Mvuvi mvivu.

Mvuvi mvivu.

Jaguar

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2011
Posts
3,440
Reaction score
1,029
Mpitanjia mmoja alimkuta mvuvi kakaa chini ya mti akipumzika huku akiwatazama wavuvi wengine wakiendelea na kazi,mazungumzo yakawa kama ifuatavyo; (MPITANJIA):We mvuvi acha uvivu,nenda kafanye kazi! (MVUVI):Nifanye kazi ili iweje? (MPITANJIA):Upate pesa nyingi! (MVUVI):Na hizo pesa zitanisaidia nini? (MPITANJIA):Utanunua boti yenye injini,utapata samaki wengi zaidi,utapata pesa nyingi zaidi na utanunua boti nyingi zaidi. (MVUVI):Na hizo boti zitanifaa nini? (MPITANJIA):Utaajili wafanyakazi wengi halafu wewe utakaa chini ya mti ukipumzika na kuwatazama wakikufanyia kazi yako! (MVUVI):Kumbe mwisho wa yote ni kukaa chini ya mti na kupumzika,kwani hapa umenikuta nafanya nini?
 
Ahahahaaah!! Mwenyewe karidhika..
 
judging the book by its cover.,!!
 
Huyo mvuvi namtengenezea picha kama nvile "Muhogo mchungu" na majibu ya nyodo.
 
Huyo mvuvi namtengenezea picha kama nvile "Muhogo mchungu" na majibu ya nyodo.
Hawa ndo watu wa pwani bwana,anakwenda baharini anavua samaki kapu moja,anauza wale samaki,akipata visenti haendi baharini tena mpaka viishe!
 
Hawa ndo watu wa pwani bwana,anakwenda baharini anavua samaki kapu moja,anauza wale samaki,akipata visenti haendi baharini tena mpaka viishe!

halafu tukakubali tuongozwe na mtu wa pwani, ukimuuliza kwanini hatulii ikulu atakwambia ikulu ni mahali patakatifu
 
Duh, hii kali! Mnasema huyo ni mtu wa Pwani? Nani, Prezidaa?
Ha ha ha haaaa!!!
 
Back
Top Bottom