Mvua kubwa katikati ya Jiji la Dar es Salaam

Mvua kubwa katikati ya Jiji la Dar es Salaam

Status
Not open for further replies.

Watu8

Platinum Member
Joined
Feb 19, 2010
Posts
76,921
Reaction score
110,354
Habari ndugu wanabodi,
Napenda tu kuwajuza wale wote wenye nia ya kuja katikati ya Jiji la Dar es Salaam, kuwa kwa sasa huku kuna mvua kubwa inayoambatana na upepo. Hivyo kwa wale wenye safari za huku na ambao hamna usafiri binafsi mzingatie hilo na kuchukua tahadhari.

Ningependa pia uzi huu utumike kujuzana hali za maeneo mengine ya Jiji, ili wadau wengine wapate kujua hali ya mvua kwa maeneo mengine.

Nawasilisha.


=========================
Update leo: 30/04/2013
=========================

Habari wadau wa jukwaa hili: kumekuwepo na mvua inayoendelea kunyesha jijini hapa tangu majira ya asubuhi na hivyo kupelekea kuwa na adha ya usafiri hasa maeneo ya katikati ya jiji kwa mnaokuja huku baadhi ya barabara zimejaa maji na uwepo wa madimbwi katikati yake hivyo ni vyema ukajichukulia tahadhari mapema.

f1.jpg


f2.jpg


Picha kwa Hisani ya Blog ya Jamii
 
hali ya foleni pia moroko road to mwenge inaelekea kuwa mbaya japo wanausalama wanakomaa.Inatupasa kuchukua tahadhari hasa kwa wale ambao hawajatoka majumbani/maofisini maana watu mvua ikianza tu wanakuwaga kama wamefukuzwa maofisini/majumbani mwao wanakimbilia kubanana barabarani.
 
Niko maeneo ya kamata huku nyerere road foleni ni ya kufa mtu! Hapo baadae hali ya usafiri inaweza kuwa mbaya zaidi!
 
Niko maeneo ya kamata huku nyerere road foleni ni ya kufa mtu! Hapo baadae hali ya usafiri inaweza kuwa mbaya zaidi!
Nipo maeneo ya Kisutu.!
Mvuani nyingi mno;maji yamejaa
 
Anayetaka kupita ubungo mataa kuko shwari, japo manyunyu yanaendelea
 
duh... kweli haka kamvua! hapa mnazi mmoja kuna foleni na nusu ya barabara ya lumumba imejaa maji...
 
Wale wabishi wamabondeni-mkwajuni,jangwani,kigogo sambusa andaeni kabisa masufuria ya kutolea maji ndani!
 
Leo ni siku ya mvua hapa DSM, japo inatofautiana kiwango mfano maeneo ya Ubungo inanyesha lakini haitishi sana sema tu miundombinu ya jiji ilivyo mibovu utasikia mara mafuriko, mitalo kujaa maji nk.
 
Hahaha...sina wasiwasi kabisa na habari ya kurudi nyumbani mkuu...nilikua tu nawajuza wengine hali ilivyo...ila sasa naona hali inaanza kuwa nzuri mvua imekata...sasa sijui kwa maneno mengine

watu8 fanya urudi nyumbani mapema maana kwa nijuavyo leo foleni itakuwa haikamatiki!!!
 
duh... kweli haka kamvua! hapa mnazi mmoja kuna foleni na nusu ya barabara ya lumumba imejaa maji...

Haya jamani wale watumiaji wa Barabara ya Lumumba na maeneo ya Mnazi Mmoja ( Hii nadhani itakuwa Uhuru Road0....hali ndio hiyo...
 
...Huku Mbezi Inn Mbezi Mwisho tunaona tu mawingu kwa huo upande wa mjini lakini kwetu ni upepo tu na tumanyuyu twa mbaaali. Poleni huko.
 
hahahaha jamani kwahiyo namtumbo hakuna mabachelor au?

hapa nani analima,zinashindwa kunyesha kwa wagogo huko zinatusababishia jam
down town,3hrs uko kwenye foleni,jahazi linaanza mpaka linaisha we upo tu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom