Mvua za vuli: Je, Wandebele walimsamehe Mugabe

Mvua za vuli: Je, Wandebele walimsamehe Mugabe

inchaji

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2019
Posts
2,650
Reaction score
5,461
Robert Mugabe ameondoka. maandiko yametimia: Kila nafsi itaonja mauti.

Pamoja na kuondoka kwake maswali ni mengi yamebaki. Moja ya maswali ni kisa cha mauaji ya mvua za vuli.

Mapema miaka ya ‘80 wakati uhuru wa zimbambwe ukiwa katika uchanga wake kulikuwa na fukuto miongoni mwa washona kabila la robert na wandebele, kabila la nkomo. Robert na Nkomo walipambana kwa pamoja kuupigania uhuru wa Zimbabwe na baada ya kuwa umepatikana, Robert alipata kuwa waziri mkuu wa nchi kufuatia kupata wingi wa viti vya bunge. Nkomo akawa waziri muandamizi.

Pamoja na hayo na kama ilivyo kwa viongozi wengi wa kiafrika, robert hakuwa akijiamini. Alikuwa na hofu kubwa kuwa nkomo anataka kumpindua. Kuona hivyo robert akaamua kujihami na moja ya mkakati ulikuwa ni huu ulioitwa mvua za vuli. Mvua zenye tabia ya kusafisha mashamba kwa ajili ya kuiandaa ardhi na kilimo. Mvua hizi zikinasibishwa na uhuru wa zimbabwe wakati huo kwamba sasa tumepata uhuru basi na tuondoe au tuzime upinzani wa aina yoyote tutawale tukavyo.

Waskari wa kikosi cha 5 waliokuwa wamepata mafunzo Korea Kaskazini walitekeleza mauaji ya wandebele zaidi ya kati ya 20,000 na 80,000. Inasemekana walitumwa na mugabe japo hakuwahi kukiri lakini kuna siku akiomboleza kifo cha nkomo alitamka maneno ambayo hakuwahi kuyarudia tena wala kutoa ufafanuzi wake kwamba mauaji ya mvua za vuli kilikuwa ni ‘kipindi cha wazimu’.

Kwa uzalendo tunao brainwash-iwa juu ya Robert Mugabe alipaswa kufia kwenye hospitali za Zimbabwe aliyokuwa anadai kuipigania maslahi yale ila sasa kafia kwa mabeberu. Wazimbabwe ni hoi bin taaban kiuchumi. Itoshe tu kusema tu kuwa Robert siyo mwanamapinduzi kama tunavyo brainwash-iwa. Alikuwa ni muuaji mwingine tu kama walivyo wauwaji wengine na alitakiwa akumbane na mkono wa sheria.

je, Wandebele walimsamehe?
 
Poa mkuu,wewe si ndo uliyewatoa mabeberu pale,basi we ndo mzalendo.
Mzee Mandela mbona alifanikiwa kuutoa utawala wa Makaburu lakini hakuwahi kuwaua wapinzani wa ANC baada ya hapo. kwa nini Mugabe aliwaua Wandebele? anastahili heshima ya kupepeza bendera nusu mlingoti huyu?
 
Madhambi ya Mugabe yanafunikwa na viongozi wa kiafrika waliopo madarakani kwa sasa kwa kuwa mikono yao wote imejaa damu za wapinzani. Pamoja na hayo, sisi tunayoijua historia yaliyoandikwa kwenye mioyo yetu ambayo haitakaa ifutike.

Hata Magufuli, matendo yake dhidi ya wapinzani na wanaharakati yanajulikana mchana kweupe. Vikundi anavyovilea vya kuendesha mauaji na vitisho vitamwandama hata katika KIFO.

Waafrika ni lazima tufike mahali tuwe wa kwanza kuongea ukweli, hata kama unauma. Haiwezekani eti kiongozi mmoja asifiwe tu, hata Nyerere ni lazima aandikwe, asemwe, na ajadiliwe law uwazi kabisa bila kuzidisha propaganda wala kumwonea kwa yale yote aliyofanya.

Kadiri tunavyozika ukweli na kuimba mapambio ya sifa ndipo tunavyodidimiza hadhi ya uafrika wetu. Mwafrika atazidi kuonekana haja-evolve kuwa binadamu kamili bado.
 
Madhambi ya Mugabe yanafunikwa na viongozi wa kiafrika waliopo madarakani kwa sasa kwa kuwa mikono yao wote imejaa damu za wapinzani. Pamoja na hayo, sisi tunayoijua historia yaliyoandikwa kwenye mioyo yetu ambayo haitakaa ifutike.

Hata Magufuli, matendo yake dhidi ya wapinzani na wanaharakati yanajulikana mchana kweupe. Vikundi anavyovilea vya kuendesha mauaji na vitisho vitamwandama hata katika KIFO.

Waafrika ni lazima tufike mahali tuwe wa kwanza kuongea ukweli, hata kama unauma. Haiwezekani eti kiongozi mmoja asifiwe tu, hata Nyerere ni lazima aandikwe, asemwe, na ajadiliwe law uwazi kabisa bila kuzidisha propaganda wala kumwonea kwa yale yote aliyofanya.

Kadiri tunavyozika ukweli na kuimba mapambio ya sifa ndipo tunavyodidimiza hadhi ya uafrika wetu. Mwafrika atazidi kuonekana haja-evolve kuwa binadamu kamili bado.
Mkuu ni kweli watawala weusi walifanya maovu makubwa ya kuuwa waafrika wenzao ,hata kuliko mkoloni.
Kwa mfano Idi Amin aliuwa watu wengi Uganda kuliko serikali ya Makaburu nchini SA
Robert Mugabe aliuwa wazimbabwe wengi kuliko serikali ya Mlowezi Ian Smith.
Sudan kusini wameua kwa kugombea madaraka kuliko vita ya MAUMAU nchini Kenya.
Rwanda nayo malaki waliteketea sababu watawala kueneza chuki za kikabila.
Msumbiji,Angola walinyukana na kuteketeza malaki ya waafrika wazawa wao kwa wao wakitetea maslahi binafsi ya kuwatawala wenzao.
Congo ya DRC haijawahi kuonja amani kwa zaidi ya miaka 100 ni mateso tu ya wakoloni weupe na wakoloni weusi.
Historia ya Afrika inabidi kuandikwa upya,hata African Union ni kichekesho kwani haizingatii maslahi ya wananchi walio wengi wa nchi za Afrika bali ni muungano wa watawala tu.
 
Madhambi ya Mugabe yanafunikwa na viongozi wa kiafrika waliopo madarakani kwa sasa kwa kuwa mikono yao wote imejaa damu za wapinzani. Pamoja na hayo, sisi tunayoijua historia yaliyoandikwa kwenye mioyo yetu ambayo haitakaa ifutike.

Hata Magufuli, matendo yake dhidi ya wapinzani na wanaharakati yanajulikana mchana kweupe. Vikundi anavyovilea vya kuendesha mauaji na vitisho vitamwandama hata katika KIFO.

Waafrika ni lazima tufike mahali tuwe wa kwanza kuongea ukweli, hata kama unauma. Haiwezekani eti kiongozi mmoja asifiwe tu, hata Nyerere ni lazima aandikwe, asemwe, na ajadiliwe law uwazi kabisa bila kuzidisha propaganda wala kumwonea kwa yale yote aliyofanya.

Kadiri tunavyozika ukweli na kuimba mapambio ya sifa ndipo tunavyodidimiza hadhi ya uafrika wetu. Mwafrika atazidi kuonekana haja-evolve kuwa binadamu kamili bado.
Magufuli is a serial killer
 
Hao wazee wanaoitwa wazalendo baadhi yao ni makatili kuliko hata makaburu.
 
Back
Top Bottom