kumtafuti urithi wake lakini si kumpatia kile alichotafuta mama ?

Huyo mtoto hana cha kurithi hapo. Yeye siyo mtoto wa ndoa na baba yake alitakiwa amsaidie akiwa bado hai. Na endapo angeandika wosia, angeweza kumpatia huyo mtoto baadhi ya mali zake kama ambavyo angeweza kumpa mtu mwingine yeyote.

Katika hii case huyo mtoto aende tu kwa mama yeka wasaidiane kuomboleza. That's all he deserves and nothing else, kwa mujibu wa sheria ya ndoa ya mwaka 1971!!
 
Back
Top Bottom