MwanaDiwani
JF-Expert Member
- Mar 22, 2013
- 5,536
- 2,268
- Thread starter
- #101
Nimeshindwa kujizuia kukupa hongera yangu kutokana na andiko lako lililobeba hoja nzito ambazo wachache hawapendi kuzisikia.Pengine sasa Jaji Warioba aulizwe alimuhoji nani hasa katika taasisi mbali aiwezekani kila kukicha wadau wanajitokeza na kusema vingine kinyume na madai ya mapendekezo ya rasimu kuhusu msimamo wa taasisi nzima.
Hivi kama hao watu wachache kati yetu waliobahatika kutoa maoni kupitia makundi yao na kwenye kutoa mapendekezo walitofautiana kuhusu muundo wa serikali moja, mbili na tatu, iweje tudhani wabunge leo wanadhamana ya wapiga kura wao mpaka wapige kura za siri wakati wengi hawajatoa maoni yoyote directly?
Swala hili ni very complicated na wapiga kura wanahaki za kujua wawakilishi wao wamechagua nini kwa niaba yao kama Kardinali alivyojuzwa (na kuamua kutoa msimamo wake binafsi) na wawakilishi wa baraza mapinduzi walivyojuzwa na kuukana kuwa ni msimamo wa wachache. Mwisho wa siku na watanzania wanahaki hizohizo za kufahamu wawakilishi wao wamewachagulia nini.
Kura ya siri ni kwa sababu ya impact ya mtu mmoja hila kama unawapigia kura watu kwa niaba yao wanahaki ya kujua umewachagulia nini na waamue kama wakurudishe au wakutose na isitoshe kama hupo kwenye chama pia chama kiamue kama hupo pale kwa mawazo ya wengi au utoke kwa kutokubali misimamo ya pamoja. Ndio demokrasia yenyewe na aitaki mzaha mzaha.
Kuna mambo ya msingi kabisa katika mchakato wa Katiba ambayo hayahitaji kutingishwa kwa hoja kama yako kabla hatujaanza kuendelea na safari katika bunge la Katiba.
Ukweli utaendelea kubainika kila siku.