Yanini umwite Pasco, soma hiyo makala ya mwanacnhi hapo juu inasema Pengo amekataa huo si msimamo wa kanisa katoliki, kwanini pengo akatae kwa niaba ya kanisa nzima na si askofu mwingine yeyote?.
Hata Ruzoka alipotoa ule Waraka alisema ni Waraka wa Kanisa Katoliki. Ruzoka amepata wapi mamlaka ya kuwasemea wakatoliki wote?
Unajua sisi wabongo tunaangalia maslahi,yakitajwa maslahi yako unafurahi yakitajwa maslahi ya mwingine unachukiaKuna baadhi ya watu wanatumia njia zote hata zile za kilaghai ili kupitisha ajenda zao. Wanashindwa kusimama wao wenyewe ili wahesabiwe kwa kutoa maoni yao kwa sababu pamoja na mambo mengine, wanasumbuliwa na inferiority complex. Hawajiamini kama kauli zao zinakubaliwa/zitakubaliwa na wanachi.
Huwezi kulitumia kanisa Katoliki kwa mambo ya kilaghai hasa ikichukuliwa kuwa kanisa ni kioo katika jamii kwenye maswala ya ubinadamu.
Kuelekea upatikanaji wa Katiba mpya, tutawasikia wengi wakija na matamko huku wakidai yametolewa na taasisi zinazo heshimika katika jamii.
Tunashukuru Baba Askofu kwa kutoa ufafanuzi mzuri kulingana na tamko la Tume ya Haki na Amani.
Ungetulia na kusoma, basi ungemuelewa Card. Pengo, na wala usingeandika hayo. Hebu rudia kusoma kipande hiki, hasa hapo kwenye bolded red font:... na Pengo anazungumziaje mamilioni ya wakatoliki ambao hawaungi mkono kauli yake??...
... Aliongeza kuwa anatumia nafasi hiyo katika mkutano na waandishi wa habari kutoa msimamo wake kama Mtanzania wa kawaida kuwa mapendekezo yake ni kuendelea kuwepo kwa serikali mbili yaani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar....
Pengo amedhihirisha ukereketwa wake kwa CCM na ku-confirm dhana inayolalamikiwa na Waislamu kuwa Serikali ya ccm inafuata sera ya mfumo Kristo.
Rasimu ya Katiba imetokana na mawazo ya wananchi yeye ni nani mpaka adharau matakwa yao? Mamlaka ya kuwasemea wananchi ameyatoa wapi?
Wakatoliki watanisamehe kwa hili, ila Mkuu wenu wa Kiroho amepotoka kuingilia na kutoa msimamo wa kisiasa!
Kufikia hapa naweza nikasema bila shaka yoyote kuwa Pengo ni mfuasi wa kambi ya Lowassa.
Kumbuka kipindi kile Lowassa amefukuzwa kazi kwa sababu ya ufisadi, baada ya muda Cardinal Pengo alimtembelea Lowassa nyumbani kwake na kuzindua kitabu cha mke wa Lowassa, Regina!!
KANISA Katoliki limekanusha taarifa iliyotolewa na vyombo vya habari kuwa msimamo wa kanisa hilo ni kuwepo kwa serikali tatu katika katiba mpya.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amesema taarifa hiyo si sahihi bali ilitolewa na Tume ya Haki ya Baraza la Maaskofu pasipo kumshirikisha.
"Wao kama Watanzania wanayo haki ya kutoa maoni, hivyo si kosa wakiwa kama Watanzania maoni yao kuwa ni kuwepo serikali tatu, ilichokosea tume hiyo ni kusema kwamba huo ni msimamo wa Kanisa Katoliki jambo ambalo si kweli," alisema.
Pengo alisema anakanusha vikali taaifa hiyo iliyotolewa juzi na vyombo mbalimbali vya habari hususan magazeti na kuwa Kanisa Katoliki lina wajibu wa kutoa msimamo wake katika mambo mawili tu yanayohusu imani na maadili.
"Kwa mfano ikitokea hoja kwamba kuwepo na vipengele kwenye katiba vinavyosema hakuna Mungu, kuwepo kwa ndoa za jinsia moja au kuhalalisha utoaji mimba hapo kanisa lina haki ya kusimama na kutoa msimamo wake kwani masuala hayo yanagusa imani na maadili,"alisema.
Aliongeza kuwa anatumia nafasi hiyo katika mkutano na waandishi wa habari kutoa msimamo wake kama Mtanzania wa kawaida kuwa mapendekezo yake ni kuendelea kuwepo kwa serikali mbili yaani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar.
"Kama kuna dosari zozote zilizojitokeza wakati wa kuasisi Muungano zinazotishia umoja wa kitaifa ni heri zikarekebishwa ili uendelee mfumo wa serikali mbili kwani serikali tatu ni mzigo," alisema.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Tume ya Haki na Amani ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) ilitoa tamko ikitaka Bunge Maalumu la Katiba kuepuka kukashifu mapendekezo ya muundo wa serikali tatu.
Chanzo:Habarileo.
Mimi ni muumini wa kanisa katoliki tena muumini kweli kweli lakini kwa hili Askofu Pengo amepotoka na naamini ili aendelee kuwa na heshima aliyonayo kwa waumini wake aseme huo ni masimamo wake yeye na sio msimamo wa kanisa katoliki!!! wananchi wameshaamua namna wanavyotaka kuongozwa na sio yeye kutulisha misimamo yake!!!!
Mnamsema bure kwa kuwa hamjamuelewa. Amesema Kanisa huwa halitoi msimamo kuwaelekeza Wakatoliki nini cha kuchagua, labda huo msimamo uwe unahusu masuala ya IMANI au MAADILI. Hata inapolazimika kutoa msimamo wa KANISA, ni Baraza la Maaskofu (TEC) pekee linaweza kutoa msimamo wa KANISA KATOLIKI kupitia Rais wake (ambaye sio yeye Kard. Pengo). Maoni mengine yanaweza yakatolewa na mtu binafsi (kama yeye Pengo) au vyombo vya kanisa (kama Baraza la Walei), na hailazimishi kila Mkatoliki kuifuata kwani haina uhusianao wa moja kwa moja na IMANI au MAADILI.
Tuwe makini tunapowanukuu viongozi wetu, hasa wanapokuwa wasomi kama Pengo, kwa maana lugha ya kisomi inaweza kumfanya mtu asimuelewe halafu akakimbilia kuanzisha thread humu kama alivyofanya huyu tpmazembe
Yaani huyu hana hata aibu, anaonyesha msimamo wake wa kisiasa kabisa.
Mnamsema bure kwa kuwa hamjamuelewa. Amesema Kanisa huwa halitoi msimamo kuwaelekeza Wakatoliki nini cha kuchagua, labda huo msimamo uwe unahusu masuala ya IMANI au MAADILI. Hata inapolazimika kutoa msimamo wa KANISA, ni Baraza la Maaskofu (TEC) pekee linaweza kutoa msimamo wa KANISA KATOLIKI kupitia Rais wake (ambaye sio yeye Kard. Pengo). Maoni mengine yanaweza yakatolewa na mtu binafsi (kama yeye Pengo) au vyombo vya kanisa (kama Baraza la Walei), na hailazimishi kila Mkatoliki kuifuata kwani haina uhusianao wa moja kwa moja na IMANI au MAADILI.
Tuwe makini tunapowanukuu viongozi wetu, hasa wanapokuwa wasomi kama Pengo, kwa maana lugha ya kisomi inaweza kumfanya mtu asimuelewe halafu akakimbilia kuanzisha thread humu kama alivyofanya huyu tpmazembe
mkuu unaonekana unajua mengi, labda ungetuelewesha kidogo, ni nini hasa kilichopo nyuma ya hii kauli ya pengo. kwani wananchi wanataka serikali 3 kwa mujibu wa tume ya warioba, na katiba ni ya wananchi, ni kwanini pengo anatumia cheo chake ndani ya mwanvuli wa usomi kuwaamlia waTz zaidi ya mil45 walioamua wawe na serikali 3?
Mkuu Lidelele, kwanza haitwi Pengo, anaitwa Mwandhama Policarp, Cardinali Pengo. Huyu ni kiongozi wa kiroho wa Wakatoliki, ila pia yeye kama Pengo, ni raia wa Tanzania mwenye haki zote sio tuu kutoa maoni bali pia kushiriki katika siasa, au serikali, toka serikali za mitaa hadi serikali kuu kwa mujibu wa katiba!.Kufikia hapa naweza nikasema bila shaka yoyote kuwa Pengo ni mfuasi wa kambi ya Lowassa.
Kumbuka kipindi kile Lowassa amefukuzwa kazi kwa sababu ya ufisadi, baada ya muda Cardinal Pengo alimtembelea Lowassa nyumbani kwake na kuzindua kitabu cha mke wa Lowassa, Regina!!
sasa hii ni nini!!???
Tulishawaachia akina warioba kazi, wakamaliza... na sasa tumewapa watu mia sita ukumbi wafanye upuuzi na maigizo, then huyu jamaa nae anakuja kivyake
where is the authorization matrix in the country, na Pengo anazungumziaje mamilioni ya wakatoliki ambao hawaungi mkono kauli yake??
HE LOST CREDIBILITY LONG AGO, AND HE SHOULD TRY TO KEEP THE SMALL RESPECT HE HAS TO HIMSELF, THIS IS A SILLY MISTAKE TO MAKE AND HE HAD NO REASON WHATSOEVER
SOMETIMES UKISHINDWA KUELEWA NAFASI YAKO, UNAISHIA KUWA KANJANJA TU KAMA KANJANJA WENGINE.... PENGO COULD AHVE MADE SOME ONE ELSE MAKE THOSE REMARKS