Wewe naona unakuja na akili zako za shule ya kata,mada ni kuwapo au kutokuwapo kwa Mungu.Hizi shule za kata ni Tatizo kubwa.Unataka kuwaomdowa watu katika mada iliyopo,uwapeleke sipo.Not true, ALLAH anaye hitaji usaidizi wa Binadamu si muweza wa kila kitu.
Pint yako nzuri mheshimiwa.
Soma maelezo yangu,nimesema kila unavyoviona duniani,wewe unauliza Mungu katengenezwa na nani wakati,hujamuona hapa Duniani.Ndio mana nikakuambia akili yako ikiona kitu,na ukasema hakijetengezwa,ujue akili zako hazina akili.Hapa ninakutajia vitu tunavyoviona duniani.Mungu hatujamuona duniani,Tutasemaje katengenezwa.Na pili Mungu hana production date wala Expiredate.chenye kutengenezwa chochote kina production date na Expire date.Ni wapi umeona pameandikwa kama Mungu alizaliwa au alitengezwa lini,na expire date yake itatokea au ilitokea lini.Si kweli.Inawezekana kabisa kwamba mungu hayupo na vilivyo duniani havijajitengeneza vyenyewe.
Ukisema hivi utajiingiza katika contradiction. Kwa sababu hata huyo mungu anayedaiwa kuvitengeneza vitu vyote, naye atahitaji kuwa ametengenezwa. Ukikataa hilo na kusema kwamba mungu hakutengenezwa, then unakubali kwamba si kila kitu ni lazima kitengenezwe na hivyo si lazima mungu awe ndiye aliyetengeneza kila kitu.
Bado unarudi palepale. Kama kila kitu kinahitaji muumba, basi hata mungu anahitaji muumba.Kama mungu hahitaji muumba, basi si kila kitu kinahitaji muumba na hivyo inawezekana vyote visiwe vimeumbwa na mungu.There is no escaping this conundrum.
Mwanadamu kushindwa kupata ufumbuzi wa matatizo fulani hakumaanishi kwamba mungu yupo. This is a logical non-sequitur.
The second law of thermodynamics explains death quite well. I do not need the god hypothesis.
Uwezo wa kukishinda kifo unaprove vipi kuwepo au kutokuwepo kwa mungu? Toa uwiano na mahusiano hapa.
Mifano gani? Itaje. Unajua "kujuwa" ni nini?
Soma maelezo yangu,nimesema kila unavyoviona duniani,wewe unauliza Mungu katengenezwa na nani wakati,hujamuona hapa Duniani.Ndio mana nikakuambia akili yako ikiona kitu,na ukasema hakijetengezwa,ujue akili zako hazina akili.Hapa ninakutajia vitu tunavyoviona duniani.Mungu hatujamuona duniani,Tutasemaje katengenezwa.Na pili Mungu hana production date wala Expiredate.chenye kutengenezwa chochote kina production date na Expire date.Ni wapi umeona pameandikwa kama Mungu alizaliwa au alitengezwa lini,na expire date yake itatokea au ilitokea lini.
Wengine kwa uzembe wao wanaona bora waue wenzao kwa unga.
Chenye production date na expire date ndio kimetengenezwa.Kwa maana kina mwanzo na kina mwisho.Nijibu swali moja.
Ni lazima au si lazima kwa vyote kutengenezwa?
Kwani hamwoni Steve Wonder anavyofanya mambo yake kwenye kinanda vilevile ni muimbaji na mcheza movie wa kimataifa lakini haoni. Hata hapa bongo wapo watu wa aina hiyo wengi kama yule jamaa pale UDSM ni mtaalamu sana kwa maswala ya IT.Mungu anaumba atakavyo,anaweza kumuumba kipofu na akawa na akili kukushinda wewe mwenye mach.Yupo mwalimu wa sayansi,anafundisha secondary,na ametunga vitabu vingi vya sayansi.Anakushinda hata wewe mwenye macho,hayo ndio maajabu ya Mungu,na wapo wengi ni vilema,lakini wanawashinda wenye macho.Yapo vilema matajiri,wapo maprofesa,wamewashinda wenye macho.Na Mungu ndio anaonyesha uwezo wake,kwa mwenye akili anaweza kuelewa wazi kama yupo Mungu,anayeyafanya yote haya,hata wewe akitaka kukugeuza kilema,haichukui hata dakika.Na bora kuwa kilema wa viungo,kuliko kilema cha akili.Kushindwa kufikiri na kuelewa,kama wewe yaonyesha una ukilema wa akili,unashindwa kuelewa.
Chenye production date na expire date ndio kimetengenezwa.Kwa maana kina mwanzo na kina mwisho.
Mimi ni Roman Catholic safi lakini ukiruhusu akili yako iwe huru usikilize maoni ya pande zote mbili kwa kweli unaweza ukakubali Mungu hayupo kwasababu tunaoamini Mungu yupo tunakuwa tunasadiki lakini kwa wanaosema Mungu hayupo mara nyingi wanatumia facts.
BTW, bora nisadiki Mungu yupo niende nimkose kuliko nisisadiki halafu nimkute.
Sijauliza chenye production date na "expire" (sic) date.
Nimeuliza vyote.
Hujajibu swali.
Kama hili ni swali la mtihani na unajibu hivi unapewa bonge la mkasi.
Hujajibu swali uliloulizwa, na ulichojibu hakijaulizwa.
unaposema 'vyote' unamaanisha nini au vinini?
Kiranga;
Unajuaje kwamba wewe viungo vyako vimekamilika? Wapi pamesema kwamba binadamu inabidi awe na kichwa kimoja na siyo vinne au vitano? Huyo unayemwona ni kilema anaweza akawa ni sawa tu na wewe kwa sababu pengine Mungu angekupa vichwa saba ndiyo ungekuwa uko kamili lakini sasa kaamua kukupa kimoja and still you do no what you are missing. We ukiona kila mtu ana kichwa kimoja basi unajua binadamu anatakiwa awe na kichwa kimoja. Anyway ni kwamba tu uko mbali sana na Mungu ila ukimkaribia is as easy as abc ku-experience uwepo wake. Siyo kujua ila ni ku-experience, zingatia tofauti!
ALLAH ni muweza wa kila kitu...