MWAGIA HUMO 01.

MWAGIA HUMO 01.

Huyu Mimi

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2019
Posts
2,575
Reaction score
2,121
MWAGIA HUMOHUMO:Sehemu Ya Kwanza (1)

Toka nimezaliwa nimekuwa mwanamke mwenye mkosi kila mpenzi wangu mwanzo wa mapenzi yalikuwa motomoto. Lakini baada ya muda fulani mwanaume alinimwaga bila sababu za msingi.

Kila siku ya Mungu nilishindwa kuelewa nina matizo gani mtoto wa kike miye. Kibaya zaidi ndoa niliyofunga miezi minne iliyopita ilivunjika huku mpenzi wangu akipagawa na penzi la nje. Jamani mbona makubwa, huyo mwanamke aliyenivunjia ndoa yangu hata mkonioni hajai, hanizidi kwa lolote si kwa sura wala umbile. Niliamini maneno ya watu huenda yule mwanamke ni mchawi.

Kitendo cha ndoa yangu kuvunjika na historia yangu ya nyuma ya kuachwa kwenye mataa na wanaume kiasi cha kugeuzwa jina ubao wa shabaha kila mwanaume kujifunza kulenga kwangu na akichoka hiondoka bila kwaheri.

Bahati niliyokuwa nayo mwanaume yeyote aliyenitaka, yupo radhi kunihonga hata milioni ili mradi anipate, Mungu alijilalia umbile na sura lakini niliamini kuna kitu
kikubwa kimepungua kwangu kinachofanya wanaume wanikimbie. Kwani moto anaoanza nao mwanaume kama maji ya moto lakini baada ya muda hupoa. Lakini hachelewi kupoa, wapo niliokaa nao mwezi mwili, mitatu , wiki na wengine wakionja hawarudi tena. Kuna watu walionifuata na kunieleza labda niende kwa waganga wa kienyeji ili nisafishwe nyota yangu.

Ushauri ule niliufuata baada ya kutumia dawa zile sikuchelewa kupata bwana aliyetangaza ndoa kabisa. Lakini baada ya miezi minne ndoa yangu ilivunjika, kitendo kile kilinitia aibu, yote ya kuchezewa na wanaume na kuachwa ilikuwa tisa, kumi ilikuwa kuachwa bila sababu huku mume wangu akizama kwenye penzi ya kinyago msela mwanamke asiye na mbele wala nyuma. Kitendo kile kilinidhalilisha sana, sikuweza kuvumilia bila kujieleza siku ya pili nilipanda gari mpaka Dar na kufikia kwa rafiki yangu niliyekuwa nasomanaye shule moja ambaye baada ya kumaliza shule alikwenda Dar kutafuta maisha na baadaye alinieleza amepata chumba tena anafanya kazi kwenye kampuni ya mtu binafsi. Kwa vile nilikuwa na siku yake nilipomjulisha nakwenda Dar hakunikatalia Nilipanda basi hadi Dar. Baada ya kufika nilikaa mwa muda wa mwezi mmoja na kunitafutia kibarua katika kiwanda kimoja, ajabu msimamizi alinizimikia na kuanzisha mahusiano na mimi. Kwa vile kila mmoja alikuwa na ujiko kuwa na uhusiano na bosi basin a mimi nilimkubalia.

Kama kawaida haikuchukua hata mwezi akanimwaga na kashfa nyingi kwamba heri atembee na mwanaume mwenzake kuliko kulala na mimi. Kwa kweli kitendo kile kilizidi kunidhalilisha na kuniweka kwenye wakati mgumu, kibaya kila mwanaume niliyekuwa nakutana naye na kuniacha hakunieleza tatizo langu. Kwa kweli niliumia sana na kuamua kuacha kazi, niliapa sitakuwa tayari kufanya kazi wala kuanzisha uhusiano na mwanaume yeyote. Baada ya shoga yangu kupata bwana ilinibidi nihame kwa kutafutiwa chumba sehemu za uswahili kwa bibi mmoja maarufu pale mtaani Bi Shuu, ni bibi wa miaka 55 lakini mambo yake temea chini. Bibi yule alinilea kama mwanaye wa kuzaa hata kodi yangu hakuitaka. Kuhamia kwa Bi Shuu nilijikuta nikiingia dunia nyingine kabisa, kweli nimekubali tembea uone mambo, ningekaa Arusha ningeyajua haya. Nazidi kukubali kweli vikiungwa vitamu, tena mtu ataomba aongezwe na akimaliza kula lazima ajilambe vidole. Najua una hamu kuvijua hivyo vitamu vilivyo ungwa mpaka watu wakajilamba, Naomba twende pamoja tuipate wote faida ya kuwa karibu na makungwi kama Bi Shuu. ******** Katika mambo niliyokuwa siyapendi katika maisha yangu ni pamoja na kusumbuliwa na mwanaume wakati wa kilimo cha mhogo. Ooh! Inama, mara jipinde hivi, mara geuka hivi. Siku zote nilijiuliza kwani bila kukusumbua hivyo mwanaume hawezi kufikisha mzigo wake. Kitendo cha kijana huyu ambaye alinipata kupitia kwa Bi Shuu kutaka kunisumbua kilinikera sana. “Manka mbona hivyo sasa raha ya mapenzi ipo wapi?” “Nimesema sifanyi unavyotaka, sipo kwenye mazoezi ya yoga hapa kama huwezi hivi, vaa nguo zako ondoka, ” nilisema kwa ukali bila kumuangalia nyuma yangu alipokuwa amekaa. “Lakini Man…,” “Ee..ee..eeh, nasema hivi kwani tatizo nini bila hivyo unavyotaka hufiki safari yako?” Nilimkata kauli Edward. “
ITAENDELEA
 
Sehemu Ya Pili (2)

Lakini pamoja na yote sikuwa na sifa ya kumteka mwanaume kimapenzi zaidi ya kunionja na kuniacha. Wasiwasi wangu huenda mwili wangu hauna asali itakayo mfanya mwanaume yoyote atakaye nionja anirudie mara mbili. Basi baada ya kupokea aligeuka na kuondoka kurudi ofisini kwangu.
Nilipofika mlangoni nilikumbuka kitu nilitaka kumuuliza bosi, niligeuka ili nimuulize kitu. Niligeuka ghafla na kukutanisha macho na bosi ambaye kumbe nyuma yangu alikuwa akinifuatia. Maskini kaka wa watu alishtuka mpaka akadondoka chini, nilijikuta namuonea huruma.
Nilirudi hadi chini alipokuwa amekaa bila kuonesha kujinyanyua, mwili wake haukuwa mkubwa sana nilimshika mkono ili kumnyanyua.
“Hapana Manka nitanyanyuka mwenyewe.”
“Hapana bosi naomba unipe mkono,” nilimwambia kwa sauti ya huruma yenye kubembeleza. Alinipa mkono na kumnyanyua, baada ya kunyanyuka nilitoa kitambaa changu na kumfuta sehemu yenye vumbi.
“Tosha Manka sehemu zingine nitafuta mimi.”
“Hapana bosi ni wajibu wangu kufanya hili.”
Aliniacha nimfute kisha nilimtengenezea kiti na kumuomba akae.
“Unaweza kukaa.”
Bila kuongeza neno alikaa kwenye kiti chake huku uso wake ukionesha aibu imemtawala.
“Pole bosi,” nilimwambia kwa sauti ya chini.
“Asante.”
“Hukuumia?”
“Nipo sawa.”
“Pole sana.”
“Asante Manka, nipo sawa kaendelee na kazi.”
Niligeuka na kuondoka hata nilichotaka kumuuliza nilikiacha na kupanga kumuuliza kupitia simu yangu ya mezani. Nilitoka hadi ofisini kwangu kuendelea na kazi, kabla ya kuanza kazi nilijikuta nikijiuliza kilichomdondosha bosi wangu ni nini.
Wasiwasi ulikuwa uleule bosi kapagawa na mimi, kitu ambacho sikutaka kinitokee kwa muda ule kwani ilikuwa mapema sana. Niliamini kabisa bosi kwa mtazamo wa nje alikuwa amepata bonge la mwanamke, lakini ndani sikuwa na sifa zile za kukaa na mwanaume kwa muda mrefu.
Niliyapuuza na kuendelea na kazi, nilikumbuka kuna kazi nilitaka kupata maelekezo kwa bosi. Nilimnyanyua simu kumpigia baada ya kuita kwa muda ilipokelewa.
“Haloo bosi.”
“Ooh..Aah…Nani Manka,” maskini bosi wangu alionesha kiwewe bado hakijamtoka.
“Bosi mbona hivyo?”
“Aah, kawaida tu, unasemaje?”
“Ok, bosi nilikuwa nauliza hii kazi ya malipo kuna maandishi ya mkono nayo niyaandike?”
“Hakuna tatizo, yaandike kama ilivyoandikwa.”
Nilikata simu na kuendelea ka kazi yangu kama kawaida, baada ya muda nikiwa bize simu ya mezani iliita, nilinyanyua na kupokea.
“Haloo bosi.”
“Ndiyo Manka jiandae tukapate lunch.”
“Nashukuru bosi.”
Baada ya kukata simu, niliangalia saa kubwa ya ukutani iliyokuwa mbele yangu, ilionesha ni saa saba kasoro kumi mchana. Nilimalizia kazi yangu ili nipate muda wa kwenda kula, nikiwa bado nimeinama nikirekebisha tatizo la kisarufi nilishtuliwa na sauti ya bosi.
“Manka tunaweza kwenda.”
“Hakuna tatizo bosi, namalizia kurekebisha sarufi.”
“Utamalizia tukirudi.”
Nilisave kisha nilizima computer na kunyanyuka, nilijitengeneza vizuri nguo niliyovaa. Kwa chati nilimuona bosi wangu koo likimcheza kama mtu mwenye kiu kikali. Baada ya kuhakikisha nipo sawa tulitoka hadi kwenye gari lake kisha tulikwenda kwenye moja ya hoteli ya kifahari ambayo ilinikumbusha mbali enzi nipo kwenye ndoa yangu.
Tulipofika Mateja alionesha kutojiamini sana kwangu kitu ambacho sikuamini mwanaume kama yeye kuwa katika hali ile. Sikuwa na sifa kubwa zaidi ya mwanamke aliyepoteza matumaini ya kupata hadhi mbele ya mwanaume. Niliamini kaniona kwa nje hanijui ndani nilivyo ndio maana ananipapatikia.
Nilijua akikipata anachokitafuta kwangu pengine ndiyo siku ya kunifukuza kazi, lakini sikuwa na jinsi kila mwanaume mwenye pesa aliamini mwanamke sahihi wa kukaa naye ni mimi. Baada ya kuketi kwenye viti vyetu muhudumu alifika na kutaka oda zetu.
“Manka agiza chochote ukitakacho kwa bei yoyote.”
“Asante, nataka kula unachokipenda wewe,” utanishangaa kwa nini nimesema vile, nilifanya vile ili kumtoa wasiwasi na kumfanya awe huru kwangu japo si katika suala la mapenzi.
“Hapana Manka nataka wewe leo ndio uchague chakula tutakacho kula.”
“Sawa,” nilichagua chakula
 
Sehemu Ya Pili (2)

Lakini pamoja na yote sikuwa na sifa ya kumteka mwanaume kimapenzi zaidi ya kunionja na kuniacha. Wasiwasi wangu huenda mwili wangu hauna asali itakayo mfanya mwanaume yoyote atakaye nionja anirudie mara mbili. Basi baada ya kupokea aligeuka na kuondoka kurudi ofisini kwangu.
Nilipofika mlangoni nilikumbuka kitu nilitaka kumuuliza bosi, niligeuka ili nimuulize kitu. Niligeuka ghafla na kukutanisha macho na bosi ambaye kumbe nyuma yangu alikuwa akinifuatia. Maskini kaka wa watu alishtuka mpaka akadondoka chini, nilijikuta namuonea huruma.
Nilirudi hadi chini alipokuwa amekaa bila kuonesha kujinyanyua, mwili wake haukuwa mkubwa sana nilimshika mkono ili kumnyanyua.
“Hapana Manka nitanyanyuka mwenyewe.”
“Hapana bosi naomba unipe mkono,” nilimwambia kwa sauti ya huruma yenye kubembeleza. Alinipa mkono na kumnyanyua, baada ya kunyanyuka nilitoa kitambaa changu na kumfuta sehemu yenye vumbi.
“Tosha Manka sehemu zingine nitafuta mimi.”
“Hapana bosi ni wajibu wangu kufanya hili.”
Aliniacha nimfute kisha nilimtengenezea kiti na kumuomba akae.
“Unaweza kukaa.”
Bila kuongeza neno alikaa kwenye kiti chake huku uso wake ukionesha aibu imemtawala.
“Pole bosi,” nilimwambia kwa sauti ya chini.
“Asante.”
“Hukuumia?”
“Nipo sawa.”
“Pole sana.”
“Asante Manka, nipo sawa kaendelee na kazi.”
Niligeuka na kuondoka hata nilichotaka kumuuliza nilikiacha na kupanga kumuuliza kupitia simu yangu ya mezani. Nilitoka hadi ofisini kwangu kuendelea na kazi, kabla ya kuanza kazi nilijikuta nikijiuliza kilichomdondosha bosi wangu ni nini.
Wasiwasi ulikuwa uleule bosi kapagawa na mimi, kitu ambacho sikutaka kinitokee kwa muda ule kwani ilikuwa mapema sana. Niliamini kabisa bosi kwa mtazamo wa nje alikuwa amepata bonge la mwanamke, lakini ndani sikuwa na sifa zile za kukaa na mwanaume kwa muda mrefu.
Niliyapuuza na kuendelea na kazi, nilikumbuka kuna kazi nilitaka kupata maelekezo kwa bosi. Nilimnyanyua simu kumpigia baada ya kuita kwa muda ilipokelewa.
“Haloo bosi.”
“Ooh..Aah…Nani Manka,” maskini bosi wangu alionesha kiwewe bado hakijamtoka.
“Bosi mbona hivyo?”
“Aah, kawaida tu, unasemaje?”
“Ok, bosi nilikuwa nauliza hii kazi ya malipo kuna maandishi ya mkono nayo niyaandike?”
“Hakuna tatizo, yaandike kama ilivyoandikwa.”
Nilikata simu na kuendelea ka kazi yangu kama kawaida, baada ya muda nikiwa bize simu ya mezani iliita, nilinyanyua na kupokea.
“Haloo bosi.”
“Ndiyo Manka jiandae tukapate lunch.”
“Nashukuru bosi.”
Baada ya kukata simu, niliangalia saa kubwa ya ukutani iliyokuwa mbele yangu, ilionesha ni saa saba kasoro kumi mchana. Nilimalizia kazi yangu ili nipate muda wa kwenda kula, nikiwa bado nimeinama nikirekebisha tatizo la kisarufi nilishtuliwa na sauti ya bosi.
“Manka tunaweza kwenda.”
“Hakuna tatizo bosi, namalizia kurekebisha sarufi.”
“Utamalizia tukirudi.”
Nilisave kisha nilizima computer na kunyanyuka, nilijitengeneza vizuri nguo niliyovaa. Kwa chati nilimuona bosi wangu koo likimcheza kama mtu mwenye kiu kikali. Baada ya kuhakikisha nipo sawa tulitoka hadi kwenye gari lake kisha tulikwenda kwenye moja ya hoteli ya kifahari ambayo ilinikumbusha mbali enzi nipo kwenye ndoa yangu.
Tulipofika Mateja alionesha kutojiamini sana kwangu kitu ambacho sikuamini mwanaume kama yeye kuwa katika hali ile. Sikuwa na sifa kubwa zaidi ya mwanamke aliyepoteza matumaini ya kupata hadhi mbele ya mwanaume. Niliamini kaniona kwa nje hanijui ndani nilivyo ndio maana ananipapatikia.
Nilijua akikipata anachokitafuta kwangu pengine ndiyo siku ya kunifukuza kazi, lakini sikuwa na jinsi kila mwanaume mwenye pesa aliamini mwanamke sahihi wa kukaa naye ni mimi. Baada ya kuketi kwenye viti vyetu muhudumu alifika na kutaka oda zetu.
“Manka agiza chochote ukitakacho kwa bei yoyote.”
“Asante, nataka kula unachokipenda wewe,” utanishangaa kwa nini nimesema vile, nilifanya vile ili kumtoa wasiwasi na kumfanya awe huru kwangu japo si katika suala la mapenzi.
“Hapana Manka nataka wewe leo ndio uchague chakula tutakacho kula.”
“Sawa,” nilichagua chakula
 
*MWAGIA HUMO HUMO EP 03*


Sehemu Ya Tatu (3)

Baada ya kusema vile aliingiza mkono mfukoni na kutoa pochi alihesabu noti tatu za kumi kumi na kunipa.

“Mpelekee hizi mwambie nitakuja.”

Nilizipokea na kufunga kazi zangu, pamoja na penzi letu kufa bado nilipelekwa na kurudishwa nyumbani na gari. Nilipofika nyumbani nilikwenda chumbani kwangu, kabla ya kufanya kitu chochote nilivua nguo zangu na kubakia mtupu kama nilivyozaliwa mbele ya kioo kikubwa na kujitazama upya kasoro katika mwili wangu.

Nilituliza macho na kuyazungusha taratibu mwilini mwangu kuangalia nina kasoro gani inayonifanya kila kukicha nipoteze wanaume. Kila hatua niliyokuwa nikipiga katika kusafirisha macho yangu nilijigundua nina sifa kubwa sana ya kuitwa mwanamke mrembo tena mwenye kumtia hamu ya mapenzi mwanaume rijali.
Umbile langu kwa mimi mwenyewe kama ningekuwa mwanaume na kukutana na mwanamke mwenye umbile kama langu ningemganda kama ruba, lakini kwangu ilikuwa na tofauti kubwa sana. Baada ya kujigundua sina kasoro mwilini nilijikuta nikilia huku nikisema kwa sauti ya chini.

“Hali hii mpaka lini?”
”Hali ipi?” Sauti ya Bi Shuu iliuliza nyuma yangu ilionesha Bi Shuu alikuwa ameingia kitambo bila mwenyewe kujua. Niligeuka na kwenda kujitupa kifuani kwake huku nikilia kwa uchungu.

“Vipi tena mwali?”

“Bi Shuu huu mkosi.”

“Wa nini?”

“Na Mateja kanimwaga.”

“Kwa nini unasema hivyo?” Nilimweleza yaliyotokea ofisini huku nikilia.

“Ulimwambia namwita?”

“Amesema atakuja wikiend.”

“Basi kazi hiyo niachie mimi.”

“Siamini kama atakusikiliza.”

“Ngoja aje, nitajua mbichi na mbivu.”

“Mmh, sina matumaini.”

“Hebu kaoge nikupe michapo.”

Nilikwenda kuoga ili nipate michapo ya Bi Shuu ambaye alinihakikishia kunipigania mpaka mwisho.

Nini kitaendelea? Tukutane wiki ijayo.

Mwisho wa wiki Mateja alikuja kuonana na Bi Shuu, alipofika waliingia kwa Bi Shuu. Nilikuwa na hamu ya kusikia alitaka kumuuliza nini juu yangu, nilijitahi kusikiliza dirisha la sebuleni la Bi Shuu lakini sauti walizokuwa wakizungumza zilikuwa za chini sikuweza kusikiliza waliyokuwa wakizungumza japo kuna muda nilisikia Mateja akisema.

“Ilikuwa vigumu kuja kuyasema haya kwako, kwa vile mpaka anafikia umri alionao niliamini ni vigumu kubadilika.”

“Mmh kama ni hivyo nina kazi nzito, naomba unipe muda vinaonesha chukuchuku havijaungwa.”

“Hapana Bi Shuu nakuheshimu sana, lakini tumechelewa ungeniita mapema tungeweza kulipatia ufumbuzi. Sasa hivi nipo katika mipango ya harusi na kila kitu kipo katika hatua za mwisho,” kauli ile ilinikata maini.

“Mmh, sawa nimekuelewa.”

“Basi bibie wacha nikuache tutaonana,” nilimsikia Mateja akiaga ili aondoke.

“Lakini naomba usimfukuze kazi mjukuu wangu.”

“Bi Shuu suala la kazi haliingiliani na mapenzi, sitamgusa katika kazi hilo usihofu.”

“Kama ni hivyo nashukuru, lakini Manka kapoteza dume la haja.”

“Kila kitu mipango ya Mungu.”

Nilimshuhudia Mateja akihesabu nyekundu tano na kumpatia Bi Shuu ambaye alishukuru nusra amlambe viguu Mateja kwa pesa aliyompa.
“Asante bwana yangu,” Bi Shuu alishukuru.

“Kawaida Bi Shuu ukiwa na shida mtume Manka usiogope.”

Mateja aliaga ili aondoke, nilitoka haraka dirishani kwa Bi Shuu na kukimbilia chumbani haraka. Nilijikuta nikiangua kilio kutokana na niliyoyasikia nusu kwa Bi Shuu, niliamini nilikuwa nimechelewa kuyasikia ya mwanzo kuhusu tatizo langu.

Niliamini kosa lilikuwa langu nilitakiwa nimueleze mapema Bi Shuu kuhusiana na mabadiliko ya Mateja. Kwa kauli ya Mateja kama ningewahi ningeweza kulikoa penzi langu. Nikiwa nimejiinamia kitandani nilikia nilishtushwa na mlango kugongwa.

Nilijua ni Bi Shuu ambaye hakutakiwa kugonga, lakini sikutaka kumlazimisha nilipaza sauti yangu ya kilio.

“Ingia mlango upo wazi.”

Mlango ulifunguliwa macho yangu yalimshuhudia Mteja akiingia ndani mwangu baada ya miezi sita toka alipokata mawasiliano na mimi. Alikuwa wa kwanza kuniuliza baada ya kukutana na michirizi ya machozi kwenye mashavu yangu.

“Vipi Manka unaumwa?”

“Ndiyo,” nilidanganya kwa vile sikuwa na cha kumwambia.

“Nini tena?”

“Kichwa.”

“Ooh, pole sana, umemeza dawa?”

“Bado.”

“Basi nyanyuka nikupeleke hospital.”

“Kitapoa tu.”

“Basi kama utazidiwa utakwenda hospitali.”

Mateja alisema huku akinisogelea mkononi alikuwa ameshikilia pochi na kunikabidhi elfu hamsini huku akisema.

“Kama utazidiwa zitakusaidia kwenda hospital.”

Nilitaka kuzikataa zile pesa kwa vile shida yangu haikuwa pesa bali yeye mwenyewe. Nilitaka kumuuliza tatizo langu nini lakini niliamini nilikuwa nimechelewa nilitakiwa kuuliza mapema na si muda ule ambao alinionesha mpenzi wake mbele ya macho yangu.

Nilipokea zile pesa Mateja aligeuka na kuondoka akiniacha nilikilia kilio cha kwikwi, baada ya kuondoka Bi Shuu aliingia na kunisimamia kama jini la kutumwa mkono kiunoni.

“Manka kwenu hakuna unyago?” Lilikuwa swali la kwanza bila kujali kilio changu.

“Unyago! Ndio nini?”

“Mafunzo ya msichana kujitambua na jinsi ya kumridhisha mwanaume kitabia na kimapenzi?”

“Sikuwahi kuyasikia.”

“Mmh, ndiyo maana.”

“Una maana gani kusema hivyo?”

“Umepoteza wapenzi kwa kutojua mwanamke anatakiwa kumridhisha vipi mwanaume.”
“Kwani kuna kitu gani amekueleza Mateja?”

“Tutazungumza na kulifanyia kazi.”

Baada ya kusema vile alitoka na kuniacha na mawazo kibao juu ya maswali yake na kitu alichoambiwa na Mateja. Nilijiuliza kutopata mafunzo ya usichana yanahusiana vipi na kukataliwa na wanaume. Nilijikuta nikijizoazoa hadi kwa Bi Shuu kutaka kujua Mateja kamwambia nini.

Nilipofika nilimkuta akizurudia kuzihesabu pesa alizopewa na Mateja, aliponiona aliziweka pembeni na kunitupia macho.

“Mmh, mwali una jipya gani?”

“Bi Shuu naomba unieleze ulichopelezwa na Mateja juu yangu?”

“Nitakueleza kwa vitendo si la maneno.”

“Matendo! Una maana gani?”

“Nimepata sababu ya wewe kukorofishana na wanaume, inaonesha wazi hukupitia mafunzo ya usichana. Nina kazi na wewe, mi ndo Bi Shuu bwana kila mwali aliyepitia mikononi mwangu kila aliyeonja hakutema. Najua wanakutema kwa vile unawalisha vya chukuchuku.”

“Vya chukuchuku! Una maana gani?”

“Utajua baada ya kuviunga kisha uwaonjeshe kama hukuolewa narudi kijijini kwetu japo toka nitoke kwetu kumebakia magofu. Lakini nakuhakikishia nakutia mikononi mwangu halafu nisikie, eti bwana bwana kaniacha,” Bi Shuu alishikilia pua na kusemea puani.

“Nakwambia najua kuviunga vya chunguni mpaka vya mwilini, wala hujachelewa sasa hivi mtu akigusa amenasa.”

“Utafanyaje?”

“Nataka uombe likizo ya mwezi mmoja tena nitakuombea mimi kwa Mateja ili niviunge viwe vitamu.”

“Vitamu! Vipi hivyo?”

“Nataka ukiguswa usisimke, ujue mwiko upo katika chungu au upo juu ya mfuniko, kumpa mwanaume mpaka asuse. Usilale kama gogo uoneshe basi upo safarini na si kukapua macho kama kibaka akimvizia mtu.”

“Mmh, mbona umeniacha njia panda.”

“Leo nataka kumbadili Mchaga awe kama Mmakonde.”

Mmh, kila alilozungumza kwangu lilikuwa geni, nilisubiri niungwe ili niwe mtamu kwa mwanaume.

Niliendelea na kazi yangu huku moyo ukiniuma kulipoteza penzi la Mateja, na mpenzi wake kutaka sifa kila muda wa chakula cha mchana lazima ampitie na wakitoka walikumbatiana na kuzidi kuniumiza. Lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kukubali matokeo.

Wiki moja baadaye Bi Shuu alinituma nimwite Mateja, kama kawaida nilimfikishia ujumbe wake, naye hakuwa na hiyana alikubali wito. Ilikuwa ajabu katikati ya wiki Mateja kukubali kwenda kumsikiliza Bi Shuu, tena aliniomba nikitoka kazini niongozane nae.

Baada ya muda wa kazi niliongozana na Mateja hadi nyumbani, tulipofika aliingia kwa Bi Shuu na kuniacha nikiingia chumbani kwangu. Nilijikuta nikijawa na mawazo juu ya wito ule Bi Shuu alikuwa na kitu gani ambacho alichomuitia Mateja.

Niliamini kabisa kama kutaka kumrudisha kwangu itakuwa ngumu kutokana na kila kitu kujionesha juu ya Mateja na mpenzi wake mpya. Nilipofika ndani hata hamu ya kuvua nguo iliniisha na kujikuta nikitoka na kujipitisha jirishani ili nisikie alichoitiwa na Bi Shuu.
Lakini sauti ya Bi Shuu ilinishtua kwa kuniita, moyo ulinishtuka kutaka kujua naitiwa nini? Niliingia sebuleni na kumkuta Mateja amekaa kwenye kochi akiwa ametulia. Bi Shuu aliponiona aliniambia.

“Manka kwenye friji yako kuna soda?”

“Mmh, jana nilimalizia nilikuwa na mpango wa kuweka leo.”

“Basi nifuatie dukani.”

“Bi Shuu si lazima achana nayo,” Mateja aliingilia kati.

“Hapana babu lazima unywe soda.”

Siku zote Mateja hakuwa na makuu alimkubalia Bi Shuu, baada ya kupewa pesa nilipitia chupa na kwenda dukani haraka ili niwahi mazungumzo yao.

Nilipofika dukani nusra nipasuke kwa hasira baada ya kukuta wateja wengi kwenye duka la Mpemba. Sikutaka kusubiri nilikimbilia kwenye grosary iliyokuwa mbali kidogo. Nilinunua soda haraka haraka na kurudi hadi karibu na nyumba na kuanza kunyata hadi dirishani ili nisikilize wanazungumza nini.

Nilipofika dirishani nilimsikia Mateja akisema.

“Hakuna tatizo Bi Shuu kila kitu kitakwenda kama unavyotaka.”

“Kama hivyo nitashukuru.”

Baada ya mazungumzo yale palipita ukimya mfupi huku sauti za nyayo zikielekea mlangoni, nilichepua mwendo hadi mlangoni na kukutana uso kwa uso na Bi Shuu.

“Vipi mwali mbona umechelewa?”

“Dukani kwa Mpemba kumejaa watu ilibidi nisogee mbele kwenye grosary.”

Bi Shuu aliipokea soda na kuingia nayo ndani, nilibakia mlangoni nikijiuliza niingie au niende chumbani kwangu. Kupata jibu la nifanye nini lilinifanya nisimame kwa muda pembeni ya mlango. Kabla sijapata jibu nilishtushwa na sauti ya Mateja.

“Manka kumbe upo hapa?”

“Ndi..ndi..yo,” maskini nilipata kugugumizi cha ghafla.

“Wacha niondoke zangu.”

“Haya, karibu,” nilijibu kwa aibu huku nikiangalia chini.

Mateja kweli alinichoka bila kuongeza neno alinitipa na kuelekea kwenye gari lake, Bi Shuu alimsindikiza mpaka kwenye gari. Nilibakia nikimsindikiza kwa macho.

Baada ya Mateja kuondoka Bi Shuu alirejea, alipofika alinishangaa kunikuta nimetawaliwa na simanzi usoni mwangu.

“Vipi mwali?”

“Aah, kawaida tu.”

“Acha kujitia ukiwa, kila kitu kina wakati wake na wakati ndio unakuja.”

“Kwani Mateja kasemaje?”

“Aseme nini?”

“Kwa hiyo amekubali?”
“Akubali nini?”

“Kwani ulimuitia nini?”

“Kuhusu likizo yako.”

“Kasemaje?”

“Amekubali.”

“Naanza lini?”

“Sijajua lakini amekubali.”

“Mmh, haya.”

Niliachana na Bi Shuu na kwenda chumbani kwangu kujiandaa na kujimwagia maji ili nipumzike.

*********

Siku ya pili nikiwa ofisini niliitwa na Mateja kunitaarifu kukubaliwa likizo yangu ambayo ingeanza wiki itakayofuata kwa kukamilisha kazi zangu zote muhimu. Nilipewa pesa ya likizo na kujiandaa kwenda kwenye unyago wa kiutu uzima ili niugwe niwe mtamu mwanaume akigusa anate.

Baada ya kumalizia kazi za ofisi kwa wiki niliyopewa, niliruhusiwa kurudi nyumbani kuanza likizo. Nilirudi nyumbani na kumkuta Bi Shuu ambaye kabla ya kuweka makalio chini aliniuliza.

“Mmh, umepewa likizo?”

“Nimepewa.”

“Basi kazi yote niachie mimi.”

Siku ile nilipumzika bila kugusiwa kitu chochote, lakini alfajiri niliamshwa na kupelekwa kuogeshwa maji baridi kisha nilifungwa upande wa kanga bila nguo ingine ndani. Aliniongoza hadi katika chumba kimoja cha ndani kilichokuwa kitupu.

Chini kwenye sakafu kulikuwa na maji kuonesha amemwagwa, baada ya kuingizwa mule ndani wakati huo kibaridi kilikuwa kikinichanyata. Bi Shuu alifunga mlango kwa nje na kuniacha nimesimama nikijiuliza ameleta mule ndani nifanye nini? Ajabu muda ulikatika nikiwa nimesimama, miguu ilichoka na kujiuliza mbona harudi ameniweka mule ndani ili iwe nini.

Kukaa chini nilishindwa kutokana chini kuwa na maji na muda ule ubaridi kilikuwa kikali sana. Niliposhika mlango ulikuwa umefungwa kwa nje nilijaribu kuita kwani nilikuwa nimechoka kusimama zaidi ya saa moja. Hakukuwa na jibu la mtu yoyote.

Nilijawa na mawazo juu ya kuwekwa chenye chumba chenye maji kisha kusimamishwa kwa muda mrefu. Nilijiuliza unyago wenyewe kama ndio ule kwangu niliamini nitashindwa. Niliamua kukaa kwenye maji huku kibaridi kikizidi kunichonyota, kutokana na uchovu nilijiegemeza kwenye ukuta na usingizi ulinipitia.

Nilishtushwa na maji ya baridi niliyomwagiwa ndoo nzima, Bi Shuu alikuwa mbele yangu akiwa amekunja uso kwa hasira na kunifokea kwa sauti ya juu.

“Haya ndiyo yanakufanya ukose wanaume kila kukicha, mwanamke mvivu kama nini, kukuacha muda mfupi umeshindwa kuvumilia na kuuchapa usingizi kwenye maji.”

“Samahani Bi Shuu.”

“Haya fanya usafi haraka,” alisema huku akinitupia tambara kukausha maji.

Nilichukua tambara na kuanza kufanya usafi kwa kukamilia maji kwenye ndoo mpaka nilipokausha, Bi Shuu alirudi na mkeka ambao aliutandika kisha alitoka na kurudi na chai. Tulikunywa chai kisha aliniacha nipumzike kwa kuniacha na kipande cha kanga tu.
Jioni ilipofika Bi Shuu aliingia ndani na kuniketisha kitako na kuanza kuniuliza maswali.

“Manka kitu gani wakati wa mapenzi hukipendi?”

“Mmh, vingi lakini tabia ya wanaume kunisumbua wakati wa kilimo huna sikupendi.”

“Mmh, kingine?”

“Ni hilo hilo tu.”

“Nimekuelewa, kuna vitu vingi vya kike vimekupita kushoto, siku hizi wanaume hawapendi mwanamke anayelala kama gogo, husisimki wala hutingishiki.”

“Bi Shuu nitikisike vipi au nisisimke vipi?”

“Ndiyo maana leo umo humu ndani, ukitoka utajua unasisimka vipi na unatikisika vipi?”

“Mmh, haya.”

Mmh, hukuwepo ila malaika wako alikuwepo, sikujua alichonipa Bi Shuu kilikuwa adhabu au mateso. Niliwekwa mikao ambayo haikuwa tofauti na ile niliyokuwa nikiwakatalia wanaume, kila nilipotegea nilitandikwa bakora ya mgongo iliyotua sawia kwenye mgongo mtupu.

Kila siku nilikuwa nikifanyishwa mazoezi yagumu ya viungo ambayo yalikuwa mateso mazito, kuna kipindi nilifikiria kumwambia bora aniache nilivyo kuliko mateso yale. Lakini Bi Shuu alikuwa mkali kama pilipili hakutaka mchezo hata kidogo hata nilipochoka bado alinilazimisha huku akisema.

“Kushinda kuchoka ndiyo siri ya kumkata kiu mwanaume.”

Nilibebeshwa mzigo kichwani nikiwa mtupu na kuanza kuchomwa na sindano kiunoni kitu kilichinifanya nishtuke kwa kuchezesha kiuno. Haikuishia hapo nililazwa chini na kubebesha mzigo kiunoni na kuendelea kuchomwa na kitu cha ncha ambacho kilinifanya nijinyonge nyonge bila kupenda.

Niliendelea na mazoezi makali chini ya kungwi wangu Bi Shuu huku akinipa mbinu nyingi za kumchanganya kimapenzi mwanaume. Kuna mambo mengine siwezi kuyasema gazetini lakini Bi Shuu koma. Toka nizaliwe sikuwahi kukutana na mwanamke Shankupe kama yeye.

Mtoto wa kike nilifundishwa maneno ya kusema mtu akiwa juu ya mnazi wangu, pumzi za kutoa wakati mwiko upo ndani ya chungu na akianza kugeuza maini nilitakiwa nilegee vipi huku macho na pumzi nizifanye vipi. Najua mwenzangu mie mwenye viuno kama vimefungwa mbao na wakati wa mapishi unatulia unasubiri mtu amwage mzigo akimaliza anyanyuke. Lakini ukikutana na bibi huyu lazima bwana akutaje jina.

Mwezi mmoja mtoto wa kike nilipikwa nikapikika, baada ya mafunzo mazito Bi Shuu kwa ushambenga wake alinitafutia mwanaume ili kutaka kunipima baada ya mazoezi. Sikukataa kwa vile nilijua kile ndicho kipimo, mtoto wa kike nilijiandaa kuonesha kilichoniweka ndani kwa mwezi mzima. Cha ajabu Bi Shuu alitaka mchezo ule nichezee chumbani kwake, mmh, makubwa madogo yana nafuu.

Sikutaka kumbishia kwa vile nilikuwa na usongo na mafunzo ya Bi Shuu ambayo yalinifanya nijiamini na kumtamani mwanaume nimtoe kamasi nyembamba. Baada ya kijana aliyechaguliwa na Bi Shuu kufika alikaribishwa chumbani kwa Bi Shuu, nilijikuta nikiwa na usongo na yule kijana ambaye alikuwa mmoja wa vijana walioninanga sijui kucheza nilipokutana naye siku ya kwanza.

Baada ya kuingia ndani nilimpokea juu juu na kumtoa nguo maungoni kama kuku aliyechinjwa na kunyonyolewa manyoya. Baada ya kumuandaa mtoto wa kike huku mwili ukinisisimka baada ya kukiona kijiti cha kupokezana kwenye mbio fupi.

Mtoto wa kike nikiwa nataka kufanya mtihani wangu wa kwanza kwa umakini mkubwa huku nikipitia hatua moja baada ya nyingine. Nilimlamba mwili mzima kama mama mbuzi akimsafisha mwanaye baada ya kumzaa, nilijua kutumia ulimi wangu.

Nilipofika kwenye shina la mnazi mtoto wa kike nilitulia kwa muda huku vidole laini na ulimi ukifanya kazi yake. Mara nilimuona kijana wa watu akitetemeka kama amekunywa coka ‘ngriiiiiiiiii’, maskini kumbe alikuwa akilia chozi lisilo na msiba.
Kijana wa watu naye akabadili upepo na kunirudishia mashambulizi.

Mtoto wa kike nilipoguswa nililegea na kuzitoa pumzi huku jicho likipoteza kiini cheusi. Kwa mara ya kwanza niligundua kumbe mwili kila sehemu una raha yake kuishinda nyingine. Kama nilivyofundishwa na Bi Shuu kila nilipoguswa nilisema neno lake.

Baada ya mshike mshike wa maandalizi cha chakula, hatimaye kiliiva na kutengwa mezani. Nilimpokea juujuu huku nilionesha jinsi gani mtoto wa kike nilivyoshikika, mtoto wa kike sikuwa na haraka nilifuata mwiko ulivyogeuza maini ili kumfanya mpigaji na mwimbaji wasitofautiane.

Mtoto wa kike nilimaliza maneno yote mdomoni, sikuamini kutatalika kama bisi kwenye chungu cha moto. Mpaka mchezo unakwisha nilikuwa nipo hoi kwani niliamini vilikuwa vitamu kijana wa watu kila alipomaliza alileta sahani aongezewe. Nami nilimpakulia naye alijilia huku akigugumia kama dume la njiwa lenye wivu. Huku nikilia mara nne kwa utamu wa msiba.

Lazima niseme ukweli kuna kipindi nilitaka kunyanyua mikono, maji yalikuwa shingoni, nyonga iligoma kutokana na kutokuwa na uzoefu wa kuyakata mawimbi.

Bi Shuu alinieleza kumfurahisha mwanaume si nyonga tu, hata kujua kuyapangilia maneno hasa kumsifia hakuna mwanaume kama yeye pia anajua kumshikisha punda adabu kwa kumtandika bakora balabala. Baada ya nyonga kugoma na kukiona kiuno kikiwaka moto, nilitumia sauti kumsindikiza mwenzangu mpaka alipofika juu ya mnazi.

Kijana wa watu hakuamini ilibidi aniulize.

“Manka, kumbe mambo unayaweza mbona ulikuwa uninikatili, mambo haya ungenipa tokea zamani sasa hivi ungekuwa mke wangu.”

“Nilikulisha vya chukuchuku lakini sasa vimeungwa ndio maana unaviona vitamu.”

Kijana wa watu bila kutegemea alinipa elfu 50 kama asante ya kumpa penzi tamu ambalo alikiri hakuwahi kulipata kwa mwanaume yoyote. Baada ya kuondoka na kuniacha nimejilaza baada ya kuhisi uchovu kila kona ya mwili kutokana na mshike mshike wa kufanya majaribio ya vitendo. Bila ya kujigeuza usingizi mzito ulinipitia juu ya kitanda cha Bi Shuu.

Nilishtuka baada ya masaa matatu nikiwa nausikia mwili mchovu kila kona, Bi Shuu aliniamsha na kukuta ameniandalia maji ya kuoga. Nilioga kupunza uchovu na kurudi ndani ambako chakula kilikuwa tayari. Tulikula pamoja kisha tulipumzika sebuleni, cha ajabu niligundua Bi Shuu akiniangalia kwa kuniibia kitu kilichonifanya nimuulize.

“Bi Shuu vipi?”

“Kuhusu nini?”

“Naona kama unanivizia kunitazama kuna nini si uniambie.”

“Mmh, kweli ulikuwa na usongo.”

“Wa nini Bi Shuu?”

“Kazi umeifanya vizuri japo kuna kipindi ulichemsha.”

“Ulijuaje?”

“Nilikuwepo muda wote toka unaanza mpaka unamaliza, kwenye maandalizi nakupa mia kwenye sauti na pumzi sabini kwenye mchezo wenyewe hamsini.”

“Jamani Bi Shuu kujitahidi kote unanipa hamsini.”

“Manka kwanza nashangaa mtu ulikuwa hujui lolote umeweza kupata hamsini wengi huwa chini ya hapo.”

“Bi Shuu kama nina hamsini nimeweza kupewa zawadi nikipata mia itakuwaje?”

“Mia kupata ni kazi kwa vile maungo yako yalikakamaa muda mrefu lakini utaweza kufika hata sabini kwa bidii yako.”
“Mapungufu yangu ni nini?”

“Kutumia nguvu nyingi ambazo hukufanya upumue kwa kasi sana kitu kinachokufanya uchoke sana, pia papala ya kukata nyonga. Mwanzo uliweza kwenda sawa lakini ulipoanza kuchoka alifanya bora liende. Lakini mwanzo ni mzuri.

Kwa uwezo wako huo na kuonesha ulikuwa makini kwa kuyashika mafunzo, inaonesha nikikuongezea matirio kama kwenye mpira ni ujanja wa kuweza kumsoma mwanaume. Kila mwanaume ana amambile tofauti na mwenzake na wengine wana nguvu kama kirafu unatakiwa kufanya nini.”

“Bi Shuu nitashukuru nimeteseka sana, kwa nini sikuyapata mafunzo haya mapema ili kuweza kumdhibiti Mateja,” Nilijikuta nikidondosha chozi kulikumbuka penzi la Mateja nililolipoteza kutokana na kutokujua sheria za kitandani na kunifanya niendeshe ovyo na kusababisha ajali za kutoelewa alama za kitandani.

“Manka usiwe kama kipofu aliyefumbua macho na kumuona chura na kuamini hakuna kama chura chini ya jua, mbona kuwa wanaume zaidi ya Mateja”

“Bi Shuu ni kweli usemayo lakini Mateja niliamini ni mwanaume sahihi kwangu.”

“Ni kweli, lakini kisicho riziki hakiliki we jipange ukikolea utamu nakuhakikishia nitakutafutia bwana Mateja cha mtoto. Kwanza nataka niyafanyie kazi makosa madogo madogo ambayo yatakufanya kila atakaye gusa atangaze ndoa. Nataka umlize mwanaume kama mtoto mdogo, umeisha ona mtoto akinyang’anywa ziwa jinsi anavyolia?”

“Ndiyo.”

“Basi nataka mwanaume chozi limtoke, kuna vitu vidogo wanawake hawajui, vitu hivyo ukimfanyia mwanaume kama ameoa lazima aitelekeze nyumba yake. Mchele mmoja lakini unatofautiana katika mapishi, hii nyumba jasho la mwili wangu pale nilipompata mume wa mtu. Leo hii naishi kwangu nawe nataka uwe mara mbili yangu.”

“Bi Shuu mbona wasichana hatuna vitu hivi?”

“Siku hizi uzungu umetawala na kujikuta wakipoteza vitu vingi vya kumfurahisha mwanaume. Kumfurahisha mwanaume kitandani si kigezo pekee cha kuilinda nyumba yako. Kuna vitu vingi ambavyo vipo nje ya kitanda.

“Kuna wasichana wengi wana nyonga laini kama unakula keki lakini wana mapungufu kama chujui la nazi ambayo hayawezi kumfanya atulie kwa kwenye ndoa yake. Kama tabia yako nzuri ulichanganya na machejo ya kitandani hata utakita hata ndege utanunuliwa japo mwenzio hana uwezo wa kununua baskeri.”

“Mbona hujanifunda na hivyo?”

“Siwezi kukuichanganya kimoja kimoja, kwanza tunatengeneza mtego akiingia anase, ukimaliza mafunzo ya mwili tunarudi tena kilingeni ili mumeo aone tofauti ya magumegume na mwanamke.”

“Bi Shuu mbona nimechoka sana.”

“Umelia mara ngapi?”

“Mara nne.”
“Mara ya mwisho ulilia mara ngapi ulipokutana na mwanaume kabla ya leo?”
“Mara mbili sijawahi kulia zaidi ya hapo.”
“Ndio maana, lazima uchoke umeukamua mwili sana na shughuli haikuwa ya kitoto kuna kipindi kidogo nisimamishe mpambano mlikuwa kama mnataka kutoana roho.”
“Bi Shuu umejuaje?”
“Nikuambie mara ngapi nilikuwa nafuatilia toka mwanzo mpaka mnamaliza”
“Jamani Bi Shuu kumbe ulikuwa unanipiga chabo,” Mbona niliona aibu mtoto wa kike, jamani bibi huyu ana mambo kumbe mwenzie nahenyeka yeye anapiga chabo.
“Sasa ningejuaje mapungufu yako.”
“Mmh, makubwa madogo yana nafuu.”
“Na hayo mengine lini maana muda wa kurudi kazini umekaribia.”
“Wiki iliyobakia inatosha, kapumzike jioni kama kawa mpaka kieleweke.”
“Wacha nikalale naona mwili sio wangu, kwenye pesa hiyo chukua nusu niachie nusu”
“Asante mwali, nina imani sasa umeamini nilichokisema kinatimia”
“Wee mwisho Bi Shuu je, ungenikamata ndio unavunja ungo naona kila aliyenionja angeniganda kama ruba.”
Baada ya mazungumzo nilimuomba Bi Shuu nikapumzike mwili ulikuwa na uchovu, nilikwenda chumbani kwangu kulala kwa kulifungulia feni mpaka mwisho mtoto wa kike nilijiachia kitanda kizima.
*******
Kama kawaida Bi Shuu aliniamsha kwenye chakula cha mchana na baada ya chakula cha mchana nilioga na kupanda tena kitandani. Sikuamini mwili kuchoka kiasi kile, Bi Shuu alinieleza ni kutokana na kuzoea kulala kama gogo kitandani lakini siku ile niliushughulisha mwili hata kumwaga machozi manne kitu ambacho hakikuwa kawaida yangu.
Nilipogusa kitandani usingizi haukuchelewa kunichukua, Bi Shuu aliniamsha saa mbili za usiku nilikwenda kuoga kisha nilipata chakula cha usiku. Baada ya chakula nilipumzika kidogo na kuingizwa unyagoni kumalizia muda ulipobakia kwa kunipa mbinu za kummiliki mwanaume kwa sauti na matendo huku tabia ikiwa ndiyo uliyochukua sehemu kubwa.
Katika mafunzo siku moja alinipa nipike chakula baada ya kupika tulikula wote, kesho yake alinipa nipike tena chakula kilekile, lakini hakunipa chumvi. Nilipomuuliza alisema nipike vile vile na muda wa kula nilishindwa kumuelewa baada ya kunieleza nipakue, nilipakua na kukila bila chumvi. Tulikula wote bila kujua chakula kile kwa nini tulikila bila chimvi.
Sikutaka kumuuliza kwa vile hakikuwa kingi tulikuwa na kukimaliza wote. Baada ya chakula usiku Bi Shuu akiwa ameniweka chini aliniuliza.
“Manka kuna tofauti gani ya chakula ulichopika jana na leo?”
“Tofauti yake cha jana kina chomvi lakini cha leo hakina chimvi.”
“Kipi chakula kizuri?”
“Cha jana.”
“Kwa sababu gani?”
“kina chumvi lakini cha leo hakina chimvi.”
“Mbona umekila.”
“Nilishindwa kuelewa ulikuwa na maana gani.”
“Lakini bila hivyo usingekula?”
“Nisingekula.”
“Unajua nilikuwa nina maana gani?”
“Hata sijui”
“Hii nakuonesha yaisha ya ndani ya ndoa, wanawake wengi wanawalisha wanaume chakula kisicho na chumvi. Wapo wanaokosa uvumilivu huvunja ndoa lakini wanaoburuzwa na mapenzi hula chakula kisicho na chumvi kila siku na kuishia kunung’unika moyoni.”
“Lakini Bi Shuu kama mkewe hamuwekei chumvi anashindwa vipi kuchukua mwenyewe kuweka kwenye chakula”
“Swadakta swali zuri, ndio maana kukuweka huku ndani vitu vingi huvifanya kwa mafumbo jibu lake huwa ndio maisha yako ndani ya mahusiano yako. Chakula na chumvi sikuwa na maana hiyo bali kukueleza matatizo ndani ya nyumba nyingi wanawake wengi ndoa zao uziondoa chumvi bila wao wenyewe kujua”
“Kivipi?”
“Nyumba nyingi mwanzo wa mapenzi huwa moto moto kama kumpokea mpenzio akirudi kumtengea chakula kula pamoja kuoga pamoja kuwa karibu yake kumpoza uchovu wa kutwa nzima ambao ndiyo tiba ya mwanaume kutoitafuta faraja nje ya ndoa yake.
“Wengi baada ya muda baadhi ya vitu hundoka kabisa na ndoa kuendeshwa kimazoea, moyoni lazima utasema hivi nisivyofanya kuna nini kwani hawezi kufanya mwenyewe. Kuacha kuyafanya hayo ni sawa kuondoa chumvi kwenye mahusiano yako na kumfanya mpenzio kula chakula kisicho na chumvi.
“Wengi huvumilia na kuumia moyoni lakini wasio na uvumilivu huitafuta chumvi hiyo nje ya ndoa. Hapo ndipo tatizo linapoanza na kuipoteza ndoa yako bila kujua tatizo ni wewe mwenyewe. Kuondoa baadhi ya vitu ndani ya ndoa yako kama kutompokea mumeo au kutokula na kuoga pamoja ni vitu vinavyo mwanaume huona vya kawaida lakini ni ufa mkubwa katika ndoa.
“Penzi halizeeki bali mwili ndio unazeeka, vyote nilivyokueleza usikipunguze hata kimoja ukiingia katika ndoa yako. Nakuhakikishia bwana atakaye kuoa watu watasema umemuwekea libwata, limbwata mwali ni kumlea mumeo kama mtoto. Nina imani umenielewa”
“Mmh, kweli nimekubali Mungu kakujalia kumtengeneza mwanamke, nina imani ungenieleza kwa maneno ningekuelewa nusu lakini kwa vitendo nimekuelewa zaidi. Asante Bi Shuu”
“Nashukuru kuonesha ni muelewa na mtu mwenye usongo na mafunzo”
“Lazima Bi Shuu niwe na usongo nimeteseka sana”
Nilimalizia mafunzo huku akilekebisha mapungufu aliyoyaona kwenye mtihani wangu wa kwanza.”
Nilikuwa sijawahi kula kungu mtoto wa kike nilikula kungu jicho ukiniangalia utanionea huruma. Nilimaliza mafunzo salama, kabla ya kuanza kazi alinitafutia tena mwanaume mwingine naye alikuwa mmoja wa wale walioninanga mwanzo.
Nilikuwa na imani alikuja akijua ni yule Manka wa mwaga msigo babangu kisha uondoke. Mafunzo niliyopata ya mwisho mtoto wa kiume chozi lilimtoka, kwenye maandalizi tu alilia zaidi ya mara tatu. Mtindo huu nilifundishwa kama sitaki kutumika sana kwanza namchosha mwanaume mwenye maandalizi.
Hata ulipoingia baharini nusra anifie maji baada ya kushikwa na pumu katikati ya safari, machejo yalimfanya aifukuze Land Curuser VX kwa bajaj. Ilibidi niingie kazi ya kumpepea asinifie, baada ya kurudi katika hali yake ya kawaida aliniangalia mara mbili.
“Ni wewe Manka au naota”
“Kwani vipi?”
“Hata siamini, kumbe ulikuwa unafanya makusudi”
“Ulikuwa vya chukuchuku sasa vimeungwa”
”Una maana gani?”
“Si umeona mwenyewe si la kusimuliwa”
“Nimekubali lazima nirudie”
”Mmh, cha kunifia kifuani hapa namefungulia injini moja katika injini nne si ungebadilika jina.”
“Manka naomba nikuoe.”
“Ni haraka sana vuta subra”
“Lakini niwe mmoja wa watu wa mbele kufikiriwa.”
“Hakuna tatizo”
Yule kijana ambaye alikuwa kama mlevi aliniachia laki moja ya asante”
Baada ya kuondoka Bi Shuu kama kawaida yake alitoa tathimini yake.
“Mwali japo mpinzani wako hakuonesha upinzani lakini umejitahidi sana tena sana, sasa nina uwezo wa kukueleza kapambane na mtu yoyote. La muhimu kuzingatia niliyokueleza hakika kila atakayehusa lazima anate sasa hivi mwili wako ni asali yenye ulimbo”
Maneno ya Bi Shuu yalinifanya nijiamini nimeanza kuiva kimapigano, kwa vile muda ulikuwa umekwisha jumatatu ilipofika nililipoti kazini kwangu. Nilimkuta aliyekuwa amenishikia, baada ya kunipokea alinielekeza kazi za kufanya na yeye kuendelea na majukumu mengine. Kuna kitu kimoja nilisahau kukueleza baada ya kukaa ndani kuchezwa nilipotoka nilitakata na kunawili mtoto wa kike.
Nikiwa naendelea na kazi bosi wangu dear zilipendwa aliingia ofisini, ilionesha hakujua kama naanza kazi siku ile. Alipofika hakuniangalia alinisalimia.
“Za saizi?”
“Nzuri”
“Ile kazi tayari?”
“Ndiyo namalizia”
’Baada ya muda gani”
”Dakika kumi”
“Ok, fanya haraka.”
Baada ya kusema vile aliingia ofisini kwake, ilionesha hakujua kama nipo mimi. Baada ya kumaliza kazi niliyoikuta niliprinti na kumpelekea, alikuwa bado ameinama nilipofika mbele yake nilisema.
“Bosi kazi tayari”
Sauti yangu ilimshtua na kunyanyua macho, kwa mshangao wa ajabu alisema.
“Ha! Manka umekuja saa ngapi?”
“Toka asubuhi”
“Ina maana nimekupita kwenye ofisi yako?”
“Ndiyo bosi”
“Ooh, samahani sana”
“Kawaida tu bosi wala usijisikie vibaya,” mtoto wa kike nilikuwa nimekwenda kimitego na kumuomba Mungu Mateja ajichanganye sijui aonje kidogo. Niliapa ningefanya aliyofundishwa na mengine nisiyo yajua ili kuhakikisha anakutana na vitu vipya katika medani ya mapenzi.
Mtoto jicho lilikuwa limelegea kidogo jicho lilionekana kwa kujipaka wanja chini na juu na kuongeza uzuri wangu. Japo nilijijua mi mzuri, lazima mzuri ujijue kabla hujasifiwa na watu, lakini mapungufu yangu Bi Shuu aliyamaliza mengi niliyokuwa nayo.
Mateja ilionekana kama kuchanganyikiwa kuniona nimebadika nimependeza na ninavutia tena kimitego ya kike hasaa.
“Manka ulikuwa unakula nini?”
“Kwa nini bosi?” nilimuuliza kwa sauti laini huku nikimchanulia tabasamu ya kufa mtu huku jicho nalo likizungumza.
“Hapana, umependeza na unavutia”
“Nashukuru kwa hilo ila moja umesahau”
“Lipi hilo?”
“Sasa hivi si Manka chukuchuku ila Manka huyu kaungwa akaungika”
“Una maana gani?”
“Bosi nitakuomba kesho nikukaribishe chakula cha usiku”
“Mmh, hakuna tatizo kwa vile wiki hii ni ya mwisho baada ya hapo nitakuwa katika maandalizi ya harusi.”
“Hakuna tatizo kazi njema.”
“Na wewe pia.”
Baada ya kumkabidhi kazi yake nilirudi kuendelea na kazi yangu, moyoni niliapa kama kweli atakubali mwaliko wangu amekwisha.Muda wa mchana Mchumba wake alimuijia kama kawaida na kwenda naye kupata chakula cha mchana.
Japo moyo uliniuma lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kukubali matokeo kutokana na makosa kuyafanya awali. Jioni niliporudi nilimueleza Bi Shuu mwaliko niliompa Mateja kuja kula chakula cha usiku.
“Mwali akiingia amekwisha, hakikisha anaisahau ndoa yake”
“Bi Shuu la kuuliza hilo”
“Nakuaminia mtu wangu.”
“Naiona kama kesho inachelewa”
“Itafika punguza munkari, usije yakakamia maji”
“Si hivyo Bi Shuu nakuhakikishia kuyafanya yote kwa umakini mkubwa labda asije.”
*****
Siku ya pili nilikwenda ofisini na kuendelea na kazi bosi alipokuja alinisalimia.
“Mrembo hujambo”
“Sijambo bosi simshindi wifi”
“Manka mbona umefika mbali salamu umeijibu sivyo”
“Samahani bosi, za nyumbani”
“Mmh, salama sijui zako.”
“Nami namshukuru Mungu, haya nipo ndani”
“Sawa bosi”
Kabla ya kuingia ofisini aligeuka na kuniuliza.
“Mwaliko wa usiku upo vile vile au kuna mabadiliko”
“Hakuna mabadiliko”
“Haya,” alisema huku akifungua mlango na kuingia ofisini kwake.
Baada ya kuingia ofisi nilibaki nilikuwa siamini kama nimesikia vizuri kuulizia mwaliko, niliona dalili njema zimeanza asubuhi jioni ni kumalizia tu. Huwezi amini siku hiyo nilifanya kazi kwa furaha ya ajabu kama Mateja amenikubali nirudiane naye.
Jioni kabla ya kuondoka aliniaga na kuniahidi angekuja usiku.
“Kweli Mateja utakuja?”
“Kama siji ningekuambia”
“Karibu sana mpe..” Mungu wangu nilitaka kujisahau kumwita mpenzi wakati tuliisha achana long time a go.
“Niite tu mpenzi wala usijisikie vibaya,”
“Hapana bosi”
“Haya baadae”
Mateja aliondoka na kuniacha nikipanga vizuri vitu vyangu kabla ya kurudi nyumbani.
*********
Nilkipofika nyumbani Bi Shuu aliniomba siku ile aandae chakula cha mgeni, sikuwa na hiyana mtoto wa kike nilimuacha afanye mambo yake. Nilikiandaa chumba changu na kukiweka katika hali ya usafi wa hali ya juu, kama kawaida Bi Shuu alinipatia mafusho ya manukato mazuri.
Baada ya kuhakikisha chumba changu kinapendeza niliingia kuoga mtoto wa kike na kujifusha utuli huku nikipaka wanja wa sina mume ambao lazima mwanaume barabarani akusalimie.
Baada ya kusimama mbele ya kioo kujitathimini, nilizidi kujisifia mtoto wa kike kwa upendeleo niliopewa na mwenyezi. Baada ya kuhakikisha nipo sawa, nilikunywa kungu na kuanza kujisikia nikisisimka mtoto wa kike kama mamba mwenye njaa.
Nikiwa nimekaa mkao wa kula kumsubiri Mateja, mara aliingia Bi Shuu na kuniongezea mambo fulani ya muhimu pindi Mateja akiingia chumbani kwangu.
“Mwali nilitaka kusahau kwa vile anajua anakuja kula chakula na kuondoka cha kufanya akiingia tu, ukimvamia kwa kumkumbatia huku akimbusu hakikisha mikono yako inafanya kazi ya haraka kumvua nguo bila kuchelewa mpatie upande wa kanga.
Wakati huo mimi nitakuwa tayari nimepeleka maji ya kuoga bafuni niliyoyawekea viungo. Nani alikuambia wanawake wa Tanga ndio wanajua mahaba, nataka Mateja akiondoka kila kitakachokuja mbele yake akione shombo.”
“Nimekuelewa Bi Shuu.”
“Sio umenielewa bahati hairudi mara mbili, itumie kubadili matokeo.”
“Matokeo ya nini Bi Shuu?”
“Ukimaliza kilicho tupotezea muda nitakwambia.”
“Nitafuata maelekezo yako.”
Baada ya kutoa maelekezo Bi Shuu alirudi kumalizia kutengeneza maajumati ya mgeni rasmi.
Majira ya saa moja na nusu gari la Mateja lilisimama mbele ya nyumba yetu, ajabu usongo wote niliokuwa nao uliyeyuka kama donge la mafuta katika kikaango cha moto. Nilijikuta nikijawa na hofu juu ya nilichokipanga kumpa Mateja kama ataingia katika mtego wangu.
Nilijihisi kupoteza ujasiri niliokuwa nao kabla ya Mateja hajaja, niliikandamiza mikono yangu kifuani na kubana pumzi na kukaa kwa muda kuvuta ujasiri kisha niliitoa na kushusha pumzi nzito.
Baada ya kujipa ujasiri nilijitengeneza haraka haraka ili kujiweka sawa japo nilikuwa nimejiweka kimitego ya kike hasa. Ndani nilivalia kufuri la bikini la rangi nyekundu juu nilivalia kanga nyepesi ukituliza macho unaona kila kitu cha ndani.
Wakati huo chumba kilikuwa kikinukia utuli kila kona mimi mwenyewe nilikuwa kama Hululaini malaika wa daraja la juu. Jicho mtoto lilikuwa lemelegea kwa kungu huku mwili ukisisimka kama nyoka mwenye hasira aliyepandisha sumu kwa ajili ya kumgonga mtu.
Wakati nikifanya matayarisho ya mwisho kabla ya kumpokea Mateja mbele ya kioo, Bi Shuu muda huo alikuwa amempokea.
“Wawooo mwanaume huyo.”
“Niambie kipenzi changu?” Sauti ya Mateja ilisikika.
“Niseme nini mkeo nawe umetupa jongoo na mti wake.”
“Bi Shuu kama ningetupa leo ningeonekana hapa?”
“Mateja kula nisishibe heri nisipewe.”
“Bi Shuu heri nusu shari kuliko shari kamili na kidogo si haba kuliko kukosa kabisa.”
“Nitakuwezea wapi mtoto wa Kisukuma aliyejifanya Mzaramo kwa kujifanya unajua kuyageuza maneno.”
“Vipi nimewakuta?” Mateja aliuliza mimi ndani kiroho paa!
“Umewakuta wamejaa tele wewe tu,” mmh, maneno ya Bi Shuu yalijaa nahau na misemo na kuzidi kuniweka njia panda.
Wakati nikijua hodi itapigwa wakati wowote nilipandisha tena pumzi na kuzishusha kisha nilijiandaa kumpokea. Mara mlango uligongwa.
“Hodi ndani?”
“Karibu,” nilimkaribisha huku nikikaa mkao wa chura kuruka.
Mara mlango ulifunguliwa na Mateja aliingia, mtoto wa kike nilijizoazoa na kumkumbatia.
“Ooh, karibu mpenzi.”
“Asante za hapa?”
“Nzuri.”
Mtoto wa kike niliutambaza mdomo wangu na kutua kwenye mdomo wa Mateja ambaye alikuwa bado amepigwa na butwaa, nikihema kama mgonjwa wa pumu. Mateja alinipokea na kubadilishana mate, mikono yangu alipata nafasi ya kumvua shati.
Baada ya kumvua shati nilimsukumia kitandani na kumlalia juu, kwa haraka nilimalizia na vilivyokuwa vimebaki chini kisha nilimpatia upande wa kanga. Kila nililolifanya siku ile kwa Mateja kilikuwa kigeni kwake niliamini alijua bado Manka wa mwaka 47 hohehahe asiyejua chochote.
Niliamini muda huo Bishuu alikuwa ameisha peleka maji yaliyochanganywa na viungo bafuni. Nilimshika mkono Mateja na kutoka naye nje kumpeleka bafuni kuoga, Bi Shuu kweli alikuwa amepania mlangoni nilikuta kuna ndala mpya. Mateja alivaa na kuongozana naye hadi bafuni.
“Karibu mpenzi uoge.”
“Asante.”
Nilimwacha Mateja bafuni na kurudi ndani kujiandaa kumlisha vilivyoungwa na Bi Shuu. Kabla sijaweka tako chini Bi Shuu aliingia bila hodi na kusema kwa sauti ya juu.
“Wee mwana, ndio unafanya nini?” Kauli ile ilinishtua sana.
Kutokana na makosa ya kuruka baadhi ya sehemu katika hadithi ya wiki iliyopita kufikia hatua ya kuwachanganya wasomaji. Leo tutaelezea kwa ufupi toka Mateja alipomuona Manka ofisini mpaka kufikia hatua ya kumsubiri chumbani. Baada ya Mateja kushtuka kumuona Manka jinsi alivyopendeza kwa muda ambao hakuwepo kazini alimsifia kuwa amependeza mara dufu. Naye Manka alitumia nafasi ile kumkaribisha Mateja chakula cha jioni kwake. Mateja alimkubalia na kumuahidi angefika jioni kwa ajili ya chakula.
Manka aliporudi nyumbani alimueleza Bi Shuu kuwa Mateja amekubali kuja kula chakula cha jioni. Bi Shuu alimueleza asiipoteze nafasi ile adimu ahakikishe kama atakubali kuvila vilivyoungwa basi achanganyikiwe. Bi Shuu alimuomba kazi ya kupika chakula aifanye yeye ya kuandaa chakula cha ujanani kwake pale alipokuwa akimtengenezea mpenzi wake.
Baada ya makubaliano na Bi Shuu Manka aliingia ndani kujiandaa kwa ajili ya kumpokea Mateja kwa kufanya usafi wa mwili na chumba huku akifusha udi na asumini kumwagia kitandani. Yalikuwa mafunzo tosha ya Bi Shuu ambayo Manka aliyafanyia kazi.
Baada ya kila kitu kuwa tayari Manka alimsubiri kwa hamu Mateja mpaka alipofika. Baada ya kumuandalia maji na kumuacha aoge peke yake ndipo Bi Shuu alipomfuata na kumuuliza amefanya nini.
Ili kujua kosa lake nina imani mpaka sasa tupo pamoja, haya tuserereke pamoja…
Kauli ya Bi Shuu ilinishtua na kujiuliza nimefanya kosa gani tena.
“Bi Shuu nimefanya nini?”
“Manka haya ndiyo makosa mnayafanya sana wanawake wengi, kwa nini umuache aoge peke yake. Nenda kaoge naye ikiwezekana anza kumliza kilio cha raha bafuni.”
Mmh, mtoto wa kike haraka nilitelemsha nguo ya ndani na kubakia na upande wa kanga nyepesi na kumuwahi Mateja kabla hajajipaka sabuni. Nilipokaribia bafuni Mateja alikohoa kumaanisha kuna mtu.
“Mm..mm..mmh.”
Nilisukuma mlango na kumkuta amejipaka sabuni usoni, alipofumbua macho aliniona nipo mbele yake.
“Aah, kumbe wewe?”
“Ulidhani nani?”
“Nilifikiri kuna mtu kaingia kwa bahati mbaya.”
“Nilikwenda kutoa nguo ili tuje tuoge wote,” nilidanganya.
“Sasa mbona hukuniambia kama tunaoga wote uliondoka kimya kimya.”
“Nilijua nakuwahi.”
“Haya tuoge.”

ITAENDELEA
 
*MWAGIA HUMO HUMO EP 03*


Sehemu Ya Tatu (3)

Baada ya kusema vile aliingiza mkono mfukoni na kutoa pochi alihesabu noti tatu za kumi kumi na kunipa.

“Mpelekee hizi mwambie nitakuja.”

Nilizipokea na kufunga kazi zangu, pamoja na penzi letu kufa bado nilipelekwa na kurudishwa nyumbani na gari. Nilipofika nyumbani nilikwenda chumbani kwangu, kabla ya kufanya kitu chochote nilivua nguo zangu na kubakia mtupu kama nilivyozaliwa mbele ya kioo kikubwa na kujitazama upya kasoro katika mwili wangu.

Nilituliza macho na kuyazungusha taratibu mwilini mwangu kuangalia nina kasoro gani inayonifanya kila kukicha nipoteze wanaume. Kila hatua niliyokuwa nikipiga katika kusafirisha macho yangu nilijigundua nina sifa kubwa sana ya kuitwa mwanamke mrembo tena mwenye kumtia hamu ya mapenzi mwanaume rijali.
Umbile langu kwa mimi mwenyewe kama ningekuwa mwanaume na kukutana na mwanamke mwenye umbile kama langu ningemganda kama ruba, lakini kwangu ilikuwa na tofauti kubwa sana. Baada ya kujigundua sina kasoro mwilini nilijikuta nikilia huku nikisema kwa sauti ya chini.

“Hali hii mpaka lini?”
”Hali ipi?” Sauti ya Bi Shuu iliuliza nyuma yangu ilionesha Bi Shuu alikuwa ameingia kitambo bila mwenyewe kujua. Niligeuka na kwenda kujitupa kifuani kwake huku nikilia kwa uchungu.

“Vipi tena mwali?”

“Bi Shuu huu mkosi.”

“Wa nini?”

“Na Mateja kanimwaga.”

“Kwa nini unasema hivyo?” Nilimweleza yaliyotokea ofisini huku nikilia.

“Ulimwambia namwita?”

“Amesema atakuja wikiend.”

“Basi kazi hiyo niachie mimi.”

“Siamini kama atakusikiliza.”

“Ngoja aje, nitajua mbichi na mbivu.”

“Mmh, sina matumaini.”

“Hebu kaoge nikupe michapo.”

Nilikwenda kuoga ili nipate michapo ya Bi Shuu ambaye alinihakikishia kunipigania mpaka mwisho.

Nini kitaendelea? Tukutane wiki ijayo.

Mwisho wa wiki Mateja alikuja kuonana na Bi Shuu, alipofika waliingia kwa Bi Shuu. Nilikuwa na hamu ya kusikia alitaka kumuuliza nini juu yangu, nilijitahi kusikiliza dirisha la sebuleni la Bi Shuu lakini sauti walizokuwa wakizungumza zilikuwa za chini sikuweza kusikiliza waliyokuwa wakizungumza japo kuna muda nilisikia Mateja akisema.

“Ilikuwa vigumu kuja kuyasema haya kwako, kwa vile mpaka anafikia umri alionao niliamini ni vigumu kubadilika.”

“Mmh kama ni hivyo nina kazi nzito, naomba unipe muda vinaonesha chukuchuku havijaungwa.”

“Hapana Bi Shuu nakuheshimu sana, lakini tumechelewa ungeniita mapema tungeweza kulipatia ufumbuzi. Sasa hivi nipo katika mipango ya harusi na kila kitu kipo katika hatua za mwisho,” kauli ile ilinikata maini.

“Mmh, sawa nimekuelewa.”

“Basi bibie wacha nikuache tutaonana,” nilimsikia Mateja akiaga ili aondoke.

“Lakini naomba usimfukuze kazi mjukuu wangu.”

“Bi Shuu suala la kazi haliingiliani na mapenzi, sitamgusa katika kazi hilo usihofu.”

“Kama ni hivyo nashukuru, lakini Manka kapoteza dume la haja.”

“Kila kitu mipango ya Mungu.”

Nilimshuhudia Mateja akihesabu nyekundu tano na kumpatia Bi Shuu ambaye alishukuru nusra amlambe viguu Mateja kwa pesa aliyompa.
“Asante bwana yangu,” Bi Shuu alishukuru.

“Kawaida Bi Shuu ukiwa na shida mtume Manka usiogope.”

Mateja aliaga ili aondoke, nilitoka haraka dirishani kwa Bi Shuu na kukimbilia chumbani haraka. Nilijikuta nikiangua kilio kutokana na niliyoyasikia nusu kwa Bi Shuu, niliamini nilikuwa nimechelewa kuyasikia ya mwanzo kuhusu tatizo langu.

Niliamini kosa lilikuwa langu nilitakiwa nimueleze mapema Bi Shuu kuhusiana na mabadiliko ya Mateja. Kwa kauli ya Mateja kama ningewahi ningeweza kulikoa penzi langu. Nikiwa nimejiinamia kitandani nilikia nilishtushwa na mlango kugongwa.

Nilijua ni Bi Shuu ambaye hakutakiwa kugonga, lakini sikutaka kumlazimisha nilipaza sauti yangu ya kilio.

“Ingia mlango upo wazi.”

Mlango ulifunguliwa macho yangu yalimshuhudia Mteja akiingia ndani mwangu baada ya miezi sita toka alipokata mawasiliano na mimi. Alikuwa wa kwanza kuniuliza baada ya kukutana na michirizi ya machozi kwenye mashavu yangu.

“Vipi Manka unaumwa?”

“Ndiyo,” nilidanganya kwa vile sikuwa na cha kumwambia.

“Nini tena?”

“Kichwa.”

“Ooh, pole sana, umemeza dawa?”

“Bado.”

“Basi nyanyuka nikupeleke hospital.”

“Kitapoa tu.”

“Basi kama utazidiwa utakwenda hospitali.”

Mateja alisema huku akinisogelea mkononi alikuwa ameshikilia pochi na kunikabidhi elfu hamsini huku akisema.

“Kama utazidiwa zitakusaidia kwenda hospital.”

Nilitaka kuzikataa zile pesa kwa vile shida yangu haikuwa pesa bali yeye mwenyewe. Nilitaka kumuuliza tatizo langu nini lakini niliamini nilikuwa nimechelewa nilitakiwa kuuliza mapema na si muda ule ambao alinionesha mpenzi wake mbele ya macho yangu.

Nilipokea zile pesa Mateja aligeuka na kuondoka akiniacha nilikilia kilio cha kwikwi, baada ya kuondoka Bi Shuu aliingia na kunisimamia kama jini la kutumwa mkono kiunoni.

“Manka kwenu hakuna unyago?” Lilikuwa swali la kwanza bila kujali kilio changu.

“Unyago! Ndio nini?”

“Mafunzo ya msichana kujitambua na jinsi ya kumridhisha mwanaume kitabia na kimapenzi?”

“Sikuwahi kuyasikia.”

“Mmh, ndiyo maana.”

“Una maana gani kusema hivyo?”

“Umepoteza wapenzi kwa kutojua mwanamke anatakiwa kumridhisha vipi mwanaume.”
“Kwani kuna kitu gani amekueleza Mateja?”

“Tutazungumza na kulifanyia kazi.”

Baada ya kusema vile alitoka na kuniacha na mawazo kibao juu ya maswali yake na kitu alichoambiwa na Mateja. Nilijiuliza kutopata mafunzo ya usichana yanahusiana vipi na kukataliwa na wanaume. Nilijikuta nikijizoazoa hadi kwa Bi Shuu kutaka kujua Mateja kamwambia nini.

Nilipofika nilimkuta akizurudia kuzihesabu pesa alizopewa na Mateja, aliponiona aliziweka pembeni na kunitupia macho.

“Mmh, mwali una jipya gani?”

“Bi Shuu naomba unieleze ulichopelezwa na Mateja juu yangu?”

“Nitakueleza kwa vitendo si la maneno.”

“Matendo! Una maana gani?”

“Nimepata sababu ya wewe kukorofishana na wanaume, inaonesha wazi hukupitia mafunzo ya usichana. Nina kazi na wewe, mi ndo Bi Shuu bwana kila mwali aliyepitia mikononi mwangu kila aliyeonja hakutema. Najua wanakutema kwa vile unawalisha vya chukuchuku.”

“Vya chukuchuku! Una maana gani?”

“Utajua baada ya kuviunga kisha uwaonjeshe kama hukuolewa narudi kijijini kwetu japo toka nitoke kwetu kumebakia magofu. Lakini nakuhakikishia nakutia mikononi mwangu halafu nisikie, eti bwana bwana kaniacha,” Bi Shuu alishikilia pua na kusemea puani.

“Nakwambia najua kuviunga vya chunguni mpaka vya mwilini, wala hujachelewa sasa hivi mtu akigusa amenasa.”

“Utafanyaje?”

“Nataka uombe likizo ya mwezi mmoja tena nitakuombea mimi kwa Mateja ili niviunge viwe vitamu.”

“Vitamu! Vipi hivyo?”

“Nataka ukiguswa usisimke, ujue mwiko upo katika chungu au upo juu ya mfuniko, kumpa mwanaume mpaka asuse. Usilale kama gogo uoneshe basi upo safarini na si kukapua macho kama kibaka akimvizia mtu.”

“Mmh, mbona umeniacha njia panda.”

“Leo nataka kumbadili Mchaga awe kama Mmakonde.”

Mmh, kila alilozungumza kwangu lilikuwa geni, nilisubiri niungwe ili niwe mtamu kwa mwanaume.

Niliendelea na kazi yangu huku moyo ukiniuma kulipoteza penzi la Mateja, na mpenzi wake kutaka sifa kila muda wa chakula cha mchana lazima ampitie na wakitoka walikumbatiana na kuzidi kuniumiza. Lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kukubali matokeo.

Wiki moja baadaye Bi Shuu alinituma nimwite Mateja, kama kawaida nilimfikishia ujumbe wake, naye hakuwa na hiyana alikubali wito. Ilikuwa ajabu katikati ya wiki Mateja kukubali kwenda kumsikiliza Bi Shuu, tena aliniomba nikitoka kazini niongozane nae.

Baada ya muda wa kazi niliongozana na Mateja hadi nyumbani, tulipofika aliingia kwa Bi Shuu na kuniacha nikiingia chumbani kwangu. Nilijikuta nikijawa na mawazo juu ya wito ule Bi Shuu alikuwa na kitu gani ambacho alichomuitia Mateja.

Niliamini kabisa kama kutaka kumrudisha kwangu itakuwa ngumu kutokana na kila kitu kujionesha juu ya Mateja na mpenzi wake mpya. Nilipofika ndani hata hamu ya kuvua nguo iliniisha na kujikuta nikitoka na kujipitisha jirishani ili nisikie alichoitiwa na Bi Shuu.
Lakini sauti ya Bi Shuu ilinishtua kwa kuniita, moyo ulinishtuka kutaka kujua naitiwa nini? Niliingia sebuleni na kumkuta Mateja amekaa kwenye kochi akiwa ametulia. Bi Shuu aliponiona aliniambia.

“Manka kwenye friji yako kuna soda?”

“Mmh, jana nilimalizia nilikuwa na mpango wa kuweka leo.”

“Basi nifuatie dukani.”

“Bi Shuu si lazima achana nayo,” Mateja aliingilia kati.

“Hapana babu lazima unywe soda.”

Siku zote Mateja hakuwa na makuu alimkubalia Bi Shuu, baada ya kupewa pesa nilipitia chupa na kwenda dukani haraka ili niwahi mazungumzo yao.

Nilipofika dukani nusra nipasuke kwa hasira baada ya kukuta wateja wengi kwenye duka la Mpemba. Sikutaka kusubiri nilikimbilia kwenye grosary iliyokuwa mbali kidogo. Nilinunua soda haraka haraka na kurudi hadi karibu na nyumba na kuanza kunyata hadi dirishani ili nisikilize wanazungumza nini.

Nilipofika dirishani nilimsikia Mateja akisema.

“Hakuna tatizo Bi Shuu kila kitu kitakwenda kama unavyotaka.”

“Kama hivyo nitashukuru.”

Baada ya mazungumzo yale palipita ukimya mfupi huku sauti za nyayo zikielekea mlangoni, nilichepua mwendo hadi mlangoni na kukutana uso kwa uso na Bi Shuu.

“Vipi mwali mbona umechelewa?”

“Dukani kwa Mpemba kumejaa watu ilibidi nisogee mbele kwenye grosary.”

Bi Shuu aliipokea soda na kuingia nayo ndani, nilibakia mlangoni nikijiuliza niingie au niende chumbani kwangu. Kupata jibu la nifanye nini lilinifanya nisimame kwa muda pembeni ya mlango. Kabla sijapata jibu nilishtushwa na sauti ya Mateja.

“Manka kumbe upo hapa?”

“Ndi..ndi..yo,” maskini nilipata kugugumizi cha ghafla.

“Wacha niondoke zangu.”

“Haya, karibu,” nilijibu kwa aibu huku nikiangalia chini.

Mateja kweli alinichoka bila kuongeza neno alinitipa na kuelekea kwenye gari lake, Bi Shuu alimsindikiza mpaka kwenye gari. Nilibakia nikimsindikiza kwa macho.

Baada ya Mateja kuondoka Bi Shuu alirejea, alipofika alinishangaa kunikuta nimetawaliwa na simanzi usoni mwangu.

“Vipi mwali?”

“Aah, kawaida tu.”

“Acha kujitia ukiwa, kila kitu kina wakati wake na wakati ndio unakuja.”

“Kwani Mateja kasemaje?”

“Aseme nini?”

“Kwa hiyo amekubali?”
“Akubali nini?”

“Kwani ulimuitia nini?”

“Kuhusu likizo yako.”

“Kasemaje?”

“Amekubali.”

“Naanza lini?”

“Sijajua lakini amekubali.”

“Mmh, haya.”

Niliachana na Bi Shuu na kwenda chumbani kwangu kujiandaa na kujimwagia maji ili nipumzike.

*********

Siku ya pili nikiwa ofisini niliitwa na Mateja kunitaarifu kukubaliwa likizo yangu ambayo ingeanza wiki itakayofuata kwa kukamilisha kazi zangu zote muhimu. Nilipewa pesa ya likizo na kujiandaa kwenda kwenye unyago wa kiutu uzima ili niugwe niwe mtamu mwanaume akigusa anate.

Baada ya kumalizia kazi za ofisi kwa wiki niliyopewa, niliruhusiwa kurudi nyumbani kuanza likizo. Nilirudi nyumbani na kumkuta Bi Shuu ambaye kabla ya kuweka makalio chini aliniuliza.

“Mmh, umepewa likizo?”

“Nimepewa.”

“Basi kazi yote niachie mimi.”

Siku ile nilipumzika bila kugusiwa kitu chochote, lakini alfajiri niliamshwa na kupelekwa kuogeshwa maji baridi kisha nilifungwa upande wa kanga bila nguo ingine ndani. Aliniongoza hadi katika chumba kimoja cha ndani kilichokuwa kitupu.

Chini kwenye sakafu kulikuwa na maji kuonesha amemwagwa, baada ya kuingizwa mule ndani wakati huo kibaridi kilikuwa kikinichanyata. Bi Shuu alifunga mlango kwa nje na kuniacha nimesimama nikijiuliza ameleta mule ndani nifanye nini? Ajabu muda ulikatika nikiwa nimesimama, miguu ilichoka na kujiuliza mbona harudi ameniweka mule ndani ili iwe nini.

Kukaa chini nilishindwa kutokana chini kuwa na maji na muda ule ubaridi kilikuwa kikali sana. Niliposhika mlango ulikuwa umefungwa kwa nje nilijaribu kuita kwani nilikuwa nimechoka kusimama zaidi ya saa moja. Hakukuwa na jibu la mtu yoyote.

Nilijawa na mawazo juu ya kuwekwa chenye chumba chenye maji kisha kusimamishwa kwa muda mrefu. Nilijiuliza unyago wenyewe kama ndio ule kwangu niliamini nitashindwa. Niliamua kukaa kwenye maji huku kibaridi kikizidi kunichonyota, kutokana na uchovu nilijiegemeza kwenye ukuta na usingizi ulinipitia.

Nilishtushwa na maji ya baridi niliyomwagiwa ndoo nzima, Bi Shuu alikuwa mbele yangu akiwa amekunja uso kwa hasira na kunifokea kwa sauti ya juu.

“Haya ndiyo yanakufanya ukose wanaume kila kukicha, mwanamke mvivu kama nini, kukuacha muda mfupi umeshindwa kuvumilia na kuuchapa usingizi kwenye maji.”

“Samahani Bi Shuu.”

“Haya fanya usafi haraka,” alisema huku akinitupia tambara kukausha maji.

Nilichukua tambara na kuanza kufanya usafi kwa kukamilia maji kwenye ndoo mpaka nilipokausha, Bi Shuu alirudi na mkeka ambao aliutandika kisha alitoka na kurudi na chai. Tulikunywa chai kisha aliniacha nipumzike kwa kuniacha na kipande cha kanga tu.
Jioni ilipofika Bi Shuu aliingia ndani na kuniketisha kitako na kuanza kuniuliza maswali.

“Manka kitu gani wakati wa mapenzi hukipendi?”

“Mmh, vingi lakini tabia ya wanaume kunisumbua wakati wa kilimo huna sikupendi.”

“Mmh, kingine?”

“Ni hilo hilo tu.”

“Nimekuelewa, kuna vitu vingi vya kike vimekupita kushoto, siku hizi wanaume hawapendi mwanamke anayelala kama gogo, husisimki wala hutingishiki.”

“Bi Shuu nitikisike vipi au nisisimke vipi?”

“Ndiyo maana leo umo humu ndani, ukitoka utajua unasisimka vipi na unatikisika vipi?”

“Mmh, haya.”

Mmh, hukuwepo ila malaika wako alikuwepo, sikujua alichonipa Bi Shuu kilikuwa adhabu au mateso. Niliwekwa mikao ambayo haikuwa tofauti na ile niliyokuwa nikiwakatalia wanaume, kila nilipotegea nilitandikwa bakora ya mgongo iliyotua sawia kwenye mgongo mtupu.

Kila siku nilikuwa nikifanyishwa mazoezi yagumu ya viungo ambayo yalikuwa mateso mazito, kuna kipindi nilifikiria kumwambia bora aniache nilivyo kuliko mateso yale. Lakini Bi Shuu alikuwa mkali kama pilipili hakutaka mchezo hata kidogo hata nilipochoka bado alinilazimisha huku akisema.

“Kushinda kuchoka ndiyo siri ya kumkata kiu mwanaume.”

Nilibebeshwa mzigo kichwani nikiwa mtupu na kuanza kuchomwa na sindano kiunoni kitu kilichinifanya nishtuke kwa kuchezesha kiuno. Haikuishia hapo nililazwa chini na kubebesha mzigo kiunoni na kuendelea kuchomwa na kitu cha ncha ambacho kilinifanya nijinyonge nyonge bila kupenda.

Niliendelea na mazoezi makali chini ya kungwi wangu Bi Shuu huku akinipa mbinu nyingi za kumchanganya kimapenzi mwanaume. Kuna mambo mengine siwezi kuyasema gazetini lakini Bi Shuu koma. Toka nizaliwe sikuwahi kukutana na mwanamke Shankupe kama yeye.

Mtoto wa kike nilifundishwa maneno ya kusema mtu akiwa juu ya mnazi wangu, pumzi za kutoa wakati mwiko upo ndani ya chungu na akianza kugeuza maini nilitakiwa nilegee vipi huku macho na pumzi nizifanye vipi. Najua mwenzangu mie mwenye viuno kama vimefungwa mbao na wakati wa mapishi unatulia unasubiri mtu amwage mzigo akimaliza anyanyuke. Lakini ukikutana na bibi huyu lazima bwana akutaje jina.

Mwezi mmoja mtoto wa kike nilipikwa nikapikika, baada ya mafunzo mazito Bi Shuu kwa ushambenga wake alinitafutia mwanaume ili kutaka kunipima baada ya mazoezi. Sikukataa kwa vile nilijua kile ndicho kipimo, mtoto wa kike nilijiandaa kuonesha kilichoniweka ndani kwa mwezi mzima. Cha ajabu Bi Shuu alitaka mchezo ule nichezee chumbani kwake, mmh, makubwa madogo yana nafuu.

Sikutaka kumbishia kwa vile nilikuwa na usongo na mafunzo ya Bi Shuu ambayo yalinifanya nijiamini na kumtamani mwanaume nimtoe kamasi nyembamba. Baada ya kijana aliyechaguliwa na Bi Shuu kufika alikaribishwa chumbani kwa Bi Shuu, nilijikuta nikiwa na usongo na yule kijana ambaye alikuwa mmoja wa vijana walioninanga sijui kucheza nilipokutana naye siku ya kwanza.

Baada ya kuingia ndani nilimpokea juu juu na kumtoa nguo maungoni kama kuku aliyechinjwa na kunyonyolewa manyoya. Baada ya kumuandaa mtoto wa kike huku mwili ukinisisimka baada ya kukiona kijiti cha kupokezana kwenye mbio fupi.

Mtoto wa kike nikiwa nataka kufanya mtihani wangu wa kwanza kwa umakini mkubwa huku nikipitia hatua moja baada ya nyingine. Nilimlamba mwili mzima kama mama mbuzi akimsafisha mwanaye baada ya kumzaa, nilijua kutumia ulimi wangu.

Nilipofika kwenye shina la mnazi mtoto wa kike nilitulia kwa muda huku vidole laini na ulimi ukifanya kazi yake. Mara nilimuona kijana wa watu akitetemeka kama amekunywa coka ‘ngriiiiiiiiii’, maskini kumbe alikuwa akilia chozi lisilo na msiba.
Kijana wa watu naye akabadili upepo na kunirudishia mashambulizi.

Mtoto wa kike nilipoguswa nililegea na kuzitoa pumzi huku jicho likipoteza kiini cheusi. Kwa mara ya kwanza niligundua kumbe mwili kila sehemu una raha yake kuishinda nyingine. Kama nilivyofundishwa na Bi Shuu kila nilipoguswa nilisema neno lake.

Baada ya mshike mshike wa maandalizi cha chakula, hatimaye kiliiva na kutengwa mezani. Nilimpokea juujuu huku nilionesha jinsi gani mtoto wa kike nilivyoshikika, mtoto wa kike sikuwa na haraka nilifuata mwiko ulivyogeuza maini ili kumfanya mpigaji na mwimbaji wasitofautiane.

Mtoto wa kike nilimaliza maneno yote mdomoni, sikuamini kutatalika kama bisi kwenye chungu cha moto. Mpaka mchezo unakwisha nilikuwa nipo hoi kwani niliamini vilikuwa vitamu kijana wa watu kila alipomaliza alileta sahani aongezewe. Nami nilimpakulia naye alijilia huku akigugumia kama dume la njiwa lenye wivu. Huku nikilia mara nne kwa utamu wa msiba.

Lazima niseme ukweli kuna kipindi nilitaka kunyanyua mikono, maji yalikuwa shingoni, nyonga iligoma kutokana na kutokuwa na uzoefu wa kuyakata mawimbi.

Bi Shuu alinieleza kumfurahisha mwanaume si nyonga tu, hata kujua kuyapangilia maneno hasa kumsifia hakuna mwanaume kama yeye pia anajua kumshikisha punda adabu kwa kumtandika bakora balabala. Baada ya nyonga kugoma na kukiona kiuno kikiwaka moto, nilitumia sauti kumsindikiza mwenzangu mpaka alipofika juu ya mnazi.

Kijana wa watu hakuamini ilibidi aniulize.

“Manka, kumbe mambo unayaweza mbona ulikuwa uninikatili, mambo haya ungenipa tokea zamani sasa hivi ungekuwa mke wangu.”

“Nilikulisha vya chukuchuku lakini sasa vimeungwa ndio maana unaviona vitamu.”

Kijana wa watu bila kutegemea alinipa elfu 50 kama asante ya kumpa penzi tamu ambalo alikiri hakuwahi kulipata kwa mwanaume yoyote. Baada ya kuondoka na kuniacha nimejilaza baada ya kuhisi uchovu kila kona ya mwili kutokana na mshike mshike wa kufanya majaribio ya vitendo. Bila ya kujigeuza usingizi mzito ulinipitia juu ya kitanda cha Bi Shuu.

Nilishtuka baada ya masaa matatu nikiwa nausikia mwili mchovu kila kona, Bi Shuu aliniamsha na kukuta ameniandalia maji ya kuoga. Nilioga kupunza uchovu na kurudi ndani ambako chakula kilikuwa tayari. Tulikula pamoja kisha tulipumzika sebuleni, cha ajabu niligundua Bi Shuu akiniangalia kwa kuniibia kitu kilichonifanya nimuulize.

“Bi Shuu vipi?”

“Kuhusu nini?”

“Naona kama unanivizia kunitazama kuna nini si uniambie.”

“Mmh, kweli ulikuwa na usongo.”

“Wa nini Bi Shuu?”

“Kazi umeifanya vizuri japo kuna kipindi ulichemsha.”

“Ulijuaje?”

“Nilikuwepo muda wote toka unaanza mpaka unamaliza, kwenye maandalizi nakupa mia kwenye sauti na pumzi sabini kwenye mchezo wenyewe hamsini.”

“Jamani Bi Shuu kujitahidi kote unanipa hamsini.”

“Manka kwanza nashangaa mtu ulikuwa hujui lolote umeweza kupata hamsini wengi huwa chini ya hapo.”

“Bi Shuu kama nina hamsini nimeweza kupewa zawadi nikipata mia itakuwaje?”

“Mia kupata ni kazi kwa vile maungo yako yalikakamaa muda mrefu lakini utaweza kufika hata sabini kwa bidii yako.”
“Mapungufu yangu ni nini?”

“Kutumia nguvu nyingi ambazo hukufanya upumue kwa kasi sana kitu kinachokufanya uchoke sana, pia papala ya kukata nyonga. Mwanzo uliweza kwenda sawa lakini ulipoanza kuchoka alifanya bora liende. Lakini mwanzo ni mzuri.

Kwa uwezo wako huo na kuonesha ulikuwa makini kwa kuyashika mafunzo, inaonesha nikikuongezea matirio kama kwenye mpira ni ujanja wa kuweza kumsoma mwanaume. Kila mwanaume ana amambile tofauti na mwenzake na wengine wana nguvu kama kirafu unatakiwa kufanya nini.”

“Bi Shuu nitashukuru nimeteseka sana, kwa nini sikuyapata mafunzo haya mapema ili kuweza kumdhibiti Mateja,” Nilijikuta nikidondosha chozi kulikumbuka penzi la Mateja nililolipoteza kutokana na kutokujua sheria za kitandani na kunifanya niendeshe ovyo na kusababisha ajali za kutoelewa alama za kitandani.

“Manka usiwe kama kipofu aliyefumbua macho na kumuona chura na kuamini hakuna kama chura chini ya jua, mbona kuwa wanaume zaidi ya Mateja”

“Bi Shuu ni kweli usemayo lakini Mateja niliamini ni mwanaume sahihi kwangu.”

“Ni kweli, lakini kisicho riziki hakiliki we jipange ukikolea utamu nakuhakikishia nitakutafutia bwana Mateja cha mtoto. Kwanza nataka niyafanyie kazi makosa madogo madogo ambayo yatakufanya kila atakaye gusa atangaze ndoa. Nataka umlize mwanaume kama mtoto mdogo, umeisha ona mtoto akinyang’anywa ziwa jinsi anavyolia?”

“Ndiyo.”

“Basi nataka mwanaume chozi limtoke, kuna vitu vidogo wanawake hawajui, vitu hivyo ukimfanyia mwanaume kama ameoa lazima aitelekeze nyumba yake. Mchele mmoja lakini unatofautiana katika mapishi, hii nyumba jasho la mwili wangu pale nilipompata mume wa mtu. Leo hii naishi kwangu nawe nataka uwe mara mbili yangu.”

“Bi Shuu mbona wasichana hatuna vitu hivi?”

“Siku hizi uzungu umetawala na kujikuta wakipoteza vitu vingi vya kumfurahisha mwanaume. Kumfurahisha mwanaume kitandani si kigezo pekee cha kuilinda nyumba yako. Kuna vitu vingi ambavyo vipo nje ya kitanda.

“Kuna wasichana wengi wana nyonga laini kama unakula keki lakini wana mapungufu kama chujui la nazi ambayo hayawezi kumfanya atulie kwa kwenye ndoa yake. Kama tabia yako nzuri ulichanganya na machejo ya kitandani hata utakita hata ndege utanunuliwa japo mwenzio hana uwezo wa kununua baskeri.”

“Mbona hujanifunda na hivyo?”

“Siwezi kukuichanganya kimoja kimoja, kwanza tunatengeneza mtego akiingia anase, ukimaliza mafunzo ya mwili tunarudi tena kilingeni ili mumeo aone tofauti ya magumegume na mwanamke.”

“Bi Shuu mbona nimechoka sana.”

“Umelia mara ngapi?”

“Mara nne.”
“Mara ya mwisho ulilia mara ngapi ulipokutana na mwanaume kabla ya leo?”
“Mara mbili sijawahi kulia zaidi ya hapo.”
“Ndio maana, lazima uchoke umeukamua mwili sana na shughuli haikuwa ya kitoto kuna kipindi kidogo nisimamishe mpambano mlikuwa kama mnataka kutoana roho.”
“Bi Shuu umejuaje?”
“Nikuambie mara ngapi nilikuwa nafuatilia toka mwanzo mpaka mnamaliza”
“Jamani Bi Shuu kumbe ulikuwa unanipiga chabo,” Mbona niliona aibu mtoto wa kike, jamani bibi huyu ana mambo kumbe mwenzie nahenyeka yeye anapiga chabo.
“Sasa ningejuaje mapungufu yako.”
“Mmh, makubwa madogo yana nafuu.”
“Na hayo mengine lini maana muda wa kurudi kazini umekaribia.”
“Wiki iliyobakia inatosha, kapumzike jioni kama kawa mpaka kieleweke.”
“Wacha nikalale naona mwili sio wangu, kwenye pesa hiyo chukua nusu niachie nusu”
“Asante mwali, nina imani sasa umeamini nilichokisema kinatimia”
“Wee mwisho Bi Shuu je, ungenikamata ndio unavunja ungo naona kila aliyenionja angeniganda kama ruba.”
Baada ya mazungumzo nilimuomba Bi Shuu nikapumzike mwili ulikuwa na uchovu, nilikwenda chumbani kwangu kulala kwa kulifungulia feni mpaka mwisho mtoto wa kike nilijiachia kitanda kizima.
*******
Kama kawaida Bi Shuu aliniamsha kwenye chakula cha mchana na baada ya chakula cha mchana nilioga na kupanda tena kitandani. Sikuamini mwili kuchoka kiasi kile, Bi Shuu alinieleza ni kutokana na kuzoea kulala kama gogo kitandani lakini siku ile niliushughulisha mwili hata kumwaga machozi manne kitu ambacho hakikuwa kawaida yangu.
Nilipogusa kitandani usingizi haukuchelewa kunichukua, Bi Shuu aliniamsha saa mbili za usiku nilikwenda kuoga kisha nilipata chakula cha usiku. Baada ya chakula nilipumzika kidogo na kuingizwa unyagoni kumalizia muda ulipobakia kwa kunipa mbinu za kummiliki mwanaume kwa sauti na matendo huku tabia ikiwa ndiyo uliyochukua sehemu kubwa.
Katika mafunzo siku moja alinipa nipike chakula baada ya kupika tulikula wote, kesho yake alinipa nipike tena chakula kilekile, lakini hakunipa chumvi. Nilipomuuliza alisema nipike vile vile na muda wa kula nilishindwa kumuelewa baada ya kunieleza nipakue, nilipakua na kukila bila chumvi. Tulikula wote bila kujua chakula kile kwa nini tulikila bila chimvi.
Sikutaka kumuuliza kwa vile hakikuwa kingi tulikuwa na kukimaliza wote. Baada ya chakula usiku Bi Shuu akiwa ameniweka chini aliniuliza.
“Manka kuna tofauti gani ya chakula ulichopika jana na leo?”
“Tofauti yake cha jana kina chomvi lakini cha leo hakina chimvi.”
“Kipi chakula kizuri?”
“Cha jana.”
“Kwa sababu gani?”
“kina chumvi lakini cha leo hakina chimvi.”
“Mbona umekila.”
“Nilishindwa kuelewa ulikuwa na maana gani.”
“Lakini bila hivyo usingekula?”
“Nisingekula.”
“Unajua nilikuwa nina maana gani?”
“Hata sijui”
“Hii nakuonesha yaisha ya ndani ya ndoa, wanawake wengi wanawalisha wanaume chakula kisicho na chumvi. Wapo wanaokosa uvumilivu huvunja ndoa lakini wanaoburuzwa na mapenzi hula chakula kisicho na chumvi kila siku na kuishia kunung’unika moyoni.”
“Lakini Bi Shuu kama mkewe hamuwekei chumvi anashindwa vipi kuchukua mwenyewe kuweka kwenye chakula”
“Swadakta swali zuri, ndio maana kukuweka huku ndani vitu vingi huvifanya kwa mafumbo jibu lake huwa ndio maisha yako ndani ya mahusiano yako. Chakula na chumvi sikuwa na maana hiyo bali kukueleza matatizo ndani ya nyumba nyingi wanawake wengi ndoa zao uziondoa chumvi bila wao wenyewe kujua”
“Kivipi?”
“Nyumba nyingi mwanzo wa mapenzi huwa moto moto kama kumpokea mpenzio akirudi kumtengea chakula kula pamoja kuoga pamoja kuwa karibu yake kumpoza uchovu wa kutwa nzima ambao ndiyo tiba ya mwanaume kutoitafuta faraja nje ya ndoa yake.
“Wengi baada ya muda baadhi ya vitu hundoka kabisa na ndoa kuendeshwa kimazoea, moyoni lazima utasema hivi nisivyofanya kuna nini kwani hawezi kufanya mwenyewe. Kuacha kuyafanya hayo ni sawa kuondoa chumvi kwenye mahusiano yako na kumfanya mpenzio kula chakula kisicho na chumvi.
“Wengi huvumilia na kuumia moyoni lakini wasio na uvumilivu huitafuta chumvi hiyo nje ya ndoa. Hapo ndipo tatizo linapoanza na kuipoteza ndoa yako bila kujua tatizo ni wewe mwenyewe. Kuondoa baadhi ya vitu ndani ya ndoa yako kama kutompokea mumeo au kutokula na kuoga pamoja ni vitu vinavyo mwanaume huona vya kawaida lakini ni ufa mkubwa katika ndoa.
“Penzi halizeeki bali mwili ndio unazeeka, vyote nilivyokueleza usikipunguze hata kimoja ukiingia katika ndoa yako. Nakuhakikishia bwana atakaye kuoa watu watasema umemuwekea libwata, limbwata mwali ni kumlea mumeo kama mtoto. Nina imani umenielewa”
“Mmh, kweli nimekubali Mungu kakujalia kumtengeneza mwanamke, nina imani ungenieleza kwa maneno ningekuelewa nusu lakini kwa vitendo nimekuelewa zaidi. Asante Bi Shuu”
“Nashukuru kuonesha ni muelewa na mtu mwenye usongo na mafunzo”
“Lazima Bi Shuu niwe na usongo nimeteseka sana”
Nilimalizia mafunzo huku akilekebisha mapungufu aliyoyaona kwenye mtihani wangu wa kwanza.”
Nilikuwa sijawahi kula kungu mtoto wa kike nilikula kungu jicho ukiniangalia utanionea huruma. Nilimaliza mafunzo salama, kabla ya kuanza kazi alinitafutia tena mwanaume mwingine naye alikuwa mmoja wa wale walioninanga mwanzo.
Nilikuwa na imani alikuja akijua ni yule Manka wa mwaga msigo babangu kisha uondoke. Mafunzo niliyopata ya mwisho mtoto wa kiume chozi lilimtoka, kwenye maandalizi tu alilia zaidi ya mara tatu. Mtindo huu nilifundishwa kama sitaki kutumika sana kwanza namchosha mwanaume mwenye maandalizi.
Hata ulipoingia baharini nusra anifie maji baada ya kushikwa na pumu katikati ya safari, machejo yalimfanya aifukuze Land Curuser VX kwa bajaj. Ilibidi niingie kazi ya kumpepea asinifie, baada ya kurudi katika hali yake ya kawaida aliniangalia mara mbili.
“Ni wewe Manka au naota”
“Kwani vipi?”
“Hata siamini, kumbe ulikuwa unafanya makusudi”
“Ulikuwa vya chukuchuku sasa vimeungwa”
”Una maana gani?”
“Si umeona mwenyewe si la kusimuliwa”
“Nimekubali lazima nirudie”
”Mmh, cha kunifia kifuani hapa namefungulia injini moja katika injini nne si ungebadilika jina.”
“Manka naomba nikuoe.”
“Ni haraka sana vuta subra”
“Lakini niwe mmoja wa watu wa mbele kufikiriwa.”
“Hakuna tatizo”
Yule kijana ambaye alikuwa kama mlevi aliniachia laki moja ya asante”
Baada ya kuondoka Bi Shuu kama kawaida yake alitoa tathimini yake.
“Mwali japo mpinzani wako hakuonesha upinzani lakini umejitahidi sana tena sana, sasa nina uwezo wa kukueleza kapambane na mtu yoyote. La muhimu kuzingatia niliyokueleza hakika kila atakayehusa lazima anate sasa hivi mwili wako ni asali yenye ulimbo”
Maneno ya Bi Shuu yalinifanya nijiamini nimeanza kuiva kimapigano, kwa vile muda ulikuwa umekwisha jumatatu ilipofika nililipoti kazini kwangu. Nilimkuta aliyekuwa amenishikia, baada ya kunipokea alinielekeza kazi za kufanya na yeye kuendelea na majukumu mengine. Kuna kitu kimoja nilisahau kukueleza baada ya kukaa ndani kuchezwa nilipotoka nilitakata na kunawili mtoto wa kike.
Nikiwa naendelea na kazi bosi wangu dear zilipendwa aliingia ofisini, ilionesha hakujua kama naanza kazi siku ile. Alipofika hakuniangalia alinisalimia.
“Za saizi?”
“Nzuri”
“Ile kazi tayari?”
“Ndiyo namalizia”
’Baada ya muda gani”
”Dakika kumi”
“Ok, fanya haraka.”
Baada ya kusema vile aliingia ofisini kwake, ilionesha hakujua kama nipo mimi. Baada ya kumaliza kazi niliyoikuta niliprinti na kumpelekea, alikuwa bado ameinama nilipofika mbele yake nilisema.
“Bosi kazi tayari”
Sauti yangu ilimshtua na kunyanyua macho, kwa mshangao wa ajabu alisema.
“Ha! Manka umekuja saa ngapi?”
“Toka asubuhi”
“Ina maana nimekupita kwenye ofisi yako?”
“Ndiyo bosi”
“Ooh, samahani sana”
“Kawaida tu bosi wala usijisikie vibaya,” mtoto wa kike nilikuwa nimekwenda kimitego na kumuomba Mungu Mateja ajichanganye sijui aonje kidogo. Niliapa ningefanya aliyofundishwa na mengine nisiyo yajua ili kuhakikisha anakutana na vitu vipya katika medani ya mapenzi.
Mtoto jicho lilikuwa limelegea kidogo jicho lilionekana kwa kujipaka wanja chini na juu na kuongeza uzuri wangu. Japo nilijijua mi mzuri, lazima mzuri ujijue kabla hujasifiwa na watu, lakini mapungufu yangu Bi Shuu aliyamaliza mengi niliyokuwa nayo.
Mateja ilionekana kama kuchanganyikiwa kuniona nimebadika nimependeza na ninavutia tena kimitego ya kike hasaa.
“Manka ulikuwa unakula nini?”
“Kwa nini bosi?” nilimuuliza kwa sauti laini huku nikimchanulia tabasamu ya kufa mtu huku jicho nalo likizungumza.
“Hapana, umependeza na unavutia”
“Nashukuru kwa hilo ila moja umesahau”
“Lipi hilo?”
“Sasa hivi si Manka chukuchuku ila Manka huyu kaungwa akaungika”
“Una maana gani?”
“Bosi nitakuomba kesho nikukaribishe chakula cha usiku”
“Mmh, hakuna tatizo kwa vile wiki hii ni ya mwisho baada ya hapo nitakuwa katika maandalizi ya harusi.”
“Hakuna tatizo kazi njema.”
“Na wewe pia.”
Baada ya kumkabidhi kazi yake nilirudi kuendelea na kazi yangu, moyoni niliapa kama kweli atakubali mwaliko wangu amekwisha.Muda wa mchana Mchumba wake alimuijia kama kawaida na kwenda naye kupata chakula cha mchana.
Japo moyo uliniuma lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kukubali matokeo kutokana na makosa kuyafanya awali. Jioni niliporudi nilimueleza Bi Shuu mwaliko niliompa Mateja kuja kula chakula cha usiku.
“Mwali akiingia amekwisha, hakikisha anaisahau ndoa yake”
“Bi Shuu la kuuliza hilo”
“Nakuaminia mtu wangu.”
“Naiona kama kesho inachelewa”
“Itafika punguza munkari, usije yakakamia maji”
“Si hivyo Bi Shuu nakuhakikishia kuyafanya yote kwa umakini mkubwa labda asije.”
*****
Siku ya pili nilikwenda ofisini na kuendelea na kazi bosi alipokuja alinisalimia.
“Mrembo hujambo”
“Sijambo bosi simshindi wifi”
“Manka mbona umefika mbali salamu umeijibu sivyo”
“Samahani bosi, za nyumbani”
“Mmh, salama sijui zako.”
“Nami namshukuru Mungu, haya nipo ndani”
“Sawa bosi”
Kabla ya kuingia ofisini aligeuka na kuniuliza.
“Mwaliko wa usiku upo vile vile au kuna mabadiliko”
“Hakuna mabadiliko”
“Haya,” alisema huku akifungua mlango na kuingia ofisini kwake.
Baada ya kuingia ofisi nilibaki nilikuwa siamini kama nimesikia vizuri kuulizia mwaliko, niliona dalili njema zimeanza asubuhi jioni ni kumalizia tu. Huwezi amini siku hiyo nilifanya kazi kwa furaha ya ajabu kama Mateja amenikubali nirudiane naye.
Jioni kabla ya kuondoka aliniaga na kuniahidi angekuja usiku.
“Kweli Mateja utakuja?”
“Kama siji ningekuambia”
“Karibu sana mpe..” Mungu wangu nilitaka kujisahau kumwita mpenzi wakati tuliisha achana long time a go.
“Niite tu mpenzi wala usijisikie vibaya,”
“Hapana bosi”
“Haya baadae”
Mateja aliondoka na kuniacha nikipanga vizuri vitu vyangu kabla ya kurudi nyumbani.
*********
Nilkipofika nyumbani Bi Shuu aliniomba siku ile aandae chakula cha mgeni, sikuwa na hiyana mtoto wa kike nilimuacha afanye mambo yake. Nilikiandaa chumba changu na kukiweka katika hali ya usafi wa hali ya juu, kama kawaida Bi Shuu alinipatia mafusho ya manukato mazuri.
Baada ya kuhakikisha chumba changu kinapendeza niliingia kuoga mtoto wa kike na kujifusha utuli huku nikipaka wanja wa sina mume ambao lazima mwanaume barabarani akusalimie.
Baada ya kusimama mbele ya kioo kujitathimini, nilizidi kujisifia mtoto wa kike kwa upendeleo niliopewa na mwenyezi. Baada ya kuhakikisha nipo sawa, nilikunywa kungu na kuanza kujisikia nikisisimka mtoto wa kike kama mamba mwenye njaa.
Nikiwa nimekaa mkao wa kula kumsubiri Mateja, mara aliingia Bi Shuu na kuniongezea mambo fulani ya muhimu pindi Mateja akiingia chumbani kwangu.
“Mwali nilitaka kusahau kwa vile anajua anakuja kula chakula na kuondoka cha kufanya akiingia tu, ukimvamia kwa kumkumbatia huku akimbusu hakikisha mikono yako inafanya kazi ya haraka kumvua nguo bila kuchelewa mpatie upande wa kanga.
Wakati huo mimi nitakuwa tayari nimepeleka maji ya kuoga bafuni niliyoyawekea viungo. Nani alikuambia wanawake wa Tanga ndio wanajua mahaba, nataka Mateja akiondoka kila kitakachokuja mbele yake akione shombo.”
“Nimekuelewa Bi Shuu.”
“Sio umenielewa bahati hairudi mara mbili, itumie kubadili matokeo.”
“Matokeo ya nini Bi Shuu?”
“Ukimaliza kilicho tupotezea muda nitakwambia.”
“Nitafuata maelekezo yako.”
Baada ya kutoa maelekezo Bi Shuu alirudi kumalizia kutengeneza maajumati ya mgeni rasmi.
Majira ya saa moja na nusu gari la Mateja lilisimama mbele ya nyumba yetu, ajabu usongo wote niliokuwa nao uliyeyuka kama donge la mafuta katika kikaango cha moto. Nilijikuta nikijawa na hofu juu ya nilichokipanga kumpa Mateja kama ataingia katika mtego wangu.
Nilijihisi kupoteza ujasiri niliokuwa nao kabla ya Mateja hajaja, niliikandamiza mikono yangu kifuani na kubana pumzi na kukaa kwa muda kuvuta ujasiri kisha niliitoa na kushusha pumzi nzito.
Baada ya kujipa ujasiri nilijitengeneza haraka haraka ili kujiweka sawa japo nilikuwa nimejiweka kimitego ya kike hasa. Ndani nilivalia kufuri la bikini la rangi nyekundu juu nilivalia kanga nyepesi ukituliza macho unaona kila kitu cha ndani.
Wakati huo chumba kilikuwa kikinukia utuli kila kona mimi mwenyewe nilikuwa kama Hululaini malaika wa daraja la juu. Jicho mtoto lilikuwa lemelegea kwa kungu huku mwili ukisisimka kama nyoka mwenye hasira aliyepandisha sumu kwa ajili ya kumgonga mtu.
Wakati nikifanya matayarisho ya mwisho kabla ya kumpokea Mateja mbele ya kioo, Bi Shuu muda huo alikuwa amempokea.
“Wawooo mwanaume huyo.”
“Niambie kipenzi changu?” Sauti ya Mateja ilisikika.
“Niseme nini mkeo nawe umetupa jongoo na mti wake.”
“Bi Shuu kama ningetupa leo ningeonekana hapa?”
“Mateja kula nisishibe heri nisipewe.”
“Bi Shuu heri nusu shari kuliko shari kamili na kidogo si haba kuliko kukosa kabisa.”
“Nitakuwezea wapi mtoto wa Kisukuma aliyejifanya Mzaramo kwa kujifanya unajua kuyageuza maneno.”
“Vipi nimewakuta?” Mateja aliuliza mimi ndani kiroho paa!
“Umewakuta wamejaa tele wewe tu,” mmh, maneno ya Bi Shuu yalijaa nahau na misemo na kuzidi kuniweka njia panda.
Wakati nikijua hodi itapigwa wakati wowote nilipandisha tena pumzi na kuzishusha kisha nilijiandaa kumpokea. Mara mlango uligongwa.
“Hodi ndani?”
“Karibu,” nilimkaribisha huku nikikaa mkao wa chura kuruka.
Mara mlango ulifunguliwa na Mateja aliingia, mtoto wa kike nilijizoazoa na kumkumbatia.
“Ooh, karibu mpenzi.”
“Asante za hapa?”
“Nzuri.”
Mtoto wa kike niliutambaza mdomo wangu na kutua kwenye mdomo wa Mateja ambaye alikuwa bado amepigwa na butwaa, nikihema kama mgonjwa wa pumu. Mateja alinipokea na kubadilishana mate, mikono yangu alipata nafasi ya kumvua shati.
Baada ya kumvua shati nilimsukumia kitandani na kumlalia juu, kwa haraka nilimalizia na vilivyokuwa vimebaki chini kisha nilimpatia upande wa kanga. Kila nililolifanya siku ile kwa Mateja kilikuwa kigeni kwake niliamini alijua bado Manka wa mwaka 47 hohehahe asiyejua chochote.
Niliamini muda huo Bishuu alikuwa ameisha peleka maji yaliyochanganywa na viungo bafuni. Nilimshika mkono Mateja na kutoka naye nje kumpeleka bafuni kuoga, Bi Shuu kweli alikuwa amepania mlangoni nilikuta kuna ndala mpya. Mateja alivaa na kuongozana naye hadi bafuni.
“Karibu mpenzi uoge.”
“Asante.”
Nilimwacha Mateja bafuni na kurudi ndani kujiandaa kumlisha vilivyoungwa na Bi Shuu. Kabla sijaweka tako chini Bi Shuu aliingia bila hodi na kusema kwa sauti ya juu.
“Wee mwana, ndio unafanya nini?” Kauli ile ilinishtua sana.
Kutokana na makosa ya kuruka baadhi ya sehemu katika hadithi ya wiki iliyopita kufikia hatua ya kuwachanganya wasomaji. Leo tutaelezea kwa ufupi toka Mateja alipomuona Manka ofisini mpaka kufikia hatua ya kumsubiri chumbani. Baada ya Mateja kushtuka kumuona Manka jinsi alivyopendeza kwa muda ambao hakuwepo kazini alimsifia kuwa amependeza mara dufu. Naye Manka alitumia nafasi ile kumkaribisha Mateja chakula cha jioni kwake. Mateja alimkubalia na kumuahidi angefika jioni kwa ajili ya chakula.
Manka aliporudi nyumbani alimueleza Bi Shuu kuwa Mateja amekubali kuja kula chakula cha jioni. Bi Shuu alimueleza asiipoteze nafasi ile adimu ahakikishe kama atakubali kuvila vilivyoungwa basi achanganyikiwe. Bi Shuu alimuomba kazi ya kupika chakula aifanye yeye ya kuandaa chakula cha ujanani kwake pale alipokuwa akimtengenezea mpenzi wake.
Baada ya makubaliano na Bi Shuu Manka aliingia ndani kujiandaa kwa ajili ya kumpokea Mateja kwa kufanya usafi wa mwili na chumba huku akifusha udi na asumini kumwagia kitandani. Yalikuwa mafunzo tosha ya Bi Shuu ambayo Manka aliyafanyia kazi.
Baada ya kila kitu kuwa tayari Manka alimsubiri kwa hamu Mateja mpaka alipofika. Baada ya kumuandalia maji na kumuacha aoge peke yake ndipo Bi Shuu alipomfuata na kumuuliza amefanya nini.
Ili kujua kosa lake nina imani mpaka sasa tupo pamoja, haya tuserereke pamoja…
Kauli ya Bi Shuu ilinishtua na kujiuliza nimefanya kosa gani tena.
“Bi Shuu nimefanya nini?”
“Manka haya ndiyo makosa mnayafanya sana wanawake wengi, kwa nini umuache aoge peke yake. Nenda kaoge naye ikiwezekana anza kumliza kilio cha raha bafuni.”
Mmh, mtoto wa kike haraka nilitelemsha nguo ya ndani na kubakia na upande wa kanga nyepesi na kumuwahi Mateja kabla hajajipaka sabuni. Nilipokaribia bafuni Mateja alikohoa kumaanisha kuna mtu.
“Mm..mm..mmh.”
Nilisukuma mlango na kumkuta amejipaka sabuni usoni, alipofumbua macho aliniona nipo mbele yake.
“Aah, kumbe wewe?”
“Ulidhani nani?”
“Nilifikiri kuna mtu kaingia kwa bahati mbaya.”
“Nilikwenda kutoa nguo ili tuje tuoge wote,” nilidanganya.
“Sasa mbona hukuniambia kama tunaoga wote uliondoka kimya kimya.”
“Nilijua nakuwahi.”
“Haya tuoge.”

ITAENDELEA
 
*MWAGIA HUMO HUM EP 04*


Sehemu Ya Nne (4)

Nilimsogelea na kuusugua mwili wangu kwake, joto langu lilimsisimua. Mmh, kuangalia kwenye kikosi wa miziga,mtutu wa mziga ulikuwa juu. Manshala mtoto wa kike niliupandia mtutu na kuufanyia ukaguzi kabla ya kuingia vitani. Mmh, weee acha tu hukuwepo bali shetani wako alikuwepo.

Mateja alikuwa kama mtu aliyekula mishikaki yenye chachandu ya Kihindi jinsi alivyotoa miguno. Taratibu nilishughulika na mtutu wa mzinga ambao ulionekana ulikuwa tayari kutupa makombora mazito kwa adui. Kutokana na utaalamu niliopewa na Bi Shuu na kujua kuufanyia usafi mtutu wa mziga, mara nilimuona Mateja akitetemeka na kutoa machozi laini.

“Vipi?”

“Aa..aah.”

“Pole.”

“Asante.”

Niliendelea kumpa mshike mshike kwa kugusa hapa na pale, najua unataka kujua niligusa wapi. Vuta subra tukikutana nitakueleza mwanaume anatakiwa aguswe wapi ili kumuongezea mahanjamu. Ila lazima mikono yako iwe laini sio migumu kama mpasua kokoto utamchubua mwenzio. Nilisahau kama tupo bafuni kwa kuendeleza mateso bila chuki.

Nilimsikia Mateja akisema.

“Manka si tunarudi ndani tumalize kwanza kuoga.”

“Waaawooo,” nilifurahia kimoyo moyo kwa kuamini mbwa mwenyewe kakimbilia kichaka cha nyani asubiri vibao vya mashavu.

Tulimalizia kuoga huku nikimsugua kila kona ya mwili kisha nilimfuta maji na kumfunga taulo nami nilipitia upande wa kanga na kutoka naye kurudi chumbani. Wakati nakaribia chumbani kwangu Bi Shuu alitokea nyuma ya bafu na kunifanyia ishara ya mdomo.
Niligeuka na kusimama ili nimsikilize alikuwa na jambo gani.

“Manka,” alisema huku akiachia tabadamu.

“Abee.”

“Hongera.”

“Ya nini?”

“Unajua kuifanya kazi umeiva kwelikweli mambo uliyofanya mimi mwenyewe hoi.”

“Asante Bi Shuu.”

“Basi usiniangushe yote tisa kumi huko mnakokwenda ukifanya makosa umetia nazi kwenye supu.”

“Bi Shuu wee acha nina usongo naye ile mbaya”

“Usikamie sana ukashindwa kuyanywa.”

“Nimekuelewa.”

Niliagana na Bi Shuu na kuelekea chumbani kwangu na maswali mengi juu ya tabia ya Bi Shuu kunipiga chapo kila nililokuwa nafanya. Mmh, niligeuka nielekee chumbani Bi Shuu tena aliniita.

“Manka usizime taa pia dirisha lako la nyuma liache wazi”

Niliingia ndani nikijiuliza mengi juu ya tabia za Bi Shuu Kunipiga chabo, nilijua mwanzo alitaka kujua uwezo wangu lakini baada ya kuona nimeweza hakukuwa na haja ya kunipiga tena chabo zaidi ya kusubiri matokeo. Lakini kwa upande mwingine niliamini ile ndiyo ilikuwa fainali yangu ya kujua nimefundika au nilibahatisha kwa wachovu.

Pamoja na kutaka kujua nipo katika kiwango gani, wasiwasi wangu mkubwa ulikuwa kutojiamini kwa asilimia zote kutokana na kujua kuna mtu ananiangalia. Bora angenivizia nisingejua kinachoendelea na mimi kufanya makamuzi ya nguvu.

Ndani nilimkuta Mateja amekaa kitandani, mtoto wa kike kwa usongo niliokuwa nao niliivuta kanga aliyokuwa amejifunga na kubakia kama kuku anayesubiri kuingizwa kwenye mafuta. Nami yangu nikaitupa pembeni na kubakia sale sale maua si unajua asiyejua kuchagua kabila lake Mzigua. Jamani maneno mengine sijui ni kweli au wimbo ina maana Wazigua ndiyo wasiojua kuchagua?

Tuachane na hayo wanajua waliosema si mimi, baada ya kuwa sale sale kama kuku wanaosubiri kuingizwa kwenye kalai la mafuta ya moto. Kupitia mafunzo ya Bi Shuu mwanamke kabla ya kusafiri katika bahari ya huba unatakiwa kukiandaa chombo. Sehemu hii naomba twende pamoja huonekana wanawake wengi tunakosea.

Kosa kubwa kwa wanawake wengi wakiishafika kitandani husubiri kuandaliwa wao kisha wapande kwenye chombo kuanza safari ya huba wakati mwenzake naye alihitaji kusisimliwa kama yeye. Au wengine ambao huwa kama mimi Manka kabla ya kuingia unyagoni kwa Bi Shuu kujua kabla ya safari vitu gani vinatakiwa kufanywa.

Wengi wetu hutangulia kitandani na kutega kama kicheche anavyotega kuku, akiingiza kichwa tu anatimua naye mbio kichakani. Lazima sehemu hii uitumie kuandaana kila mmoja tui likikolea nazi ruksa kutia mchele, tuko pamoja nataka nilichokipata kwa Bi Shuu nawe upande japo kiduchu.

Basi mtoto wa kike nilikiwa nimepandwa na maruhani ya mapenzi nilikuwa kama chatu aliyeshiba na kujivuta kushida huku pumzi zikinitoka kwa shida. Nilitambaza mikono yangu laini toka kona moja kwenda nyingine hasa sehemu muhimu zenye kupandisha mahanjamu.

Nilianza kumsikia Mateja akisisimka na kuninyonga taratibu kama nyoka anavyopata shida ya kutambaa kwenye sakafu. Nilizipapasa sehemu ambazo humfanya mwanaume asisimke na kumpandisha mzuka wa mapenzi. Kila nilipogusa sehemu nilimuona akitaka kunyanyuka kama samaki pomboo anavyojitupa kwenye maji kwa madoido.
Baada ya safari ndefu nilifika mji mkuu na kufanya kituo cha muda mrefu kwa kutumia mikono mdomo na ulimi ambao ulimfanya Mateja agugumie kama dume la njiwa lenye wivu. Niliendelea kuwajibika mpaka alipolia bila msiba huku akiomba tuingie chomboni kuianza safari ya huba yenye utamu usiisha hamu hasa kwa wanaoufahamu shati uwe mtaalamu wa kuitumia yako kalamu ndipo utaipata tamu na kukufanya mahamumu kila uikumbukapo tamu lazima upitate hamu ya kuutafuta utamu.

Sijui tupo pamoja au nimekuchanganya, mwa kwetu siku zote chakula maandalizi, na chakula kitamu kinahitaji maandalizi ya kina na katika mwili vile vile. Huwezi kudandiwa kama baskeri na kupigwa pedeli, wakati unachemka mwenzio kesha fika zamani kalala pembeni hoi kuendelea na safari hawezi wakati mwenzake waduduuu wadogowadoooo ndo wamecharuka Wananyemvuanyemvua.

Hapa pia kuna somo nililopata kwa Bi Shuu usikubali kuianza safari hakikisha mwakwetu kwako nawe kumetiwa mchuzi wa kutosha sio kula mkavu utakukwama kooni. Nina imani tupo pamoja au nimekuacha njia panda, mwakwetu hakikisha mpenzi wako amekuandaa mpaka hatua ya mchuzi kukolea kwenye ubwabwa hapo ruksa chakula kiliwe. Lazima wote mtakifurahia sio kuwahi kitandani kusubiri hukumu bila kujitetea.

Baada ya Mateja mchicha kukolea nazi shetani wa ngono kumpanda alitaka kuchupa mchupo wa mkizi, lakini mtoto wa kike nilimshika kifuani na kumueleza.

“Mpenzi pangu pakavu tia mchuzi,” nilikuwa na maana bado hajaniandaa ili tufurahia safari kwa pamoja. Mateja alinielewa ndipo alipoanda kuniandaa kwa kufanya ziara ya mkono na ulimi mwilini kwangu, jamani chakula kitamu kikipata muandalizi asiye na papara. Nakiri sikuwahi kukutana na raha za mwili siku zote niliamini raha zipo chini tu kumbe mwenyezi Mungu aliumba kila kiungo mwilini na makusudio yake.

Kila nilipoguswa nilihisi raha tofauti na aliponigusa kwanza, mtoto wa kike nilimaliza maneno yote mdomoni kuomba hukumu baada ya kulia zaidi ya mara mbili bila huruma ya Mateja kuendelea kunipa mateso bila chuki. Baada ya tui kukolea nazi, kile nilichotaka kukionesha kwa Mateja kilitimia.

Mtoto wa kike tuliingia kilingeni kujua mbivu na mbichi, najua unahamu kujua kilichoendelea, samahani tukutane wiki ijayo.

Mtoto wa kike nilipoguswa tu nililegea mwili ulikuwa kama umepigwa shoti ya umeme, mchezo upoanza tu nilijiachia huku nikizitoa pumzi kwa kufuata mdundo, japo nyonga haikuwa laini sana kama wamakonde nami taratibu nilinyambulika kuhakikisha sitoki nje ya biti. Hakukuwa na ushindani kila mtu alitaka kuonesha uwezo wake kwenye medani ya mapenzi.

Kila dakika ilivyokwenda ndivyo kila mtu alipoteza ustaarabu na kutaka kuonekana anaweza kuliko mwenzake. Kila dakika iliyokwenda ilikuwa ni maajabu saba ya dunia kwa Mateja. Nina imani kabisa mwanzo aliona kama nabahatisha kutokana na kunizoe Manka wa kulala kama gogo Manka mbishi nisiyekubali usumbufu wa kugeuzwa kama chapati.

Manka nilimpania Mateja bila kujua wito ule ulikuwa na sababu, kila alivyotaka nilifanya bila hiyana kila aliponituma nilikwenda bila kubisha kila alivyoniweka nilikaa bila tatizo. Muda wote niliwajibika bila kuchoka huku nikimmwagia sifa ambazo nina imani hakuwa kupewa toka azaliwe.

Kuna kipindi mtoto wa kike nilalamika kama mtoto aliyeny’ang’anywa ziwa na mama yake, kutokana na kuufurahia mchezo nilijikuta nikilia kama naonewa kumbe raha zilikuwa zimekonga kila kona ya mwili.

“Mateja kwa nini unanitesa…kosa langu nini?” Nililalama huku nikiwajibika.

Siku zote raha ya kurap uendane na mdindo, nilibadilika mtoto wa kike na kuongeza nijuavyo nisivyofunzwa na Bi Shuu. Jamani makubwa ukishangaa ya Musa utayaona ya firauni. Ghafla Mateja machozi yakaanza kumtoka baada ya kuvamia shamba la mihogo kwa mikono na mdomo jembe nililitoa kwenye mpini na kuchimba muhogo kwa mkono.

Kila nilivyoutafuta muhongo nilimuona mtoto wa kiume akihama upande mmoja kwenda mwingine. Mmh, sikuamini nilimuonea huruma lakini siku zote ukitaka kumtiba mgonjwa wa jipu usimuonee huruma. Mateja uzalendo uliomshinda aliamua kusema.

“Manka kwa nini ulinitenda?”

“Kivipi mpenzi?”
“Vitu hivi mbona hukunipa mwanzo?”

“Mpenzi vilikuwa havijaungwa, hata vya chukuchuku havikuiva.”

“Hapana…hapana…sikubali.”

“Hukubali nini tena mpenzi?”

“Siwezi kula nisishibe heri nisipewe.”

“Mateja leo utakula mpaka utasaza nipo kwa ajili yako.”

“Na baada ya leo?”

“Mi nipo tu.”

“Hapana..hapana …lazima nikuoe.”
“Na mchumba wako?”
“Wewe ndiye uliyekuwa mchumba wangu.”
“Kama nilikuwa mchumba wako kwa nini uliniacha?”
Huwezi kuamini wakati tukizungumza hivyo kilimo kiliendelea huku Mateja akishinda kukaa chini kama kakalia moto.

“Vipi?” Nilimuuliza huku nikimtazama usoni kwa jicho lilililegea kama mtu mwenye usingizi mzito.
“Mm..mm..mmh,” Mateja aligugumia kama dume la panya kwenye ghala la mahindi.
Baada ya muda maskini mateja machozi yasiyo na kilio yalimtoka, niliyahifadhi hakugusa chini.
“Asante Manka…asante mpenzi.”
Mtoto wa kike sifa hazikunivimbisha kichwa niliuchukua mpini na kuurudisha kwenye jembe kilimo kiliendelea. Mmh, kweli kila kiumbe na sehemu zake, kurudisha mpini kwenye jembe kulikuwa kama kumtupia samaki majini. Mateja alikuja juu kama moto wa kifuu kila nilipotaka kumtuliza ndivyo raha zilivyogonga kila kona ya mwili na kujikuta nikiwacha autawale mchezo.
Nilifika kipindi duniani nikawa sipo mbinguni sipo nikawa naelea kati, nakiri sikujua kilichokuwa kikiendelea zaidi ya kuhisi kama mtu kanivua nguvu zote mwilini kilichoendelea sikujua. Niliposhtuka nilijikuta nimelala pembeni ya Mateja ambaye alikuwa hajitambua kwa usingizi mzito.
Kilinichonishangaza kujikuta sote tumo ndani ya shuka moja, nilijiuliza inawezekana Mateja ndiye aliyenifunika. Nilipotaka kunyanyuka nilihisi kama kizungungu nilijirudisha kulala. Wakati nataka kufumba macho nilisikia naitwa.
“Manka…Manka,” niliposikiliza vizuri niligundua ni Bi Shuu.
“Abee.”
“Amka ujimwagie maji.”
“Sina nguvu.”
“Jitahidi hivyo hivyo.”
Nilijinyanyua kwa kuzilazimisha miguu ikiwa haina nguvu, nilijizoazoa na kwenda kujimwagia maji, Bi Shuu maji alikwisha yapeleka bafuni. Nilioga maji yaliyokuwa ya baridi sijui aliyatoa kwenye friji. Baada ya kujimwagia maji mwili ulichangamka kidogo, hapo ndipo nilipoanza kuisikia njaa.
“Manka kamuamshe na mwenzako naye akajimwagie maji ili mle pamoja”
“Kwa saa ngapi sasa”
“Saa sita kasoro.”
“Mtume!”
Nilikwenda kumuamsha Mateja aliyekuwa akikoroma ilionekana kalinyekarinde lilimpeleka puta na kujikuta akipoteza nguvu nyingi. Inawezekana kabisa alijua ni yule Manka wa mwaka 47 na kuingia kichwa kichwa matokeo kanyolewa bila maji.
Kila nilipomtikisa alionekana yupo hoi kwa kugeuka kama umekufa, niliendelea kumtikisa.
“Mateja..Mateja.”
“Mmh.”
“Amka.”
“Niache nilale kidogo.”
“Najua umechoka, amka ujimwagie maji upate nguvu.”
“Manka naomba nipumzike nimechoka sana.”
“Matejaaaa, hebu amka.”
Nilimwambia huku nikimshika mkono na kunyanyua, alinyanyuka na kukaa kitako kitandani. Akiwa kama mtu aliyekunywa pombe ambayo ilikuwa bado kichwani, aliinama mkono mmoja alishika kitandani na mwingine kichwani. Sikutaka kumpa nafasi nilimsimamisha na kumfunga upande wa kanga.
Huwezi kuamini nilivyokuwa nimechoka bila kuelekezwa na Bi Shuu nisingeweza kuyafanya yale. Maji ya baridi niliyojimwagia ndiyo yaliyonipa nguvu, nilimshika mkono mpaka bafuni ambako nilikuta tayari Bi Shuu ameisha tayarisha maji ya baridi.
Kwa kuwa nilijua ubaridi wa maji Mateja atauogopa nilipomtoa kanga nimwagia kwa kumshtukiza kama makopo mawili. Japo alilalamika lakini alinieleza kweli maji yale yameupa tena nguvu mwili wake. Alimuongeza maji mengine na kuufanya mwilini wake uchangamke zaidi.
Alipomaliza kujimwagia maji ya baridi tulirudi ndani, sikuamini macho yangu kukuta Bi Shuu amekwisha andaa chakula mezani kukiwa na kila kitu. Muda wa Mateja kujimwagia maji, yeye aliutumia kuandaa chakula. Yaani sijui niseme nini, nimekutana na watu wengi lakini Bi Shuu kiboko.
Japo usiku ulikuwa mkubwa lakini mama wa watu hakulala alikwenda sambamba na mimi. Kilichonishangaza baada ya mtinange na kupitiwa usingizi nilijiuliza yeye alikuwa wapi? Kama sisi tulilala kwa zaidi ya masaa matatu yeye muda huo alikuwa anafanya nini?
Mateja baada ya kuona nilimsikia akisema.
“Manka umejuaje kama nina njaa, maana hapa nahisi tumbo jeupe.”
Kwa vile na mimi nilikuwa na njaa tulivamia wote mezani kukishambulia chakula kilichokuwa kimepikwa kwa ustadi wa hali ya juu na Bi Shuu. Tukiwa mezani baada ya kufunua kawa lililikuwa na maneno RAHA YA MUWASHO UKUNWE . Ajabu ya Mungu kawa lile lilionekana jipya halijawahi kutumika, baada ya kulifunua harufu nzuri ya chakula ilijaa puani mwetu. Nilimnawisha mikono kisha nilimkaribisha kama nimepika mie.
“Karibu mpenzi.”
“Asante,’” Mateja alijibu huku akijipakulia kwenye sahani yake, wakati anaweka kijiko cha kwanza nilisikia kitu kikigongwa dirishani. Ilionesha kuna kosa nimefanya. Nilinyanyuka haraka huku nikisema.
“Samahani dear nakuja,” nilitoka nje na kukutana na Bi Shuu.
“Vipi Bi Shuu?”
“Manka nilikueleza nini?”
“Kuhusu nini?”
“Mwanaume kama mtoto asiguse kitu kazi yote ifanye wewe.”
“Ulikuwa una maana gani?”
“Asijipakulie, mpakulie ikiwezekana hata vijiko vya awali mlishe kisha mwache ale mwenyewe.”
“Nimekulewa,” nilimjibu bila kusubiri maelezo mengine kumuwahi Mateja asijipakulie zaidi. Nilipofika nilikuta ndio anataka kuongeza kijiko cha tatu. Nilikidaka kijiko na kusema.
“Mpenzi kwa nini usumbuke wakati nipo.”
“Aah, si kila kitu ukifanye.”
“Hapana wewe ni mgeni wangu, kila kitu mimi ndiye dereva.”
“Haya mama.”
Nilimpakulia chakula cha kiasi kisha nilimuwekea mchuzi na kipande cha ndizi, tonge la kwanza nililikusanya kisha nilimlisha huku nikiweka mkono chini ya kidevu kuzuia punje ya wali isianguke. Baada ya kulisha nilimsubiri atafune ili nimuongeze tonge lingine nami nianze kula. Baada ya kutafuna kwa muda nilimsikia aliguna kitu kilichonitisha na kuwa na wasi wasi huenda chakula si kizuri.
“Vipi mpenzi?”
“Mmh, chakula kitamu kweli kweli, sijawahi kula chakula kitamu kama hiki, kama nikikuoa na kula hivi kila siku nitenenepa mlangoni nitakuwa sipiti.”
“Asante mume wangu,” nilijibu makusudi, moyoni niliisifia kazi nzuri ya Bi Shuu.
“Manka,” Mateja aliniita huku akivuta glasi ya maji iliyokuwa pembeni.
“Abee.”
“Manka mbona leo naona kama nipo ndotoni?”
“Kivipi?”
“Mbona siku za nyuma hukunifanyia mambo kama haya, mapenzi ya ukweli na chakula kitamu kweli kweli.”
“Vimeungwa.”
“Una maana gani?”
“Mateja mimi ni Manka mpya.”
“Una maana gani?”
“Ulichokiona kazi kubwa ya Bi Shuu.”
“Bado umeniacha njia panda Bi Shuu amefanya nini?”
Nilimuelezea bila kumficha kazi kubwa ya Bi Shuu kuniunga na leo kuvionjwa akaviona vitamu.
“Upo hapo baba?”
“Mmh, nimekubali kweli aliomba likizo yenye mafanikio.”
“Basi habari ndio hiyo.”
Baada ya chakula tulirudi kuoga tena kisha tulipanda kitandani kulala hakuna aliyekuwa na hamu na mwenzake tulipeana migongo mpaka asubuhi. Mlio wa dirisha uliniamsha toka kwenye usingizi mzito, jicho langu lilitua kwenye saa ya ukutani kunionesha ni saa kumi na moja alfajiri.
Nilijinyanyua kivivu na kwenda hadi mlangoni kumsikiliza Bi Shuu alitaka kunielaza nini, nilifungua mlango huku nikifikicha macho kutokana na kuzingirwa na usingizi ulioambatana na uchovu wa mwili. Nilikumbuka usiku wa jana nilitumia nguvu nyingi ili kumuonesha Mateja mimi ni nani.
Nakumbuka kuna kipindi niliona kama chini nachochewa kuni jinsi moto ulivyokuwa ukiwaka. Lakini nilikumbuka maneno ya Bi Shuu sifa kubwa ya mwanamke kwa mwanaume ni uvumilivu na kutokukubali kushindwa mapema hata siku ya kwanza unapotaka kuandika CV.
Baada ya kufungua mlango nilikutana na Bi Shuu akiwa na upande wa shuka.
“Shikamoo Bi Shuu.”
“Marahaba mama Shughuli.”
“Mmh! Bi Shuu jina gani tena hilo.”
“Kwani uongo shughuli unaiweza, mwana wewe temea chini.”
“Aii jamani,” nilijikuta nikiona aibu kwa kujua kila nilichokifanya Bi Shuu alikiona ‘live’ bila chenga.
“Sasa Manka sicho nilichokuamshia, vipi ushampa cha alfajiri?”
“Kipi hicho?”
“Ooh, kweli hili sikukuelekeza, raha ya mapenzi ukilala na mwanaume mpe cha asubuhi ili kiwachangamshe, kijasho kikiwatoka mkaoge mjiandae kwenda kazini.”
“Si tutachoka sana.”
“Uchoke nini, hiyo sawa na kuzimua baada ya kulala na hang over asubuhi ukizimua unajiona sawa hata uzito wa kichwa unapotea sawa na kupata cha asubuhi.”
“Mmh! Sawa wacha basi nifanye hivyo.”
Niliagana na Bi Shuu na kurudi ndani, Mateja alikuwa bado amelala nilimshtua kwa kumpa mshikemshike wa kuvamia shamba lake kwa kuufukua muhogo taratibu kitu kilichomshtua kunikuta nipo shambani na tayari muhogo nilikuwa nimeisha ufukua upo mkononi.
“Vipi mpenzi?” aliniuliza kwa sauti ya usingizi.
“Kawaida tu.”
“Niache nilale nimechoka.”
“Kumekucha mpenzi tunazimua kisha tunakwenda kuoga.”

ITAENDELEA
 
*MWAGIA HUMO HUMO EP 05*

MWISHOOOOOOOO


Sehemu Ya Tano(5)

Nilimweleza huku nikimuongeza mahanjamu yaliyomfanya ajikute katikati ya shamba akipalilia mazao bila kutumia nguvu.
Kama alivyonielezea Bi Shuu tulikuwa tukizimua ili kuuchangamsha mwili kutokana na mtanange wa kukata na shoka. Hatukutumia nguvu sana zaidi ya kuichangamsha miili yetu. Baada ya kila mmoja kupata kifungua kinywa kikombe kimoja kikavu kijasho kilitutoka na kwenda kuoga. Huwezi amini Bi Shuu muda wote alikuwa karibu yangu kwa kila hatua.
Nilikuta maji ya moto tayari yapo bafuni, tulioga pamoja huku tukishikana hapa na pale. Baada ya kuoga tulirudi ndani, juu ya meza kulikuwa na chupa ndogo ya chai na sahani iliyokuwa imefunikwa sikujua kwenye chupa kuna nini na kwenye sahani kumefunikwa kitu gani. Mateja alipoona chupa ya chai na vikombe vya udongo ambavyo vilionekana mahususi alisema. “Mmh, kweli toka jana umenipania, alfajiri yote hii umeamka saa napi kuandaa kila kitu.” “Kila mwanamke anajua wajibu wake.”
“Asante nimekubali.” Moyoni nilibakia na maswali Bi Shuu amelala saa ngapi maji ya moto na kifungua kinywa amevitayarisha saa ngapi. Nilijikuta nikumuonea huruma bibi wa watu na kujiona kama namtesa bure.
Lakini kwa upande mwingine alinisaidia sikuamini vitu vile kama mwenyewe ningeviweza. Nilisogea kwenye meza na kuangalia kwenye chupa kulikuwa na tangawizi na kwenye sahani kulikuwa na mayai manne. Mateja alipoviona vile vitu aliniambia.
“Nikuambie kitu Manka?” “Niambie.” Mateja anataka kumwambia nini Manka? Kuyajua yote tukutane wiki ijayo. “Kipi nilikifanya kwa ufasaha?” Nilimuuliza kutaka kujua hizo maksi tisini nilizipata vipi. “Vingi sana.” “Vipi hivyo?” “Mwana wee, hata hujapumzika una pupa kama umemuona Mateja kadondosha taulo?”
“Jamani Bi Shuu yamekuwa hayo!” “Umerudi pumzika jimwagie maji kisha uache mwili upumue kwa muda, kwa vile muda bado tunaweza kuzungumza kwa kituo, siyo juu juu kama malaya wa Magoti, lamba raha, nipe changu.
” Mmh! Maneno ya bibi huyu yalinifanya niwe mdogo kama pilitoni na kukoma kuuliza swali kama lile.
“Basi wacha nikaoge.” “Haya ndiyo maneno, mtoto wa kike huambiwa sio aulize vingine aibu, ushanizoea eeeh.
” Bi Shuu aliniuliza huku akinikata jicho la dharau.
“Hapana Bi Shuu.” “Ndivyo nilivyokufunda, eeeh jambo la ndani kulisema hadharani?”
He! Makubwa Bi Shuu aligeuka mbogo. “Bi Shuu, samahani basi.” “Samahani basi, ndiyo nini?” Bi Shuu alishika pua. Mmh, niliamini kisebusebu changu ndicho kilichoniponza baada ya kuamini Bi Shuu wa kawaida wa kumuuliza kila nitakacho. “Bi Shuu samahani sana kama nimekukosea.”
“Nshakusamehe, nenda kaoge pumzika kisha njoo.
” Nilikwenda chumbani kwangu kubadili nguo kisha niliingia bafuni kuoga, baada ya kuoga nilijilaza kitandani na kupuliziwa upepo mwanana wa feni. Nikiwa nimejilaza nilikumbuka Mateja alitaka chakula cha usiku, nilikurupuka na kumfuata Bi Shuu aliyekuwa amekaa sebuleni kwake akiangalia cd ya taarabu. “
Vipi?”
Aliniuliza baada ya kuniona. “Bi Shuu Mateja anataka chakula cha usiku.” “We mwali! Chako amekiona hakifai anataka na changu?” “Jamani Bi Shuu maneno gani hayo?” Jamani Bi Shuu alinipeleka sipo kabisa. “Sasa kosa langu nini, kama angetaka chako usingeniambia ungempa tu, lakini baada ya mwali anataka na vya kungwi wake, naona kanogewa sasa anataka kuku na mayai yake.”
“Jamani Bi Shuu sina maana hiyo.” “Ulimaanisha nini?” “Chakula ulichompikia jana kimemrusha akili kimeniongezea maksi mtoto wa kike na kutaka awe anakula kila siku, kitu kitakacho harakisha ndoa.” “Na mchumbake?” “Amechoka kula vya kuchemshwa bila kuungwa.”
“Hooooya weee, kweli kula uhondo kwahitaji matendo, umeona eeeh?”
“Nimeamini mtembea bure si mkaa bure, Mateja kachanganyikiwa ingekuwa ndoa ni viocha ya simu, mbonaangenifuta na kuniiingiza na sasa hivi angekuwa hewani kwa raha zake.”
“Manka huyoo, ushakuwa mtoto wa Kizaramo mineno kama umebemendwa.” “Bi Shuu kweli wewe nyani huoni makalio yako.”
“Haya tuachane na hayo anataka chakula gani?” “Kama cha jana.” “Lakini leo utapika mwenyewe.”
“He! Bi Shuu mbona unaniumbua mchana, nitaweza wapi kupika chakula kitamu au ndiyo unanivua nguo ukweni.”
“Wachina wana methari zao kuwa ukitaka kumsaidia mtu usimpe samaki bali mfundishe kuvua ili aweze kupata zaidi.” “Kwa hiyo nami unanifunza kuvua?” “Ndiyo maana yake, kama ningejitoa kwa Mateja angekupenda wewe au mimi?” “Wewe?” “Basi, leo nina kazi ya kukufundisha kupika baadhi ya vyakula, ushaona chai ina paliliwa.” “Ha!” “Unashangaa, kupika kunataka kituo kutuliza akili sio nyanya hazijaiva wewe unatosa kitoweo, ndiyo maana vikiiva havieleweki kila kitu kipo kivyake.”
“Si kuna mafunzo ya kupika mtu anapata cheti?” “Cha darasani si kitamu kama cha asili, wee nenda kanunue vitu ili tuingie jikoni pamoja, siku ya pili umuandalie peke yako bila msaada wangu.” “Nikijua kupika nitafurahi.” “Unatosheka? Hata ukijua kupika bado utajigundua una mapungufu.” Bi Shuu alinielekeza vitu vya kwenda kununua, sikutaka kupoteza muda nilibadili nguo na kwenda kudandia daladala mpaka sokoni, baada ya manunuzi yote muhimu.
Nilirudi mara moja na kumkabidhi Bi Shuu ambaye alinieleza nitulie atanishtua. Nilirudi chumbani kwangu na kujilaza chali nikiwa kama nilivyozaliwa na kula upepo wa feni kwa raha zangu. Nilijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu juu ya mambo ya Bi Shuu, mtu mmoja alikuwa na mambo mia moja. Nilikubali mzee wa watu kutoa huduma pasina kinyongo, kweli alipewa mambo yaliyo katika mzani.
Majira ya jioni Bi Shuu aliniamsha na kuanza maandalizi ya kupika, maandalizi ya awali ya kumenya vitunguu maji na swaumu nyanya na viungo vingine nilijua kuandaa baada ya kuandaa tuliingia jikoni. Niligundua makosa yangu mengi katika kupika. Kwa upande wangu nilikuwa natumia muda mchache kupika tofauti na Bi Shuu hakuwa na papara katika kupika hata chuzi lilionekana kweli linajitengeneza tofauti na kina sisi wakina mama kuchemsha, kweli niliamini vitamu vinahitaji utulivu. Nini kitaendelea? Kuyajua yote tukutane wiki ijayo.
Baada ya kuandaa chakula kwa kufuata maelekezo ya Bi Shuu, nilikiandaa kwa ajili ya Mateja. Mtoto wa kike nilioga na kumuandalia Mateja maji ya kuoga niliyoweka viungo. Nilirudi chumbani kujiandaa kumpokea mpenzi wangu, kama nilivyoelekezwa na Bi Shuu mwanamke anayetaka kumpokea mpenzi wake hasa penzi linapokuwa changa.
Nilijifukiza udi wa manukato kila kona ya mwili hata kanga zangu nilizokuwa nimejifunga na shuka nilizotandika nazo zilikuwa zinanukia. Yote haya yataka kituo huwezi kuyafanya kwa kulipua utaona mzigo. Kujipulizia manukato ya al udi, jicho lililoregea kwa ajili ya kungu manga liliongezwa uzuri na wanja mwembamba wa mwezi mchanga.
Nilijilaza kitandani huku nikisindikizwa na muziki wa taarabu wa zamani kidogo ulioporomoswhwa na kikundi cha taarabu cha TOT, kilichoimbwa na bibi Hadija Kopa kisemacho ‘TX mpenzi.’ Niliyakumbuka baadhi ya mashairi yake: Tx mpenzi daktari wangu wa thamani, Kiitikio: Ayaa ayaa ayaaa.
Amesipeshalaizi digii yake surgeon (Mtaalamu wa upasuaji) Kiitikio: Aya aya Ayaaa. Aminyapo dawa zake ganzi tele maungoni, Tx nipasua toa maradhi ya ndani. Kiitikio: Nipasue Tx nipasue eeh toa maradhi ya ndani wee nipasue. Siku za nyuma nilipousikia wimbo huo sikuuelewa, lakini nilipojua zuri na baya na kuelezewa maana ya wimbo huo. Nilijitambua kumbe mimi mgonjwa na daktari wangu Mateja niliyemsubiri kwa hamu aje atoe maradhi ya ndani kwa kunifanyia upasuaji.
Wimbo huu ukiusikiliza kisha uusikie wimbo wa Mwanaidi Shaabani uitwao Dereva akiwa na kikundi cha Muungano Culture Troop, wimbo huunao kuna maneno kama haya: Dereva nimempata ananiendesha vyema sukani akikamata chombo hakiendi mrama. Breki akikamata wakati wa kusimama ziozile za kugota za kishindo na kuzama.

Uniacha naitaita kwa uroda nihema. Hebu niambie mumeo sifa hizi za dereva makini anazo, basi wimbo huu niliupanga baada ya mtinange na Mateja nimewekee.
Mwa kwetu sina haja ya kukuwekea wimbo, la hasha nakuomba hasa wewe msichana wa siku hizi tafuta nyimbo hizi kisha zisikilize na upate mnaana zake hakika utaungana nami kumwita mumeo au mpenzio Tx wa mapenzi na mwisho wa safari lazima umwite dereva wako makini mwenye reseni ya kimataifa. Basi mwa kwetu najua nilikupeleka mbali lakini kina mama na dada zetu waliokuwa wakitesa enzi za miaka 95 watakubaliana na yote niliyoyasema, basi nikiwa nimejiandaa vilivyo mtoto wa kike.
Jicho lililoregea la kungu manga nilinogeswa na wacha mwembamba wa mwezi mchanga niofundishwa kujipaka na Bi Shuu wanja huu aliniambia unaitwa karibu mpenzi. Baada ya kukamilisha na kujifisha udi mpaka kwa bi mkubwa. Nilijilaza kitandani nikiendelea kutumbuizwa na wimbo wangu wa Tx mahususi ya Mateja wangu.
Nikiwa nimejilaza Mateja aliwasiri, kwa vile mlango ulikuwa wazi alipogonga tu mtoto wa kike nilinyanyuka kwenda kumpokea huku nikideka, jicho langu liliongea kama nina usingizi mzito, yote haya mwanzo sikuwa nayo kazi kubwa ya Bi Shuu. “Karibu Tx wangu.” “Una maana gani kuniita Tx.” “Sikiliza huu wimbo” Mateja alisikiliza kwa muda kisha alishusha pumzi ndefu na kutikisa kichwa huku akiniangalia mara mbili mbili.
“Vipi Tx wangu?”
“Mmh! Haya.”
“Sema tu naona kama una maswali yanayohitaji majibu toka kwangu?” “Sina swali, ila kila naona mambo mapya, wee mchaga mambo ya pwani umeyajulia wapi?”
“Kwani Bi Shuu ni mtu wa Pwani, Mmanyema mtu wa Kigomayeye kayajulia wapi? Si watu wa mwambao wa Pwani tu wanajua mapenzi.” “Mmh, nimekubali.”
Nilimpokea koti lake na kuliweka kwenye kochi, alipokaa alimvua viatu kisha nilihamia kwenye shati nikatelemka kwenye suruali, nikatoa na nanihii kisha nikampa upande wa kanga ili nimpeke bafuni tukaoge.
Utajiuliza kwa nini nimempa kanga badala ya taulo, mwa kwetu kanga ina raha yake, huwezi kwenda nyumba ya wageni ukakuta kanga lazima utakuta taulo. Kama mpenzi wako alizoea kwenda nyumba ya wageni ukimpa kanga lazima akili yake ataona kuna tofauti ya nyumba ya wageni na nyumbani kwa mpenzi wake.

Baada ya kuoga tulirudi ndani kisha nilijifanya kama kuna kitu kinaniwasha na kujikuna kwa kuipandisha nguo, nilijua lazima Mateja ataangalia, nilirudisha haraka mtego wangu ulinasa, ukimuoneshamaungo nyeti nusu, lazima atataka aone kabisa kufanya vile ilikuwa kumuongezea mahanjamu. Mmh! Mtoto wa kume uzalendo ulimshinda, nimnyime ili iweje, shoga mwili wako mali ya mpenzio, hasa yule mliyeshibana.
Alipotaka nikampa kwa nguvu zote, huku nikumuuliza baba chagua kipapatio ili usichoke sana kabla ya kula au paja ushibe kabisa. Mateja alitaka kipapatio, ushaanza- kipapatio ni nini? Wapo waliotafuta maana zao, jamani kipapatio penzi jepesi lisilochosha, nina imani hata paja ushajua. Haya twende kazi, mmh, mtoto wa kike nilijisahau na kumuongezea paja baada ya kumuona kabisa kipapatio hakimtoshi. Mwisho wa shughuli nilimwacha kajilaza na kumuwekea wimbo wa dereva huku nikimbadili jina toka Tx mpaka Dereva.
Mateja kila aliponiangalia alitikisa kichwa. Nilimnyanyua na kumpeleka bafuni kisha nilimualika mezani. Baada ya kutafuna tonge la kwanza alitikisa kichwa na kusema: “Hakika wewe ni chura,” kauli ile ilinitisha iweje aniite chura mdudu tena nisiye mpenda. “Mpenzi kwa nini umeniita chura?” “Sina nia mbaya, nina maana chura anaishi kotekote majini na nchi kavu. Umekamili kila idara, nikiwa na na wewe raha zangu hazitakuwa na kikomo.”

“Ha! Kumbe, Asante mpenzi.” Nilimkumbatia Mateja kwa furaha. Baada ya chakula tulipumzika chakula kiende sehemu zake baada ya hapo mtoto hakutumwa dukani. Sitaki kukuchosha sasa hivi mimi ni mke halali wa Mateja, tunapendana kwa dhati huku nikiendelea kupokea mawazo ya Bi Shuu bibi ambaye sitamsahau mpaka nakufa. Mwisho nawaomba wanawake wenzangu kutafuta dawa ya mapenzi ambayo ni kujifunza kwa waliotutangulia ili viungwe viwe vitamu wa wapenzi wetu kwani siku zote ukikitoa hamu kitakosa utamu.

******************************************MWISHO*(************************************
 
Screenshot_20190421-111231.jpeg
 
*MWAGIA HUMO HUMO EP 05*

MWISHOOOOOOOO


Sehemu Ya Tano(5)

Nilimweleza huku nikimuongeza mahanjamu yaliyomfanya ajikute katikati ya shamba akipalilia mazao bila kutumia nguvu.
Kama alivyonielezea Bi Shuu tulikuwa tukizimua ili kuuchangamsha mwili kutokana na mtanange wa kukata na shoka. Hatukutumia nguvu sana zaidi ya kuichangamsha miili yetu. Baada ya kila mmoja kupata kifungua kinywa kikombe kimoja kikavu kijasho kilitutoka na kwenda kuoga. Huwezi amini Bi Shuu muda wote alikuwa karibu yangu kwa kila hatua.
Nilikuta maji ya moto tayari yapo bafuni, tulioga pamoja huku tukishikana hapa na pale. Baada ya kuoga tulirudi ndani, juu ya meza kulikuwa na chupa ndogo ya chai na sahani iliyokuwa imefunikwa sikujua kwenye chupa kuna nini na kwenye sahani kumefunikwa kitu gani. Mateja alipoona chupa ya chai na vikombe vya udongo ambavyo vilionekana mahususi alisema. “Mmh, kweli toka jana umenipania, alfajiri yote hii umeamka saa napi kuandaa kila kitu.” “Kila mwanamke anajua wajibu wake.”
“Asante nimekubali.” Moyoni nilibakia na maswali Bi Shuu amelala saa ngapi maji ya moto na kifungua kinywa amevitayarisha saa ngapi. Nilijikuta nikumuonea huruma bibi wa watu na kujiona kama namtesa bure.
Lakini kwa upande mwingine alinisaidia sikuamini vitu vile kama mwenyewe ningeviweza. Nilisogea kwenye meza na kuangalia kwenye chupa kulikuwa na tangawizi na kwenye sahani kulikuwa na mayai manne. Mateja alipoviona vile vitu aliniambia.
“Nikuambie kitu Manka?” “Niambie.” Mateja anataka kumwambia nini Manka? Kuyajua yote tukutane wiki ijayo. “Kipi nilikifanya kwa ufasaha?” Nilimuuliza kutaka kujua hizo maksi tisini nilizipata vipi. “Vingi sana.” “Vipi hivyo?” “Mwana wee, hata hujapumzika una pupa kama umemuona Mateja kadondosha taulo?”
“Jamani Bi Shuu yamekuwa hayo!” “Umerudi pumzika jimwagie maji kisha uache mwili upumue kwa muda, kwa vile muda bado tunaweza kuzungumza kwa kituo, siyo juu juu kama malaya wa Magoti, lamba raha, nipe changu.
” Mmh! Maneno ya bibi huyu yalinifanya niwe mdogo kama pilitoni na kukoma kuuliza swali kama lile.
“Basi wacha nikaoge.” “Haya ndiyo maneno, mtoto wa kike huambiwa sio aulize vingine aibu, ushanizoea eeeh.
” Bi Shuu aliniuliza huku akinikata jicho la dharau.
“Hapana Bi Shuu.” “Ndivyo nilivyokufunda, eeeh jambo la ndani kulisema hadharani?”
He! Makubwa Bi Shuu aligeuka mbogo. “Bi Shuu, samahani basi.” “Samahani basi, ndiyo nini?” Bi Shuu alishika pua. Mmh, niliamini kisebusebu changu ndicho kilichoniponza baada ya kuamini Bi Shuu wa kawaida wa kumuuliza kila nitakacho. “Bi Shuu samahani sana kama nimekukosea.”
“Nshakusamehe, nenda kaoge pumzika kisha njoo.
” Nilikwenda chumbani kwangu kubadili nguo kisha niliingia bafuni kuoga, baada ya kuoga nilijilaza kitandani na kupuliziwa upepo mwanana wa feni. Nikiwa nimejilaza nilikumbuka Mateja alitaka chakula cha usiku, nilikurupuka na kumfuata Bi Shuu aliyekuwa amekaa sebuleni kwake akiangalia cd ya taarabu. “
Vipi?”
Aliniuliza baada ya kuniona. “Bi Shuu Mateja anataka chakula cha usiku.” “We mwali! Chako amekiona hakifai anataka na changu?” “Jamani Bi Shuu maneno gani hayo?” Jamani Bi Shuu alinipeleka sipo kabisa. “Sasa kosa langu nini, kama angetaka chako usingeniambia ungempa tu, lakini baada ya mwali anataka na vya kungwi wake, naona kanogewa sasa anataka kuku na mayai yake.”
“Jamani Bi Shuu sina maana hiyo.” “Ulimaanisha nini?” “Chakula ulichompikia jana kimemrusha akili kimeniongezea maksi mtoto wa kike na kutaka awe anakula kila siku, kitu kitakacho harakisha ndoa.” “Na mchumbake?” “Amechoka kula vya kuchemshwa bila kuungwa.”
“Hooooya weee, kweli kula uhondo kwahitaji matendo, umeona eeeh?”
“Nimeamini mtembea bure si mkaa bure, Mateja kachanganyikiwa ingekuwa ndoa ni viocha ya simu, mbonaangenifuta na kuniiingiza na sasa hivi angekuwa hewani kwa raha zake.”
“Manka huyoo, ushakuwa mtoto wa Kizaramo mineno kama umebemendwa.” “Bi Shuu kweli wewe nyani huoni makalio yako.”
“Haya tuachane na hayo anataka chakula gani?” “Kama cha jana.” “Lakini leo utapika mwenyewe.”
“He! Bi Shuu mbona unaniumbua mchana, nitaweza wapi kupika chakula kitamu au ndiyo unanivua nguo ukweni.”
“Wachina wana methari zao kuwa ukitaka kumsaidia mtu usimpe samaki bali mfundishe kuvua ili aweze kupata zaidi.” “Kwa hiyo nami unanifunza kuvua?” “Ndiyo maana yake, kama ningejitoa kwa Mateja angekupenda wewe au mimi?” “Wewe?” “Basi, leo nina kazi ya kukufundisha kupika baadhi ya vyakula, ushaona chai ina paliliwa.” “Ha!” “Unashangaa, kupika kunataka kituo kutuliza akili sio nyanya hazijaiva wewe unatosa kitoweo, ndiyo maana vikiiva havieleweki kila kitu kipo kivyake.”
“Si kuna mafunzo ya kupika mtu anapata cheti?” “Cha darasani si kitamu kama cha asili, wee nenda kanunue vitu ili tuingie jikoni pamoja, siku ya pili umuandalie peke yako bila msaada wangu.” “Nikijua kupika nitafurahi.” “Unatosheka? Hata ukijua kupika bado utajigundua una mapungufu.” Bi Shuu alinielekeza vitu vya kwenda kununua, sikutaka kupoteza muda nilibadili nguo na kwenda kudandia daladala mpaka sokoni, baada ya manunuzi yote muhimu.
Nilirudi mara moja na kumkabidhi Bi Shuu ambaye alinieleza nitulie atanishtua. Nilirudi chumbani kwangu na kujilaza chali nikiwa kama nilivyozaliwa na kula upepo wa feni kwa raha zangu. Nilijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu juu ya mambo ya Bi Shuu, mtu mmoja alikuwa na mambo mia moja. Nilikubali mzee wa watu kutoa huduma pasina kinyongo, kweli alipewa mambo yaliyo katika mzani.
Majira ya jioni Bi Shuu aliniamsha na kuanza maandalizi ya kupika, maandalizi ya awali ya kumenya vitunguu maji na swaumu nyanya na viungo vingine nilijua kuandaa baada ya kuandaa tuliingia jikoni. Niligundua makosa yangu mengi katika kupika. Kwa upande wangu nilikuwa natumia muda mchache kupika tofauti na Bi Shuu hakuwa na papara katika kupika hata chuzi lilionekana kweli linajitengeneza tofauti na kina sisi wakina mama kuchemsha, kweli niliamini vitamu vinahitaji utulivu. Nini kitaendelea? Kuyajua yote tukutane wiki ijayo.
Baada ya kuandaa chakula kwa kufuata maelekezo ya Bi Shuu, nilikiandaa kwa ajili ya Mateja. Mtoto wa kike nilioga na kumuandalia Mateja maji ya kuoga niliyoweka viungo. Nilirudi chumbani kujiandaa kumpokea mpenzi wangu, kama nilivyoelekezwa na Bi Shuu mwanamke anayetaka kumpokea mpenzi wake hasa penzi linapokuwa changa.
Nilijifukiza udi wa manukato kila kona ya mwili hata kanga zangu nilizokuwa nimejifunga na shuka nilizotandika nazo zilikuwa zinanukia. Yote haya yataka kituo huwezi kuyafanya kwa kulipua utaona mzigo. Kujipulizia manukato ya al udi, jicho lililoregea kwa ajili ya kungu manga liliongezwa uzuri na wanja mwembamba wa mwezi mchanga.
Nilijilaza kitandani huku nikisindikizwa na muziki wa taarabu wa zamani kidogo ulioporomoswhwa na kikundi cha taarabu cha TOT, kilichoimbwa na bibi Hadija Kopa kisemacho ‘TX mpenzi.’ Niliyakumbuka baadhi ya mashairi yake: Tx mpenzi daktari wangu wa thamani, Kiitikio: Ayaa ayaa ayaaa.
Amesipeshalaizi digii yake surgeon (Mtaalamu wa upasuaji) Kiitikio: Aya aya Ayaaa. Aminyapo dawa zake ganzi tele maungoni, Tx nipasua toa maradhi ya ndani. Kiitikio: Nipasue Tx nipasue eeh toa maradhi ya ndani wee nipasue. Siku za nyuma nilipousikia wimbo huo sikuuelewa, lakini nilipojua zuri na baya na kuelezewa maana ya wimbo huo. Nilijitambua kumbe mimi mgonjwa na daktari wangu Mateja niliyemsubiri kwa hamu aje atoe maradhi ya ndani kwa kunifanyia upasuaji.
Wimbo huu ukiusikiliza kisha uusikie wimbo wa Mwanaidi Shaabani uitwao Dereva akiwa na kikundi cha Muungano Culture Troop, wimbo huunao kuna maneno kama haya: Dereva nimempata ananiendesha vyema sukani akikamata chombo hakiendi mrama. Breki akikamata wakati wa kusimama ziozile za kugota za kishindo na kuzama.

Uniacha naitaita kwa uroda nihema. Hebu niambie mumeo sifa hizi za dereva makini anazo, basi wimbo huu niliupanga baada ya mtinange na Mateja nimewekee.
Mwa kwetu sina haja ya kukuwekea wimbo, la hasha nakuomba hasa wewe msichana wa siku hizi tafuta nyimbo hizi kisha zisikilize na upate mnaana zake hakika utaungana nami kumwita mumeo au mpenzio Tx wa mapenzi na mwisho wa safari lazima umwite dereva wako makini mwenye reseni ya kimataifa. Basi mwa kwetu najua nilikupeleka mbali lakini kina mama na dada zetu waliokuwa wakitesa enzi za miaka 95 watakubaliana na yote niliyoyasema, basi nikiwa nimejiandaa vilivyo mtoto wa kike.
Jicho lililoregea la kungu manga nilinogeswa na wacha mwembamba wa mwezi mchanga niofundishwa kujipaka na Bi Shuu wanja huu aliniambia unaitwa karibu mpenzi. Baada ya kukamilisha na kujifisha udi mpaka kwa bi mkubwa. Nilijilaza kitandani nikiendelea kutumbuizwa na wimbo wangu wa Tx mahususi ya Mateja wangu.
Nikiwa nimejilaza Mateja aliwasiri, kwa vile mlango ulikuwa wazi alipogonga tu mtoto wa kike nilinyanyuka kwenda kumpokea huku nikideka, jicho langu liliongea kama nina usingizi mzito, yote haya mwanzo sikuwa nayo kazi kubwa ya Bi Shuu. “Karibu Tx wangu.” “Una maana gani kuniita Tx.” “Sikiliza huu wimbo” Mateja alisikiliza kwa muda kisha alishusha pumzi ndefu na kutikisa kichwa huku akiniangalia mara mbili mbili.
“Vipi Tx wangu?”
“Mmh! Haya.”
“Sema tu naona kama una maswali yanayohitaji majibu toka kwangu?” “Sina swali, ila kila naona mambo mapya, wee mchaga mambo ya pwani umeyajulia wapi?”
“Kwani Bi Shuu ni mtu wa Pwani, Mmanyema mtu wa Kigomayeye kayajulia wapi? Si watu wa mwambao wa Pwani tu wanajua mapenzi.” “Mmh, nimekubali.”
Nilimpokea koti lake na kuliweka kwenye kochi, alipokaa alimvua viatu kisha nilihamia kwenye shati nikatelemka kwenye suruali, nikatoa na nanihii kisha nikampa upande wa kanga ili nimpeke bafuni tukaoge.
Utajiuliza kwa nini nimempa kanga badala ya taulo, mwa kwetu kanga ina raha yake, huwezi kwenda nyumba ya wageni ukakuta kanga lazima utakuta taulo. Kama mpenzi wako alizoea kwenda nyumba ya wageni ukimpa kanga lazima akili yake ataona kuna tofauti ya nyumba ya wageni na nyumbani kwa mpenzi wake.

Baada ya kuoga tulirudi ndani kisha nilijifanya kama kuna kitu kinaniwasha na kujikuna kwa kuipandisha nguo, nilijua lazima Mateja ataangalia, nilirudisha haraka mtego wangu ulinasa, ukimuoneshamaungo nyeti nusu, lazima atataka aone kabisa kufanya vile ilikuwa kumuongezea mahanjamu. Mmh! Mtoto wa kume uzalendo ulimshinda, nimnyime ili iweje, shoga mwili wako mali ya mpenzio, hasa yule mliyeshibana.
Alipotaka nikampa kwa nguvu zote, huku nikumuuliza baba chagua kipapatio ili usichoke sana kabla ya kula au paja ushibe kabisa. Mateja alitaka kipapatio, ushaanza- kipapatio ni nini? Wapo waliotafuta maana zao, jamani kipapatio penzi jepesi lisilochosha, nina imani hata paja ushajua. Haya twende kazi, mmh, mtoto wa kike nilijisahau na kumuongezea paja baada ya kumuona kabisa kipapatio hakimtoshi. Mwisho wa shughuli nilimwacha kajilaza na kumuwekea wimbo wa dereva huku nikimbadili jina toka Tx mpaka Dereva.
Mateja kila aliponiangalia alitikisa kichwa. Nilimnyanyua na kumpeleka bafuni kisha nilimualika mezani. Baada ya kutafuna tonge la kwanza alitikisa kichwa na kusema: “Hakika wewe ni chura,” kauli ile ilinitisha iweje aniite chura mdudu tena nisiye mpenda. “Mpenzi kwa nini umeniita chura?” “Sina nia mbaya, nina maana chura anaishi kotekote majini na nchi kavu. Umekamili kila idara, nikiwa na na wewe raha zangu hazitakuwa na kikomo.”

“Ha! Kumbe, Asante mpenzi.” Nilimkumbatia Mateja kwa furaha. Baada ya chakula tulipumzika chakula kiende sehemu zake baada ya hapo mtoto hakutumwa dukani. Sitaki kukuchosha sasa hivi mimi ni mke halali wa Mateja, tunapendana kwa dhati huku nikiendelea kupokea mawazo ya Bi Shuu bibi ambaye sitamsahau mpaka nakufa. Mwisho nawaomba wanawake wenzangu kutafuta dawa ya mapenzi ambayo ni kujifunza kwa waliotutangulia ili viungwe viwe vitamu wa wapenzi wetu kwani siku zote ukikitoa hamu kitakosa utamu.

******************************************MWISHO*(************************************

Safi sana...

Ila simulizi ina mipasho aisee...


Chapter Closed...


Cc: mahondaw
 
Huyo bi shuu anapatikana wap? Na mm nimlete dem wangu apate mafunzo maana siitaji kumcheat
 
Back
Top Bottom