Mvua za El nino: Serikali inasubiri nini kufunga shule

USSR

JF-Expert Member
Jul 15, 2015
9,896
22,666
Leo nikiwa napita maeneo mbalimbali nikitokea Dodoma hadi nafika Dar es Salaam naona watoto wadogo njiani wakiwa wameshika viatu huku wakitembea kwenye njia zilizojaa maji, wakinyeshewa, wakiloanishiwa madaftari na vitabu huku wakionesha kujuta kuzaliwa katika jamii iliyo na roho ngumu isiyojali hatari ya usalama wa watoto.

Kuna maeneo barabara zimefunikwa na maji, madaraja yamejaaa maji hupita juu ya maji. Kuna watoto walio upande wa pili wa mito, mabonde na mabwawa ya misimu ya maji sasa yamejaa watoto wanalazimika kuvuka ili waende shule.

Nilidhani kuwa zile kelele za El nino zilizingatia na usalama wa watoto wetu hasa miji mikubwa ambapo usafiri sasa ni kero sana.

Serikali isisubiri mpaka watoto hawa wafe au kupata madhara ndio eti waje kuchukua hatua za kuzuia huku tumeambiwa mvua bado zipo sana tu tena kubwa.

Note: Mimi nikiwa mzazi ninajali usalama wa watoto wagu nimezuia wasiende shule (japo huijiwa na gari la shule) mpaka hapo mvua hizo za El nino zitakapokoma.

USSR
 
Hoja yako ni ya msingi na inafaa kuungwa mkono na kila mtu mwenye utu.

Haiwezekani watoto wanaenda shule Kwa tabu namna hiyo tena wakifofia maisha yao.

Na wakifika shuleni akili zao zinabaki kuwaza mvua na wasiwe na uwezo wa kumsikiliza mwalimu wao.

Wakati huohuo waonaporudi majumbani usalama ni nusu.

Serikali ifunge shule Kwa Chekechea na shule za msingi mikoa yenye El nino
 
Hoja yako ni ya msingi na inafaa kuungwa mkono na kila mtu mwenye utu.

Haiwezekani watoto wanaenda shule Kwa tabu namna hiyo tena wakifofia maisha yao .

Na wakifika shuleni akili zao zinabaki kuwaza mvua na wasiwe na uwezo wa kumsikiliza mwalimu wao .

Wakati huohuo waonapo rudi majumbani usalama ni nusu .

Serikali ifunge shule Kwa Chekechea,na shule za msingi mikoa yenye El nino
Mie mtoto leo, kesho haendi shule
 
Back
Top Bottom